Image

Madhara ya kuvimba tezi dume

Tezi dume ni sehemu mojawapo ya mfumo wa uzazi wa kiume. Mojawapo ya kazi za tezi dume ni kutoa majimaji yanayochanganyika na mbegu za kiume (sperms) wakati wa kilele cha tendo la ngono. Mchanganyiko huu wa mbegu pamoja na majimaji hayo hufanya shahawa (semen). Mchanganyiko huu wa mbegu pamoja na majimaji hayo hufanya shahawa (semen). Aidha majimaji hayo husaidia kuzipa mbegu za kiume nguvu ya kusafiri kwenye uke mpaka kufikia kwenye mirija ya fallopian tayari kwa utungisho na yai la kike.

Kwa kadiri mwanaume anavyozeeka, ni jambo la kawaida pia kwa tezi dume kuongezeka ukubwa na kuvimba. Hali hii kitabibu huitwa Benign Prostate Hyperplasia.(BPH)

Pichani, ni muonekano wa tezi dume ya kawaida(normal prostate) na tezi dume iliyovimba(enlarged prostate) zinavyokuwa

Madhara ya BPH

BPH kama ilivyo saratani ya tezi dume, inaweza kumletea mgonjwa madhara (complications) kadhaa. Madhara hayo ni pamoja na

  • Mkojo kushindwa kutoka (retention of urine)
  • Mgandamizo kwenye kibofu cha mkojo
  • Vijiwe kwenye kibofu cha mkojo
  • Uambukizi katika njia ya mkojo (UTI)
  • Madhara katika figo au kibofu
  • Shinikizo la damu
  • Kushindwa kutoa shahawa kwenye uume (retrograde ejaculation)
  • Maambukizi mbalimbali
  • Nimonia (Pneumonia)
  • Damu kuganda
  • Uhanithi

Kuhusu dalili zake, vipimo,uchunguzi na matibabu fuatilia hapo Kuvimba kwa Tezi Dume (Benign Prostate Hyperplasia BPH)

Imesomwa mara 5533 Imehaririwa Ijumaa, 08 Februari 2019 16:42
Sophia Mangapi

Web Developer

Anwani ya barua pepe hii inalindwa kutokana na spambots. JavaScript lazima iwe itawezeshwa kwa kuweza kuona.