Image

Dengue ni ugonjwa unaosababishwa na virusi viitavyo Dengue vinavyosambazwa na mbu aina ya Aedes . Mbu huyu anayeambukiza homa ya dengue hupendelea kuishi karibu na makazi ya watu na huweza kuuma binadamu mchana na usiku. Ugonjwa huu huathiri sana nchi za tropiko kama Amerika ya kusini na Africa. Ni moja kati ya homa kali inayodhoofisha na  kuambatana na maumivu makali. Kwa sasa, hakuna kinga ya homa ya dengue, njia pekee ya kuepuka ugonjwa huu ni kuzuia kuumwa na mbu anayesambaza homa ya dengue.

Je ni wapi homa hii upatikana zaidi duniani?

•India

•China

•Visiwa vya pasifiki

•Mexico

•Afrika

Dalili za homa ya dengue

•Homa kali ya ghafla

•Maumivu makali ya kichwa

•Macho kuuma

•Maumivu ya viungo

•Kichefuchefu

•Kutapika

•Vipele ambavyo hutokea siku nne baada ya homa kuanza

•Kutoka damu puani, kwenye fizi na kuchubuka kirahisi

Mara nyingi dalili huwa sio kali na wengi hudhania ni homa ya mafua au maambikizi mengine ya virusi. Dalili hizi huanza kutokea baada ya wiki mbili, lakini kwa wengi huchukua wiki moja ya kwanza na tayari utaanza kuona dalili za dengue.

Usonji ni tatizo linalojitokeza mapema utotoni, ambapo mtoto huwa na mapungufu kwa kupenda kujitenga na kutotaka kuwa karibu na watu (Impaired social interaction), hupata matatizo ya lugha na shida ya mawasiliano (impaired language and communication skills) na huwa na  tabia ya kurudia rudia kitu anachokifanya mara nyingi (restrictive repetitive behaviour).

Mara nyingi wazazi hugundua watoto wao wana tatizo hili katika kipindi cha  miaka miwili ya umri wa mtoto.Chanzo halisi cha tatizo hili la usonji hakijulikani ingawa  matatizo ya kijenetiki (Neurodevelopmental disorder) ndio uhusishwa na tatizo la usonji.Maaambukizi ya Rubella  au matumizi ya pombe na madawa ya kulevya aina ya coccaine wakati wa ujauzito na hata sababu za kimazingira, yote haya  uhusishwa na tatizo hili la usonji.

Watoto wa kiume huathirika sana ikilinganishwa na watoto wa kike. Kwa kila watoto watatu wa kiume wenye kupata usonji ni mtoto mmoja tu wa kike anaepata usonji.

Jarida la The Lancent la mwaka 2013, linasema watu wapatao milioni 21.7 wameathirika  kwa tatizo hili la usonji  ulimwenguni kote 1. Tabia za kujirudia rudia kwa mtoto aliyeathirika na tatizo la usonji zimegawanyika katika makundi yafuatayo;

  • Tabia zilizozoeleka - Kama  kupiga piga mikono, kutikisa tikisa kichwa mara kwa mara na kujibiringisha mwili
  • Tabia ambazo huchukua sana muda kama za kupanga panga vitu kwa mpangilio maalum au kuosha mikono mara kwa mara
  • Tabia ya kung’ang’ania vitu visihamishwe kwa mfano viti au kutokubali kukatizwa katizwa

Ugunduzi (Diagnosis)

Ugunduzi wa tatizo hili la usonji hufanyika kwa

  • Daktari wa watoto  (Pediatrician) kumpima vipimo vya kawaida pamoja  na kuchukua historia ya  ukuaji wa mtoto husika (Developmental milestones)
  • Daktari bingwa wa watoto aliyebobea kwenye matatizo ya kisaikolojia ya watoto (Pediatric neuropsychologists) kumpima ili kuangalia tabia za mtoto huyu  na uwezo wake wa kiakili (Cognitive skills)
  • Vipimo vya kijenitikia (genetics testing) kama high-resolution chromosome and  fragile X testing. Hufanyika baada ya   kugundulika kwamba chanzo cha  tatizo la usonji ni matatizo ya kijenetiki

Kadri mtoto anavyoendelea kukuwa ndio usonji unavyoweza kutambulika kwa urahisi zaidi kwani madhara yake yanaonekana kwa urahisi wakati wa  ukuaji wa kiakili wa mtoto.

Uchunguzi

Mchunguze mtoto wako kwa viashiria vya tatizo la usonji mapema zaidi kwani kumchelewesha mtoto mwenye usonji kupimwa na kupewa tiba mapema huchangia tatizo hili kuwa kubwa zaidi na hivyo kuathiri matokeo ya matibabu ya tatizo hili. Nusu ya wazazi hugundua watoto wao wana tabia zisizo za kawaida ndani ya miezi 18 ya umri wa mtoto, na moja ya tano ya wazazi hugundua ya kwamba watoto wao wana tabia zisizo za kawaida ndani ya kipindi cha miezi 24 ya umri wa mtoto 2.Tabia hizi ambazo si za kawaida katika ukuaji wa mtoto ni;

  • Kutotamka maneno ya kitoto (no babbling)  mpaka anapotimiza umri wa mwaka mmoja
  • Kushindwa kuotesha kidole au kumpungia (waving, gesturing etc) mzazi/mtu yoyote mkono mpaka anapotimiza umri wa miezi 12
  • Kushindwa kutamka neno lolote mpaka anapotimiza umri wa miezi 16
  • Kutotamka maneno mawili kwa pamoja au sentensi mpaka umri wa miezi 24
  • Kupoteza uwezo wa kuongea au kutokuwa na tabia ya kutangamana/kuchanganyikana na watu wengine wakati wowote ule katika umri wa mtoto

Matibabu

Familia yenye mtoto mwenye tatizo la usonji huhitaji kuelemishwa jinsi ya kuishi na mtoto huyo pamoja na kusaidiwa katika malezi yake. Kwa kuwa tatizo hili  halitibiki ni muhimu mtoto kupata:

  • Tiba ya Tabia
    • Uchambuzi wa tabia (ABA): Kutumia utaalamu wa kisaikolojia kufundishia na kuwahusisha na jamii, kuboresha mawasiliano, na usimamizi wa kitabia
    • Matibabu na elimu ya usonji kwa kuboresha mawasiliano kwa watoto wenye ulemavu (TEACCH)
  • Tiba nyingine muhimu ni kuelimisha jamii kuhusu watoto wenye usonji , jinsi ya kuishi nao na kuwaanzishia watoto wenye usonji matibabu mapema. 

 

Marejeo

  1. Global Burden of Disease Study 2013 Collaborators (2015)."Global, regional, and national incidence, prevalence, and years lived with disability for 301 acute and chronic diseases and injuries in 188 countries, 1990–2013: a systematic analysis for the Global Burden of Disease Study 2013."Lancet386: 743–800. doi:1016/S0140-6736(15)60692-4PMC 4561509PMID 26063472.
  2. Landa RJ (2008). "Diagnosis of autism spectrum disorders in the first 3 years of life". Nat Clin Pract Neurol. 4 (3): 138–47. doi:10.1038/ncpneuro0731PMID 18253102

Goita (Goiter) ni hali ya kuvimba kwa tezi ya thyroid. Uvimbe huu hautokani na saratani na kwamba goita si saratani. Tezi ya thyroid ipo sehemu ya mbele ya shingo. Kazi kuu za tezi ya thyroid ni kuzalisha homoni mbalimbali ambazo husaidia mwili kuthibiti na kufanya kazi zake mbalimbali.

Aina za goita na visababishi vyake

Kuna aina kadhaa za goita. Goita ya kawaida (simple goiter) inaweza kutokea bila kuwepo kwa chanzo chochote cha kueleweka. Wakati mwingine, yaweza kutokea wakati tezi ya thyroid inaposhindwa kuzalisha homoni/vichocheo vya kutosha vya thyroid kwa ajili ya mahitaji ya mwili. Ili kuweza kuendana na hali hii, tezi ya thyroid huongezeka ukubwa ili kufidia upungufu wa homoni za thyroid.

Kuna aina mbili za goita ya kawaida, Goita inayowapata wakazi wa eneo fulani (endemic goiter). Aina hii pia huitwa colloid goiter, na Goita inayotokea maeneo tofauti (sporadic goiter). Aina hii pia hujulikana kama nontoxic goiter.

Endemic goiter au colloid goiter huwapata makundi ya watu wanaoishi maeneo yenye udongo wenye upungufu mkubwa wa madini ya Iodine. Maeneo ya aina hii mara nyingi ni yale yaliyo mbali kutoka pwani ya bahari au yaliyo katika nyanda za juu kutoka usawa wa bahari kama vile mikoa ya Mbeya, Iringa na Rukwa. 

Iodine ni madini muhimu yanayohitajika katika utengenezaji wa homoni mbalimbali zinazozalishwa na tezi ya thyroid. Watu wanaoishi kwenye maeneo kama haya wapo katika hatari ya kupata goita kwa vile hawapati madini ya kutosha ya Iodine katika chakula chao.

Matumizi ya chumvi ziliongezwa madini ya Iodine yamesaidia sana kupunguza matatizo ya upungufu wa Iodine miongoni mwa watu wengi nchini Tanzania na duniani kwa ujumla. Hata hivyo, upungufu wa madini ya Iodine bado umeendelea kuzikumba sehemu nyingi za Afrika ya kati, Amerika ya kusini pamoja na Asia ya kati.

Chanzo cha sporadic goiter au nontoxic goiter bado hakifahamiki vema miongoni mwa wagonjwa wengi. Hata hivyo, matumizi ya baadhi ya dawa kama vile lithium pamoja na aminoglutethimide yameelezwa kuwa chanzo kimojawapo cha aina hii ya goita.

Ugonjwa wa vidonda vya tumbo hutokea iwapo kidonda cha ukubwa wa angalau wa nusu sentimita kitatokea kwenye sehemu yeyote ya ukuta wa tumbo au utumbo wa binadamu.

Kwa kawaida tatizo hili huleta maumivu makali sana ya tumbo ingawa si lazima kila maumivu ayapatayo mgonjwa husababishwa na vidonda vya tumbo. Aidha tafiti zinaonyosha takribani asilimia 70 za madoda ya tumbo hazionyeshi dalili yoyote. mara nyingi aina hii ya tukia (presentation) hupelekea madhara makubwa kwa ghufla kama madonda kutoa damu (bleeding) na matumbo kutoboka (perforation)

Tafiti zimeonesha kwamba karibu asilimia 70 mpaka 90 ya vidonda vya tumbo husababishwa na aina ya vimelea vya bakteria wajulikanao kama Helicobacter pylori. Aidha matumizi ya baadhi ya dawa za kutuliza maumivu za jamii ya Non Steroid Anti-inflamatory Drugs kama aspirin au diclofenac huweza kusababisha au kuongeza uwezekano wa kupata ugonjwa huu.

Kuna dhana iliyozoeleka kuwa vidonda vya tumbo huathiri zaidi mfuko wa kuhifadhia chakula yaani tumbo (stomach). Dhana hii si kweli kwani sehemu inayoathiriwa zaidi na tatizo hili ni sehemu ya kwanza ya utumbo mdogo ijulikanayo kama duodenum.

Ugonjwa wa kisukari ni ugonjwa tishio sana hasa kwa wale wanaougua ugonjwa huu kutokana kuwa na athari nyingi sana kama mgonjwa kupata kiharusi, kupoteza viungo mbalimbali  vya mwili kama vile kukatwa mguu/miguu, kidole/vidole na hata kupoteza uwezo wa kuona (diabetes retinopathy), na athari hizi hutokea endapo ugonjwa  wa kisukari haujadhibitwa vyema.

Ugonjwa huu wa kisukari unaweza usiwe ugonjwa  wa kutisha endapo tu mwenye kisukari ataweza kuishi kwa kujiamini na kujikubali, wataalam wanasema kuwa mtu kuishi na ugonjwa  huu wa kisukari anahitaji mambo makuu manne :-

Kujikubali

 Kujikubali ni jambo  muhimu sana, kutayarisha akili yako na kuikubali hali hiyo ya kuwa na  ugonjwa wa kisukari,na kuiambia akili yako kuwa ugonjwa huu hauponi ni hali ambayo itakuwepo katika umri wa maisha yako yote na kuwa tayari kubadili mfumo wako mzima wa maisha.Hii ni sawa na mtu aliyezaliwa upya.

Kubadili mfumo wa Ulaji

Ukijikubali kuwa una  ugonjwa wa kisukari ni rahisi sana kubadili mfumo wako mzima wa ulaji, hii inamaanisha kuwa mfumo wako wa ulaji unaweza kusababisha kupanda kwa sukari (glucose level) au kushuka kwa sukari. Ulaji wa vyakula vya wanga kwa wingi husababisha sukari kupanda. Kuacha kabisa ulaji na matumizi ya vitu ama vyakula vyenye sukari, kwa mfano soda, keki, barafu za sukari (ice cream), chokoleti n.k.

Pia kupunguza matumizi ya mafuta wakati wa uandaaji  wa chakula na kuacha matumizi ya vyakula vyenye mafuta mengi kwa mafano ulaji wa viazi vya kukaanga (chips), maandazi, vitumbua, n.k. Ulaji wa mboga za majani/salad/kachumbari kwa wingi ni muhimu sana. Sahani ya chakula itawaliwe na mboga za majani,na hii ni kwa kila mlo yaani chakula cha asubuhi,mchana na cha jioni.

Mazoezi ya Viungo

Mazoezi ni muhimu kwa afya, mazoezi huchangamsha mwili,hupunguza mapigo wa moyo na kuyafanya kuwa ya wastani pamoja na kuongeza mzunguko wa damu kwa mtu wenye ugonjwa kisukari (hivyo hupunguza hatari ya kupoteza kiungo cha mwili kwa mgonjwa wa kisukari kutokana kuwa na mzunguko mzuri wa damu kwenye viungo vyake), mazoezi yana nafasi kubwa sana kwa sababu husaidia kuyeyusha lehemu (cholesterol)  mwilini na kuondosha hatari ya kupata tatizo la kiharusi (stroke). Mazoezi yanayohitajika hapa ni yale ya kuchoma mafuta na sio ya kupanua misuli, mazoezi hayo ni kama kukimbia, kuruka kamba,kuogelea,kutembea kwa mwendo kasi. Mazoezi haya yafanyike kwa muda wa nusu saa au saa moja kila siku asubuhi au jioni.

Utangulizi

Saratani ya shingo ya kizazi ni saratani inayoongoza kwa kusababisha vifo vya wanawake wengi duniani. Inakadiriwa kuwa asilimia 85 ya vifo hivi hutokea katika nchi zinazoendelea. Kwa Tanzania, wastani wa wanawake 6,241 huugua saratani hii kila mwaka, ambapo 4,355 kati yao hufa, hii ni kwa mujibu wa ripoti ya shirika la afya duniani (W.H.O) ya mwaka 2010

Saratani ya shingo ya kizazi ndio saratani ya kwanza kwa wanawake nchini Tanzania, na Saratani namba moja kwa wanawake walio kati ya umri wa miaka 15 hadi 44. Tanzania ina wanawake milioni 10.97 walio na umri wa miaka 15 na kuendelea, ambao wako kwenye hatari kubwa ya kupata saratani hii. Kwa afrika mashariki, asilimia 33.6 ya wanawake wote, wanasadikiwa kuwa na virusi aina ya human papilloma virus ambavyo ndio visababishi vya ugonjwa huu.

Je nini kinasababisha saratani ya shingo ya kizazi?

Maambukizi ya human papilloma virus ndio yanayosababisha saratani ya shingo ya kizazi. Kuna zaidi ya aina 150 ya virusi hivi vya human papilloma virus, ambapo aina tatu (yaani ainaya 26,53,66) ndio venye hatari sana ya kusababisha ugonjwa huu, aina ya 16 na 18 ndivyo vinavyojulikana kusababisha zaidi ya asilimia 70 ya ugonjwa wa saratani ya shingo ya kizazi. Virusi hivi huambukizwa kwa njia ya kujamiana au kugusana kwa ngozi ya mtu mmoja na mwengine, na huambukiza wanaume na wanawake.

Vihatarishi vya saratani ya shingo ya kizazi

  • Kuanza kufanya ngono mapema – Wanawake wanaoanza kujamiana wakiwa na umri wa miaka 16 wako kwenye hatari baadae kupata saratani ya shingo ya kizazi.
  • Kuwa na wapenzi wengi – Mwanamke mwenye wapenzi wengi au mwenye mwanamume mwenye wapenzi wengi yupo kwenye hatari ya kupata ugonjwa huu. Utumiaji wa kondomu hupunguza hatari ya kupata saratani hii, lakini ikumbukwe ya kwamba kondomu sio kinga ya ugonjwa huu.
  • Maambukizi ya human papilloma virus
  • Uvutaji sigara – Kemikali zilizopo kwenye sigara huchanganyikana na seli au chembechembe za shingo ya kizazi hivyo kuleta mabadiliko katika shingo ya kizazi hatimaye kusababisha saratani.
  • Utumiaji wa vidonge vya kupanga uzazi kwa muda mrefu hasa wale wanaotumia kwa zaidi ya miaka mitano (miaka 5)
  • Ugonjwa wa genital warts ( dalili ni matezi na muda mwingine vidonda katika sehemu ya siri ya mwanamke). Hii husababishwa na virusi vya human papilloma virus.
  • Lishe duni au utapia mlo
Ugonjwa wa uti wa mgongo hutokea iwapo utando unaofunika ubongo na uti wa mgongo utapatwa na maambukizi.

Ugonjwa wa Uti wa mgongo husababishwa na nini?

Ugonjwa huu husababishwa na vimelea mbalimbali vya makundi ya bakteria, virus na hata fungus. Tukivigawanya visababishi hivi katika makundi haya, tutaona kuwa bakteria wanaosababisha ugonjwa wa uti wa mgongo ni kama vile; bakteria wajulikanao kama Beta-streptococci, Hemophilus influenza, Escherichia coli, Listeria monocytogenes, Neisseria meningitides, Streptococci pneumoniae pamoja na Mycobacteria tuberculosis, ambao pia ni maarufu kwa kusababisha ugonjwa wa kifua kikuu.

Aidha kutoka kundi la virus, virus wanaojulikana kwa kusababisha ugonjwa huu wa uti wa mgongo ni pamoja na Herpes simplex type 2, HIV pamoja na Varicella zoster.

Vimelea vya fungus ambavyo hujulikana kwa kusababisha ugonjwa wa uti wa mgongo ni pamoja na wale wajulikanao kama Coccoidiodomycosis pamoja na Cryptococci meningetides.

Dalili za ugonjwa wa uti wa mgongo

Dalili na viashiria vya uti wa mgongo ni pamoja na

  • Shingo kukakamaa na kuwa ngumu isivyo kawaida
  • Mgonjwa kujihisi homa kali
  • Maumivu makali ya kichwa
  • Mgonjwa kupoteza fahamu
  • Mgonjwa kupatwa na degedege (seizures) na mwili kukakamaa
  • Mgonjwa kushindwa kuvumilia mwanga (photophobia)
  • Mgonjwa kutoweza kukaa sehemu yenye makelele (phonophobia)
  • Kwa watoto, kuvimba utosi

Aidha, wakati wa kumfanyia mgonjwa uchunguzi, daktari anaweza kuangalia pia viashiria vingine vinavyoonesha kuwepo kwa ugonjwa wa uti wa mgongo. Ishara hizi ni kama vile

  • Mgonjwa uhisi maumivu kwenye uti wa mgongo yanayozuia kukunjua goti wakati anapofanyiwa uchunguzi wa kukunjua goti lake (pain limits passive extension of the knee). Ishara hii huitwa ishara ya Kerning au Kerning's sign.
  • Wakati mwingine mgonjwa anapoelekezwa kujitahidi kukunja shingo, miguu (yaani paja pamoja na goti) navyo hujikunja pia (flexion of the neck causes involuntary flexion of the knee and hip). Ishara hii huitwa ishara ya Brudzinski au Brudzinski’s sign.

Matokeo haya yaliyochapishwa kwenye jarida la utafiti wa kisayansi la Cell Regeneration, yalionyesha kuwa mkojo unaweza kutumika kuunda celi ambazo zinaweza kutumika kukuza vimelea vinavyofanana kama meno.

Wanasayansi kutoka China waliofanya utafiti huo wanatumai kuwa utafiti huu unaweza kutumika kuwapa watu wasio na meno fursa ya kuwa nayo.Hata hivyo watafiti wa celi za mwili, wanaonya kuwa utafiti huu unakabiliwa na changamoto nyingi.

Vikundi vya wanasayansi kote duniani wanatafuta mbinu za kukuza meno kwa njia ya mahabara ili kukabiliana na tatizo la wazee kung'oka meno na hata wale wanaong'oka meno kutokana na afya mbaya.
Seli zijulikanazo kama Stem cells ambazo wanasayansi wanaweza kutumia kukuza aina yoyote ya seli, hutumika sana katika sekta ya utafiti. Wanasayansi wa China waliofanya utafiti huo, walitumia mkojo wa binadamu, mwanzoni mwa utafiti wao.

Mojawapo kati ya magonjwa yanayohusishwa na umaskini na uchafu wa kupindukia ni ugonjwa wa Kipindupindu. Inaripotiwa kuwa Kipingupindu ni miongoni mwa magonjwa ambayo huathiri jamii maskini zaidi kwa kiasi kikubwa hasa hasa kwenye nchi zinazoendelea, kiasi kwamba Shirika la Afya Duniani (WHO) limeuweka ugonjwa huu kama mojawapo ya viashiria vya maendeleo ya jamii husika. Nchini Tanzania hususani katika jiji la kibiashara la Dar es Salaam, haishangazi basi kusikia kila mwaka kuna mlipuko wa ugonjwa huu pamoja na juhudi kubwa za serikali na mamlaka zake kujitahidi kuhimiza wananchi kupambana na ugonjwa huu.

Kwanini nchi zinazoendelea?

Moja wapo ya changamoto zinazokabili nchi zinazoendelea ni jamii kutokuwa na uhakika wa kupata Maji safi na salama, pamoja na kutokuwa na mazingira safi kwa ujumla. Ndio maana mpaka leo nchi zinazoendelea ndizo zinazokumbwa na mlipuko wa kipundupindu au huwa katika hatari ya mlipuko wa ugonjwa huo.

Prostatitis ni ugonjwa unaosababishwa na maambukizi  ya vimelea vya bakteria katika tezi dume (prostate) kwa wanaume.

Kuna aina kuu nne za ugonjwa huu wa prostatitis

1. Maambukizi ya ghafla ya tezi dume (Acute bacterial prostatitis)

2. Maambukizi sugu ya tezi dume (Chronic bacterial prostatitis)

3. Chronic prostatitis without infection/Chronic pelvic pain syndrome/chronic non bacterial prostatitis

4. Asymptomatic inflammatory prostatitis 

Tuangalie aina moja baada ya nyingine za ugonjwa huu 

Maambukizi ya ghafla ya tezi dume (Acute bacterial prostatitis)

Ni maambukizi ya tezi dume yanayosababishwa na vimelea vya bakteria aina ya E.coli, Klebsiella, Proteus, Pseudomonas, Enterobacter, Staphylococcus aureus, Enterococcus, Serratia na vimelea vinavyosababisha magonjwa ya zinaa. Maambukizi haya yanaweza kufika katika tezi dume moja kwa moja kupitia kwenye damu, au kutoka kwenye kiungo kilicho na maambukizi karibu na tezi dume au huweza kufika kwenye tezi dume kutokana na athari za kufanyiwa kipimo cha kuchukua nyama ya tezi dume kuipeleka  maabara kwa uangalizi zaidi au kwa lugha ya kitaalamu tunaita prostate biopsy. 

Dalili na viashiria vya maambukizi ya ghafla ya tezi dume

     - Homa

     - Kuhisi baridi

     - Kutetemeka kutokana na baridi

     - Maumivu chini ya mgongo 

     - Maumivu katika maeneo ya sehemu za siri

     - Kupata haja ndogo /kukojoa mara kwa mara

     - Kupata haja ndogo wakati wa usiku inayomfanya mtu kushindwa kuivumilia na hivyo kukimbia chooni

     - Maumivu/kichomi wakati wa kukojoa/haja ndogo

     - Maumivu ya mwili mzima

Ukurasa 8 ya 11