- Kwenye sufuria tia nyama, saga nyanya na thomu, pilipili mbichi, tangawizi. Mimina kwenye nyama na mtindi, tia na nyanya kopo, bizari paprika, vidonge vya supu, chumvi kisha changanya vyote pamoja weka motoni.
- Katika sufuria nyengine tia mafuta na samli kaanga vitunguu mpaka viwe rangi ya hudhurungi toa weka pembeni.
- Kaanga viazi weka pembeni.
- Chukua mafuta kidogo uliyokaangia tia kwenye nyama acha katika moto wa kiasi mpaka nyama iive na maji ya punguke.
- Tia viazi na vitunguu vivunje vunje tia ndani ya nyama acha moto mdogo.
Vipimo Vya Wali
Mchele 5 mug
Maji Kiasi
Chumvi Kiasi
Mafuta uliyokaangia vitunguu Kiasi
Rangi ya biriani ¼ Kijiko cha chai
*Zafarani ½ Kijiko cha chai
*Loweka rangi na zafarani kwenye kikombe na maji ¼ weka pembeni.
Namna ya Kutarisha na Kupika Wali
- Osha mchele loweka muda wa saa.
- Chemsha maji kama magi 10 hivi na chumvi tia mchele.
- Uache uchemke ukishaiva kiini nusu, mwaga maji chuja.
- Mimina juu ya nyama tia rangi na mafuta kwa juu funika.
- Acha kidogo katika oveni kwa muda wa dakika 20 hivi kisha epua ikiwa tayari.
Mandi na Nyama (Wali wa Yemen)
Vipimo
Mchele 3 Magi
Nyama ya mfupa 2 Ratili ( lb) au Kilo moja
Mafuta ¼ Kikombe
Vitunguu maji kata vikubwa vikubwa 3 Kikubwa
Bizari ya pilau ya unga (cumin) 1 Kijiko cha chakula
Pilipili manga ½ Kijicho cha chai
Hiliki ½ Kijiko cha chai
Karafuu ya unga ¼ Kijiko cha chai
Mdalasini nzima 3 Vijiti
Mdalasini wa unga ½ Kijiko cha chai
Thomu na tangawizi 2 Vijiko vya chakula
Nyanya iliyokatwakatwa 1 Nzima
Kidonge cha supu(Curry cube) 1 au 2
Zafarani (ukipenda) loweka katika maji 1 Kijiko cha chai
Zabibu kavu (ukipenda) ¼ Kikombe
Pilipili mbichi Ukipenda
Chumvi Kiasi
Namna ya Kutayarisha na Kupika
- Kwenye sufuria katakata nyama na isafishe vizuri kisha tia binzari zote pamoja na vitunguu viwili, nyanya freshi, thomu na tangawizi na chumvi kiasi acha ichemkie huku ukiongeza maji mpaka iive vizuri.
- Ikishaiva epua nyama zote tia kwenye (tray) treya ya kuchomea kisha ukipenda unaweza kuongezea viungo au hivyohivyo ukaichoma (bake) kwa moto wa 350° C mpaka rangi ibadilike.
- Ile supu inayobaki ichuje vizuri weka kando kwa ajili ya kupikia wali.
- Tia mafuta katika sufuria, kisha kaanga tena kitunguu kimoja tia mdalasini kidogo na thomu na tangawizi na kidonge cha supu 1 au 2 acha ikaangike kisha mimina ile supu, ukipenda unaweza kutia rangi ya zafarani au rangi ya biriani acha ichemke, kisia maji kutokana na mchele, kisha mimina mchele upike mpaka uive.
- Ukishaiva pakua kwenye sahani kisha weka nyama yako juu ya wali tayari kwa kuliwa na saladi au pilipili.
Kidokezo
Ukipenda unaweza kutia zabibu kavu kwenye wali. Tolea na kachumbari yake.
Biriani na Sosi ya Nyama ya Mbuzi
Vipimo
Nyama ya Mbuzi 1 Kilo
Mchele 4 Magi
Vitunguu 3
Nyanya 2
Nyanya kopo 3 Vijiko vya chai
Thomu na tangawizi iliyosagwa 2 Vijiko vya supu
Pilipili mbichi iliyosagwa 1 Kijiko cha supu
Garam Masala (mchanganyiko wa bizari) 2 Vijiko vya supu
Hiliki 1 Kijiko cha chai
Chumvi Kiasi
Mafuta ½ Kikombe
Zafarani au rangi za biriani za kijani na manjano/orenji
Namna ya Kutayarisha na Kupika Sosi ya Nyama
- Changanya nyama na thomu, pilipili, chumvi na nusu ya garam masala. Tia katika treya (tray) ya oveni uipike nyama (Bake) hadi iive. Au iivishe kwa kuichemsha.
- Katika kisufuria nyengine, tia mafuta (bakisha kidogo ya wali) kaanga vitunguu hadi vigeuke rangi, kisha tia nyanya, nyanya kopo, bizari zote nyingine zilizobakia.
Namna ya Kupika Wali
Mchele 4 magi
Mdalasini 1 Kijiti
Hiliki 3 Chembe
Kidonge cha supu(Curry cube) 1
Chumvi
- Osha na loweka mchele wa basmati au pishori.
- Tia maji katika sufuria uweke jikoni. Tia kidonge cha supu, mdalasini, hiliki na chumvi .
- Yakichemka maji tia mchele, funika upike hadi nusu kiini kisha uchuje kwa kumwaga maji.
- Tia mafuta kidogo katika mchele na zaafarani iliyolowekwa au rangi za biriani kisha rudisha mchele katika sufuria ufunike na upike hadi uive.
- Pakua wali katika sahani kisha mwagia sosi ya nyama juu yake, pambia kwa kukatia nyanya, pilipili mboga na figili mwitu (Celery) au mboga yoyote upendayo.
Makbuus Dajaaj/ Machbuus ya Kuku (U.A.E)
Vipimo
Mchele wa Basmati/pishori 4 Vikombe
Kuku (mkubwa kiasi) 1 (wa lb 6 -7) au Kilo 3 -3.5kg
Vitunguu vilivyokatwakatwa 3
Samli 4 Vijiko vya supu
Buharaat (bizari ya Machbuus) 2 Vijiko vya supu
Bizari ya manjano (haldi/tumeric) 1 Kijiko cha chai
Nyanya zilizomenywa na kukatwakatwa 3
Thomu iliyosagwa 2 Vijiko vya supu
Loomi (ndimu kavu) au ya unga ½ au ½ Kijiko cha chai
Mdalasini kijiti 1
Karafuu nzima 3
Hililiki nzima 4
*Maji 5 Vikombe
Kotmiri iliyokatwakatwa ½ Kikombe
Chumvi Kiasi
Baharaat – Bizari ya Makbuus
Pilipili Manga ½ Kikombe
Gilgilani (Corriander seeds) ¼ Kikombe
Mdalasini vijiti ¼ Kikombe
Karafuu ¼ Kikombe
Bizari ya pilau (cumin seeds) 1/3 Kikombe
Hiliki 2 Vijiko vya chai
Kungu manga 2
Paprika ya unga( Pilipili nyekundu) ½ Kikombe
Namna ya Kutayarisha Baharaat (bizari)
- Vunja kungu manga, chambua hiliki utoe kokwa zake, kisha tia vitu vyote katika mashine ya kusagia (grinder) usage hadi iwe unga.
- Changanya na Paprika bizari ikiwa tayari.
- Ihifadhi katika chupa yenye mfuniko wa kubana vizuri.
Namna ya Kutayarisha na Kupika Makbuus
- Osha na loweka mchele kwa muda kiasi.
- Msafishe kuku, mkate vipande vinne weka kando.
- Katika sufuria ya kupikia, tia samli, kaanga vitunguu hadi vigeuke rangi ya hudhurungi (brown). Tia baharaat na bizari ya manjano, kaanga kwa dakika moja hivi.
- Tia vipande vya kuku, chumvi, thomu, punguza moto na umkaange kuku katika masala ya vitunguu.
- Tia nyanya, karafuu, loomi, mdalasini, hiliki, changanya vizuri na endelea kukaanga.
- Tia maji (inategemea mchele unaotumia, huenda ukahitaji zaidi). Funika na pika kwa muda wa dakika 20-25.
- Mwaga mchele maji uliyolowekea, mimina mchele katika supu, tia kotmiri, changanya vizuri, funika uchemke mchele, punguza moto na pika wali kama inavyopikwa pilau ukoroge mara moja au mbili tu.
- Ukishaiva wali, pakua katika sinia/sahani na weka vipande vya kuku juu katikati ya wali.
Kidokezo
- Ukipenda badala ya kupika wali katika sufuria baada ya kutia mchele na kukaribia kuiva, na kabla ya kukauka supu yote, mimina katika treya ya jalbosi (Treya ya foil) upike ndani ya oveni (bake) kwa moto wa takriban 400-450º kwa muda wa dakika 20-25.
- Baharaat hiyo inatumiwa katika vyakula vya nchi za Kiarabu (Gulf States), hivyo unaweza kutumia kupikia machbuus ya vitoweo vingine kama nyama na samaki na vyakula vinginevyo kama michuzi n.k.
Maandazi
Vipimo
Unga 4 Vikombe vya chai
Sukari 1 Kikombe cha chai
Hamira 1 Kijiko cha chai
Samli 1 Kijiko cha chai
Maziwa au Tui la nazi 1 ½ Kikombe cha chai
Hiliki Kiasi
Mafuta ya kukaangia Kiasi
Namna ya Kutayarisha na Kupika
- Changanya unga Hamira, Samli, maziwa au tui, kisha vuruga na kanda ukandike kiasi.
- Kata madonge manane kisha acha uumuke.
- Ukishaumuka sukuma kila donge ukate vipande vinne.
- Panga kwenye meza tena yaumuke. Weka mafuta ya kukaangia katika karaii na yakaange kwa moto wa kiasi.
- Yatoe weka kwenye sahani tayari kwa kuliwa.
Mchuzi wa Kima na Mayai
Vipimo
Nyama ya kusaga 2 lb (Ratili) au Kilo moja
Mayai 6
Vitunguu 4
Thomu na Tangawizi 1 Kijiko cha supu
Pilipili mbichi iliyosagwa 1 Kijiko cha chai
Nyanya iliyokatwa katwa 4
Kotmiri ½ Kikombe
Pilipili Manga ¼ Kijiko cha chai
Bizari ya curry ½ Kijiko cha chai
Nyanya ya kopo 3 Vijiko vya supu
Garam masala 1 Kijiko cha supu
Mafuta ya kukaangia Kiasi
Namna ya Kutayarisha na Kupika
- Chemsha mayai, yakiiva ambua maganda na uweke kando.
- Katika sufuria weka mafuta yapate moto, Kaanga vitunguu hadi vigeuke na kuwa rangi ya hudhurungi.
- Halafu tia thomu na tangawizi kaanga kidogo tu, kisha tia bizari zote na pilipili uendelee kukaanga.
- Kisha weka nyama na uiache motoni huku unakoroga hadi iwe si nyekundu tena.
- Tia nyanya na chumvi ziache zilainike halafu tia nyanya ya kopo.
- Ongeza maji kiasi unavyopenda mchuzi wako kuwa mzito au mwepesi.
- Kisha weka yale mayai ya kuchemsha na iache itokote kidogo kwa moto mdogo.
- Mwishoe mwagia kotmiri, changanya na umimine katika bakuli na itakuwa tayari kwa kuliwa na wali au mkate upendayo.
Nyama ya Kukaanga na Pilipili Manga
Vipimo
Nyama ½ lb au Robo kilo
Kitunguu 1
Kidonge cha supu 1
Chumvi Kiasi
Pilipili manga 1 Kijiko cha chai
Bizari ya pilau (cumin) ½ kijiko cha chai
Mafuta 2 Vijiko vya supu
Thomu 1 Kijiko cha chai
Tangawizi ½ Kijiko cha chai
Namna ya Kutayarisha na Kupika
- Katika sufuria, kaanga vitunguu mpaka viwe rangi ya hudhurungi
- Tia thomu, tangawizi, bizari ya pilau, pilipili manga, kidonge cha supu, na nyama.
- Kaanga kidogo kisha tia maji kiasi tu cha kuivisha nyama.
- Funika moto mdogo mdogo mpaka iwe kavu, ikiwa haikuiva utaongeza maji kidogo mpaka ikaangike na tayari kwa kuliwa.
Juisi ya Melon na Embe
Vipimo
Tikiti la asali (honey melon) 1
Unga wa embe au embe 1
Tangawizi 1 Kijiko
Ndimu 1
Sukari ¼ Kikombe cha chai
Arki rose 2 Matone
Namna Ya Kutayarisha
- imenye melon na ulikate kate kisha tia kwenye blender
- Tia unga wa embe au embe iliyokatwa katwa
- Kisha tia ndimu iliyokatwa vipande kiasi pamoja na maganda yake
- Halafu weka sukari
- Saga vizuri hadi ilainike
- Mimina kwenye jagi kisha tia matone mawili ya arki rose ukoroge na tayari kwa kunywewa
Kidokezo
Ukiweka ndimu weka na maganda yake unapata ladha nzuri zaidi.
Juisi ya Mabungo
Vipimo Kupata takriban gilasi 6
Mabungo 3
Maji 6 au 7 Gilasi
Sukari Kiasi upendacho
Chumvi Kidogo sana
Namna ya Kutayarisha
- Kata mabungo na toa nyama yake tia katika mashine ya kusagia.
- Tia maji, sukari na chumvi usage kidogo tu.
- Chuja kisha mimina katika jagi uweke katika friji.
- Mimina katika gilasi.
Juisi ya Mapera na Karakara/pasheni (Passion fruit)
Vipimo
Mapera 5
Karakara/Pasheni (Passion fruit) 9
Sukari Kiasi
Maji Kiasi
Namna ya Kutayarisha
- Osha na katakata mapera kisha tia katika mashine ya kusagia (blender) na usage kwa maji kiasi kisha yachuje.
- Kata karakara/pasheni toa nyama yake kisha saga katika blender kwa maji kiasi.
- Changanya pamoja na juisi ya mapera na tia sukari kiasi kadiri upendavyo ikiwa tayari.
Credit kwa wavuti ya www.alhidaaya.com