Image

Baada ya kujifungua mtoto wangu wa kwanza, daktari wangu wa meno alinilalamikia kuwa situnzi vema afya yangu ya kinywa na meno. Kiukweli sikuwa nikifanya jambo lolote la ziada kuhakikisha afya yangu ya kinywa na meno iko katika hali nzuri.

Daktari wangu wa meno aliendelea kunieleza kuwa wanawake wajawazito wote na mama watarajiwa mara nyingi hupuuzia usafi wa kinywa na meno wakati wa ujauzito. Kiukweli, sikumuamini kabisa pale aliposema kuwa ujauzito husababisha mama wajawazito kubadili tabia zao za usafi wa kinywa na meno, lakini alikuwa sahihi kwa kiasi kikubwa kwa kunieleza kuwa wakati wa ujauzito vichocheo (hormones) vya mwili wa mwanamke hubadilika kwa kiwango kikubwa sana na mara nyingi huathiri afya ya fizi, hivyo ikiwa afya ya fizi ni dhaifu haiyumkini hali hii ikaathiri ukuaji wa kichanga tumboni mwa mama.

Tafiti zimethibitisha kuwa afya duni ya kinywa na meno hususani ugonjwa wa fizi unasababisha kuharibika kwa ujauzito. Tafiti iliyofanyika huko Marekani, Karolina ya Kaskazini kuangalia hali ya afya ya kinywa na meno kwa wamama watarajiwa 812, uchunguzi ulifanyika kwa kila mwanamama kwa kipindi cha majuma 26, na kisha masaa 48 baada ya kujifungua.

Watafitii walihakiki kiwango cha kuharibika mimba (chini ya majuma 28) na uzito mdogo wa kuzaliwa (chini ya 1000 gms), takwimu zilizingatia rangi ya mama (race), namba ya watoto wanaozaliwa, na jinsia ya mtoto. Asilimia 1.1 ya wamama waliokuwa na afya bora ya kinywa na meno (wamama 201) walipjifungua watoto njiti.

Kiwango hiki kiliongezeka zaid miongoni mwa wamama 566 waliokuwa na afya dhaifu ya kinywa na meno kutoka asilimia 3.5 mpaka asilimia 11.1 miongoni mwa wamama 45 waliokuwa na afya mbaya na afya mbaya zaidi ya kinywa na meno hususani magonjwa ya fizi.

Upungufu wa damu mwilini au Anemia ni miongoni mwa magonjwa yanayosumbua watu wengi duniani. Anemia humaanisha kupungua kwa kiwango cha chembechembe nyekundu za damu (RBC’s) katika mzunguko wake, au kupungua kwa wingi wa hemoglobin kwenye damu.

Kazi ya hemoglobin ambayo hupatikana ndani ya chembechembe nyekundu za damu ni kubeba gesi ya oksijeni kutoka katika mapafu na kusambaza kwenye tishu. Kwa sababu hiyo upungufu wa damu husababisha ukosefu wa hewa muhimu ya oksijeni katika viungo au hypoxia.

Kwa mujibu wa shirika la Afya duniani (WHO), viwango vya hemoglobini hutofautiana kati ya jinsia moja na nyingine, na kati ya nchi au eneo na eneo. Hata hivyo, iwapo nchi zote zitazingatia viwango hivi vya WHO, kunaweza kutokea mkanganyiko hususani kwa nchi zinazoendelea kama za Afrika hivyo basi ili kuepuka hali hiyo Wizara za afya za nchi husika zimejiwekea viwango vyao kutokana na mazingira ya nchi zao.

Kwa mujibu wa takwimu za WHO, na kulingana na jinsia, mtu aliye na chini ya viwango vifuatavyo huhesabika kuwa na upungufu wa damu, kwa wanaume chini ya 13g/dl, wanawake wasio wajawazito chini ya 12g/dl wakati wanawake wajawazito na watoto ni chini ya 11g/dl.

Upungufu wa damu husababishwa na nini?

Mambo yanayoweza kusababisha upungufu wa damu yanaweza kugawanywa katika makundi makuu matatu, ambayo ni:

  • Kupungua kwa uzalishwaji wa chembe nyekundu za damu yaani impaired production of rbcs kunakoweza kutokea iwapo kuna upungufu wa madini muhimu ya chuma (iron deficiency) hali ambayo husababishwa na mtu kuwa na minyoo aina ya hookworms au mtu kuwa na vidonda vya tumbo; upungufu wa vitamin hasa vitamin B12 pamoja na upungufu wa folic acid; na magonjwa sugu ya figo (chronic renal failure)
  • Kuongezeka uharibifu wa chembe nyekundu za damu kuliko kawaida yaani increased destruction of rbcs. Hali hii huitwa hemolytic anemia ambayo inaweza kutokea iwapo mtu ana kasoro katika umbo la chembe zake nyekundu za damu kwa mfano iwapo ana magonjwa ya hereditary spherocytosis au sickle cell; aliongezewa damu isiyoendana na kundi lake yaani blood transfusion reaction; ana malaria, au saratani ya damu kama vile chronic lymphocytic leukemia.
  • Kupoteza damu yaani blood loss ambayo yaweza kusababishwa na mambo kama ajali; kupoteza damu wakati wa upasuaji; na kupoteza damu kunakotokea kwa wanawake mara baada ya kujifungua au postpartum hemorrhage (PPH).
  • Sababu nyingine zinazoweza kusababisha upungufu wa damu mwilini ni pamoja na kuungua (burns); matumizi ya dawa au kemikali zinazoathiri sehemu laini ya mifupa inayohusika na uzalishaji wa chembe nyekundu za damu (bone marrow); magonjwa yanayosababisha kuharibika kwa chembe nyekundu za damu kabla ya muda wake kama vile thrombocytopenic purpura na hemolytic uremic syndrome

Dalili za Anemia ni zipi?

Kwa ujumla dalili za upungufu wa damu ni pamoja na

  • Mwili kuwa mchovu au mlegevu
  • Kupungua na kukosekana kwa umakini
  • Mgonjwa kushindwa kupumua vizuri hasa baada ya kutoka kufanya kazi nzito au mazoezi
  • Mapigo ya moyo kwenda haraka
  • Kucha kuwa na umbo la kijiko (Koilonchyia) na kukatika kirahisi. Hali hii hutokea kwa wenye upungufu wa madini ya chuma.
  • Kuwa na manjano (jaundice) kwenye macho, ngozi na sehemu nyingine za mwili kutokana na kuongezeka kwa uharibifu wa chembe nyekundu za damu.
  • Wakati mwingine, iwapo anemia ni kali, mgonjwa anaweza pia kuwa na dalili za moyo kushindwa kufanya kazi (heart failure) kama vile kuvimba miguu, au kushindwa kupumua wakati wa kulala bila kuinua kitanda (flat)
  • Baadhi ya wagonjwa wenye anemia inayotokana na upungufu wa madini ya chuma mwilini hupendelea kula vitu kama udongo, chaki, penseli, mchele mbichi, au vipande vya barafu, hali ambayo kitaalamu huitwa PICA.

Vipimo na Uchunguzi:

Vipimo kwa ajili ya tatizo hili vimelenga kutambua iwapo mgonjwa ana upungufu wa damu pamoja na kutambua chanzo chake. Vipimo hivyo ni

  • Kupima damu na viainishi vyake (complete blood count/full blood picture with red cell indices) kama vile MVC, MCH na MCHC.
  • Kuchunguza damu kwenye darubini (peripheral blood smear) ambayo husaidia kugundua iwapo kuna tatizo kwenye umbo la chembe nyekundu za damu.
  • Hemoglobin electrophoresis
  • Sickling test iwapo mgonjwa anahisiwa kuwa na ugonjwa wa sickle cell
  • Kuchunguza choo (stool examination) husaidia kugundua uwepo wa minyoo (hookworms)
  • Kuchunguza mkojo (urine examination)
  • Kucuhunguza uwepo wa vidonda vya tumbo kwa kutumia Endoscopy na vipimo vya barium
  • Kuchunguza sehemu ya mifupa inayozalisha chembe nyekundu za damu (bone marrow examination)

Matibabu ya Upungufu wa damu

Matibabu ya upungufu wa damu hutegemea kiwango cha upungufu (ukubwa wa tatizo) na chanzo chake. Kulingana na chanzo, matibabu yanaweza kujumuisha

  • Lishe yenye virutubisho muhimu kwa ajili ya wenye upungufu wa madini ya chuma, vitamin B12, na folic acid. Vyakula kama mboga za majani, nyama, na matunda hushauriwa sana.
  • Matumizi ya dawa za corticosteroids hasa kwa wagonjwa wenye autoimmune hemolytic anemia
  • Kuacha matumizi ya dawa au kemikali zenye kuathiri sehemu za mifupa zinazohusika na uzalishaji chembe za damu
  • Kuongezewa damu kwa wale walio poteza kiasi kikubwa cha damu au wale wenye dalili za moyo kushindwa kufanya kazi.
  • Kwa wenye minyoo ya hookworms hupewa dawa za kuua na kuondoa minyoo mwilini.
  • Kutibu malaria ipasavyo
  • Kutibu vidonda vya tumbo kwa wenye tatizo hili

Jinsi ya kuzuia upungufu wa damu: Namna ya kuzuia upungufu wa damu ni pamoja na kujitahidi kula mlo kamili wenye mchanganyiko wa nyama, mboga za majani, maziwa na matunda; kutambua dalili na kutibu haraka magonjwa yawezayo kuleta upungu wa damu; pamoja na kuwapa mama wajawazito vidonge vyenye madini ya chuma na folic acid

Ni ugonjwa unaoshambulia ini na husababishwa na virusi au bacteria wa aina za A, B, C, D

Na vile vile huweza kusababishwa na :

  • Fangasi
  • Unywaji wa pombe (alcoholic hepatitis)
  • Dawa
  • Magonjwa yanayosababishwa na kinga ya mwili kuushambulia mwili (autoimmune)
  • Magonjwa ya kimetaboliki

Magonjwa yanayosababiswa na virusi au bacteria husambazwa kutokana na aina zake:

Homa ya Ini isababishwao na aina A (Hepatitis A), E

  • Kwa kula kinyesi kilichochanganyika na aina hii ya vimelea kwenye Maji, chakula

Homa ya Ini isababishwao na aina B (hepatitis B), C, D, G

  • Mchanganyiko wa damu ambao hutokana na:
    • Ngono zembe
    • Kutumia Sindano zilikwishatumika wakati wa matumizi ya madawa ya kulevya
    • Wakati wa kuwekewa damu
    • Kwenye kusafisha figo kwa wenye shida za figo

Mwaka 2013 virusi vya homa ya ini vilishika nafasi ya saba kwenye sababu ya vifo duniani,  mara nyingi homa ya Ini husababishwa na virusi zaidi ya hizo sababu nyingine.

Na homa ya ini imeganwanyika kama ifuatavyo

  • Ya hapo kwa papo kitaalamu acute hepatitis
  • Sugu kitaalamu chronic hepatitis

Dalili za Homa ya Ini

Kwa wagonjwa wengine wanaweza kukaa bila dalili mpaka madhara ya ugonjwa huu yanapoathiri ini.

Dalili ambazo hutokea ni:

  • Kichefuchefu
  • Kutapika
  • Ladha kubadilika mdomoni
  • Kupoteza hamu ya kula
  • Uchovu
  • Kuwashwa
  • Kukojoa mkojo mweusi
  • Maumivu ya tumbo upande wa juu wa kulia
  • Manjano kuonekana kwenye viganja vya mkono na machoni
  • Maumivu ya misuli na viungo
  • Homa

Madhara ambayo yanaweza kutokea baada ya kuugua homa ya Ini

  • Ini kuoza (hepatic necrosis)
  • Ini kukakamaa na kuota vinundunundu (cirrhosis)
  • Ini kushindwa kufanya kazi (hepatic failure)
  • Saratani ya Ini (hepatocellular carcinoma)

Vipimo

  1. Maabara
  • Kipimo cha damu kujua aina ya homa ya ini
  • Kipimo cha kuangalia ufanyaji kazi wa ini, kupitia kuangalia vimenge’nyo vya kwenye ini
  1. Picha
  • Kipimo cha kuangalia ini kitaalamu ultrasound

Tiba

Ni vyema kwenda hospitali na kufanyiwa uchunguzi kusudi upewe dawa na matibabu muhimu.

Baadhi ya wagonjwa huweza kunufaika na matibabu ya dawa, na madhumuni ya dawa ni kuzuia kuendelea kuathirika kwa ini

Dawa ambazo mgonjwa hupewa kitaalamu ni: ( interferons [IFNs], antivirals, and corticosteroids)

Lamivudine na Adenofir zimeonyesha matokeo ya kuaminika kwenye matibabu ya homa ya ini aina B.

 

 

Ushawishi wa kuandika makala hii ya tatizo la kutokwa usaha wakati wa kukojoa umetokana na swali la msomaji wetu ambaye aliuliza hivi kwenye tovuti hii na hapa na mnukuu,

 " Dr khamisi samahani sana mi nasumbuliwa nikikojoa mwisho wa mkojo unatoka kama usaha na sina dalili ya kaswende ambazo umezizungumzia nakuomba unisaidie’’.

Bila shaka wapo wengi ambao wana tatizo kama hili na ambao wamewakilishwa kupitia swali hili lililoulizwa na msomaji wetu huyu. Naomba tuwe pamoja kwenye makala hii ili ujifunze kuhusu tatizo la mtu kutokwa usaha wakati wa kukojoa.

Tatizo la Kuwepo kwa chembechembe za usaha au usaha kwenye mkojo hujulikana kama pyuria ambapo linaweza kuonekana kwa kutumia hadubini (microscope) au kama tatizo ni kubwa linaweza kuonekana kwa macho.

Visababishi vya tatizo la Kutokwa Usaha Wakati wa Kukojoa ni nini?

Visababishi vya tatizo hili ni kama vifuatavyo;

  • Ugonjwa wa mfumo wa mkojo (UTI)-Maambukizi kwenye figo, kwenye mrija wa mkojo na kwenye kibofu cha mkojo (cystitis- amabayo huonekana sana)
  • Magonjwa ya Zinaa-Kama ugonjwa wa kisonono au ‘’gono’’ kama wengi wanavyoita, ugonjwa wa Chlamydia na Trichomoniasis
  • Sumu inayotokana na kemikali (Chemical poisoning) kama 4-Aminodiphenyl inayotumika kwenye maabara na kwa ajili ya tafiti
  • Tatizo linajulikana kama Reiter’s syndrome
  • Pyelonephritis-Maambukizi ya bakteria kwenye sehemu za figo zinazojulikana kama calyces, renal pelvis na tishu za figo
  • Madhara ya pyelonephritis ambayo husabababisha ugonjwa unaojulikana kama renal abscess
  • Maambukizi kwenye tezi dume-Prostatitis (Kwa wanaume)
  • Upungufu wa kinga mwilini
  • Mcharuko (Inflammation) kutokana kuwa na mawe kwenye kibofu cha mkojo au kwenye figo
  • Mzio (Allergy) au kuota uvimbe sehemu yoyote ya mfumo wa mkojo

Viashiria vya tatizo hili ni;

  • Maumivu makali ya kuchoma (Painful burning sensation) wakati wa kukojoa
  • Maumivu chini ya kitovu
  • Homa
  • Kutapika

Tatizo hii likidumu kwa muda mrefu husababisha kupungua uzito kwa mgonjwa

Ni ugonjwa unaowaathiri sana watoto mpaka kufananishwa kuwa ni moja ya hatua za ukuaji wa mtoto. Mgonjwa wa tetekuwanga hutokewa na vijipele vyenye majimaji mwili mzima. Vijipele hivi huwa vinawasha kitendo kinachomfanya mgonjwa wa tetekuwanga kutojisikia vizuri huku akishinda anajikuna mwili mzima. Tetekuwanga husababishwa na virusi kwa kitaalamu hujulikana kama Varicella Zoster (VZV).

Mara nyingi ugonjwa huu wa tetekuwanga huwa haujirudii, hii ndiyo sababu imezoeleka sana kwa wengi kusema kama haujawahi kuugua basi usikae karibu na mgonjwa wa tetekuwanga. Ikumbukwe kuwa, ugonjwa wa tetekuwanga unayo kinga ingawa hapa kwetu upatikanaji wake bado haujasambaa sehemu zote.

Dalili za ugonjwa wa tetekuwanga

Dalili kuu za ugonjwa wa tetekuwanga ni vijipele (kama malengelenge) vinavyowasha. Ugonjwa huu huchukua muda mpaka kuanza kujitokeza kwa dalili zake, mgonjwa wa tetekuwanga ataanza kuona dalili hizi baada ya siku 21 tangu virusi vya ugonjwa huu kuingia kwenye mwili wake (baada ya maambukizi). Ukiachana na vijipele vinavyowashwa, dalili nyingine za ugonjwa wa tetekuwanga ni kama;

  • Kuumwa kwa kichwa
  • Homa
  • Kupungukiwa kwa hamu ya kula

Hizi ni dalili za awali ambazo huanza kujitokeza kabla ya vipele kuanza kuchomoza, mara nyingi huchukua siku moja au mbili mara baada ya kuanza kusikia dalili hizi mpaka kuanza kujitokeza kwa vijipele. Vijipele vya tetekuwanga hupitia hatua kadhaa;

  • Vijipele vyekundu au pinki hujitokeza mwili mzima
  • Vijipele huiva na kuanza kutoa majimaji
  • Vijipele vinavywea na kuanza kukauka

Kumbuka, vijipele hivi havijitokezi kwa wakati mmmoja, hivyo wakati vingine vinapona, kuna vingine vitakuwa ndiyo vinatokeza.

Mgonjwa huendelea kujisikia vibaya mpaka vijipele vikauke, na hatua hii huweza kuchukua hadi wiki mbili mpaka kupotea kabisa.

Nini husababisha Tetekuwanga?

Kama tulivyoeleza hapo juu, tetekuwanga husababishwa na virusi ambavyo kwa kitaalamu hujulikana kama Varicella Zoster (VZV). Mara nyingi ugonjwa wa tetekuwanga huambukizwa kutokana na kugusana na mtu mwenye ugonjwa wa tetekuwanga. Virusi vya tetekuwanga huendelea kuwa na uwezo wa kuambukiza mpaka malengelenge (vijipele) viwe vimetumbuka na kukauka. Hivyo epuka makutano na mgonjwa wa tetekuwanga mpaka vipele vitakapokauka kabisa. Virusi hivi huweza kuambukizwa kwa njia zifuatazo;

Karibuni tena katika kijiwe chetu,leo kwenye muendelezo wa makala zetu kuhusu udhibiti wa kisukari  tunaangalia umuhimu wa tendo la ndoa katika kusaidia kupunguza kiwango cha juu ya sukari.

Kwa upande moja ama mwingine tendo la ndoa ni moja ya zoezi la mwili kama mazoezi mengine kama kukimbia na mazoezi mengine ya viungo na pia tendo hili linasaidia sana kushuka kiwango cha sukari, Moja ya tafiti iliyowahi kufanya na  American Journal of Medicine inasema kuwa mtu akifanya tendo la ndoa mara tatu au nne kwa wiki anajiweka kwenye nafasi ya kutopata matatizo ya msongo wa mawazo ambayo unaweza kuleta matatizo kama ya Kisukari na Presha.

 Moja ya tafiti iliyofanywa na Taasisi ya Kisukari Marekani (ADA) zinaonesha kuwa kufanya tendo la ndoa husaidia kuyeyusha mafuta na sukari mwilini kwakuwa ni moja ya mazoezi ya viungo.Tafiti zingine zinaonesha kuwa endapo mtu ukifanya tendo la ndoa mara tatu au nne kwa siku husaidia kupunguza kiasi cha mafuta mwilini.

KWA kawaida mwanaume ana korodani mbili ambazo zimehifadhiwa katika mfuko maalum wenye tabaka tatu na ndani kuna kiasi kidogo cha maji kinachozunguka korodani ili kuilinda. Mwanaume endapo atakuwa na korodani moja ni tatizo na pia akiwa hana kabisa korodani ni tatizo kubwa.

Kazi ya korodani ni kuzalisha mbegu za kiume, mwanaume anaweza kuwa na korodani zote mbili lakini akashindwa kuzalisha mbegu za uzazi kutokana na matatizo mbalimbali.

Mwanaume mwenye korodani moja anaweza kuzalisha mbegu au asizalishe kabisa, kitu cha msingi akapimwe hospitali kuona uwezo wa hiyo moja. Mwanaume ambaye hana korodani kabisa hawezi kuzalisha mbegu za uzazi hivyo hana uwezo wa kumpa mimba mwanamke. Tatizo la kuwa na korodani moja au kukosa kabisa tutakuja kuliona katika makala zijazo.

JINSI TATIZO LINAVYOTOKEA

Maumivu ya korodani hutokea katika korodani au haswa moja au zote mbili endapo zitaumizwa kwa kuumia au maambukizi. Maambukizi haya yanaweza kuwa makali na ya muda mfupi,yanakuwa makali kwa muda fulani halafu yanapoa yenyewe au kwa dawa baadaye yanarudi tena yakiwa makali sana kama mwanzo au pia huwa sugu yaani unakuwa na maumivu ambayo siyo makali ila ni ya muda mrefu na yanayokunyima raha.

Maumivu ya korodani yanaweza kuwa makali kiasi kwamba yatahitajika matibabu ya dharura mfano korodani inavimba kama jipu kubwa, ikiambatana na maumivu makali na homa, tatizo hili kitaalam huitwa ‘Fournier's gangrene' au inatamkwa ‘Fonias gangrini'.

Vilevile inaweza kutokea korodani ikajinyonga yenyewe na kusababisha ukapata maumivu makali ya ghafla yanayoelekea hadi tumboni, tatizo hili linaitwa Testicular Torsion. Matatizo haya kwa ujumla wake tutakuja kuyaona katika makala zijazo.

CHANZO CHA TATIZO

Maumivu ya korodani yana vyanzo mbalimbali, lakini maumivu sugu ni yale yanayochukua takriban zaidi ya miezi mitatu. Maumivu makali na ya ghafla huwa hayavumiliki na huwa na tiba ya dharura. Maumivu haya sugu huwa kwa kipindi fulani hasa kwa wanaume ambao wametoka kufunga uzazi Vesectomy lakini baadaye hupoa. Vilevile husababishwa na maambukizi katika korodani na kusababisha magonjwa kama Epididymits, Prostatis na Orchitis ambayo yote ni maradhi ya viungo vya uzazi vya mwanaume na husababisha ugumba.

PUMBU.jpg

 

Baadhi ya watu wana meno yaliyojipanga visivyo. Katika hali ya kawaida meno yanatakiwa yawe katika mahusiano mazuri kiasi kwamba meno ya juu yaweze kukutana vizuri na yaliyo jirani yakae vizuri pia. Utakuta baadhi ya watu meno ya juu yamechomoza mbele sana kiasi kwamba hata kufunga mdomo ni tatizo, wengine ya chini kuvutika mbele zaidi na kuwa na kidevu kilichochongoka kwenda mbele na wengine yamepandana pandana.

Mpangilio mbaya wa meno unaweza kuwa mbaya zaidi kiasi cha kumughasi mhusika na wakati mwingine meno yenyewe kushindwa kufanya kazi zake vizuri. Tatizo lingine la meno yaliyojipanga vibaya ni vigumu kuyasafisha na hivyo kuyaweka meno katika hatari ya kuoza na kusababisha magonjwa ya fizi.

Nini kinasababisha matatizo haya?

  • Maumbile yatokanayo na vinasaba na urithi
  • Tabia kama kunyonya vidole utotoni hata ukubwani kwa wengine
  • Kuwahi kutoka meno ya utotoni
  • Kuchelewa kutoka kwa meno ya utotoni hivyo kuyafanya ya ukubwani kuota upande
  • Ajali wakati wa kujifungua ambayo inaweza kuathiri maeneo ya kukua kwa taya

Matibabu

Lengo kubwa la matibabu ni kuyaweka meno katika mpangilio unaokubalika, ili kuboresha muonekano, utafunaji na hata utamkaji wa maneno.

Katika sehemu ya kwanza ya makala hii ya maambukizi ya fangasi, tuliangalia aina za fangasi, watu waliopo kwenye hatari ya kupata maambukizi ya fangasi na aina ya maambukizi ya fangasi. Katika sehemu hii ya pili na  ya  mwisho katika muendelezo wa makala hii, tutaangalia maambukizi ya fangasi kwenye damu yaani systemic mycoses.

Systemic Mycoses

Ni maambukizi ya fangasi kwenye damu ambayo huanzia kwa fangasi kuvamia mapafu ya mtu.Maambukizi haya yamegawanyika katika sehemu kuu mbili;

  • Maambukizi ya fangasi kutokana na fangasi wa kawaida kwa watu wenye afya njema (Systemic mycoses due to primary pathogens)
  • Maambukizi ya fangasi kwenye damu kutokana na fangasi nyemelezi kwa watu wenye upungufu wa kinga mwilini (Systemic mycoses due to opportunistic pathogens)

Maambukizi ya fangasi kutokana na fangasi wa kawaida kwa watu wenye afya njema (Systemic mycoses due to primary pathogens)

Maambukizi haya ya fangasi huanzia kwenye mapafu na kusambaa kwenye viungo vingine vya mwili.Yafuatayo ni maambukizi ya fangasi kwenye damu yanayoonekana sana kwa wagonjwa nayo ni;

  • Histoplasmosis
  • Blastomycosis
  • Coccidioidomycosis

Histoplasmosis

Husababishwa na fangasi Histoplasma Capsulatum, ambao huishi kwenye mazingira hasa kwenye mchanga na mtu huweza kupata maambukizi ya fangasi hawa kwa kuvuta hewa yenye mazalia ya fangasi (Fungal spores).Watu wenye maambukizi haya huweza kuambukiza watu wengine au hata kuambukiza wanyama. Maambukizi ya histoplasmosis ni hatari sana kwa watu wenye kinga dhaifu mwilini hasa kama yatasambaa kwenye viungo vingine vya mwili.

Dalili na Viashiria ya maambukizi ya Histoplasmosis

  • Homa kali
  • Uchovu
  • Kutetemeka (Chills)
  • Maumivu ya kichwa
  • Maumivu ya kifua
  • Maumivu ya mwili (Body aches) 

Vipimo vya uchunguzi

  • Uchunguzi wa maabara kwa kutumia hadubini
  • Kuotesha fangasi maabara
  • Ugunduzi wa surface markers za fangasi aina ya Histoplasma Capsulatum kwenye mkojo
  • Vipimo vya damu vya kuangalia jinsi kinga za mwili zinavyojitahidi kukabiliana na maambukizi haya (Antibody response to histoplasma)

Tiba ya Histoplasmosis

  • Mara nyingi maambukizi haya hupona yenyewe kwa wale wanaopata maambukizi ya wastani
  • Kwa wale wenye kupata maambukizi hatari, uhitaji matibabu ya dawa za kutibu fangasi

Blastomycosis

Husababishwa na fangasi aina ya Blastomyces dermatitidis.Maambukizi haya huathiri mbwa, binadamu, simba, farasi nk. Blastomycosis huweza kuenezwa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mtu mwingine au kutoka kwa mnyama kwenda kwa binadamu.

Dalili na Vishiria vya Blastomycosis

  • Homa kali inayoambatana na mtetemo (Chills)
  • Maumivu ya kifua
  • Kukohoa
  • Kushindwa kupumua vizuri
  • Maumivu ya misuli (Muscle aches)
  • Maumivu ya viunganishi vya mifupa (Joint pain)

Vipimo vya Uchunguzi

  • Kuoteshwa kwa fangasi maabara (Culture)
  • Kuchunguza tishu maabara kwa kutumia hadubini
  • Kipimo cha antigen test - Kinaweza kugundua uwepo wa fangasi kwa kupima mkojo au damu (Serum)

Tiba ya Blastomycosis

  • Dawa za kutibu fangasi – Hutumika kwa muda mrefu

Madawa ya kulevya yameleta athari sana katika jamii, kutokana na ile hali ya kufanya hisia ya utegemezi, kwamba mtu anaona hawezi kufanya chochote bila kupata japo kidogo.

Kuna aina nyingi za madawa ya kulevya ila aina mbili ndio ambayo yanasumbua sana,

  • Cocaine
  • Heroin

Cocaine hutokana na majani ya mmea uitwao kitaalamu Erythroxylon coca, na huandaliwa kwa kupitia hatua mbali mbali na hatua moja wapo ni ya kupata kinachotumika kuengenezea soda za cola, na hatua ya mbele zaidi ndio cocaine. matumizi yake ni kwa kujichoma sindano, na wengine huvuta aidha kwa kuunguza kwanza ambao huitwa‘crack’ , mpaka mwaka 2007,Marekani ilikuwa na watumiaji million 2.1, na kati ya hao million 1.6 walikuwa tegemezi au mateja , na matumizi ya kawaida au ya kupitiliza ya cocaine yalipekea asilimia 30% kuhudhuria hospitali kutokana na athari zake, na wengi hufika hospitali wakilalamika maamumivu makali ya kifua.

Kutoka katika jarida la Circulation Vol.122, issue24 liliotolewa Desemba 2010, waliripoti kati ya wagonjwa 233 ambao ni watumiaji wa cocaine katika idara ya dharura asilimia 56% walikuwa na athari kwenye moyo na asilimia 40% walilalamika kuwa na maumivu ya kifua. Taarifa za hvivi karibuni inaonyesha marekani ina watu milion 30 ambayo wametumia cocaine na milioni 5-6 ni tegemezi au mateja (taarifa kutoka jarida la national medical association)

Heroin hutoka kwenye ua kitaalamu hujulikana papaver somniferum- opium poppy, katika karne ya 18, madaktari walitumia kama dawa ya kupunguza maumivu hasa kwa wagonjwa wa saratani, pepopunda, hedhi. Mwishoni mwa karne ya 18 ndio madaktari waligundua hali ya tegemezi ya kulevya iliyoletwa na heroin.  Huandaliwa kupitia hatua mbali mbali na hatua moja wapo ni dawa ambayo hutumiwa kupunguza maumivu kitaalamu Morphine, na hatua za mbele zaidi ndio heroin.  Heroin hutumika kwa njia ya kunusa na kuvuta puani na kujichoma sindano

Cocaine na Heroin zote hulevya kukupa hali ya kujisikia furaha kitaalamu Euphoria, ila hupelekea kuwa tegemezi wa kulevya huko.

Ukurasa 6 ya 11