..
Unapohisi dalili hizi ni vyema kwenda kwa daktari ili upate tiba muafaka badala ya kuanza kutumia madawa bila ya mpangilio maalumu kitu kitakachoweza kukusababishia kukomaza ugonjwa. Pia, kuna baadhi ya dalili za UTI hufanana na zile za magonjwa ya zinaa (chlamydia, gonorrhea, and trichomoniasis), hivyo, vipimo vya maabara huitajika kuweza kutambua kama unachoumwa ni UTI au ni magonjwa ya zinaa (STD)
Vipimo:
- Kupima mkojo kuangalia kama kuna chembe chembe nyeupe,na vimelea ambacho ni kiashirio cha maambukizi
- Kuotesha mkojo kuangalia vimelea
- Ultrasound ya tumbo chini ya kitovu kuangalia njia ya mkojo na hasa kibofu
Jinsi ya kujikinga na maambukizi ya njia ya mkojo
- Kunywa maji mengi
- Baada ya haja kubwa ni vizuri kunawa kuanzia mbele kurudi nyuma
- Pendelea kwenda kukojoa pindi unapojisikia umeshikwa na mkojo. Na hakikisha umetoa mkojo wote.
- Hakikisha sehemu za siri zipo safi kabla ya kujamiana
- Ni vizuri kupata haja ndogo mara baada ya kujamiana ili kusafisha bakteria ambao wanaweza kuwepo kwenye njia ya mkojo,
- Tumia juisi ya Cranberry ina vitu kitaalamu Vitamins and antioxidants ambavyo husaidia kuzia (siyo kutibu) maambukizi haya.
- Hakikisha sehemu za siri zipo kavu, pendelea kuvaa nguo za ndani zilizotengenezwa kwa pamba, pia zenye kuacha unafasi (loose-fitting), epuka jinsi zinazobana au nguo za ndani za unailoni kwa sababu zitapelekea kuwa na hali ya unyevunyevu na kuleta mazingira rafiki kwa ukuaji wa bakteria.
- epuka matumizi ya vipandikizi vinavyowekwa kwenye njia ya uzazi vinavyotumia dawa za kuuwa shahawa kuzuia mimba
UTI kwa wajawazito
Wanawake wajawazito wapo kwenye hatari kupatwa na ugonjwa wa UTI. Homoni wakati wa ujauzito hupelekea kutokea mabadiliko kwenye njia ya mkojo. Pia, uterus huongeza mgandamizo kwenye mishipa inayopitisha mkojo kutoka kwenye kibofu (ureter) na kibofu chenyewe, hali hii husababisha mkojo kupita kwa shida kutoka kwenye figo kuja kwnye kibofu au kutoka kwenye kibofu chenyewe. UTI isiyotibiwa huweza kuleta athari kwa mjamzito ikiwemo preterm labor.
UTI kwa watoto wadogo
Watoto wadogo, pia wanaweza kupata ugonjwa wa UTI ingawa mara nyingi ni ngumu kwa mzazi kutambua kwa sababu ni ngumu kujieleza. Mara nyingi unaweza kuona dalili zifuatazo
- Homa
- Harufu tofauti ya mkojo
- Kukataa vyakula au kutapika
- Kusumbuasumbua (Fussy behaviour)
Unashauriwa kumpelekea hospitali kwa ajili ya matibabu punde unapohisi ana UIT ili kuzuia athari Zaidi. Pia, kubadilisha nepi kunasaidia kupunguza uwezekano wa maambukizi. Kumbuka, kumsafisha kutokea mbele kuja nyuma wakati unambadilisha nepi na kumsafisha.
Hatari za UTI
Hatari kubwa ya kukaa na UTI ni kuwa, bakteria wanaweza kusambaa hadi kutoka kwenye kibofu hadi kwenye figo. Bakteria hawa huweza kuathiri ufanyaji kazi wa figo kitu ambacho ni cha hatari haswa kwa watu wenye matatizo ya figo. Pia, kuna uwezekano mdogo wa bakteria hawa kuingia kwenye mfumo wa damu, endapo hatua hii itatokea, basi huweza kusababisha kuthirika kwa viungo vingine. Hatari kwa mama mjamzito kupata maambukizi ya njia ya mkojo huweza kupelekea kujifungua kabla ya wakati, au kujifungua mtoto mwenye uzito mdogo.
Kama una maswali kuhusiana na ugonjwa wa UTI, usisite kuacha maoni hapo chini.