Tabia hii ya kulala chali wakati wa ujauzito inaweza kuepukika kwa kuwashauri kina mama wajawazito madhara yanayopatikana kwa kulala chali.
Matokeo ya utafiti huu yanaonyesha ya kwamba zaidi ya robo ya idadi ya watoto wanaozaliwa wafu inaweza kuepukika kwa kubadilisha staili ya kulala tu kwa wanawake wajawazito.
Siku zote madaktari wanashauri kina mama wajawazito kulala ubavu mmoja hasa upande wa kushoto ili kuepuka kuzaa mtoto mfu au mtoto mwenye uzito mdogo kwa sababu mwanamke mjazito anapolalia ubavu wake wa kushoto huongeza mzunguko wa damu kwa kiumbe kilichomo ndani yake.
Mlalo hatari kwa mama mjamzito
Mlalo salama kwa mama mjamzito
Kwa maelezo zaidi, soma Kulala Chali kwa Mjazito ni Hatari kwa Mtoto?