Image

Katika hali isiyokuwa ya kawaida, wanaume wawili ambao walikuwa na maambukizi ya ugonjwa wa HIV huko nchini Marekani wameweza kuacha kabisa  kutumia dawa za kurefusha maisha yaani ARV’S   ambazo hupewa wagonjwa wa HIV baada ya kufanyiwa upandikizaji wa uboho (bone marrow transplant) katika mifupa yao.

Wanaume hao ambao walikuwa na ugonjwa wa HIV kwa miaka 30, walikuwa wakipewa tiba ya upandikizaji wa uboho kutokana kuugua saratani ya damu (Leukemia). Mmoja wa wanaume hao ameacha kutumia dawa hizo za kurefusha maisha miezi minne iliyopita na mwingine ameacha kuzitumia wiki saba zilizopita.

 Wanasanyansi katika chuo kikuu cha Saskatchewan cha nchini Canada wamesema ya kwamba manii(semen) yanayotolewa na mwanamume wakati wa kujamiana na mwanamke yanasaidia mwanamke kuwa na uwezo wa kushika mimba. Kulingana na utafiti mpya uliofanywa na watafiti wa kimataifa chini ya Gregg Adams na kuchapishwa katika jarida la proceedings of the National Academy of Sciences, umesema ya kwamba manii sio tu hubeba shahawa (sperm) za mwanamume kwenda kwa mwanamke bali pia huchochea mayai ya mwanamke (ovaries) kutoa mayai ya uzazi.

Protini inayopatikana katika shahawa inayojulikana kama Ovulation-Inducing Factor au IFO, ndio hasa huchochea sehemu ya ubongo inayojulikana kama hypothalamus kwenye ubongo wa mwanamke kutoa homoni ambazo hupelekwa moja kwa moja kwenye mfumo wa neva na kisha homoni hizo hupelekwa kwenye mfumo mwingine wa homoni unaojulikana kama endocrine system.

Homoni  hufika kwenye mfumo huu wa endocrine system kupitia sehemu ya ubongo inayojulikana kama pitituary gland na hivyo kuingia kwenye mzunguko wa damu.Baada ya kufika wenye mzunguko wa damu, homoni hizi huenda moja kwa moja mpaka kwenye mayai ya mwanamke (ovary) na  kuyachochea mayai haya  kutoa mayai ya uzazi(ovum) katika hatua inayojulikana kama ovulation.

Watafiti hao wamesema wamegundua protini hii aina ya IFO katika shahawa za wanyama aina ya ilamas, sungura na hata kwa binadamu. Wanyama wengi wana viungo vya ziada vya kujamiana ambavyo hutoa manii kwenda kwenye shahawa lakini umuhimu wa manii hayo bado haujagundulika. “Wazo la kuwa kuna chembechembe katika manii ya wanyama na binadamu ambayo huchochea ubongo wa mwanamke ni wazo geni kabisa, alisema Gregg Adams”.
Wanasayansi hao wameweza kugundua ya kwamba ni chembechembe hizi ndizo pia husaidia katika ukuaji, urekebishaji na ustawishaji wa seli za neva.
 
Katika utafiti huu ambao wanasayansi walitumia ngombe, ilamas na binadamu, wanasayansi hao waliweza kugundua protini aina ya Ovulation-Induced-Factor kutoka katika manii ya wanyama hawa pamoja na binadamu waliohusika katika utafiti huu. Wanasayansi hao waliwachoma sindano yenye protini hii wanyama aina ya ilamas na kuwafanya wanyama hao kupata ovulation wakati walipowachoma ngombe sindano yenye protini hii aina ya IFO, ngombe hao walishindwa kuingia katika ovulation lakini protini hiyo iliweza kuwafanya ngombe kutengeza mifuko kwenye mayai yao ambayo ndio hasa hubeba mayai ya uzazi na hivyo kuwafanya ngome kuwa tayari kwa kushika mimba.Pia ilionekana ya kwamba protini hii (IFO) ina uwezo wa kustawisha mimba kwa ngombe hawa.
 
“Utafiti huu mpya unaongeza uelewa wetu wa mfumo wa ovulation lakini pia huongeza maswali mengi juu ya ovulation hiyo’, alisema Adams”
Tafiti zaidi zinahitajika ili kujua ni kazi gani ambayo protini hii aina ya IFO hufanya katika kumpa mtu uwezo wa kutunga au kushika mimba.Wanasayansi hao wanahisi uwepo wa protini hii kwa wingi kwa baadhi ya wanaume inawezekana ikawa ndio chanzo cha kuwafanya wanaume hao kuwa na uwezo mkubwa wa kutungisha  mimba mwanamke (fertile).
 
Ovulation ni hatua ambayo yai la uzazi hutolewa na kwenda katika mfuko wa uzazi (uterus) na kusubiri shahawa ili lirutubishwe na kuwa mimba.Ovulation hii hutokea siku ya 14 baada ya mwanamke ya  kuanza hedhi yake.Yai la uzazi ambalo hutolewa wakati huu hukaa kwa masaa 48 kusubiri kurutubishwa na kama halitarutubishwa na shahawa basi yai hili huharibika na kutolewa nje kama hedhi.Ni katika ovulation, ndio mwanamke huwa na uwezo/asilimia kubwa ya kushika ujauzito kama atajamiana na mwanamume.
 
Dalili za ovulation ni pamoja na kichwa kuuma, kizunguzungu, kichefuchefu, matiti kuuma, kuongezeka kwa kiwango cha joto mwilini, kutokwa jasho kwa wingi usiku, kubadilika  ladha ya ulimi, kuwa na hasira mara kwa mara, kupata hamu ya kujamiana, kutokwa na ute katika tupu ya mwanamke ,maumivu ya tumbo, maumivu ya mgongo na nk.

 Tatizo la kuota matiti kwa wanaume na watoto limekuwa kubwa sana katika dunia ya leo. Inawezekana kabisa wakati unatembea njiani ukaona wanaume au watoto wadogo wa kiume wakiwa na matiti makubwa  ambapo watu wengi  huchukulia kama ni kawaida. Kitaalamu gynecomastia ni kukuwa kuliko kawaida yake kwa tishu ya kwenye titi inayojulikana kama glandular tissue. Tatizo hili huonekana sana kwa watoto wachanga na  wanaume waliokatika umri wa kubaleghe, lakini pia huonekana kwa watu wazima na wazee.

Ukubwa wa tatizo (epidemiology)
Asilimia 60-90 ya watoto wachanga wanapata tatizo hili la kukuwa kwa matiti kwa mpito linalojulikana kitaalamu kama transient gynecomastia kutokana na kuwepo kwa kichocheo cha aina ya estrogen kwa wingi wakati wa ujauzito wa mama. Kati ya asilimia 4-69 ya vijana walio katika umri wa kubaleghe  imeonekana wanapata tatizo hili kutokana na  kuwepo kwa wingi kwa kimengenyo aina ya estradiol.Mara nyingi huonekana katika umri kati ya miaka 10-12 na hupotea taratibu ndani ya miezi 18, si kawaida yake kuonekana kwa vijana walio na umri ya zaidi ya miaka 17.
 
Asilimia 24-65 ya watu wazima hupatwa na tatizo hili, hii hutokana na kubadilishwa  kwa wingi kwa kichocheo aina ya testerone kuwa estradiol na kutolewa kwa uchache kwa kichocheo hiki cha testerone kutoka kwenye korodani zinazoanza kuzeeka..Ikumbukwe ya kwamba kichocheo hiki testerone hutengenezwa katika korodani za mwanamume.
 
Nini hutokea?(Pathofiziolojia)  
Kuongezeka ukubwa wa matiti kwa wanaume hutokana na kuharibika kwa mfumo wa vichocheo unaojulikana kama estrogen-androgen balance na hivyo kusababisha estrogen kutolewa kwa wingi ama kuongezeka kwa msisimko (sensitivity) wa matiti kwa kiwango cha zaidi ya kawaida kwa kichocheo aina ya estrogen kilicho kwenye mzunguko wa damu.
 
Estrogen husababisha chembechembe zinazojulikana kama ductal epithelia kuongezeka kwa wingi, kurefuka (ductal elongation) na kugawanyika, kuongezeka kwa chembechembe za mafuta (ductal fibroblasts) na kuongezeka kwa mfumo wa damu kwenye matiti (increase vascularity).Estrogen hutengenezwa kutoka kwenye vichocheo vya testerone na androgen kwa kutumia kimengenyo kinachojulikana kama aromatase.

Mrija wa mkojo (urethra) ni kiungo muhimu kinachotoa mkojo nje ya mwili kutoka kwenye kibofu. Mrija huu unaposinyaa au kuziba hufanya utokaji wa mkojo kuwa wa mashaka na maumivu makubwa. Kusinyaa/ Kuziba kwa mrija wa mkojo huitwa pia urethral stricture.  

Visababishi na vihatarishi vya tatizo hili

Kusinyaa kwa mrija wa mkojo husababishwa na kovu linalotokea katika sehemu ya mrija baada ya mtu kuumia, kufanyiwa upasuaji au kupona magonjwa ya zinaa. Inaweza pia kusababishwa na uvimbe karibu na eneo la kinena unaokandamiza mrija.

Vihatarishi vya tatizo hili ni pamoja na

  • Kuwa na historia ya kuugua magonjwa ya zinaa
  • kuwahi kuwekewa mipira ya mkojo au vifaa vya namna hiyo (catheter au cystoscope)
  • Kuvimba tezi dume (BPH) kwa wanaume
  • kuwa na historia ya kuumia au kupata majeraha maeneo ya kinena. Hii hutokea sana kwa wale wanaopata ajali wakiendesha baiskeli
  • Kupata maambukizi ya mara kwa mara ya mrija wa mkojo (urethritis)

Ni nadra sana kwa tatizo hili kutokea kwa wanawake. Aidha ni nadra pia kwa mtoto kuzaliwa akiwa na tatizo hili (congenital urethral stricture). 

Dalili

Mtu mwenye tatizo hili anaweza kuwa na dalili zifuatazo,

  • Kutoa shahawa zilizochanganyika na damu
  • Kukojoa mkojo mweusi au uliochanganyika na damu
  • Kupungua kwa kiasi cha mkojo kinachotolewa
  • Kukojoa kwa shida
  • kutoa uchafu katika mrija wa mkojo
  • kukojoa mara kwa mara
  • Kushindwa kumaliza mkojo wote
  • Kushindwa kuhimili kutoka kwa mkojo (mkojo kujitokea wenyewe/kujikojolea)
  • Maumivu wakati wa kukojoa
  • Maumivu chini ya tumbo
  • Maumivu ya kinena
  • Mtiririko dhaifu wa mkojo (hutokea taratibu au ghafla)
  • Mkojo kutawanyika ovyo wakati wa kukojoa
  • Kuvimba uume

Uchunguzi

Daktari atakufanyia uchunguzi wa mwili na namna unavyokojoa. Uchunguzi wa mwili unaweza kuonesha:

  • Kupungua kwa mkondo wa mkojo
  • Uchafu kutoka katika mrija wa mkojo
  • Kibofu kilichojaa/kuvimba
  • Kuvimba kwa mitoki ya maeneo ya kinena
  • Tezi dume iliyovimba au yenye maumivu
  • Kuhisi kitu kigumu chini ya uume
  • Uume kuvimba au kuwa mwekundu

Hata hivyo, wakati mwingine uchunguzi unaweza usioneshe tatizo lolote lile.

Vipimo

Vipimo ni pamoja na

  • Kipimo cha kuchunguza mrija pamoja na kibofu cha mkojo (cystoscopy)
  • Kuangalia kiasi cha mkojo kinachobaki katika kibofu baada ya kukojo (Post-void residual (PVR) volume)
  • X-ray ya mrija wa mkojo (Retrograde urethrogram)
  • Vipimo vya magonjwa ya zinaa
  • Uchun

Matibabu

Mrija unaweza kutanuliwa wakati wa kipimo cha cystoscopy na hiyo ikawa ndiyo mojawapo ya tiba.
Iwapo njia ya kutanua mrija haioneshi mafanikio sana, upasuaji unaweza kuhitajika. Upasuaji unategemea eneo lilipo tatizo na ukubwa wa tatizo. Kama tatizo ni dogo/fupi na lipo mbali na bawabu inayotenganisha mrija na kibofu cha mkojo, linaweza kutatuliwa kwa kukata kasehemu kalikoziba wakati wa kufanya cystoscopy au kwa kuweka kifaa maalum cha kuzibua na kutanua mrija.

Kama tatizo ni kubwa zaidi, upasuaji wa wazi wa eneo husika unaweza kufanyika. Upasuaji huu unajumisha kukata sehemu iliyoziba na kisha kukarabati sehemu hiyo.

Kwa mgonjwa ambaye amepata shida ya ghafla ya kushindwa kutoa mkojo (acute retention of urine), matibabu ya dharura ya kumuwekea catheter kupitia juu ya kinena (suprapubic catherization) hufanyika. Hii husaidia kibofu kutoa mkojo nje kupitia kwenye bomba lililowekwa chini ya tumbo.

Ifahamike kuwa mpaka sasa hakuna dawa ya tatizo hili zaidi ya njia za upasuaji na nyingine zilizoelezwa hapo juu. 

Matarajio

Mara nyingi matibabu huleta matokeo mazuri na mgonjwa anaweza kuishi maisha yake kama kawaida. Hata hivyo wakati mwingine, mgonjwa anaweza kuhitaji matibabu ya mara kwa mara ili kuondoa sehemu ya kovu iliyopo katika mrija wa mkojo. 

Madhara ya tatizo hili

Tatizo hili halina budi kutibiwa haraka maana kama likiachwa linaweza kusababisha kuziba kabisa kwa njia ya mkojo na kusababisha mkojo kujaa katika kibofu, hali ambayo, pamoja na kuleta maumivu makali kwa mgonjwa inaweza pia kusababisha figo kushindwa kufanya kazi (ARF).

Kinga

Ni muhimu kujikinga dhidi ya magonjwa ya zinaa kwa kufanya ngono salama au kuacha kabisa kufanya ngono. Aidha kuwa makini na kazi au mambo ambayo yanaweza kukusababishia kuumia maeneo ya kinena.

 

Katika zama hizi za utandawazi na muingiliano baina ya tamaduni zetu za asili na tamaduni za kimagharibi, imekuwa ni kawaida kwa vijana wa rika tofauti na jinsia zote kutoga ulimi, mdomo, kitovu ama kivimbe cha nyusi kwa sababu tofauti tofauti sana.

Hivyo basi, ni muhimu sana kufahama ukweli kuhusu faida ama hasara za kutoga ulimi ama mdomo kabla hujatekeleza azma yako ya kutoga viungo hivi vya mwili.

Kutoga Ulimi ama Mdomo kunaweza kukusababishia madhara yasiyotarajiwa

Matokeo mazuri zaidi ya kutoga ulimi ama mdomo ni kutokutokea kwa kidonda ama kivimbe, wakati matokeo mabaya kutokea kwa baadhi ya watu ni pamoja na kuvunjika kwa meno/jino, kuvuja kiasi kikubwa cha damu, ama maambukuzi ya bakteria kwenye kidonda. Kutoga ulimi hujumuisha kutumika kwa sindano inayopenyezwa katikati ulimi ili kupitisha na kuhifadhi kipini, ama ndoana ama hereni ya urembo. Kazi hii ya kutoga ulimi mara nyingi ganzi huwa haitumiki. Baada ya kutoga, kuvimba kwa ulimi na maumivu ya muda hutokea.

Madhara ya kutoga Ulimi

  • Kuvuja damu kiasi kidogo hutarajiwa, kuna hatari ya mishipa ya damu kuharibiwa wakati wa kutoga ulimi, hali inayoweza kusababisha kuvuja damu kwa kiasi kikubwa kuliko ilivyotarajiwa.
  • Ingawa kuvimba kwa ulimi kunatarajiwa baada ya kitendo cha kutoga ulimi, wakati mwingine ulimi huvimba kwa kiasi cha kuziba kwa njia ya hewa. Kuziba kwa njia ya hewa kunaweza kusababisha kifo.
  • Ikiwa fundi wako wa kutoga ulimi hana uzoefu wa kutosha kufanya kazi hiyo, anaweza kuharibu mishipa ya fahamu ya ulimi hivyo kuharibu uwezo wa ulimi kuhisi/kutambua hisia za joto,baridi ama ladha ya chakula na vinyaji, vile vile kuathiri mienendo ya viungo vya eneo la kinywa na uso. Kwani nyuma ya ulimi kuna mishipa ya fahamu,mishipa hii ikiharibiwa ulimi utapooza hivyo kusababisha ganzi la kudumu, kuathirika kwa uwezo kuongea na kushindwa kutambua ladha za chakula/vinywaji
  • Vilevile kutoga ulimi kunakuweka kwenye hatari ya kupata maambukizi kwenye ulimi hasa ikiwa hutaweza kutunza hali ya usafi wa kinywa na meno kila wakati, hivyo kusababisha wadudu jamii ya bakteria kupenya na kuingia ndani ya ulimi na kusababisha maambuzi kwenye ulimi.
  • Hali ya kutoga ulimi inapodumu kwa muda mrefu, inaweza kusababisha nyufa kwenye meno, ama kuvunjika kwa nyuso za jino/meno kwa sababu ya msuguano wa muda mrefu kati ya jino/meno na hereni/kipini ama ndoana ya chuma/plastiki iliyohifadhiwa kwenye ulimi kwa muda mrefu. Nyufa hizi kwenye meno, kwa kawaida husababisha maumivu makali ya jino/meno. Hivyo basi meno haya yenye nyufa yanaweza kutibiwa kwa kuvalishwa kofia “ dental crown”. Si kawaida kupata magonjwa ya fizi ama kuta za ndani za shavu ikiwa umetoga ulimi na unatunza afya ya kinywa na meno vizuri.

Kutoga Mdomo

Kutoga mdomo ni pale pete ya urembo inapovalishwa ama kuhifadhiwa ndani ya mdomo. Majeraha ya kutoga mdomo hupona haraka zaidi, hata hivyo unapaswa kutunza kidonda cha jeraha hili kwa umakini mkubwa wakati wa kupona. Vyakula, vinywaji na moshi wa sigara vinapofikia kidonda hiki, vinaongeza hatari ya kupata maambukizi kwenye kidonda.

Kishikizo vishikizo vya pete hii ya urembo kinaweza kusababisha vidonda kwenye fizi ama kuharibu jino. Kwa baadhi ya watu, tiba ya kupandikiza fizi hutumika kurejesha fizi zilizoathirika. Kama ilivyo kwa kutoga ulimi, kutoga mdomo pia kunaweza kuathiri mshipa wa fahamu hivyo kuathiri mienendo ya misuli  ya kwenye eneo la kinywa na mdomo.

Je, una mpango wa kutoga Ulimi ama Mdomo?

Ikiwa unapanga kutoga viungo hivi vya mwili, unashauriwa ufanye mambo yafuatayo yatakayo kuwezesha kupata huduma ambayo haita athiri afya yako:

  • Hakikisha ngariba mtoga ulimi ama mdomo sio tu ana uzoefu wa kutosha kwenye kazi anayofanya, bali pia anazingatia usafi kufanya kazi zake.
  • Nenda hospitali kupata ushauri tiba mara tu unapoona ama maumivu ni makali sana, kuvimba kwa ulimi ama damu zinavuja kwa muda mrefu (zaidi ya dakika 30) ama ikiwa jeraha linapata maambukizi ya bakteria.
  • Unapokuwa na hereni, pete ama ndoana ya urembo kwenye ulimi ama mdomoni, unashauriwa kumwona daktari wa kinywa na meno kila baada ya miezi sita (6). Daktari wa meno atafanya kazi ya kuhakiki ikiwa kidude kilichovalishwa kina madhara kwenye meno ama fizi, hivyo kudhibiti athari zinazoweza kutokea kwa kutoga ulimi ama mdomo.
  • Wana michezo wanashauriwa kutovaa hereni, pete ama ndoana ya urembo iliyopo kwenye ulimi ama mdomoni wanapokuwa mchezoni, kwani vyombo hivi vya urembo vinaweza kunasa kwenye ngozi bila kutarajia hivyo kusababisha madhara yasiyotarajiwa.

Utafiti uliofanywa na chuo kikuu cha State University cha Jijini New York nchini Marekani umesema ya kwamba manii ni nzuri kwa wanawake kwani huwaondolea msongo wa mawazo.Pia watafiti hao wamesema wanawake wanaofanya tendo la ndoa mara kwa mara bila kutumia kinga (mapenzi salama) wanakuwa na kiwango idogo cha msongo wa mawazo na hufanya vizuri katika vipimo vya akili.

Hali hii wamesema inatokana na manii kuwa na kemikali ambazo humfanya mtu kuwa vizuri kihisia, huongeza upendo/unyenyekevu, huchochea mtu kupata usingizi na huwa na angalau aina tatu za kemikali za kuondoa msongo wa mawazo (anti-depressants).
Utafiti huo uliofanywa kwa kuwahoji wanawake 293 kwa kufuatilia maisha yao ya kujamiana dhidhi ya afya za akili zao (mental health).Manii huwa na mchanganyiko wa kemikali aina ya cortisol ambayo huongeza upendo, kemikali aina ya esterone na oxytocin ambazo zote humfanya mtu kuwa vizuri  kihisia (elevates mood).
Pia huwa na homoni aina za thyrotropin releasing hormone ambayo huondoa msongo wa mawazo, melatonin ambayo huchochea usingizi na serotonin homoni inayoondoa msongo wa mawazo.
Kutokana kuwepo kwa mchanganyiko wa kemikali na homoni hizo kwenye manii, watafiti  Gallup na Burch pamoja na mtaalamu wa saikolojia  Steven Platek wamesema ya kwamba wanawake ambao hujamiana na wanaume bila kinga yoyote (mapenzi salama) wana asilimia ndogo ya msongo wa mawazo tofauti na wale wasiojamiana.
Matokeo muhimu ya utafiti huu ambao umechapishwa katika jarida la Archives of Sexual Behavior ni kwamba hata baada ya baadhi ya watafitiwa kuongeza kiwango chao cha kujamiana, wale ambao walikuwa hawatumii kinga yoyote walikuwa na kiwango kidogo cha msongo wa mawazo tofauti na wale ambao walikuwa wakitumia kinga kama kondomu wakati wa kujamiana.Pia wanawake hawa ambao hawakutumia kinga walikuwa na kiwango kidogo cha msongo wa mawazo tofauti na wale ambao hawakushiriki tendo la ndoa kabisa.
Hata wale wanawake ambao ni wasagaji na wana wapenzi wengi pia wameonekana kuwa na kiwango kikubwa cha msongo wa mawazo  kama wale wanawake ambao hawakushiriki tendo la ndoa kabisa.
Watafiti hao wamesema sio tu kujamiana huongeza furaha kwa mwanamke na hivyo kumuondolea msongo wa mawazo bali kiwango cha furaha pia huendana na wingi wa manii katika mili yao.
Utafiti huu usiwe chanzo cha watu kufanya mapenzi bila kinga bali uwe chanzo cha ufanya mapenzi salama na mwenza unayemuamini.Pia tunakemea na kupinga wale wote wanaofanya vitendo vya usagaji kwani ni hatari kwa afya zao kwani ni chanzo kimojawapo cha magonjwa ya akili.Tutakuletea makala ya uhusiano kati ya usagaji na ugonjwa wa akili.
 
Tete kuwanga ni ugonjwa  ambao unaombukiza na kusababishwa na virusi vinavyojulikana kama Varicella zoster virus.Maambukizi ya tete kuwanga huonekana sana kwa watoto wadogo ingawa hata watu wakubwa pia hupata maambukizi ya ugonjwa huu. Tete kuwanga hupatikana duniani kote.Katika nchi zenye kupata majira ya baridi, maambukizi ya ugonjwa huu huonekana sana wakati wa kipindi cha majira ya baridi na kipindi cha masika. 
 
Watoto walio na umri wa miaka 4-6 wako kwenye hatari kubwa ya kupata maambukizi ya tete kuwanga na ndio katika umri huu ambapo maambukizi ya ugonjwa huu yapo kwenye kiwango cha juu sana.Inakadiriwa ya kwamba, tete kuwanga huambukiza kwa kiwango cha asilimia 90.
 
Watoto wengi hupata maambukizi ya tete kuwanga kabla ya kufikia umri wa kubaleghe ingawa asilimia 10 ya vijana bado wanakuwa kwenye hatari ya kupata maambukizi ya tete kuwanga. Katika nchi za tropiki,maambukizi ya tete kuwanga huonekana kwa watu wakubwa na  huenda yakawa maambukizi ya hatari sana.

Maambukizi ya tete kuwanga hupatikana vipi?

Tete kuwanga huambukizwa kupitia njia ya hewa au endapo mtu atagusana mwili na mgonjwa wa tete kuwanga(kupitia majimaji yanayotoka kwenye vipele vya mgonjwa).Mtu yoyote yule anaweza kuambukizwa ugonjwa huu kutoka kwa mgonjwa wa tete kuwanga kwa njia ya kucheka, kupiga chafya, kukohoa .Hii inatokana na kusambazwa kwa virusi ya Varicella zoster kwa njia ya hewa pindi mgonjwa anapocheka,kupiga chafya au anapokohoa.
Nini hutokea kipindi cha maambukizi (Pathofiziolojia)
 
Maambukizi ya tete kuwanga kwa mtoto husababisha mtoto kutoa kinga aina ya Immunoglobulin G (IgG), Immunoglobulin M, (IgM) na Immunoglobulin A,(IgA). Kinga hizi  pamoja na kinga zinazosaidiwa na chembechembe za mwili (Cell mediated responses)husaidia kupunguza madhara na urefu wa maambukizi haya ya awali ya tete kuwanga.Immunoglobulin G hubakia kipindi chote cha maisha na huweka kumbukumbu ya maambukizi ya tete kuwanga na hivyo kuwa chanjo dhidhi ya ugonjwa huu hapo baadae maishani.
 
Baada ya kupata maambukizi ya Varicella zoster virus, virusi hivi husambaa hadi kwenye tishu za ngozi, kamasi (mucosal) na hata kwenye mishipa ya fahamu (sensory nerves).Virusi hivi baada ya muda huwa kimya (dormant) {‘’ambapo ndio tunasema mgonjwa amepona’’} kwenye kifundo cha mishipa ya fahamu vinavyojulikana kama dorsal ganglion of sensory nerves.Kuchepuka tena kwa virusi hivi ambavyo awali vilikuwa vimekaa kimya ndio husababisha ugonjwa wa ukanda wa jeshi (herpes zoster),postherpetic neuralgia, na Ramsay Hunt Syndrome Type II.
 
Ramsay Hunt Syndrome type II inaambatana na dalili za kupooza sehemu mbalimbali za uso,maumivu kwenye sikio/masikio, kupoteza ladha ya ulimi (taste loss),mdomo kukauka, macho kuwa makavu na vipele kwenye mwili.

Dalili na viashiria vya Tete kuwanga

 Dalili za kwanza ni

• Kichefuchefu
• Kupungua kwa hamu ya kula
• Maumivu ya kichwa
• Maumivu ya misuli
• Kuumwa tumbo
 
Dalili hizi baadae hufuatiwa na hatua ya mgonjwa kutoka vipele, uchovu na homa ambayo sio kali sana, hatua hii ndio huonyesha kuwepo kwa ugonjwa wa tete kuwanga.
Vipele hivi mwanzo huonekana kama alama nyekundu ndogo kwenye uso, kichwa, tumbo,kifua, sehemu za juu za  kwenye mikono na miguu ambapo baada ya masaa 10-12 alama zile nyekundu hugeuka kuwa uvimbe, uvimbe huu kisha hujaa maji na kupasuka. Baadae vipele vipya (blisters) huanza kuchipuka  kwa makundi kwenye sehemu za tupu ya mwanamke (vagina), kope (eyelids) na mdomoni ambavyo hupasuka na kuwa vidonda vidogo vidogo kwenye sehemu hizi.
 
Hatua hii ya kutokea vipele huanza kuonekana kuanzia siku ya 10-21 baada ya mtu kupata maambukizi ya Varicella zoster virus na huambatana na kuwashwa sana mwili.Vipele vinaweza kutokea kwenye viganja vya mkono, nyayo na hata kwenye pua, lips, masikio, njia ya haja kubwa.
 
Vipele venye majimaji (blisters) hutokea siku ya 4-7 baada ya hatua ya kutoka vipele kuanza na hupotea kuanzia siku ya 5 na kuendelea.
Mtu ambaye ana maambukizi ya tete kuwanga huweza kuambukiza watu wengine siku moja au mbili kabla ya kuanza kutoka vipele na kuendelea kuwa na uwezo wa kuambukiza wengine kwa  siku 4-5 baada ya vipele kutokea.
Dalili ya kwanza ya tete kuwanga kwa watoto ni vipele kabla ya  dalili nyingine  nilizotaja awali hapo juu kufuata.Kwa watu wakubwa, vipele husambaa katika maeneo mengi mwilini kwa wingi na homa huwa ya muda mrefu sana na pia huweza kupata homa ya mapafu inayosababishwa na virusi vya Varicella zoster virus.
 
Baadhi ya watoto ambao walipata chanjo ya ugonjwa huu hapo awali huweza kupata tena maambukizi ya tete kuwanga ingawa yanakuwa sio makali sana(hutoka vipele 30 kwa wastani) lakini watoto hawa bado wana uwezo wa kuambukiza wengine ugonjwa huu.Kwa kawaida mtoto hutokea wastani wa vipele 250 hadi 500 wakati wa maambukizi ya ugonjwa wa tete kuwanga.
Ugonjwa huu ni nadra sana kuwa na madhara makubwa ingawa madhara huweza kuonekana kwa wagonjwa walio na upungufu wa kinga mwilini, wenye kuugua magonjwa sugu au wanawake wajawazito ambao hawakupata chanjo ya ugonjwa huu.

Vipimo vya uchunguzi

  • Utambuzi wa ugonjwa huu hufanywa kwa kuangalia dalili na viashiria vya ugonjwa huu(Kichefuchefu, kupungua kwa hamu ya kula,maumivu ya kichwa,maumivu ya misuli, kuumwa tumbo na vipele)
  • Kupima majimaji ya ndani ya vipele kwa kutumia direct immunoflorescent test
  • Kipimo cha damu kuangalia wingi wa Immunglobin M (IgM), ambapo kiwango chake huongezeka panapotokea maambukizi mapya au kuangalia uwepo wa Immunoglobulin G (IgG) ili kuthibitisha kuwepo kwa maambukizi hapo awali.
  • Kipimo cha ultrasound kwa wanawake wajawazito ili kuangalia dalili za kuwepo kwa maambukizi ya ugonjwa huu kwa kiumbe kilichomo tumboni (Fetal Varicella Infection).Inashauriwa kuchelewesha kipimo hiki kwa wiki 5 toka mama apate maambukizi ya tete kuwanga ili kuweza kutambua kama mtoto ameathirika au la.
  • Kipimo cha kuangalia vina saba (DNA) ya virusi vya Varicella zoster virus kwa mama wajawazito kwa kuchukua maji kwenye chupa ya uzazi ya mama (amniotic fluid). Kipimo hiki kina madhara kama kusababisha mimba kutoka au mtoto kupata Fetal Varicella Syndrome

Matibabu

Matibabu ya ugonjwa huu yanalenga kupunguza athari za dalili na viashiria vya ugonjwa huu na si kuua virusi vinavyosababisha ugonjwa huu
 
Matibabu ya tete kuwanga yanahusisha
  • Kuwakata watoto kucha ili kuepusha kujikuna na hatimaye kukata vipele hivyo kuongeza kutokea kwa vipele mwilini
  • Dawa za maumivu kama paracetamol n.k
  • Antihistamines-Dawa za kupunguza kuwashwa mwili
  • Calamine lotion ingawa hakuna tafiti zilizofanyika kuthibitisha ubora wa matumizi yake dhidhi ya ugonjwa huu.Dawa hii ni salama
  • Kuongeza kiwango cha usafi wa mwili, kuosha mwili kwa maji ya uvuguvugu
  • Kukaa sehemu zenye baridi ili kupunguza kuwashwa mwili
  • Kuepuka kujikuna vipele
  • Dawa dhidhi ya virusi (antiviral medication) kama acyclovir au valacyclovir ambazo hutolewa saa 24-48 baada ya vipele kuanza,dawa hizi hupunguza kusambaa kwa virusi lakini haziui virusi hao.Dawa hizi hutolewa kwa wale ambao wana upungufu wa kinga mwilini na kwa wanawake wajawazito.Watoto chini ya miaka 12 au wale wenye umri wa zaidi ya mwezi mmoja hawaruhusiwi kutumia dawa hizi kama hawana tatizo la upungufu wa kinga mwilini ili kuwaepusha na madhara wanayoweza kupata kutokana na matumizi ya madawa haya.

 Madhara ya tete kuwanga kwa wajawazito

Maambukizi ya tete kuwanga wakati wa ujauzito yanaweza kuathiri mtoto hasa kama mama atapata maambukizi haya wiki 28 baada ya kushika mimba.Wanawake ambao wana kinga dhidhi ya ugonjwa huu hawawezi kupata tete kuwanga kipindi cha ujauzito na wasiwe na wasiwasi kuhusu mtoto wao kupata madhara.Madhara ya tete kuwanga kwa mtoto ni kutokana na uwezo wa Varicella zoster virus kuwa na uwezo wa kuvuka kondo la uzazi (placenta) kutoka kwa mama mwenye tete kuwanga na hivyo kumuathiri mtoto.
Maambukizi ya tete kuwanga kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto kipindi cha ujauzito hujulikana kama fetal varicella syndrome au congenital varicella syndrome na huambatana na;
  • Madhara kwenye ubongo wa mtoto-Kichwa maji (hydrocephalus), kichwa kuwa kidogo, maambukizi ya ubongo (encephalitis),aplasia of brain
  • Madhara ya macho kama mtoto wa jicho (cataract), optic cup, optic stalk,microphthalmia, cataracts, chorioretinitis, optic atrophy n.k. 
  • Madhara ya mishipa ya fahamu
  • Madhara ya kibofu cha mkojo, miguu, njia ya haja kubwa,vidole kutoota vizuri n.k.
  • Matatizo ya ngozi kama hypopigmentation na n.k.
Watoto wenye umri wa mwezi mmoja au watoto wachanga wanatakiwa kulindwa wasipate tete kuwanga kwa kuweka mbali na wagonjwa wa tete kuwanga kwa siku 10-21. Uwezekano wa mtoto kupata tete kuwanga ni mkubwa iwapo mama atapata maambukizi ya tete kuwanga siku saba kabla ya kujifungua au wiki moja baada ya mtoto kuzaliwa.
 

Zamani ilikuwa ni kawaida kuona wanawake wanatoboa  masikio, pua, ili kuvaa aina mbalimbali za herini na shemeri. Siku hizi si ajabu kuona wanaume na wanawake wakijitoboa au kuchorwa alama (tattoo) sehemu mbalimbali za miili yao kama kwenye pua, mdomo, ulimi, tumbo, masikio, mikono, miguu, kwenye kichwa, mapaja, mgongo  na hata sehemu za siri yote haya kwa ajili ya urembo, miila au desturi zao, kutaka kujinasibu na tabaka fulani au kutaka kuonyesha ubunifu wao (artistic expression). 

Kutoboa/kuchorwa mwili kama kutafanywa na mtaalamu wa kutoboa/kuchora mwili hakuna madhara yoyote ya kiafya, madhara ya kutoboa/kuchorwa mwili  hupatikana pale tu ambapo kitendo hiki  hufanywa na mtu ambaye si mtaalamu na mjuzi wa fani hii bila kutumia njia salama za kiafya.
 
Katika utafiti uliofanywa nchini Marekani na madaktari bingwa wa ngozi (dermatologists) katika chuo kikuu cha Northwestern University Feinberg School of Medicine na kuchapishwa katika jarida la   American Journal of Clinical Dermatology umesema tatizo kubwa la kutoboa/kuchorwa mwili ni maambukizi (infection) yanayokisiwa kufika asilimia 20 ya kutoboa/kuchorwa sehemu mbalimbali za mwili. Maambukizi haya mara nyingi husababishwa na bakteria na huonekana katika sehemu ya mwili iliyotobolewa/kuchorwa.Madhara mengine ya kutoboa/kuchorwa mwili ni kuvuja damu, mzio/aleji, ngozi kuchanika pamoja  na ngozi kuwa na baka au scarring.

Ni mambo gani ya kuzingatia kabla ya kutoboa/kuchorwa  mwili wako?

  • Unatakiwa kujua  uwezekano wako wa kupata maambukizi - Kama tayari una maambukizi au una kidonda kilichowazi, ni bora ukaacha kutoboa/kuchorwa mwili mpaka utakapopona na kuwa na afya njema. Hatari ya kupata maambukizi ni kubwa kama utatobolewa/kuchorwa na mtu ambaye si mtaalamu na hana ujuzi wa kufanya kazi hii. Hakikisha anayekufanyia  hivi awe anafahamu masuala ya kukinga wateja wake na maambukizi ambayo ni pamoja na kusafisha vifaa vyake kila baada ya kazi, kuvichemsha vifaa hivyo au kuhakikisha vipo salama na havina bakteria wowote kwa kutumia kemikali za kusafishia, kuvifunika vifaa hivyo baada ya kuvisafisha na yeye mwenyewe kuvaa gloves salama (surgical gloves) wakati wa kufanya kazi yake hiyo ili hata kama ana magonjwa ya kuambukiza asiweze kukuambukiza wewe kwani zipo taarifa ambazo watu wameambukizwa ugonjwa wa ukimwi  au wamepata ugonjwa wa tetanus wakati wa kutobolewa/kuchorwa miili yao.
  • Hakikisha huna maradhi yoyote sugu - Kama una maradhi ya kisukari, ni bora ukaepuka kutoboa/kuchorwa mwili kwani kidonda chake kinaweza kisipone haraka na hatari ya maambukizi kwa wagonjwa wa sukari iko juu kupitia kwenye vidonda.
  • Fahamu kuhusu uwezo wako wa kupona - Unatakiwa uwe na ufahamu juu ya uwezo wa mwili wako katika kupona (healing tendencies) kidonda chochote kile. Kuna watu wengine wanapopata mchubuko au kukatika ngozi zao hupona kwa ngozi ile kufanya kama baka na uvimbe unaojulikana kama keloids. Kama wewe ni mmoja wa watu wa aina hii basi unahitaji kuepuka kufanya kitendo hiki cha kutoboa/kuchora mwili wako. Sehemu ambazo huchukua muda mrefu kupona baada ya kutoboa/kuchora mwili ni pamoja na kwenye maeneo ya tumboni, kwenye chuchu na hata sehemu za siri kwa wanawake.

Taarifa iliyotolewa na shirika la habari la Uingereza BBC, Julai 8 kuhusu utafiti uliofanyika nchini Uingereza uliowahusisha watoto 11,000 wakifuatiliwa kuhusu ratiba zao za kulala na kupima uwezo wa bongo zao.

Watafiti hao walisema ya kwamba wale watoto waliolala baada ya saa tatu usiku na waliokuwa hawana ratiba maalumu walikuwa na alama za chini kwenye hisabati na uwezo wa kusoma.

Na vilevile waliripoti kuwa ni vigumu ubongo kujifunza vitu vipya kutokana na ukosefu wa usingizi. Walichukua watoto wa kati ya miaka 3, 5 na 7 wakifuatilia uwezo wao wa kujifunza ukilinganisha na ratiba zao za kulala. Ratiba ilikuwa mbaya zaidi kwa watoto wa miaka 3. Na mpaka wanapofika miaka saba huwa na ratiba inayoeleweka kati ya saa moja na nusu usiku na saa mbili na nusu usiku.

Kwa takribani miongo mitatu sasa, tumeshuhudia ongezeko kubwa la mlipuko wa ugonjwa wa mkanda wa jeshi linaloendana na ongezeko la hususani ugonjwa wa UKIMWI. Hali hii imefanya baadhi ya watu kuamini kuwa, ugonjwa huu ni dalili ya wazi kabisa ya mtu kuwa na VVU, imani ambayo kwa kiasi kikubwa ina ukweli ndani yake ingawa si kwa wote wanaopatwa nao.

Mkanda wa jeshi au shingles au herpes zoster kwa majina ya kitabibu ni ugonjwa unaosababishwa na virus wa aina ya Varicella-zoster ambao pia husababisha ugonjwa wa tetekuwanga au chickenpox. Ugonjwa huu huathiri ngozi ambapo huambatana na vipele na michubuko kama ya kuungua yenye kuambatana na maumivu makali.

Visababishi

Kama tulivyokwisha tangulia kueleza hapo juu, ugonjwa huu husababishwa na virus aina ya Varicella-zoster ambao pia husababisha ugonjwa wa tetekuwanga. Baada ya mtu kupatwa na tetekuwanga, virus hawa hubaki katika hali ya kupooza/kutokuwa na madhara (dormant) katika neva fulani za mwili. Baada ya miaka kadhaa, iwapo itatokea kinga ya mwili ikashuka kwa sababu yoyote ile, virus hawa hupata tena nguvu/kuwa na madhara (active), kuibuka na kusababisha ugonjwa wa mkanda wa jeshi.

Kwa kawaida shambulio la mkanda wa jeshi hutokea mara moja maishani ingawa laweza kujirudia.

Vihatarishi

Mkanda wa jeshi unaweza kumpata mtu wa umri wowote ule ingawa watu walio katika makundi haya wapo katika hatari kubwa zaidi:
• Wenye umri wa zaidi ya miaka 60
• Mtu aliyewahi kuugua ugonjwa wa tetekuwanga kabla ya umri wa mwaka mmoja
• Watu ambao kinga yao ya mwili imepungua kwa sababu mbalimbali kama vile matumizi ya aina fulan za dawa, magonjwa kama vile maambukizi ya VVU (HIV/AIDS), saratani na utapiamlo.

Ukurasa 2 ya 3