Image
×

Onyo

JUser: :_load: Haiwezi kupakia mtumiaji aliye na kitambulisho: 797

Moja ya matatizo yanayoathiri sana jamii kubwa ya watanzania hususani watoto ni ugonjwa wa sickle cell. Ugonjwa huu wa kinasaba huathiri hemoglobin, sehemu iliyo muhimu sana katika muundo na ufanisi wa chembe nyekundu za damu.

Kazi kuu ya hemoglobin katika chembe nyekundu za damu ni kubeba, kusafirisha na kusambaza wa hewa ya oksijeni katika mwilini.

Watu wenye ugonjwa huu, hupata mabadiliko ya vinasaba ambayo hutokea katika nafasi ya sita ya mnyororo wa beta globin (beta chain) katika hemoglobin ambapo kiasili cha valine ambacho ni mojawapo ya tindikali muhimu za amino (amino acid) huchukua nafasi ya kiasili cha glutamate na hivyo kubadili kabisa umbo la chembechembe nyekundu za damu na kuzifanya zishindwe kufanya kazi zake vile inavyopaswa.

Kuna aina mbali mbali za sickle cell, nazo ni HbSS, HbAS, HbSC, HbSD na HbSO. HbSS huwaathiri watu wengi zaidi wakati wenye HbAS huitwa carriers au sickle cell traits kwa vile ndiyo wanaobeba tatizo hili la kijenetekia na kueneza kwa wengine ingawa wao mara nyingi kama siyo zote hawaoneshi dalili zozote za ugonjwa huu.

Dalili za ugonjwa wa sickle cell ni zipi?

Dalili za ugonjwa wa sickle cell hutegemea sana na kiwango cha uathirikaji wa chembe nyekundu za damu.

Kiujumla dalili zinaweza kuwa ni zile zinazohusiana na upungufu wa chembe nyekundu za damu mwilini yaani anemia, unaotokana na kuharibika kwa chembe hizo. Hizi ni pamoja na

  • Kushindwa kupumua vizuri
  • Kizunguzungu
  • Maumivu ya kichwa
  • Ubaridi katika viganja na miguuni
  • Unjano katika macho na ngozi au jaundice
  • Weupe katika viganja, na eneo la macho liitwalo conjuctiva, ulimi na midomo
  • Maumivu ya tumbo
  • Homa
  • Maumivu ya viungo (joint pains)
  • Maumivu ya kifua
  • Damu katika mkojo (hematuria)

Tatizo hili la kujikojolea bila sababu yoyote ya msingi ni tatizo linaloathiri watu wengi sana na ambalo huleta usumbufu  na aibu kubwa kama litampata mtu. Tatizo hili huwakumba sana wanawake kuliko wanaume  na inakisiwa kuwa asilimia 35 ya watu walio na umri zaidi ya miaka 60 wana tatizo hili, kati ya hawa wanawake ni mara mbili ya wanaume wanaopata tatizo hili.

Hakuna uhusiano wowote wa tatizo hili na vitendo vya kujaamiiana kinyume cha maumbile au ngono kwa njia ya haja kubwa (anal sex) au ushoga (homosexuality).
 
Miongoni mwa sababu zinazochangia kutokea kwa tatizo hili ni
  • Jinsia – Hutokea zaidi kwa wanawake kuliko wanaume (stress incontinence), kutokana na ujauzito, kujifungua, wanawake ambao wameacha kupata hedhi (menopausal women) na maumbile ya kawaida ya mwanamke (normal  female anatomy), hata hivyo, urinary incontinence huwa zaidi kwa wanaume wenye matatizo ya kwenye tezi dume (prostate) kama saratani ya tezi dume,  uvimbe katika tezi dume (BPH) nk.
  • Umri  – Kutokana na kuongeza umri, muscle za kwenye kibofu cha mkojo na kwenye mrija wa kupitisha mkojo yaani urethra, zinaanza kuwa legevu (weak) na hivyo kusababisha mtu kushindwa kuzuia mkojo au kujikojolea. Hii haimanishi ya kwamba kila mtu ambaye ana umri mkubwa hupata tatizo hili, la hasha, linaweza kuonekana kwa baadhi tu ya watu wenye umri mkubwa. Mara nyingi huonekana kwa watoto wadogo au wachanga kutokana na kutokukomaa kwa viungo vyao (kibofu cha mkojo na mrija wa kupitisha mkojo)
  • Uzito uliopitiliza – Kuwa na uzito uliopitiliza (obesity) ni moja ya chanzo kinachochangia kutokea kwa tatizo hili kwani uzito huu huongeza shinikizo katika kibofu cha mkojo na kufanya muscle zinazozunguka kibofu hiki kuwa legevu na matokeo yake ni mtu kujikojolea pindi anapopiga chafya au kukohoa

Upungufu wa akili ni tatizo ambalo kwa ujumla hutokea kabla ya mtu kuwa mkubwa (adulthood) na huambatana na dalili za kupunguwa uwezo wa akili ya utambuzi na kutafakari (cognitive functions) pamoja na kushindwa kukua kwa tabia za kuendana na mazingira yanayomzunguka mtu (adaptive behavior). Pia kitaalamu, upungufu wa akili hujulikana kama mtu yoyote mwenye IQ (Intelligence Quotient) chini ya 70.

Upungufu wa akili ni hali ya kuwa na mapungufu katika ukuaji (development deficit) yanayoanza utotoni ambayo husababisha kupungua uwezo wa kusoma (intellect), kutafakari, utambuzi na kutoweza kuendana na majukumu ya kila siku ya maisha.

Ukubwa wa Tatizo (Epidemiology)

Upungufu wa akili ni tatizo kubwa sana duniani.Huathiri asilimia 1-2 ya watu wote duniani.Huonekana sana kwa wanaume kuliko wanawake (inakisiwa huonekana mara mbili zaidi kwa wanaume kuliko wanawake). Upungufu wa akili wa kati (mild mental retardation) huonekana sana kwa watu wa kipato cha chini lakini upungufu wa akili wa kiwango cha juu hutokea uwiano sawa katika jamii ya matabaka yote na huonekana sana katika umri kati ya miaka 10 hadi 14.

Upungufu wa akili sio ugonjwa (axis II disorder in DSM-IV) kutokana na dalili na viashiria vyake bali ni tatizo la mfumo wa utambuzi wa watu wenye kuhitaji huduma za kijamii na elimu maalum ili kuweza kumudu majukumu yao ya kila siku. Mara nyingi upungufu wa akili hutokea kabla ya mtu kufikisha umri wa miaka 18.

Tungependa kwa yoyote mwenye takwimu kutoka afrika mashariki za tatizo hili la upungufu wa akili kutoka katika hospitali za magonjwa ya akili za Butabika National Referral and Teaching Mental Hospital (Kampala, Uganda), Port Reitz District Hospital (Mombasa, Kenya), Mathare Mental Hospital (Nairobi, Kenya), Lutindi Mental Hospital (Tanga, Tanzania) na Mirembe Psychiatric Referral Hospital (Dodoma, Tanzania).

Tabia za Kuendana na Mazingira (Adaptive behavior) ni nini?

Utangulizi

Kibofu cha mkojo kinapatkana sehemu ya chini ya maeneo ya tumbo na ni kiungo ambacho kina uwazi/tundu ndani yake na kazi yake kubwa ni kukusanya na kuhifadhi mkojo unaotolewa na figo kabla ya kuutoa nje ya mwili wa binadamu. Kibofu cha mkojo kina kuta (layers) aina tatu za tishu ambazo ni;

1.Mucosa layer – Kuta ya ndani kabisa ambayo ndio inayokutana na mkojo wa binadamu. Kuta hii nayo inakuta nyingi sana za seli au chembechembe zinazojulikana kama transitional epithelium cells ambazo pia hupatikana kwenye sehemu ya mirija inayojulikana kama ureters, urethra na kwenye figo. Seli hizi zinazuia uvujaji wa mkojo kwenda kwenye sehemu nyengine ya mwili.

Ureter huingiza mkojo kutoka kwenye figo na urethra hutoa mkojo kutoka kwenye kibofu cha mkojo wakati wa kukojoa.

2.Lamina propia – Kuta ya katikati nyembamba sana kati ya kuta  hizi tatu na  ambayo mishipa ya damu na neva inapatikana hapa na ni muhimu sana  wakati wa kupanga makundi ya saratani ya kibofu cha mkojo wakati wa tiba.

3.Muscularis layer -  Kuta ya nje ambayo ndani yake kuna destrusor muscle na ndio kuta nene kati ya hizi tatu. Kazi yake kubwa ni kupumzisha kibofu cha mkojo ili mkojo uingie ndani na ukishajaa basi hukaza kibofu (contracts) na kufanya mkojo kutoka nje.

Nje ya hizi kuta tatu, kibofu cha mkojo kimezungukwa na  mafuta ambayo hukinga kibofu kutokana na mtikisiko wowote na kukitenganisha na viungo vengine. Kuna saratani aina tatu kutokana na kuta hizi tatu nilizotaja hapo juu za kibofu cha mkojo

Tatizo la kufunguka mlango wa kushoto wa moyo unaotenganisha chumba kidogo na kikubwa cha moyo na  kuzuia  kupita kwa damu ya kutosha kwenda kwenye mshipa mkubwa wa damu (Aorta) ambao huhusika kuzungusha damu ndani ya mwili hujulikana kama mitral stenosis

Visababishi

Tatizo hili la kufunguka mlango wa kushoto wa moyo unaotenganisha chumba kidogo na kikubwa husababishwa na;

  • Homa inayojulikana kama rheumatic fever
  • Mtu anaweza kuzaliwa na hali hii
  • Matibabu ya saratani za kifua kwa kutumia tiba ya mionzi
  • Mkusanyiko wa madini aina  calcium kwenye milango hiyo ya moyo

Kati ya hizi sababu hapo juu, inayosababisha kutokea kwa  tatizo hili kwa wakubwa ni homa ya rheumatic fever, ambayo hufuatia maambukizi ya vimelea vya bakteria aina ya  streptococci kwenye koo au ngozi ambayo hayakutibiwa kikamilifu

Tafiti iliyofanywa na Chama cha Kisukari Tanzania mwaka 1999, ilionesha kuwa maradhi yasiyo ya kuambukiza (maradhi ya moyo,figo,saratani, kisukari na mengineyo yasiyo ya kuambukiza) huchangia karibu asilimia 60 ya vifo vyote duniani na asilimia 43 ya ukubwa wa tatizo la maradhi hayo kote duniani.Maradhi haya yasiyo ya kuambukiza yanaongezeka na kukua kwa kasi hasa katika nchi zinazoendelea ikiwepo Tanzania. Tanzania inakisiwa kuwa ifikapo mwaka 2020 maradhi haya yatasababisha asilimia 73 ya vifo vyote duniani na ukubwa wa tatizo litaongezeka mpaka asilimia 60. (Tanzania Diabetes Association. 2013)

Kwa aina ya kwanza ya kisukari,ambayo hii huwapata watoto kwenye umri wa mwaka 1-25 inazidi kuongezeka katika nchi nyingi duniani,baadhi ya tafiti zilizowahi kufanywa zinaonesha katika watoto 79,000 ambayo wapo chini ya umri wa miaka 15 wapo katika hatari ya kupata tatizo la aina ya kwanza ya kisukari duniani kote,aina hii ya kwanza sio kama aina ya pili,aina ya ya kwanza,hasababishwi na mfumo wa maisha, au uzito uliopitiliza, na pia aina ya kwanza haiwezi kuzuilika tofauti na aina ya pili ya kisukari.inakadiriwa kuwa takriban 497,000 ya watoto wanaishi na aina ya kwanza ya kisukari duniani kote na pia nusu ya idadi hiyo ya watoto wanaishi katika mazingira magumu hasa kimatibabu na dawa.(International Diabetes Federation, IDF Diabetes Atlas.2014)

Watu takriban milioni 371 wamepata  kisukari kote duniani,ikiwa asilimia 80 ya idadi hiyo wanaishi katika nchi zenye uchumu wa kati na nchi masikini.katika tanzania, inasemekana kuwa katika watu 9 kwa kila watu 100 ya watanzania wenye umri wa miaka 25 na kuendelea wana tatizo la kisukari na pia katika idadi hiyo ya watu 9 ni wawili tu wanajijua kuwa wana tatizo la kisukari.(Tanzania Diabetes Association. 2013)

Namba, idadi na takwimu zinaonesha dhahiri shahiri ni kiasi gani kisukari ni tatizo kubwa endapo tu kama jamii haitapewa elimu ya kutosha kuhusu tatizo hili, jamii pia ni lazima ijue kwa upana na undani zaidi kuhusu chanzo,dalili na jinsi ya kuepuka na kuishi na kisukari.tatizo hili la kisukari mara nyingi napenda kusema sio ugonjwa ila inakuwa ni ugonjwa endapo tu mtu hatakuwa makini katika kudhibiti kiwango cha sukari.

 

 Shinikizo la damu ni moja ya tatizo linaloathiri watu wengi duniani.

Nini maana ya shinikizo la damu?

Ni msukumo wa damu ulioko juu kuliko inavyotakiwa kwa muda mrefu. Msukumo wa damu huitajika mwilini ili kusambaza chakula,oksijeni na kutoa uchafu.

Uanishaji wa shinikizo la damu

Uanishaji

Systolic BP

Diastolic BP

Kawaida (normal)

<120

<80

Prehypertension

120-139

80-89

Kali (mild hypertension)

140-159

90-99

Kali kiasi (moderate hypertension)

160-179

100-109

Kali sana (severe Hypertension)

≥180

≥110

Shinikizo la damu hupimwa kutumia kifaa kinachoitwa Sphygmomanometer

Shinikizo la damu husababishwa na nini?

Aina ya kwanza

Asilimia 90-95 sababu huwa hazijulikani na kitaalamu huitwa primary or essential hypertension. Ingawa vitu vifuatavyo vimehusishwa kupelekea kupata aina hii ya shinikizo la damu. Navyo ni:

  • Uvutaji sigara
  • Unene (visceral obesity)
  • Unywaji wa pombe
  • Upungufu wa madini ya potassium
  • Upungufu wa vitamin D
  • Kurithi
  • Umri mkubwa
  • Chumvi na madini ya sodium kwa ujumla
  • Ongezeko la kemikali kwenye figo (renin)
  • Kushindwa kufanyakazi kwa kichocheo kiitwacho insulin

Aina ya Pili

Asilimia 5 huwa na sababu dhahiri zinazopelekea kupata aina hii ya shinikizo la damu na huitwa kitaalamu secondary hypertension. Na sababu hizi ni:

  • Hali ya kukosa hewa usingizini (sleep Apnea)
  • Kasoro ya kuzaliwa nayo katika mshipa mkubwa wa damu (Coarctation of Aorta)
  • Saratani za figo (wilm’s tumor, renal cell carcinoma)
  • Saratani ya tezi iliyo juu ya figo (pheochromocytoma)
  • Ujauzito – wapo wakina mama wajawazito ambao hupata shinikizo la damu na huwa hatarini kupata kifafa cha mimba (eclampsia)
  • Magonjwa ya figo (renal artery stenosis, glomerulonephritis)

Dalili

Mara nyingi huwa hamna dalili zozote, na kama zikiwepo mgonjwa huwa na dalili zifuatazo

  • Uchovu
  • Maumivu ya kichwa
  • Kuhisi mapigo ya moyo kwenda haraka
  • Kichefuchefu
  • Kutapika
  • Damu kutoka puani
  • Kutoweza kuona vizuri (blurred vision)
  • Kusikia kelele masikioni
  • Na mara chache kuchanganyikiwa

Vipimo na uchunguzi

Huitaji kupima angalau mara tatu angalu wiki moja tofauti ilikuweza kusema mgonjwa ana shinikizo la damu kwa kutumia kifaa kinachoitwa kitaalamu Sphygmomanometer. Vipimo vingine ni:

  • Damu kuchunguza wingi wa lijamu mwilini (cholesterol), na pia vitu kama (BUN, na electrolytes)
  • Kipimo cha mkojo (Urinalysis)
  • Electrocardiogram (ECG)
  • Echocardiography
  • Ultrasound ya mafigo

Matibabu

Lengo ni kuzuia madhara ambayo yanaweza kuletwa na shinikizo la damu. Dawa zifuatazo hutumika kutibu shinikizo la damu: dawa jamii ya Alpha blockers, dawa jamii ya Angiotensin converting enzyme inhibitor (ACEI), dawa jamii ya Angiotensin receptor blocker (ARB), dawa jamii ya Beta blocker, dawa jamii ya Calcium channel blocker, dawa jamii ya Diuretics, dawa jamii ya Renin inhibitors na dawa jamii ya Vasodilators.

Madhara yanayoweza kuletwa na shinikizo la damu

  • Kiharusi
  • Moyo kushindwa kufanya kazi ( congestive heart failure)
  • Madhara katika mshipa mkubwa wa damu ambapo ukuta wa ndani huchanika na damu hukusanyika katika ukuta wa mshipa huo(aortic dissection)
  • Magonjwa ya mishipa ya damu
  • Kushindwa kuona
  • Athari katika ubongo

Jinsi ya kuzuia shinikizo la damu

Chakula cha afya kisicho na mafuta mengi na chenye madini ya potassium kitaalamu kinaitwa DASH diet (dietary approaches to stop hypertension)

  • Mazoezi mara kwa mara- angalau nusu saa kwa siku
  • Kwa wavutaji sigara kuacha kuvuta sigara
  • Punguza au kama unaweza acha unywaji wa pombe ( kwa wanaume angalau bia 2 kwa siku na wanawake bia 1)
  • Punguza utumiaji wa chumvi hasa ya kuongeza mezani (usitumie zaidi ya gramu 1.5)
  • Punguza msongo mawazo
  • Hakikisha unakuwa kwenye uzito wa afya, kama uko kwenye uzito wa hatari fanya mpango wa kupunguza uzito.
  • Matumizi ya mafuta ya samaki husaidia kupunguza shinikizo la damu, kwa wenye shinikizo la damu.

Tatizo la kiakili la kujihisi mnene na kupoteza hamu ya kula au Anorexia nervosa ni tatizo linawaathiri watu wengi na kuwafanya kupoteza uzito zaidi ya ule unaokubalika kulingana na umri na urefu wa muhusika.

Watu wenye tatizo hili wana hali ya kuwa na hofu isiyo kifani ya kuongezeka uzito hata kama, kiukweli, wana uzito mdogo (wamekonda) kuliko kawaida. Wanaweza kujinyima au kupunguza kula makusudi (dieting), kufanya mazoezi ya kupunguza uzito kuliko kawaida au hata kufanya njia nyingine zozote ilimradi wapungue uzito.

Chanzo na vihatarishi vya tatizo hili

Chanzo halisi cha tatizo hili bado hakifahamiki rasmi. Hata hivyo, mambo kadhaa yanahusishwa na kutokea kwake. Mambo hayo yanajumuisha sababu za kinasaba (genetic factors) na vichocheo mwili (hormones). Aidha masuala ya kijamii yenye kuchochea wana jamii kama vile baadhi ya wasichana kupenda maumbo madogo (vimodo) nayo pia yanahusishwa.

Kipindi cha nyuma, masuala kama matatizo katika familia yalikuwa yakihusishwa na uwepo wa tatizo hili pamoja na matatizo mengine yanahusiana na ulaji wa muhusika ingawa kwa sasa uhusiano wake unaonekana kuwa si wa nguvu sana.

Vihatarishi vya anorexia nervosa vinajumuisha

Wiki iliyopita niliongelea kulika kwa meno kama hali inayotokea wakati sehemu ngumu ya nje ya meno huondoka na kusababisha sehemu ya ndani kuwa wazi.

Nilitaja kuwa ziko aina mbali mbali za kulika kwa meno kulingana na nini kinasababisha tatizo. Aidha kinga au tiba hutegemea nini kinasababisha tatizo hilo. Nikaongelea kwa undani kulika kwa meno kunakosababishwa na meno kusagana yaani attrition.

Leo nitaongelea aina nyingine ya kulika kwa meno

Kuyeyuka kwa meno (tooth erosion)

Huku ni kulika kwa meno kunakosababishwa na kemikali hasa tindikali. Tindikali inayoyeyusha meno haya yaweza kutoka nje au ndani ya mwili wenyewe.

Kuyeyuka kwa meno kunakosababishwa na tindikali toka nje ya mwili: Baadhi ya vyakula na vinywaji tunavyokula na kunywa vina kiwango kikubwa cha tindikali (acid), hivyo vyakula na vinywaji hivyo vikikaa kinywani kwa muda huweza kusababisha meno kuyeyuka.

Ugonjwa wa pumu ni ugonjwa ambao huathiri sehemu ya kupitisha hewa kwenda kwenye mapafu ya binadamu zinazojulikana kitaalamu kama bronchioles.

Mtu mwenye pumu huwa na mcharuko mwili sugu (chronic Inflammation) kwenye mirija yake ya kupitishia hewa (bronchioles tubes) hali ambayo husababisha kuvimba kwa kuta za mirija hii, kujaa kwa ute mzito (mucus) na kupungua kwa njia ya kupitishia hewa, hali ambayo humfanya muathirika kushindwa kuvuta na kutoa hewa nje na hivyo kupumua kwa shida sana. Hali hii inaweza kudumu kwa muda mfupi au mrefu kiasi cha kuhitaji tiba ili kumuwezesha mgonjwa kupata nafuu.

Kutokana na  kuwepo kwa msuguano na uzuiaji wa kupitisha hewa wakati wa kupumua  nje, pumu hujulikana pia kama obstructive lung disease . Mtu aliye na pumu, huwa nayo kipindi chote cha maisha yake.  

Makundi ya Pumu

Pumu inaweza kugawanywa katika makundi mawili;

  • Pumu ya ghafla (Acute asthma):  Wagonjwa wanaopatwa na kundi hili la pumu huwa na hali ya kawaida  katika njia zao za hewa isiyobadilika kati ya shambulizi moja na jingine.
  • Pumu sugu (Chronic Asthma): Kundi hili la pumu huwa na tabia ya kuwa na njia nyembamba za kupitisha hewa  na kadiri jinsi mgonjwa anavyoendelea kupata matukio zaidi ya pumu, njia za hewa huzidi kuwa nyembamba zaidi.

Aina za ugonjwa wa pumu

Bila kujalisha mgonjwa anaingia katika kundi gani, ugonjwa wa pumu unaweza kugawanywa katika aina kuu nne, ambazo ni

1.Pumu inayobadilika (brittle asthma): Kulingana na tabia ya kujirudia rudia kwa matukio ta ugonjwa huu na madhara yake kwa mgonjwa, aina hii ya pumu inaweza kugawanywa zaidi katika aina nyingine mbili, ambazo ni

  • Aina ya kwanza ya pumu inayobadilika (type 1 brittle asthma) ni pumu yenye tabia ya kuwa na matukio na mashambulizi ya kubadilika kila mara japokuwa mgonjwa anaweza kuwa anapata matibabu kadhaa.
  • Aina ya pili ya pumu inayobadilika (type 2 brittle asthma)  ni pumu ambayo mgonjwa anatokea kupata shambulizi la ghafla (asthmatic attack) wakati hapo awali ugonjwa wake uliweza kuthibitiwa kwa matibabu.
Ukurasa 2 ya 11