Image

KWA kawaida mwanaume ana korodani mbili ambazo zimehifadhiwa katika mfuko maalum wenye tabaka tatu na ndani kuna kiasi kidogo cha maji kinachozunguka korodani ili kuilinda. Mwanaume endapo atakuwa na korodani moja ni tatizo na pia akiwa hana kabisa korodani ni tatizo kubwa.

Kazi ya korodani ni kuzalisha mbegu za kiume, mwanaume anaweza kuwa na korodani zote mbili lakini akashindwa kuzalisha mbegu za uzazi kutokana na matatizo mbalimbali.

Mwanaume mwenye korodani moja anaweza kuzalisha mbegu au asizalishe kabisa, kitu cha msingi akapimwe hospitali kuona uwezo wa hiyo moja. Mwanaume ambaye hana korodani kabisa hawezi kuzalisha mbegu za uzazi hivyo hana uwezo wa kumpa mimba mwanamke. Tatizo la kuwa na korodani moja au kukosa kabisa tutakuja kuliona katika makala zijazo.

JINSI TATIZO LINAVYOTOKEA

Maumivu ya korodani hutokea katika korodani au haswa moja au zote mbili endapo zitaumizwa kwa kuumia au maambukizi. Maambukizi haya yanaweza kuwa makali na ya muda mfupi,yanakuwa makali kwa muda fulani halafu yanapoa yenyewe au kwa dawa baadaye yanarudi tena yakiwa makali sana kama mwanzo au pia huwa sugu yaani unakuwa na maumivu ambayo siyo makali ila ni ya muda mrefu na yanayokunyima raha.

Maumivu ya korodani yanaweza kuwa makali kiasi kwamba yatahitajika matibabu ya dharura mfano korodani inavimba kama jipu kubwa, ikiambatana na maumivu makali na homa, tatizo hili kitaalam huitwa ‘Fournier's gangrene' au inatamkwa ‘Fonias gangrini'.

Vilevile inaweza kutokea korodani ikajinyonga yenyewe na kusababisha ukapata maumivu makali ya ghafla yanayoelekea hadi tumboni, tatizo hili linaitwa Testicular Torsion. Matatizo haya kwa ujumla wake tutakuja kuyaona katika makala zijazo.

CHANZO CHA TATIZO

Maumivu ya korodani yana vyanzo mbalimbali, lakini maumivu sugu ni yale yanayochukua takriban zaidi ya miezi mitatu. Maumivu makali na ya ghafla huwa hayavumiliki na huwa na tiba ya dharura. Maumivu haya sugu huwa kwa kipindi fulani hasa kwa wanaume ambao wametoka kufunga uzazi Vesectomy lakini baadaye hupoa. Vilevile husababishwa na maambukizi katika korodani na kusababisha magonjwa kama Epididymits, Prostatis na Orchitis ambayo yote ni maradhi ya viungo vya uzazi vya mwanaume na husababisha ugumba.

PUMBU.jpg

 

Watafiti kutoka kampasi ya chuo cha Gustave Roussy Cancer Campus cha nchini Ufaransa wamesema ya kwamba matibabu ya saratani ya uume kwa kutumia brachytherapy (mionzi) husaidia wagonjwa wa saratani hii kuwa na uwezo wa kushiriki katika tendo la ndoa hata baada ya matibabu.

Katika utafiti wao uliwahusisha wagonjwa 201 wenye saratani ya uume (penile cancer) na wenye umri zaidi ya miaka 45, asilimia 79 ya wagonjwa wote walichagua tiba ya mionzi (brachytherapy) na hivyo kuweza kuishi kwa angalau miaka kumi baada ya kufanyiwa matibabu haya.Chama cha  saratani (American Cancer Society)  nchini Marekani kinasema, ni aslimia 85 tu ya wagonjwa wote wa saratani ya uume wanaotibiwa kwa njia ya upasuaji  ambao huweza kuishi kwa angalau miaka kumi baada ya kufanyiwa upasuaji.

Utafiti huu uliofanyika nchini Ufaransa, ulifanyika kwa  wagonjwa wote 201 kutahiriwa kwanza na baadae kutibiwa kwa brachytherapy.Tiba hii ya brachytherapy hufanywa kwa mgonjwa kuwekewa kipande cha waya chenye kutoa mionzi kwa dozi ndogo kwenye uvimbe wa saratani au karibu na saratani yenyewe na hivyo kufanikiwa kuua chembechembe za saratani katika sehemu husika.

Uwezekano wa mgonjwa kuishi (survival rate) na uume wake kamili, miaka mitano baada ya matibabu ni asilimia 85.Kwa ujumla, ni asilimia 79 tu ya wagonjwa ambao waliweza kuishi kwa miaka kumi baada ya matibabu na kati yao, aslimia 82 hawakupata tena saratani hii ya uume.

Wagonjwa 8 walilazimika kuondolewa dhakari (penis) zao kabisa na 18 wengine waliondolewa baadhi ya sehemu za dhakari zao.

Wagonjwa wa saratani ya uume ambao wapo kwenye hatari ya kupata saratani hii tena baada ya matibabu ni wale ambao kabla ya kupatiwa matibabu, saratani yao ilikuwa tayari imeshasambaa kwenye mafundo fundo (lymph nodes) yaliyopo kwenye nyonga.

Kati ya wale waiotibiwa, wagonjwa 13 (asilimia 6) walihitaji tiba ya upasuaji ili kuondoa madhara  ya saratani hii ambayo yalikuwa ni vidonda venye kuambatana na maumivu makali.

Hata hivyo, ilionekana ya kwamba wagonjwa waliokuwa na  uvimbe wa saratani  wenye upana wa zaidi ya 4cm kabla ya matibabu, ndio walikuwa kwenye hatari zaidi ya kupata tena saratani hii ya uume.

Matokeo ya utafiti huu yameonyesha ya kwamba matibabu ya mionzi (brachytherapy)ni tiba nzuri kwa wagonjwa wa saratani ya uume ambayo haijasambaa kwenye eneo la uume linalojulikana kama corpus cavernosum.Tiba hii ya mionzi mbali na kutibu saratani hii husaidia wagonjwa kubakiwa na dhakari zao (intact penis).Na iwapo maambukizi ya saratani ya uume yatajirudia, basi yanaweza kutibiwa tena kwa tiba hii ya mionzi au kutumia tiba ya upasuaji pasipo kuwa na hofu ya kufariki kwa mgonjwa.

Hii inamaanisha ya kwamba, wanaume wanaotibiwa kwa kutumia tiba ya mionzi, wanakuwa ni watu wenye kujiamini kwa kuwa bado wanamiliki sehemu muhimu ya mwili wao (uume) hivyo  bado kuwa na uwezo  wa kushiriki tendo la ndoa pamoja na kutoa mkojo kupitia sehemu hii husika.

Saratani hii ya uume (penile cancer) huonekana sana katika nchi zinazoendelea kama nchi za Paraguay, Uruguay,Uganda na Brazil ambapo katika nchi ya Uganda, huathiri watu 4.4 kwa kila watu 100,000.

Visabababishi vya saratani hii ni pamoja na ugonjwa wa HIV, virusi vya Human Papilloma Virus, Genital Warts, uchafu kwenye uume, matumizi ya tumbaku, kuwepo kwa uchafu mweupe kwenye ngozi ya uume hasa kwa wale ambao hawajatahiriwa.

Tiba ya saratani hii ya uume ni pamoja na tiba ya upasuaji (inayoweza kuondoa baadhi ya sehemu tu ya uume au kuondoa uume wote kwa ujumla) na tiba ya mionzi.

Wanasayansi nchini Marekani wako mbioni kutengeneza korodani bandia (artificial testicle) zitakazokuwa zikitengeneza shahawa ili kusaidia wanaume wenye matatizo ya uzazi.

Timu ya wanasayansi katika jimbo la San Fransisco nchini Marekani chini ya Dk Paul Turek wamepewa ruhusa ya kuendelea na utafiti huu baada ya kuahidiwa kupewa pesa za kutosha kutekeleza mradi huu.

Kwa muda mrefu, wanasayansi wamejaribu kutengeneza seli za shahawa (Sperm Cells) bila mafanikio kwa vile wamefanikiwa kutengeneza robo tatu tu ya mchakato wa kupata shahawa kamili. Hii inatokana na mazingira maalum yanayopatikana katika korodani kuhitajika kukamilisha utengenezaji wa shahawa hizo. Mazingira hayo ya uhalisia ni tofauti na mazingira yoyote yale ya nje katika utengenezaji shahawa.

Korodani hizo zitakuwa katika umbo la duara (cylindrical shape) na zitakuwa na urefu wa inchi kadhaa na hazitahitaji kupachikwa kwenye mwili wa binadamu. Aidha kifaa hiki kitakuwa tofauti na korodani nyingine bandia ambazo huwekewa wanaume waliokosa korodani moja kutokana na sababu mbalimbali.Kwa kawaida korodani za namna hii huwa hazitengenezi shahawa kwa vile hujazwa maji maalum ya saline solution ili kutumika kama mapambo.