Image

Habari! Karibuni tena katika muendelezo wa makala zetu kuhusu Kisukari ambazo zinapatika katika tovuti pendwa ya TANZMED, Mara ya mwisho tulikumbushana kuwa wewe ndio tabibu ama daktari wa tatizo lako, wewe sio mgonjwa wewe ni mtu wenye kisukari, ama una ishi na kisukari, ni kitu cha kawaida sana kwa dunia ya sasa.

Sasa leo napenda kuwakumbusha ni vitu gani au ni mambo gani mtu wenye kisukari anatakiwa kuviepuka. Kama tujuavyo kuwa endapo Kisukari haitadhibitiwa ipasavyo basi inaweza kuleta madhara mengi kama kupata kiarusi,upofu, matatizo ya moyo, vidonda ndugu,matatizo ya figo na ini,kwa wanaume kukosa nguvu vya kiume, matatizo ya misuli na kadhalika. Sasa kwa sisi wenye kisukari tuishi vipi ama tufanye nini ili kuepuka haya yote?

  1. Jambo la kwanza ambalo mara nyingi napenda kuwakumbusha watu watu wenye kisukari kuwa ni muhimu sana kujikubali, hili ni jambo ya kwanza kwakuwa ukijikubali kuwa una tatizo la kisukari inakuwa rahisi sana kubadili mfumo wa maisha uliyokuwa unaishi kabla ya kupata tatizo  na mara nyingi nasisitiza umuhimu wa kumpatia ushauri nasaha kwa watu wenye kisukari.
  2. Jambo la pili ni kuepuka kabisa na kupunguza kutumia vitu ama vyakula vinavyoweza kupandisha sukari yako kwa haraka,vitu kama soda,juisi,keki,sukari,asali, Chokoleti na vitu vya kupunguza hasa hasa ni vyakula vya wanga na matunda,hapa nikisema matunda simaanishi kuwa matunda walisiwe hapana,ninachomaanisha hapa ni liliwe tunda na sio matunda na kwa muda, ima masaa mawili au lisaa limoja baada ya chakula.
  3. Jambo la tatu ni kuepuka kupata vidonda kwa kuwa kama hujaweza kudhibiti kisukari ni rahisi sana kidonda kuchelewa kupona kwa hiyo basi yafuatayo ni baadhi ya mambo muhimu ya kuizngatia;
  • Epuka kutembea bila viatu,yaani kutembea peku, kwa maana unaweza kujikata na kitu chenye ncha kali kama sindano, chumba, miiba nk
  • Epuka kutumia vitu vyenye ncha kali kutaka kucha kwa mfano usitumia wembe au mkasi kukata kucha ili kuepuka kupataka na kupata kidonda,pendelea sana kutumia nail taker.
  • Epuka kuvaa viatu na soksi za kubana, na pia hakikisha miguu yako ni mikavu kila muda, kwa hiyo basi utokapo kuoga ama kunawa miguu, hakikisha unaikausha vizuri hasa katikati ya vidole, kwa sababu kama ukiacha unyevunyevu ni rahisi kutengeneza lengelenge na pia endapo utapata lengelenge usitumbue, acha na likaule lenyewe
  • Kwa wanawake, epuka kuvaa viatu virefu kwa sababu vinazuia damu kufanya mvunguko wake wa kawaida (blood circulation)

Kwa kumalizia napenda kusisitiza tu kuwa kisukari sio mwisho wa maisha,na pia kumbuka kuwa watu wenye kisukari ni watu wanaoishi katika mfumo sahihi wa maisha.

Saratani ni aina ya ugonjwa unaosababisha ukuaji wa seli za mwili kubadilika na kukua bila mpangilio maalum.

Saratani ya matiti hutokea kwenye titi ambalo kwa kawaida lina sehemu ya kutengeneza maziwa ijulikanayo kama lobules na aina fulani ya mishipa inayounganisha hizi lobules na chuchu za titi. Sehemu kubwa iliyobakia ya matiti inajumuisha mafuta na tishu ambazo kitaalamu tunazoita connective and lymphatic tissue. Saratani ya matiti inayotokea kwenye lobules huitwa lobular carcinoma na ile inayotokea kwenye ducts huitwa ductal carcinoma.

Baadhi ya saratani ya matiti zinaongeza ukubwa kutokana na kuwa na vishikizi aina ya receptors zinazojulikana kama estrogen receptors kwenye seli zao ambazo husababisha ukuaji wa saratani ya matiti.

Kuna wanawake wengine wana viashiria vya asili vinajulikana kama HER2 positive breast cancer ambacho husaidia seli kuongezeka, kugawanyika na kujirekebisha pale zinapoharibika. Kiashiria hiki kinaaminika ndicho kinachosababisha wanawake hawa kuwa na saratani ya matiti yenye madhara zaidi na kuwa na uwezekano mkubwa wa kujirudia kwa saratani baada ya tiba tofauti na wale ambao hawana kiashiria hiki cha HRE2.

Vihatarishi vya Saratani

Kuna mambo kadhaa ambayo yameonekana kuwa na uhusiano, ama wa moja kwa moja au kwa kupitia vitu vingine, wa kusababisha saratani ya matiti, au kumfanya mtu au kundi la watu kuwa katika hatari ya kupata ugonjwa huu kuliko wengine. Mambo hayo ni pamoja na

Ugonjwa wa kichocho, ni ugonjwa unaosababishwa na vimelea vinavyojulikana kwa kitaalamu kama schistosoma. Ugonjwa huu huathiri zaidi ya watu milioni 207 duniani na kati ya hao asilimia 85% ni katika bara la Afrika. Baada ya ugonjwa wa malaria na maambukizi ya minyoo, kichocho ni wa tatu katika magonjwa makubwa ya kitropiki.

Kichocho ni ugonjwa ambao huathiri eneo fulani la jamii au eneo fulani la kijiografia kwa kitaalamu tunaita endemic, ambapo watu wanaathirika kutokana na shughuli zao za kila siku mfano wakulima, wavuvi, na vilevile kutokana na starehe kama kuogelea kwenye bwawa lisilo salama au ziwani.

Kichocho huambukizwaje?

Maambukizi ya ugonjwa huu wa kichocho hutokea pale mabuu (larvae) ya vimelea vya shistosoma yalioachiwa kutoka kwa konokono wa majini yanapopenya ngozi ya mtu aliye kwenye maji yalioathiriwa.

Ndani ya mwili wa binadamu haya mabuu (larvae) huendelea kukomaa na kuwa vimelea kamili, vimelea hivi hupenda kuishi kwenye mishipa ya damu, vimelea jike hutaga mayai, ambapo baadhi ya mayai hutolewa kwa kukojoa au kwa njia ya haja kubwa. Na mzunguko huendelea.

Kuna aina ngapi za kichocho?

Kuna aina mbili za kichocho ambazo ni:

  • Kichocho cha utumbo ama intestinal schistosomiasis na
  • Kichocho cha mfumo wa mkojo ama urinary schistosomiaisis

Kila aina ya kichocho kinaletwa na aina tofauti za vimelea hawa wa schistosoma kama ifuatavyo:

  • Kichocho cha Utumbo (Intestinal schistosomiasis) husababishwa na vimelea vya Schistosoma mansoni  na Schistosoma intercalatum
  • Kichocho cha Utumbo aina ya Asia (asian intestinal schistosomiasis) husababishwa na vimelea aina ya Schistosoma japonicum na Schistosoma mekongi
  • Kichocho cha mkojo (Urinary schistosomiasis) husababishwa na vimelea jamii ya Schistosoma hematobium

Dalili za kichocho

  • Maumivu ya tumbo
  • Kuhara damu hasa kwa kichocho cha utumbo
  • Kukojoa damu (terminal hematuria) hasa kwa kichocho cha mkojo
  • Kikohozi
  • Homa
  • Uchovu
  • Ngozi kuwasha (cercarial dermatitis) kwa jina lingine swimmers itch

Vipimo na Uchunguzi

  • Kuangalia uwepo wa mayai ya vimelea kwenye mkojo na kinyesi kwa kutumia Hadubini.
  • X-ray ya tumbo
  • Ultrasound ya tumbo
  • Kipimo cha damu (complete blood count)
  • Cystoscopy kwa kichocho cha mkojo
  • Sigmoidoscopy/proctoscopy kwa kichocho cha utumbo

Matibabu

  • Kichocho hutibiwa kwa kutumia dozi ya mara moja ya dawa iitwayo Praziquantel

Madhara ya Kichocho

  • Kansa ya kibofu cha mkojo (cancer of urinary bladder)
  • Figo kushindwa kufanya kazi
  • Cor pulmonale
  • Gastrointestinal bleeding - Kuvuja damu ndani ya mwili hasa katika mfumo mzima wa chakula
  • Portal hypertension
  • Seizures - Kifafa au degedege
  • Reflex nephropathy

Jinsi ya kuzuia kichocho

  • Kuondoa na kuangamiza konokono waliopo kwenye maji au ambao hupenda kuishi kwenye maji ambao ni muhimu katika mzunguko wa kuuwaji wa vimelea vinavyoleta kichocho kwa kutumia Acrolein, copper sulfate na niclosamide.
  • Kwa sasa kuna utafiti unaendelea kwa ajili ya kutafuta chanjo ya ugonjwa huu wa kichocho.

Watu wengi huwa na hofu ya sintofahamu hasa wanapofikiria kwenda kumwona daktari wa meno. Mambo 10 yafuatayo yatakusaidia sana kufahamu nini utarajie unapokwenda kufuata uchunguzi wa afya ya kinywa na meno ama matibabu ya magonjwa ya kinywa na meno.

1. Uchunguzi wa afya ya kinywa na meno hujuimuisha uchunguzi wa kansa kinywani

Unapokwenda kwa daktari wa kinywa na meno kwa uchunguzi wa kawaida wa kinywa na meno (dental check up visit), kwa kawaida daktari wa kinywa na meno hutazama hali ya kinywa na meno pia huchunguza uwepo wa dalili za kansa kinywani. Inakadiriwa kuwa mtu mmoja hufa kila saa la kutokana na ugonjwa wa kansa kinywani huko Marekani. Ugonjwa huu hatari unaoshambulia zaidi kuta za kinywa, midomo-hasa mdomo wa chini- pamoja na koo unatibika ikiwa utatambuliwa mapema na kutibiwa kikamilifu.

Hivyo, kumwona daktari wa meno walau mara mbili kwa mwaka (kila baada ya miezi sita) na kuepuka matumizi ya tumbaku/sigara vitakuwezesha kujikinga na ugonjwa wa kansa ya kinywa na madhara yake.

2. Magonjwa ya fizi huathiri afya ya mwili kwa ujumla

Magonjwa ya fizi na meno ni chanzo kikuu cha kupoteza meno kwa watu wenye umri mkubwa/watu wazima, na pia magonjwa haya huhusishwa na magonjwa ya moyo na kiharusi (stroke).

Ikiwa magonjwa haya ya fizi yatatambuliwa mapema (gingivitis), yanatibika vizuri na kuepusha madhara zaidi.

Ikiwa tatizo hili halitopata tiba mapema, ugonjwa hukomaa zaidi (periodontitis) ambapo mfupa unaoshikilia jino/meno hushambuliwa na kuharibiwa.

Kusafisha meno kwa kupiga mswaki mara mbili kwa siku, matumizi ya nyuzi-safishi (dental floss), kumwona daktari wa meno kwa uchunguzi mara kwa mara na kusafisha meno kitaalamu kwa tatibu wa meno, kutasaidia kuepuka madhara ya magonjwa ya fizi.

3. Uchunguzi wa kinywa na kusafisha meno kitaalamu ni tiba muhimu zaidi

Ni wangapi kati yetu wenye desturi ya kumwona daktari wa meno walau mara mbili kwa mwaka (walau kila baada ya miezi sita)? Mara nyingi wengi wetu huhangaika na foleni za kumwona daktari wa meno pale tu tunaposumbuliwa na maumivu ama ya jino ama kidonda kinywani ama kwa sababi ya hali zinginezo zinatotulazimisha kumwona daktari wa meno.

Kusubiri mpaka tusukumwe na maumivu ya meno/kidonda kinywani ama ajali yoyote kunatunyima fursa bora zaidi ya kuchunguzwa afya ya kinywa na meno na kusafishwa meno ili kuepusha madhara ya magonjwa ya kinywa na meno kabla hayajatokea ama kukomaa.

Pingamizi la upumuaji usingizini ni hali ya kushindwa kupumua kwa kutumia pua au mdomo kwa muda wa sekunde 10 wakati mtu akiwa amelala. Tatizo hili hutokea zaidi ya mara 30 katika hatua mbili za vipindi vya usingizi vinavyojulikana kitaalamu kama Rapid Eye Movement na Non Rapid Eye Movement.

Rapid Eye Movement Sleep ni kipindi kimojawapo cha usingizi wa kawaida ambacho huambatana na macho kucheza cheza yaani mtu anakuwa yupo usingizini huku macho yake yakicheza cheza. Kwa kawaida wakati mtu amelala hupitia hatua hii mojawapo ya usingizi na hutokea mara 4-5 katika usingizi, mwanzoni REM ikitokea kwa muda mfupi sana na mwishowe kipindi hiki kukawia kwa muda mrefu hasa inapokaribia asubuhi. Inakisiwa REM huchukua asilimia 20-25 ya usingizi wa mtu mzima yaani dakika 90-120 kwa ujumla.

Non Rapid Eye Movement Sleep ni hatua ambayo mtu anakuwa amelala lakini hapitii hatua ya REM, hivyo kumfanya kutochezesha macho, kuota ndoto ni nadra sana kwa wenye kupata hatua hii, akili huwa katika hali njema kabisa (mindset is more organized) viungo vya mwili wake kutolegea (muscles not paralyzed) ndio maana mtu anaweza kutembea huku akiwa usingizini (sleep walk).

Haya ni matibabu ambayo hutolewa kwa jino ambalo sehemu ya uhai wake imeharibika kiasi kwamba haliwezi kutibika kwa kuziba tu, kwa maneno mengine hii ndiyo njia mbadala ya kutibu jino bila kung’oa.

Matibabu uhusisha kutoboa jino hadi sehemu ya uhai wa jino yenye mishipa ya damu na ile ya fahamu na chembechembe za meno na kuviondoa nikimaanisha kuondoa mishipa ya fahamu, ya damu na chembe pamoja na ugonjwa na baadae kuijaza sehemu hii na vitu maalumu vinavyokubaliana na mwili (biocompatible).

Aina za matibabu ya mzizi wa jino

Kuna aina kuu mbili za matibabu ya mzizi wa jino

Njia ya kawaida (conventional root canal treatment)
Njia hii ni kama nilivyoeleza hapo juu, kuingia kwenye kiini cha jino na kuondoa kila kitu kilichomo na kisha kujaza uwazi uliobaki na vitu maalumu vinavyokubaliana na mwili

Matibabu ya mzizi wa jino yanayohusisha upasuaji
kwa njia hii mbali na kutumia njia ya kwanza, upasuaji hufanyika pia ili kondoa mfupa uliofunika ncha ya mzizi wa jino kusafisha eneo lililozunguka ncha ya mzizi na baadaye kukata ncha husika kisha kuziba kutokea kwa nyuma (retro grade filling).

Njia hii hutumika pale njia ya kawaida inaposhindwa kuondoa tatizo au inapoonekana kabisa kuwa haitaweza kuondoa tatizo. Huu ni upasuaji mdogo, unaofanyika kwa ganzi ndogo ya eneo husika (local anaesthesia). Mafanikio ya matibabu haya ni makubwa sana.

Ni meno yapi yanahitaji matibabu hayo?

•    Meno yaliyooza hadi uoza kufikia kiini cha jino (dental pulp) - sehemu ya uhai wa jino.
•    Meno yaliyopata ajali na kupasuka na kuacha kiini cha jino kikiwa wazi (traumatic pulp exposure)
•    Meno yaliyopata ajali na kusababisha mishipa ya damu kukatika au kupasuka na kuvunjika ndani ya jino, kitu ambacho hupelekea jino kufa (pulp necrosis) na baadaye kusabisha jipu au kubadilika rangi
•    Wakati mwingine japo ni mara chache, ni pale tunapokuwa tunataka kuliweka sawa jino/meno ambalo/ambayo hayapo kwenye mstari sawa ili yaendane na meno mengine.
•    Pia wakati mwingine, tunapo lisaga jino ili liweze kubeba meno bandia ya daraja (bridge) huku tukiwa na mashaka na uhai wake.

Nini dalili zinazoashiria jino kuhitaji matibabu haya?

•    Jino linalouma - kuuma kwa jino kunashiria ugonjwa kuwa umeingia ndani ya kiini cha jino na au hata kupitiliza na kuingia kwenye mfupa ulioshikilia jino
•    Jino lililooza na kusababisha uvimbe, liwe linauma au haliumi
•    Jino lililokatika na kupoteza zaidi ya nusu ya kichwa cha jino (crown) kukatika kuwe kwa ajali au kuoza au vyote kwa pamoja
•    Jino linalobadilika rangi huku kukiwa na historia ya kuligonga mahali au kuchapwa ngumi usoni, hapa jino linaweza kuanza kubadilika rangi miezi sita tangu siku ya ajali mpaka wakati mwingine hadi miaka ishirini wakati mgonjwa alishasahau hata ajali yenyewe.

Malaria ni ugonjwa unaoathiri watu wengi sana duniani. Malaria husababisha vifo vya watu milioni 2.7 duniani kote, ambapo vifo vingi hutokea barani Afrika. Ugonjwa wa malaria huonekana katika nchi 100 duniani kote.

Kwa Tanzania, mikoa ambayo inaongoza kwa maambukizi ya malaria ni Kagera (41.1%), Lindi (35.5%), Mtwara (36.6%), Mwanza (31.4%), Mara (30.3%). Mikoa ambayo  maambukizi ya malaria ni kidogo  ni Manyara (1%), Kilimanjaro (1%) na Dar-es-salaam (1.2%). Kwa Zanzibar, maambukizi ya malaria ni kwa asilimia 0.8.

Malaria huonekana sana katika kanda ya Tropiki.Ugonjwa huu wa malaria uligunduliwa mwaka 1880 na Charles Louis Alphonse Laveran, katika hospitali ya jeshi ya Constatine, Algeria, baada ya kuona vimelea vya plasmodium, kutoka kwa mgonjwa aliyefariki kwa ugonjwa huo.

Malaria ni kati ya magonjwa ya maambukizi ambao husababishwa na vimelea vya Plasmodium, ambavyo humfikia binadamu kupitia kung’atwa na mmbu aina ya Anopheles jike.

Kuna aina 5 za vimelea viletavyo malaria:

  1. Plasmodium falciparum - Hupatikana sana katika nchi zilizopo katika jangwa la sahara. Asilimia 75 ya wagonjwa wote wa malaria barani Afrika husababishwa na vimelea hivi. Mwaka 2006, kati ya watu milioni 247 duniani waliougua malaria, asilimia 91 walisababishwa na vimelea hivi (Afrika 98%) na kusababisha vifo kwa asilimia 90 mwaka huo huo barani Afrika.
  2. Plasmodium malariae - Pia hupatikana katika nchi zilizopo katika jangwa la sahara, Asia ya Mashariki, Indonesia na katika visiwa vya magharibi mwa Pacific. Kati vya vimelea vyote vya malaria, plasmodium malariae ndio huonekana kwa uchache zaidi.
  3. Plasmodium ovale - Hupatikana Afrika Magharibi, Ufilipino, Mashariki mwa Indonesia, Papua New Guinea, Cambodia, Bangladesh, India, Thailand na Vietnam.
  4. Plasmodium vivax - Huonekana katika bara la Marekani, Latin Amerika na baadhi ya sehemu za bara la Afrika.
  5. Plasmodium knowlesi - Hupatikana katika bara la Asia ya mashariki katika nchi za Bormeo, Myanmar, Malaysia, Ufilipino, Singapore na Thailand. Haipatikani katika bara la Afrika.

Mzunguko wa maisha ya vimelea vya malaria

Mwenyeji wa msingi ya vimelea vya malaria ni mbu aina ya anopheles wa kike, ambae pia ni msambazaji, na binadamu ni mwenyeji wa kati. Mbu anapokuwa anajipatia chakula kwa kunywa damu kwa kuuma binadamu mwenye maambukizi ya vimelea vya malaria, ndio mzunguko wa kwanza huanza, ambapo gametocyte za vimelea vya plasmodium hugawanyika ndani ya mbu na  kutengeneza gametocyte za kike na za kiume na baada ya hapo gametocyte hizo za kike na za kiume, hujiunga ndani ya mfumo wa chakula wa mbu na kutengeneza Ookinete ambayo hupenyeza kwenye kuta za mfumo wa chakula na kutengeneza Oocyst nje ya ukuta wa mfumo wa chakula, na hapo hupasuka na kutengeneza Sporozoites na kuhamia kwenye tezi za mate za mbu, na kuwa tayari kuambukiza binadamu mwengine pindi mbu anapojitafutia chakula.

Kwa mbu jike damu ndio lishe yake wakati dume lishe yake ni nekta ya mimea, hivyo mbu dume hasambazi ugonjwa huu. Na mbu jike aina ya anopheles hupenda kujipatia lishe kipindi cha usiku.

Maambukizi ya malaria yanaweza kupatikana kwa kuongezewa damu ingawa ni nadra sana.

Ni pale ambapo kunakuwa na mkusanyiko wa maji kati ya kuta mbili zinazozunguka  mapafu. Kujaa huku kwa maji husababisha mgonjwa kupata shida ya kupumua vizuri.


Je mapafu kujaa maji husababishwa na nini?

Sababu za Mapafu kujaa maji zinaweza kuelezewa kutokana na aina ya maji yaliyojaa:

  • Transudate – hapa maji huliki kutoka kwenye mishipa ya damu na kuingia kwenye mapafu mfano kwenye magonjwa yafuatayo:
  • Moyo kushindwa kufanya kazi kwa ufanisi (congestive cardiac failure)
  • Ini kushindwa kufanya kazi kwa ufanisi (liver failure)
  • Figo kushindwa kufanya kazi kwa ufanisi (renal failure)
  • Exudate – hapa maji hujaa kutokana na kuta zinazonguka mapafu kitaalamu pleura zinapovimba au kutokana na magonjwa ya mapafu mfano:
  • Kansa ya pafu au ya titi
  • Lymphoma
  • Kifua kikuu
  • Vichomi
  • SLE
  • Figo kushindwa kufanya kazi kwa ufanisi 
  • Asbestosis
  • Majipu ndani tumbo

Hutokea pale vimelea (bakteria) wanapovamia kuta za ndani za moyo (endocardium), zikiwepo valve na kusababisha maambukizi.

Hakuna mishipa ya damu ambayo ni mahususi kwa ajili ya kupeleka damu safi moja kwa moja kwenye valve za moyo, hivyo chembe chembe nyeupe za damu (ambazo ni mahususi kwa ajili ya kinga ya maambukizi) hufika kwa shida sana kwenye valve za moyo. Hali hii husababisha chembe chembe nyeupe kuwa butu  pale vimelea (bakteria) wanapotengeneza uoto (vegetations) kwenye valve za moyo. Na kwa sababu ya hakuna mishipa ya damu ambayo ni mahususi kwa ajili ya kupeleka damu moja kwa moja kwenye valve za moyo, matibabu yake husumbua sana kwakuwa ni vigumu dawa kufika kwenye eneo husika.

Maambukizi katika kuta za ndani za moyo yamegawanyika katika sehemu kuu mbili kutokana na  jinsi ugonjwa ulivyo-anza (onset):

Maambukizi ya kuta za ndani za moyo ya papo kwa hapo kitaalamu acute bacteria endocarditis 

huanza kati ya siku kadhaa hadi wiki kadhaa, na mgonjwa huwa maututi; na maambukizi katika kuta za ndani za moyo ndogo ya papo kwa hapo kitaalamu sub acute bacteria endocarditis- huanza kati ya wiki kadhaa hadi miezi kadhaa, na dalili hutokea pole pole

Na vile vile maambukizi haya yanaweza kugawanywa kama ifuatavyo

  • Maambukizi katika kuta za ndani za moyo ya Valve asili au kitaalamu native valve endocarditis
  • Maambukizi katika kuta za ndani za moyo ya Valve za bandia au kitaalamu prosthetic valve endocarditis
  • Maambukizi katika kuta za ndani za moyo kutokana na matumizi ya madawa ya kulevya kwa njia ya mshipa kitaalamu intravenous drug abuse endocarditis

Maambukizi ya tezi dume bila uwepo wa bakteria (Chronic non-bacterial prostatitis)

Kama jina lake linavyoeleza, maambukizi ya aina hii kwenye tezi dume husababishwa na msongo wa mawazo, matatizo katika vichocheo vya mwili (homoni) na hata matatizo katika mfumo mzima wa neva.Pia kumekuwepo na dhana ya kwamba maambukizi ya aina hii huchangiwa  na kuwepo kwa maumivu ya kibofu cha mkojo yanayotokana na maambukizi katika kibofu hicho (Cystitis) au hali ya hewa hususan baridi ambayo huongeza maumivu ya tezi dume na hali ya joto ambayo hupunguza maumivu hayo. Baridi pia huchangia kujirudia kwa dalili na viashria vya maambukizi haya. Katika utafiti uliofanyika kaskazini mwa nchi ya Finland (nchi ambayo ina majira ya baridi kali sana),umeonyesha ya kuwepo kwa maambukizi ya aina hii yanayoambatana na dalili na viashiria vyake kali sana kuliko sehemu yoyote duniani.

Maambukizi haya ya tezi dume bila uwepo wa bakteria hutokea kwa wanaume walio katika umri wa miaka 35-45 na inakisiwa kutokea kwa asilimia 90-95 ya maambukizi yote ya tezi dume .

Ukurasa 7 ya 11