Image
×

Onyo

JUser: :_load: Haiwezi kupakia mtumiaji aliye na kitambulisho: 797

"Macho mekundu" ni neno linalotumika kuelezea macho yaliyopata wekundu, kuwasha, na kuwa na viashiria vya damu (bloodshot). Wekundu huu hutokea pindi vimishipa midogo ya damu chini ya uso wa jicho vinapotanuka au kuvimba. Mara nyingi, ni athari ya ukereketaji (irritation) au mashambulizi (infection) ya kwenye jicho. 

Macho mekundu yanaweza kuathiri jicho moja au yote mawili. Pia ni hali ambayo inaweza kutokea taratibu au kwa ghafla, kama vile kwa matatizo ya mzio au jeraha la jicho.

Unaweza kuwa na macho mekundu na dalili nyingine kama vile:

  • Maumivu ya jicho.
  • Kuwasha.
  • Kutokwa na matongotongo.
  • Kuvimba kwa jicho.
  • Mabadiliko katika kuona, kama vile kuona ukungu.

Hatua na viwango tofauti vya ukali wa macho mekundu

Mara nyingi, macho mekundu athari zake huwa kubwa kwa muonekano kuliko jinsi unavyojisikia ndiyo maana kwa wengi huwa hawahisi kitu mpaka wanapoenda kujiangalia na kugundua kuwa jicho limekuwa jekundu. Katika visa vingi, macho mekundu ni ya kawaida na mara nyingi hutibiwa na matibabu ya nyumbani au matibabu ya madawa ya kawaida (OTC).

Lakini ikiwa jicho lako au macho yako yanaendelea kuwa mekundu kwa zaidi ya wiki moja, au una maumivu au matatizo kwenye kuona, hakikisha unaweka miadi ya kuonana na daktari haraka uwezavyo, unaweza kuonana na daktari wa macho ophthalmologist (eye doctor) au daktari wa miwani optometrist.

Ni nini chanzo cha kawaida cha macho mekundu?

Kuna sababu nyingi zinazoweza kupelekea kupata tatizo la macho mekundu, macho yanaweza kupata wekundu kutokana na uvaaji wa lenzi za kuweka machoni kwa muda mrefu au umekaa kwenye kompyuta kwa muda mrefu bila kupata mapumziko. Baadhi ya sababu nyingine za kawaida ni pamoja na:

  • Mzio (Allergies).
  • Tatizo la Blepharitis.
  • Mamabukizi ngozi ya juu ya gololi (Viral Keratoconjunctivitis).
  • Jicho kavu.
  • Jeraha la jicho.
  • Ugonjwa wa Glakoma (Glaucoma).

Mambukizi ya kirusi kwenye ngozi ya juu ya gololi ya jicho yajulikanayo kitaalamu "Viral Keratoconjunctivitis"

Haya ni moja ya maambukizi ambayo hulipuka sana kwenye jamii zetu, Mambukizi ya kirusi kwenye ngozi ya juu ya gololi ya jicho yajulikanayo kitaalamu "Viral Keratoconjunctivitis", ni maambukizi yanayosambaa kwa kasi kubwa. Hakuna tiba maalumu kwa ugonjwa huu na hata bila tiba, dalili huisha zenyewe ndani ya wiki mbili. Usafi ni jambo muhimu kuzuia maambukizi haya kusambaa kwa watu wengine.  Mlipuko huu husababishwa na Kirusi kijulikanacho kwa jina la Adenovirus kwa asilimia zaidi ya 80%.

Dalili huonekana kuanzia siku 5 hadi 14 baada ya kupata vimelea vya maambukizi. Aidha, mara chache inaweza kuchukua muda mrefu zaidi. Pia, mtu huchukua siku 1 hadi 2 mpaka kuanza kuonesha dalili na anaweza kuendelea kuambukiza takriban wiki mbili baada ya dalili kuanza kuonekana.

Hadi sasa hakuna tiba maalumu kwa maambukizi ya ugonjwa huu, na dalili huisha kwa muda wa wiki 2, wakati mwingine zinaweza kuendelea kwa wiki hadi 6. Wagonjwa wanashauriwa kufika kwenye kituo cha kutolea huduma za afya kwa ajili ya kupimwa na kupatiwa dawa za kupunguza madhara kulingana na ishara zitakazoonwa na Daktari.

Maambukizi haya husambazwa kwa njia zifuatazo;

  • Kugusa machozi au matongotongo kutoka kwenye macho ya mtu mwenye maambukizi.
  • Kugusana mikono na mtu mwenye maambukizi halafu ukajishika machoni. 

Macho Mekundu Yanaonekanaje na Kujisikiaje?

Wakati mwingine, jicho lako linaweza kuwa jekundu mahali ambapo palipaswa kuwa kweupe. Hii inaweza kutokea pindi vimishipa vya damu vilivyopo ndani ya macho yako vimevimba kuliosababishwa na kukereketa kwa jicho. Pia, inawezekana kabisa kuwa vimishipa vidogo vidogo vimepasuka.

Ikiwa jicho lako limekuwa jekundu kutokana na jeraha, basi inawezekana kuwa jicho limefungua zaidi (dilate) vimishipa vya damu katika jicho lako ili kuruhusu damu zaidi kufika kwenye eneo hilo kwa ajili ya kuharakisha uponyaji kwani damu ndiyo nyezo inayotumika kwenye uponyaji ndani ya mwili wa binadamu. ufungukaji mkubwa wa vimishipa hivi ndiyo inayosababisha macho kuwa mekundu.

Kulingana na hali inavyoendelea, macho yako mekundu yanaweza kujisikia:

  • Halina shida yoyote, kwa wengi wenye hali hii hawawezi kujua kama wana jicho jekundu mpaka wajiangalie au waambiwe na watu wengine.
  • Kuwasha au kuwa na kero, mara nyingi kwa wale walipata maambukizi (infection).

Jinsi ya kujisaidia

Kumbuka kuwa, kuna aina nyingi sana za macho mekundu, baadhi yake unaweza kujitibia wewe mwenyewe nyumbani na nyingine utajitaji msaada wa haraka wa daktari.

  • Pata mapumziko ya kutosha.
  • Weka kitambaa kizito juu ya macho yaliyofungwa.
  • Fanyia massage ngozi ya juu ya jicho (eyelid)
  • Kwa utaratibu kabisa safisha ngozi ya jicho (eyelid) kwa kutumia maji safi.
  • Unaweza kuweka matone ya dawa za kawaida (OTC).
  • Wakati mwingine, mtaalam wa huduma ya macho anaweza kupendekeza na kutoa dawa za viua vijasumu (antibiotics), matone maalum ya macho, au dawa za kunywa.

Ni nini hatari au madhara yanayowezekana ikiwa macho mekundu hayatibiwi?

Kwa mara nyingi, macho mekundu si hatari na inaweza hata isiwe na haja ya matibabu. Hata hivyo, kuna hali zinaweza kuwa na athari kubwa zaidi na zitakuladhimu upate matibabu ya kina.

  • Ikiwa umekaa na jicho jekundu kwa zaidi ya siku moja au mbili, au ikiwa tatizo hili limempata mtoto mdogo, basi unashauriwa uwasiliane na mtoa huduma za afya kwa uangalizi zaidi.
  • Pia, unatakiwa kuwasiliana na mtoa huduma pindi unaposikia maumivu au jicho linatoa matongotongo au uchafu wowote.
  • Endapo jicho lako kuwa jekundu ni matokeo ya athari kubwa kwenye jicho, endapo utakaa nalo bila ya matibabu linaweza kupelekea matatizo makubwa ikiwemo kupoteza uwezo wa kuona.

Jinsi ya kuepuka macho mekundu.

Si rahisi kuepuka kila macho mekundu, lakini unaweza kupunguza uwezekano wa kupata macho mekundu kwa kufuata ushauri ufuatao;

  • Usipendelee kusugua macho kwa kutumia mkono. Uchafu na vijidudu (germs) vilivyopo kwenye mikono yako vinaweza kusababisha madhara makubwa zaidi ya jicho kuwa jekundu au kukereketa (irritation).
  • Kama unatumia lenzi za ndani ya macho, hakikisha ni safi na usiweke kupitiliza muda ulioshauriwa.
  • Kwa wadada, tumia njia sahihi kuondoa urembo (make up) na hakikisha macho yako yanabaki masafi.
  • Hakikisha unapata muda wa kupumzika kila utumiapo kompyuta. Usitumie kwa muda mrefu bila kupata mapumziko.
  • Epuka vitu vinavyoweza kupelekea jicho kukereketa kama vumbi,moshi nk.
  • Hakikisha unajenga desturi ya kunawa mikono kwa maji safi na yanayotiririka kwa sabuni mara kwa mara kuzuia kupata maambukizi.
  • Onana na daktari pindi unapoona unapata macho mekundu mara kwa mara au umepata macho mekundu yasiyoisha.
  • Usichangie vipodozi na vitu vingine unavyotumia kama vile taulo za karatasi au nguo au dawa za macho.
  • Funika mdogo na pua wakati wa kukohoa au kupiga chafya ili kuzuia kuambukiza wengine.

Dalili za hatari

Ingawa macho mekundu huisha yenyewe baada ya muda, ila kuna wakati, macho mekundu ni ishara ya ugonjwa mkubwa.Wasiliana na daktari pindi unapoona;

  • Jicho linauma.
  • Umeanza kuwa na uono hafifu.
  • Macho yanakuwa yanaogopa mwanga kupitiliza (extra sensitive to light).
  • Una dalili zaidi ya wiki na zimekuwa zikiendelea kuwa mbaya.
  • Jicho limekuwa likitoa matongotongo yanayoganda kwenye kope.
  • Umepata homa au maumivu yanayoambatana na kujisikia vibaya.

Hakikisha unaenda hospitari haraka iwezekanavyo pindi unapoona moja ya dalili hizi;

  • Jicho linauma kupitiliza.
  • Unaogopa mwanga kupitiliza.
  • Jicho limevimba.
  • Unaona ukungu. 

Neno kutoka TanzMED

Kimsingi, karibu kila mtu kwa nyakati tofauti amewahi kupata changamoto ya macho mekundu. Kwa wengi wetu, macho mekundu haijawahi kuwa ni tatizo kubwa. Maranyingi husababishwa na mkereketo wa jicho na huondoka pindi mkereketo unapoisha wenyewe. Lakini, kuna wakati kwa baadhi ya hali utatakiwa kwenda kuonana na daktari kwa vipimo zaidi. Hakikisha unawahi hospitali pindi unapoona maumivu ya jicho au changamoto kwenye uono (vision). Ni maamuzi ya busara kupata ushauri wa daktari pindi unapokuwa na changamoto ambayo hauna uhakika nayo. TanzMED inakuwezesha kuweka miadi na kuongea na daktari moja kwa moja kwa njia ya mtandao. Pakua TanzMED App na uweke miadi leo.

 

Baadhi ya vifungu vimekopiwa kutoka vipeperushi vya Elimu ya Afya kwa uma  https://elimuyaafya.moh.go.tz/

Tatizo la kunyonyoka nywele hujulikana kitaalamu kama alopecia (tamka ‘’ alopesia’’). Hali hii ya kunyonyoka nywele husabababishwa na mfumo wa kinga ya mwili kushambulia mwili wa mtu husika (autoimmune disorder).

Kwenye alopecia, mfumo wa kinga ya mwili hushambulia mizizi ya nywele (hair follicles) na hivyo kusababisha kunyonyoka kwa nywele.

Wingi wa kunyonyoka nywele hutofautiana kati ya mtu mmoja na mwingine.Kwa baadhi ya watu, nywele hunyonyoka sehemu ndogo na kusababisha mabaka mabaka madogo ambayo mwanzoni sio rahisi mtu kugundua.Baadae mabaka haya huungana na kuwa sehemu moja kubwa iliyonyonyoka nywele na hatimaye mtu anaweza kugundua.

Kwa wengine, nywele hunyonyoka kwa wingi sana. Baadhi ya wagonjwa wameota  nywele baada ya awali kunyonyoka na kisha nywele hizo hunyonyoka tena. Mara chache hutokea kwa mgonjwa alienyonyoka nywele kuota tena nywele hizo kwa maisha yake yote.

Alopecia haina uhusiano wa umri wala jinsia ya mtu.Kwa hiyo, mtu yoyote anaweza kupata hali hii.

Kwa kawaida, meno ya mtoto ya utotoni (meno ya awali) huanza kutoka kuanzia miaka 6. Kwa baadhi ya watoto, huweza kuchelewa kuanza kutoka meno ya utotoni hadi wanapoanza mwaka wA 7.

Meno ya kwanza yanayoanza kutoka ni yale mawili ya chini ya kati (lower central incisors) na hufuatiwa na yale ya juu ya kati (upper central incisors) (. Baada ya hapo, hufuatiwa na meno ya kutafunia ya kwanza na ya pili.

Kwa kawaida, meno ya ya awali hukaa bila kutoka mpaka pale meno ya kudumu yanapotaka kuanza kuchomoza, hivyo hulisukuma jino la utoto na kusababisha kutoka. Endapo mtoto atatoka meno mapema au jino litatoka kwa sababu ya ajali au kuoza, basi jino la kudumu litaziba pengo hilo baada ya muda kufika. Hii inaweza kusababisha meno kutokuwa na mpangilio mzuri kwakuwa wakati linachomoza kulikuwa na meno mengine ya utotoni, hivyo unashauri kuwasiliana na daktari wa kinywa na meno kwa ushauri zaidi.

Pale mtoto anapoanza kutoka meno, tafadhali zingatia kanuni bora za Afya ya kinywa na meno kama ;

  • Kuhakikisha anasubua meno angalau mara mbili kwa siku. Mkazanie kwa sababu umakini unahitajika.
  • Msaidie mtoto kusugua meno kila siku
  • Hakikisha anakula chakula bora na kupunguza matumizi ya vyakula vitamu
  • Weka miadi na daktari wa kinywa nameno

Kwa mazingatio haya, utaweza kuhakikisha afya bora ya kinywa na meno ya mtoto wako. Pia, unaweza kusoma makala zaidi juu ya Afya ya kinywa na meno wakati wa makuzi ya mtoto

Afya bora ya kinywa na meno kwa mtoto ni muhimu sana na ina uhususiano wa moja kwa moja na afya yake kwa ujumla. Humuepusha mtoto kupata maumivu, uwezekano wa uambukizo, kumfanya aweze kutafuna vizuri ili kupata virutubisho muhimu kwa ajili ya kujenga kinga dhidi ya magonjwa, na kusaidia ukuaji. Afya nzuri ya kinywa na meno pia itamfanya mtoto aweze kuhudhuria masomo ipasavyo na hivyo kupata matokeo mazuri.

Umuhimu wa meno ya utoto

Wazazi /walezi wengi hujiuliza kwanini wahangaike kutunza meno ya utoto ambayo yanatarajiwa kung’oka na kuota ya ukubwa. Meno ya utoto ni muhimu kutokana na sababu zifuatazo:
Humsadia mtoto kutafuna na hivyo kumwezesha kupata virutubisho muhimu
Hutunza nafasi kwa ajili ya meno ya ukubwa
Hali ya afya ya meno ya utoto huathiri hali ya afya ya meno ya ukubwani
Husadia uumbaji wa maneno (kuongea)

Kama mzazi / mlezi unatakiwa kuwa mstari wa mbele kutunza meno ya mtoto wako kwani, watoto hupenda kujifunza kutokana na mfano wa wazazi.

Zifuatazo ni dondoo muhimu kwa wazazi/walezi kwa ajili ya kutunza afya bora ya mtoto:

Umri wa kuzaliwa mpaka miezi 6

  • Mnyonyeshe mtoto maziwa ya mama pekee hadi umri wa miezi sita.
  • Maziwa ya mama ni muhimu sana kwa ukuaji na kinga dhidi ya magonjwa.

Umri wa miezi 7 hadi miezi 18

  • Usimlaze mtoto akiwa na chuchu ya maziwa au chuchu ya mama mdomoni ili kuzuia ugonjwa wa kuoza kwa meno (rampant caries)
  • Mpatie mtoto maji badala ya juisi akiwa na kiu.
  • Iwapo utampa mtoto juisi ya boksi unashauriwa kuongeza kiwango cha maji sawa na kile cha juisi ili kupunguza kiasi cha sukari kilichomo ndani ya juisi.
  • Ukitengeneza juisi nyumbani kwa ajili ya mtoto, jiepushe kuiongezea sukari.
  • Jino la kwanza litakapoota, anza kusafisha kinywa cha mtoto kutumia kitambaa laini kilicholoweshwa kwenye maji safi au mswaki laini bila dawa.
  • Panga miadi ya kwanza ya kumwona daktari wa meno (first appointment) wakati mwanao hana maumivu au shida yoyote ili kujenga mahusiano mazuri kati ya mtoto na daktari

Umri wa miezi 18 hadi miaka 6

  • Dhibiti ulaji wa vyakula vyenye sukari na zingatia ulaji wa vyakula vinavyojenga afya ya mtoto kama matunda, mboga mboga, karanga, maziwa na samaki.
  • Safisha meno ya mtoto kutumia maji safi na mswaki laini na dawa ya meno (zingatia kiwango cha dawa: kiasi cha mbegu ya kunde) asubuhi na jioni kila siku.
  • Mtoto asukutue mdomoni ili kupunguza kiwango cha dawa itakayobaki.
  • Chunguza mara kwa mara meno ya mtoto ili kugundua dalili za mwanzo za ugonjwa wa kuoza kwa meno (rangi kuwa nyeupe au kahawia zaidi katika eneo husika baada ya kukausha) na pia matatizo mengine kama uvimbe, vijipu au kutoka damu kwenye fizi.
  • Mpeleke mtoto kwa daktari wa meno angalau mara moja kwa mwaka na mara unapogundua tatizo lolote kinywani mwake.

Umri wa miaka 6 hadi 12

  • Msimamie mtoto kusafisha kinywa na meno mara mbili kwa siku.
  • Mtoto ateme dawa itakayobaki ila asisukutue na maji baada ya kupiga mswaki.
  • Mjengee mtoto tabia ya kusukutua na maji kila baada ya kula vyakula vyenye sukari kama keki, chokoleti au juisi.
  • Chunguza mara kwa mara meno ya mtoto ili kugundua dalili za mwanzo za ugonjwa wa kuoza kwa meno na matatizo mengine kinywani.
  • Mpeleke mtoto kwa daktari wa meno angalau mara moja kwa mwaka na mara unapogundua tatizo lolote kinywani mwake.

Umri wa miaka 12 na zaidi

  • Mtoto anaweza kuanza kusafisha kinywa na meno bila ya usimamizi.
  • Dhibiti ulaji wa vyakula vyenye sukari na zingatia ulaji wa vyakula vinavyojenga afya ya mtoto kama matunda, mboga mboga, karanga, maziwa na samaki.
  • Mpeleke mtoto kwa daktari wa meno angalau mara moja kwa mwaka na mara unapogundua tatizo lolote kinywani mwake.

CREDIT: Muhimbili University of Health and Allied Sciences (MUHAS)

Assalamu’alaikum Warahmutullahi Wabarakatuh. Natumai mu wazima wa afya na mnaendelea vyema na majukumu ya kila siku.

Waumini wa dini ya Kiislam duniani kote wameingia katika mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani. Hivyo,katika muendelezo wa makala zinazohusu kisukari, tunaoenda tujikumbushe au tujifunze mambo machache ya kufanya kabla, wakati na baada ya kipindi takatifu cha mfungo wa Ramadhani.

Tukiwa tuna amini kuwa watu wengi wanaoishi na tatizo la Kisukari hasa aina ya pili ya kisukari wanatamani sana kufunga Ramadhani katika kutimiza moja ya nguzo za imani ya dini ya Kiislam, na kwa imani Funga ni dawa kiroho na kimwili pia.

Jambo la kwanza kwa mtu mwenye kisukari ni kujiweka tayari kwa funga miezi mitatu au minne kabla, kuitayarisha akili na nafsi,hii itakusaidia kuwa mwangalifu sana katika ulaji wako na mfumo mzima wa ulaji.

Kufanya kipimo cha hba1c ni muhimu kwa sababu inaonesha kiwango cha sukari miezi mitatu na hii inakufanya ujue kama utaweza kufunga ramadhan bila kuwa tatizo lolote au hutaweza kufunga. Kupima sukari kabla na baada ya kula kabla ya mfungo wa ramadhani pia ni muhimu,kabla ya kula ni lazima sukari iwe chini ya sita(6) na masaa mawili baada ya kula iwe chini ya nane (8) na kama majibu yatakuwa hivyo kila mara hii itakuonesha kuwa unaweza kufunga bila tatizo.

Jambo la pili ni kuhakikisha unapata ushauri kutoka kwaa daktari wako wa kisukari, Shauriana naye, usiamue kufunga Ramadhani bila ya kushauriana na daktari wako, hii ni muhimu kwa sababu anaweza kukupa ushauri kulingana na kiwango chako cha sukari kwa miezi mitatu nyuma.(hba1c) na kipimo cha sukari cha kila siku unachopima kabla na masaa mawili baada ya kula.

Wakati wa mfungo ni lazima mtu mwenye kisukari atambue kuwa anaweza kufunga baada ya ushauri na ruhusa dakitari wake,na endapo akifunga, ni lazima pia awe anapima kiwango cha sukar kabla ya kuanza ,mfungo,kwa mfano, kabla ya kula daku ni lazima apima,hii itamsaidia kujua kama ataweza kufunga kwa siku hiyo ama Lah, kama akipima na kiwango cha sukari kikiwa sita (6) au saba(7) anaweza kufunga lakini indapo akipima akikuta kwango cha sukar iki chini ya sita (6), labda ni tano(5) au nne (4) hatoweza kufunga kwa sababu moja ya kisababisho cha sukari kushuka ni kukaa bila kula kwa muda mrefu.

Kutokupata choo au kuhisi kwenda kujisaidia haja kubwa na kutofanikiwa kutoa choo au mtu kupata choo chini ya mara tatu kwa wiki hujulikana kitaalamu kama constipation.Mtu mwenye tatizo hili la kufunga choo hupata choo kigumu,kikavu na chenye kupita kwa taabu kwenye njia ya haja kubwa

Tafiti nyingi zinaonyesha kwamba angalau kila mtu katika maisha yake huwa anapata tatizo hili la kufunga choo. Kufunga choo ni tatizo ambalo watu wengi  bado huhisi ni jambo la aibu sana hata kulizungumzia na hubaki na tatizo kwa muda mrefu  mpaka pale wanapopata madhara ya kiafya ndio hutafuta msaada wa kitabibu.

Dalili  zifuatazo zinaweza kutumika kuelezea tatizo la choo kufunga;

  1. Kupata choo kigumu na kinachoambatana na maumivu makali wakati wa kwenda haja kubwa
  2. Kutokupata choo kwa muda mrefu (infrequent bowel movements)
  3. Mtu kuhisi kama hajamaliza haja kubwa licha ya kupata choo

Tafiti nyingi zilizowahi kufayika zinaonyesha kwamba takribani asilimia 16 (16%) ya watu wazima hupata tatizo hili la kufunga choo,waathirika wengi wakiwa ni watu wenye umri kati  ya 60-110 (asilimia 35%).

Kwa nini wazee hupata tatizo hili la kufunga choo?

Sababu zifuatazo huchangia wazee kutokupata choo au kufunga choo;

  1. Hali ya uzee husababisha mmeng’enyo wa chakula kufanyika taratibu (slow metabolism) 
  2. Ukosefu wa lishe bora
  3. Kutokunywa maji ya kutosha
  4. Kutofanya mazoezi
  5. Magonjwa ya uzee kama pelvic floor prolapse na utumiaji wa dawa aina ya antacids na dawa za kupunguza maumivu
  6. Pia uzee husababisha meno kung’oka hivyo wazee huchagua vyakula laini na vyenye ufumwele (fiber) kidogo

Wanawake wajawazito ni miongoni mwa watu wanaopata tatizo hili la kufunga choo mara kwa mara.

Visababishi vya choo kufunga (constipation) ni kama ifuatavyo;

  1. Kutokula mlo wenye ufumwele (fiber) wa kutosha
  2. Kutokunywa maji ya kutosha
  3. Kutumia sana dawa za kulainisha choo
  4. Kutokufanya mazoezi au
  5. kuishi maisha ya unyongovu (stressful life)
  6. Madawa kama aspirin (NSAID), morphine, dawa za presha(thiazides, verapamil, furosemide), dawa za sonono (antidpressants), madawa ya saratani n.k
  7. Magonjwa ya  mfumo wa mmengenyo wa chakula  au  vichocheo vya mwili (hormonal disorders) kama hypothyroidism
  8. Ujauzito- Mama mjamzito yupo kwenye hatari zaidi ya kupata choo kigumu au constipation hasa katika miezi ya mwisho ya ujauzaito wake kwa sababu ya kuongezeka kwa vichocheo mwili aina ya sex hormones, kupungua kwa mmeng’enyo kwenye tumbo na kuchelewa kwa tumbo kupitisha chakula (delayed interstinal emptying)
  9. Magonjwa ya tumbo kama colorectal dysfunction, diverticulitis, irritable bowel syndrome, saratani za matumbo hasa utumbo mkubwa
  10. Chronic Idiopathic constipation- Sababu zisizojulikana

Kama ambavyo tumejifunza sababu na makundi wa watu ambao wapo kwenye hatari zaidi. Tatizo hili linaweza kumpata mtu yoyote wa rika lolote hata watoto wachanga. Hivyo fuatilia makala zetu zijazo ili kujua uchunguzi,matibabu na jinsi ya kuepukana na tatizo hili la kufunga choo.Kama tayari una tatizo hili  tafadhali fika kituo cha afya kilichokaribu nawe kwa ajili ya uchunguzi, matibabu na ushauri wa kitaalamu.

Watoto wanapozaliwa, tayari wanakuwa na meno ambayo  yamefunikiwa kwa fizi. Meno huanza kutoka kwa mara ya kwanza mtoto akiwa na umri wa miezi sita ( 6) japo umri huu unaweza tofautiana kutoka kwa mtoto mmoja hadi mwingine.

Meno mawili ya kwanza yanayoonekana mara nyingi ni yale ya kinywa cha chini katikati yakifuatiwa na ya kinywa cha  juu katikati. Watoto wengi hufikisha meno yote 20 ya kwanza wakiwa na umri wa miaka 3.

Baadhi ya watoto hawaoti meno kama watoto wengine, yao huchelewa au kutokuota kabisa. Hii husababishwa na vitu mbalimbali. Kama mtoto wako hajaota jino hata moja hadi umri wa miezi 18 basi ni muhimu umpeleke hospitali aonane na daktari wa kinywa na meno kwa ajili ya uchunguzi zaidi.

Sababu za meno kuchelewa kuota

Zipo sababu nyingi za meno kuchelewa kuota. Wakati mwingine tatizo la meno kuchelewa kuota huwa ni tatizo la kwenye familia  hivyo linaweza kurithishwa kwa vizazi vinavyokuja. Mzazi pia ujiulize kama meno yako yalichelewa kuota, kama ni ndio basi tambua kwamba hata ya mwanao yataota tu japo kwa kuchelewa.

Sababu zinazochangia meno kuchelewa kuota kwa mtoto ni kama zifuatazo;

  1. Utapia mlo na upungufu wa madini na vitamini mwilini- Watoto wenye utapia mlo meno huchelewa kuota kwa sababu ya kukosa virutubisho muhimu vya ukuaji wa meno. Aidha madini ya calcium na vitamini  D ni muhimu sana katika ukuaji wa meno. Hivyo mtoto akipungukiwa na virutubisho hivi meno huchelewa kuota.
  2. Ugonjwa wa jeni unaofahamika kama Down Syndrome- Huu ni miongoni mwa mgonjwa wa kuzaliwa nayo (congenital).Ugonjwa huu unatokana na hitilafu kwenye kinasaba cha 21 (chromosome 21). Ugonjwa huu huambatana na tatizo la meno kuchelewa kuota.
  3. Magojwa ya yatokanayo na hitalifu kwenye chromosomes (chromosome anomalies)
  4. Mtoto kuzaliwa njiti-Kuzaliwa njiti au na kuzaliwa  na uzito mdogo kupita kawaida (chini ya 1.5kg) kunahusishwa na kuchelewa kuota kwa meno kwa mtoto. Watoto hawa wanaweza kuwa na matatizo ya meno yenyewe.
  5. Magonjwa kama Amelogenesis na Regional Odontodysplasia

Amelogenesis ni ugonjwa wa kuzaliwa nao (congenital disease) ambapo mtoto anazaliwa na hitilafu kwenye kwenye protini zinazotengeneza enameli (nyeupe ngumu ya jino) hii hupelekea kuwa  na enameli isiyo ya kawaida na meno yanakuwa ya njano. Hii huambatana na meno kuchelewa kuota.

Regional odondodysplasia ni hitilafu katika ukuaji inayohusisha mesodermal na ectoderm (hizi ndizo zinazotengeneza jino la ndani na nje) za meno. Ugonjwa huu huwa unaathiri sehemu moja tu ya kinywa (localized). Huu sio ugonjwa wa kurithi.

Kwanini uwe na wasiwasi kuhusu meno ya mtoto yanapochelewa kuota?

Watoto ambao hawajaota meno hadi umri wa miezi 18 wapelekwe kumuona daktari wa meno. Watoto wengi huwa na meno manne wakifikia umri wa miezi 12 na huwa na yote 20 wakiwa na miezi 27.

Kama meno ya mtoto wako hayajaota kwa wakati inaweza kuwa ni ishara ya ugonjwa  au upungufu wa madini  au vitamini fulani mwilini.

Je, meno kuchelewa kutoa ni dalili mbaya?

Meno kuchelewa kuota sio jambo kubwa sana ila linaweza kuongeza uwezekano wa mtoto kupata matatizo ya meno ukubwani. Tafiti nyingi zinaonyesha kuwa watoto waliopata tatizo la meno kuchelewa kuota wana nafasi kubwa ya kuhitaji matibabu ya meno wakiwa na umri wa miaka 30.

Meno kuota kwa wakati kwa mtoto humsaidia kutafuna vizuri na husaidia meno ya pili kujipanga vizuri kwenye kinywa.

Meno yakichelewa kuota husababisha mtoto kukosa au kupata virutubisho vichache maana atakuwa hawezi kutafuna vizuri hivyo kupata shida ya kumeng’enya chakula.

Jinsi ya kutunza meno mapya ya mtoto wako

  1. Epuka vyakula na vinywaji vyenye sukari
  2. Safisha fizi kwa kutumia kutambaa kisafi mara mbili kwa siku
  3. Epuka kumlaza mtoto na chupa ya maziwa kitandani
  4. Kumbuka kuswaki na kusafisha meno yaliyoota

Utaanza kutumia dawa ya meno pindi mtoto akifikisha miaka 2.

 

Naweza Kunywa Pombe kama nina Ugonjwa wa kisukari?

Wagonjwa wengi wa kisukari wameniuliza kuhusu swali hili.Aghalabu, hata wengine ambao wanasoma makala hii pia watakuwa na shauku ya kutaka kujua kama kweli wanaweza kunywa pombe ilihali wanaugua ugonjwa wa kisukari bila kupata madhara yoyote ya afya.Swali hili ni la msingi sana hasa unapokuwa kwenye matibabu ya ugonjwa wa kisukari.

Ugonjwa wa kisukari ni moja kati ya magonjwa mengi yasiyoambukiza (non-communicable diseases) ambayo yanongezeka kwa kasi na kusababisha vifo na ulemavu.

Taarifa ya International Diabetes Federation imesema watu millioni 463 duniani wanaishi na kisukari na millioni 19 ya hao wapo bara la Afrika pekee.

Shirika hili katika taarifa yake ya mwaka 2020 limesema kwamba uwezekano wa kupata ugonjwa wa kisukari  nchini Tanzania ni kwa asilimia 3.7 huku idadi ya wagonjwa wa kisukari watu wazima imefika takribani watu 997,400.

Unywaji wa pombe uliopitiliza kwa watu wenye kisukari husababisha madhara makubwa ikiwemo kuongeza hatari ya kupata shinikizo la damu, magonjwa ya moyo,macho na kuharibika kwa mishipa ya fahamu.

Aidha Pombe au vileo vingi vina idadi kubwa ya wanga na sukari hivyo husababisha kupanda kwa haraka kwa sukari kwenye damu. Pia vina kalori nyingi hii upelekea kuwepo hatari ya kuongezeka uzito uliopitiliza ambapo hupunguza unyeti (sensitivity) na utolewaji wa kichocheo aina ya insulin  mwishowe husababisha ugumu wa kudhibiti sukari yako mwilini.

Sasa je naweza kunywa pombe kama ni ugonjwa wa kisukari?

jibu ni NDIO japo inabidi ujenge tabia ya kuwa na tahadhari pindi unapokunywa pombe.

Utatumia pombe pale tu ambapo sukari yako imedhibitiwa vizuri na kwa hali yoyote epuka unywaji pombe kupitiliza.

Najua kuna swali unaliwaza kuwa nisinywe kupitiliza unaamanisha nini?

Hili ni swali zuri na la msingi.Kulingana na shirika la ugonjwa wa kisukari la marekani (American Dabetes Association), imetoa vipimo vifuatavyo vya unywaji wa pombe kwa watu wenye kisukari.

Mwanamke mwenye kisukari asinywe zaidi ya chupa moja ya bia  sawa na 350mls, au 147 mls za wine na 44 mls za pombe kali kwa siku.

Kwa mwanamume, asinywe zaidi ya bia mbili sawa na 700mls, au 294 mls za wine au  88 mls za pombe kali.

USHAURI

Kabla ya kunywa pombe hebu jiulize masawali yafuatayo;

Je sukari yangu imedhibitiwa?

Je daktari wangu anakubali nitumie pombe au kilevi cha aina yoyote ile?

Je najua jinsi pombe inaweza kuniathiri mimi pamoja na sukari yangu?

Kama majibu yako yote ni ndio basi waweza kunywa pombe. Ila kumbuka pombe pia husababisha sukari kushuka. Ni vizuri kufahamu kiwango cha sukari yako mwilini kabla, wakati na baada ya kunywa pombe angalau kwa kipindi cha masaa 12.

Usikose kutembelea TanZMED kwa makala zaidi za afya kwa lugha ya kiswahili.

 

U-hali gani msomaji wetu wa makala zetu za kisukari, karibuni tena katika makala nyingine ya kisukari, leo tunaangalia kwa ufupi tu  siku na mwezi ya kisukari duniani, na pia tutadadavua kwanini kuna mwezi wa kisukari na malengo yake hasa ni nini na pia kwa kuwa sio wote wananojua kuhusu mwezi wa kisukari, karibuni.

Kila mwaka ifikapo mwezi wa November ni siku ya kisukari duniani, mwezi huu wote umetengwa kuwa ni mwezi maalum kwa kueleza elimu na uelewa juu ya tatizo hili ya kisukari, pia kuboresha matibabu ya maradhi yanayotokana na kisukari, maadhimisho wake ni tarehe kumi na nne (14) ya mwezi November.

Kwanini iwe mwezi wa November, tarehe kumi na nne(14)? Inawezekana unajiuliza hili swali kila mara na kila ifikapo mwezi November, shirika ya afya duniani na shirikisho ya kimataifa la kisukari yalikutana na kukubalia kutenga tarehe kumi na nne (14)  November  kuwa ni mwezi wa kisukari duniani kwa sababu ni mwezi ambayo  ndugu Frederick Banting ambaye ni mgunduzi wa kichocheo kiitwacho INSULIN ambacho hutumika kama dawa kwa wengi aina ya kwanza ya kisukari alizaliwa. Katika kumuenzi mgunduzi huyu mashirika haya mawili wakaona ni busara kutenga mwezi huu na tarehe hii kuwa ni siku ya kisukari duniani kote.

 

Ni moja kati ya magonjwa sugu yahusuyo mfumo wa kinga ya mwili kushambulia mwili wako na huwa na mtindo wa kuwa na kipindi cha kupata nafuu na kuwa kama umepona na kipindi cha kushambulia na kuwa hoi.

Huathiri zaidi wanawake, hadi asilimia 90 ya wagonjwa huwa wanawake. Na mara nyingi huanza kwenye umri wa uwezo wa ubebaji mimba.

Vipele ambavyo hutokea kipindi cha jua huathiri Ngozi (picha kwa hisani ya Dr. Erik Stratman, Marshfield Clinic)

 

Dalili

Ugonjwa huu huathiri karibu kila kiungo kwenye mwili

Dalili 3 kubwa ambazo hutokea ni:

  • Homa
  • Maumivu ya viungo
  • Vipele

Picha  inaonyesha vipele usoni hasa kwenye mashavu na pua kitalaamu Butterfly rash (Picha Kwa hisani ya affordablehealthinsurance.org)

Dalili nyingine ni:

  • Uchovu
  • Kupungua uzito
  • Figo kushindwa kufanya kazi vizuri
  • Dege dege
  • Maji kujaa kwenye mapafu, shinikizo la mapafu
  • Maumivu ya tumbo, kichefu chefu
  • Upungu wa damu, upungufu wa chembe chembe sahani

Vipimo:

Vipimo vya uhakika kuthibitisha ugonjwa huu ni;

  • Kipimo cha vinasaba kitaalamu double strand DNA antibodies na
  • Kingine kitaalamu Antinuclear antibody (ANA)

Vipimo vingine ni:

  • CBC- kujua wingi wa damu, na chembe chembe sahani
  • Kipimo cha damu kujua uwezo wa figo kufanya kazi (RFT)
  • Kipimo cha damu cha kujua uwezo wa ini kufanya kazi (LFT)

Matibabu:

Ugonjwa huu hauna tiba ziaidi ni kutibu dalili na kupunguza makali yake

Moja kati ya dawa ambazo hutumika ni:

  • Dawa za malaria - ambazo husaidia kupunguza makali yak inga kuushambulia mwili bila kuishusha kinga ya mwili. Dawa hizi pia huzuia na kutibu vipele ambavyo husababishwa na ugonjwa huu. Mfano wa dawa hizi ni: Hydroxychloroquine sulfate (Plaquenil)
  • Dawa za maumivu- ambazo husaidia kupunguza homa, maumivu ya kichwa na maumivu ya viungo. Mfano wa dawa hizi ni: Ibuprofen (advil, motrin)
  • Dawa za kupunguza kinga ya mwili- dawa hizi hupunguza kinga ya mwili hivyo kupunguza makali ya kushambulia mwili hivyo kupunguza makali ya ugonjwa, mfano wa dawa hizi ni: cyclophosphamide na methotrexate
  • Na kutibu kila dalili zitakazo jitokeza ipasavyo

 

 

Ukurasa 1 ya 11