Image

Magonjwa ya Moyo ya Kuzaliwa (Congenital Heart Diseases)

Muundo ya moyo  na mishipa ya damu ni mojawapo ya vinavyooathirika katika magonjwa ya moyo ya kuzaliwa nayo. Vijusi(fetuses) kati ya 8 hadi 10 huathirika kwa kila 1000.

Magonjwa ya moyo ya kuzaliwa nayo huweza kutoa dalili mara tu baada ya kuzaliwa, utotoni na wakati mwingine husubiri mpaka ukubwani. 

Magonjwa ya Moyo ya Kuzaliwa husababishwa na nini?

Kwa wengi sababu huwa haijulikani. Ila huwa kuna vitu hatarishi ambavyo hupelekea kuongezeka kwa uwezekano wa kupata magonjwa ya moyo ya kuzaliwa nayo, vitu hivyo hatarishi ni:

  • Matatizo ya kijenetekia utotoni kama Downs syndrome, Turner’s syndrome, Marfan syndrome, 
  • Matumizi ya dawa ya kutibu chunusi (acne)  aina ya retinoic acid, madawa ya kulevya na unywaji wa pombe wakati wa ujauzito
  • Maambukizi ya virusi vya Rubella (German measles) kipindi cha kwanza cha ujauzito (1st trimester)

Kuna aina mbili za magonjwa ya moyo ya kuzaliwa

  • Cyanotic
  • Non-cyanotic

Cyanosis ni hali ya kuwa na rangi ya samawati (katika midomo,ulimi, ganja za mikono na miguuni) kutokana na kukosa oksijeni ya kutosha mwilini.

Cyanotic

Magonjwa ya moyo ya asili ambayo yanaangukia katika kundi hili ni pamoja na

  • Tetralogy of fallots
  • Transposition of great vessels
  • Tricuspid atresia
  • Total anomalous pulmonary venous return
  • Truncus arteriousus
  • Hypoplastic left heart
  • Pulmonary atresia
  • Ebstein anomaly

Non-cyanotic

Magonjwa ya moyo ya asili yaliyo kwenye kundi hili hujumuisha 

  • Ventricular septal defect (tundu katika kuta za ventrikali)
  • Atrial septal defect (tundu katika kuta za atria)
  • Patents ductus arteriousus 
  • Aortic stenosis
  • Pulmonic stenosis
  • Coarctation of the aorta
  • Atrioventricular canal (endocardial cushion defect)

Dalili za Magonjwa ya Moyo ya Kuzaliwa

Kwa ujumla, wagonjwa wa moyo wa asili huwa na dalili zifuatazo

  • Kupumua kwa shida 
  • Kushindwa kula vizuri
  • Matatizo ya ukuaji
  • Matatizo ya ukuaji wa misuli ya mikono na miguu
  • Maambukizi ya mfumo wa hewa
  • Cyanosis kwa aina ya kwanza(rangi ya samawati katika midomo,ulimi, viganja vya mikono na miguuni)
  • Ongezeko la sauti ya ziada katika sauti za moyo kutokana na tatizo (heart murmur)
  • Mabadiliko kwenye kucha hasa za vidole vya mikononi (digital clubbing)

Vipimo na Uchunguzi

Baadhi ya vipimo vinavyotumika kwa ajili ya uchunguzi wa magonjwa haya ni

  • Echocardiogram/transesophageal echocardiogram
  • Cardiac catheterization
  • Magnetic Resonance Imaging
  • Electrocardiogram
  • Chest x-ray

Matibabu

Matibabu hutegemea aina ya ugonjwa wa moyo wa kuzaliwa nao, hivyo hapa nitaelezea kwa kifupi ila, maelezo zaidi nitatoa katika makala zinazokuja za ugonjwa mmoja mmoja.

Aina nyingi za magonjwa haya huwa na madhara makubwa hivyo huhitaji upasuaji kurekebisha kasoro hizo, pamoja na matibabu ya dawa (diuretics ambazo husaidia kupunguza maji na chumvi mwilini, digoxin ambayo husaidia kuongeza nguvu katika mapigo ya moyo).

Vilevile kuna tiba nyengine ambayo badala ya upasuaji kitaalamu Transcatheter ambapo kifaa cha kufunga au kupachika huwekwa kwenye catheter maalumu ambayo hupita kwenye mishipa ya damu mpaka kwenye kasoro na kurekebisha kwa kuziba tundu nakadhalika.

 

Imesomwa mara 34068 Imehaririwa Jumatano, 12 Juni 2019 17:43
Dr.Mayala

Dr.Henry A Mayala ni daktari bingwa Wa Tiba ya moyo katika taasisi ya Jakaya Kikwete Cardiac Institute (JKCI), ambaye kwasasa anasomea shahada ya uzamivu (PhD) ya Tiba ya Moyo katika Chuo Kikuu cha Tongji  nchini China.

Anwani ya barua pepe hii inalindwa kutokana na spambots. JavaScript lazima iwe itawezeshwa kwa kuweza kuona.

Makala shabihana