Image

Hiki ni kirusi cha aina gani?

Corona ni jamii kubwa ya virusi vinavyosababisha maradhi kwa wanyama na binadamu. Kwa binadamu, jamii kadhaa za virusi vya Corona vinafahamika kusababisha maambukizi kwenye njia ya hewa na mfumo wa upumuaji.  Maradhi yaliyowahi kusababisha madhara makubwa kutokana na virusi vya Corona ni pamoja na MERS na SARS yaliyozuka mwanzoni mwa miaka ya 2000. Kirusi cha Corona kilichogundulika hivi karibuni kinasababisha ugonjwa unaofahamika kama COVID-19.

COVID-19 ni nini?

COVID-19 ni ugonjwa wa kuambukiza unaosababishwa na virusi vya Corona. Virusi hivyo vipya havikuwa vikifahamika hapo kabla na sayansi ya tiba. Na vilianzia nchini China mwezi Disemba mwaka 2019.

Dalili za Corona ni zipi?

Mnamo mwaka 2007, watafiti nchini Marekani walifanikiwa kutoa ripoti inayojaribu kuhusisha ukosefu wa usingizi na upungufu wa homoni ya testosterone miongoni mwa wanaume watu wazima.

Kwa kawaida kiwango cha homoni ya testosterone hupungua kadiri mwanaume anavyozidi kuwa mtu mzima, na kwa baadhi ya wanaume, kupungua huku kwa testosterone huweza kusababisha ulegevu wa mwili, kukosa hamu ya ngono na hata kuvunjika mifupa ya mwili.

Matatizo ya kukosa au kupungua hamu ya kujamiana yanatambulika kama tatizo linalojirudia kwa muda mrefu ambapo huathiri mzunguko wa tendo la kujamiana (kusisimka, kufikia kilele, kurudia) na hivyo kusababisha msongo wa mawazo au kuharibu uhusiano kati ya mtu na mwenza wake. Katika makala hii, mwandishi wako Dk. Khamis Hassan anachambua vitu vinavyoweza kusababisha tatizo hili na jinsi ya kuliepuka.

Kupungua au kukosa hamu ya kufanya mapenzi ni suala linaloonekana kuathiri wenza wengi. Jamii imeshuhudia visa vingi vinavyosababishwa na mwenza mmoja kutoka nje ya ndoa au uhusiano kwa kisingizio cha kutoridhishwa na utendaji wa mwenzake katika suala la kujamiana. Kadhalika jambo hili limesababisha kuvurugika kwa ndoa nyingi na wakati mwingine kusababisha magonjwa au hata vifo kwa mmoja au wenza wote wawili.

Lakini nini hasa sababu ya kuwepo kwake?

Kwa ujumla visababishi vya tatizo hili kwa wanaume na wanawake ni pamoja na msongo wa mawazo uliokithiri. Asilimia kubwa ya ukosefu wa hamu ya kujamiana husababishwa na msongo wa mawazo unaompata mwenza mmojawapo kwa sababu ya ugumu wa maisha (uchumi), matatizo katika uhusiano (ugomvi, kutoelewana, kutoaminiana au kukosa uaminifu katika uhusiano {infidelity} n.k) au magonjwa mbalimbali. Sababu nyingine ni kupungua au kukosekana upendo/mapenzi katika uhusiano/ndoa, unywaji pombe kupindukia, na utumiaji wa dawa za kulevya.

Aidha kujifungua mtoto nako kunaelezwa kuwa ni chanzo kingine cha kuwepo kwa tatizo hili kwa wanawake. Hii inatokana na ukweli kuwa, mama anaponyonyesha, homoni aina ya prolactin huwa katika kiwango cha juu. Pamoja na kazi nyingine za Prolactin, homoni hii pia humfanya mtu kuridhika baada ya kujamiana (sexual refractory period) kwa kuingiliana na ufanyaji kazi wa homoni nyingine ya dopamine ambayo humfanya mtu kufikia kilele.

Sababu nyingine ni kupungua kwa mzunguko wa damu katika sehemu za siri za mwanamke na hivyo kumsababishia maumivu wakati wa kujamiana, na kwa wanawake wenye matatizo ya homoni ya tezi la thyroid yajulikanayo kama hypothyroidism hupatwa na tatizo hili zaidi kuliko wanaume. Wapo baadhi ya wanawake wanaokumbwa na tatizo la vaginismus ambalo husababisha sehemu za siri za mwanamke kuwa ndogo wakati wa kujamiana na hivyo kumsababishia maumivu makali na kumfanya akose hamu ya kujamiana tena.

Aidha utumiaji wa vidonge vya kupanga uzazi au vya majira kwa muda mrefu (kwa wanawake), ugonjwa wa kisukari (wa wanaume na wanawake), uzito uliopitiliza (obesity) pamoja ugonjwa wa viungo vya mifupa yaani arthritis navyo vinaelezwa kuwa chanzo cha kuwepo kwa tatizo hili.

Ujauzito pia unaelezwa kuwa sababu nyingine ya baadhi ya wanawake kukosa hamu ya kujamiana. Hii inatokana na kuwepo kwa mabadiliko katika mfumo wa homoni na maumbile ya wanawake wakati wa ujauzito, hali inayowafanya baadhi ya wanawake kutojiamini.

Wanawake waliowahi kufanyiwa upasuaji wa kuondoa mfuko wa uzazi (hysterectomy) na kusababisha madhara katika neva inayohusika na kuongeza msisimko wakati wa kujamiana (pudendal nerve damage) huwa katika hatari ya kupata tatizo hili. Madhara ya neva hii pia huonekana hata kwa wanaume.

Visababishi vingine ni pamoja na madhara yatokanayo na matumizi ya baadhi ya dawa kama vile za kutibu shinikizo la damu (antihypertensives), msongo wa mawazo (antidepressants) na saratani; kuwa na ugonjwa wa moyo, saratani ya aina yoyote ile, au kuwa na wasiwasi (anxiety).

Kwa wanawake, uchovu unaotokana na kuzidiwa na majukumu ya kulea mtoto/watoto, kazi na kumhudumia mume wake nao unaweza kuchangia kukosa hamu ya kujamiana. Aidha mwanamke mwenye historia ya kubakwa, au aliyewahi kupata maumivu wakati wa kujamiana siku za awali kutokana na kutokuwa tayari kujamiana au kutotayarishwa vyema naye pia ana hatari ya kukumbwa na tatizo hili.

Kupenda mtandao (internet) kupita kiasi (internet addiction) nako kumeelezwa kuwa sababu nyingine ya kuwafanya wenza kukosa hamu ya kujamiana. Kwa mujibu wa utafiti mmoja uliofanyika mwaka 2011 huko nchini Marekani, ilionekana kwamba kati ya ndoa 6,000 zilizovunjika, asilimia 57 ya ndoa hizo zilisababishwa na mwenza mmoja au wote wawili kupenda kuchat au kutumia mtandao kupita kiasi na hivyo kusababisha kupotea kwa msisimko kati ya wenza na hatimaye kupungua uwezo au hamu ya kujamiana.

Uvutaji sigara ni chanzo kingine cha kukosa au kupungua hamu ya kujamiana na huathiri wote wanaume pamoja na wanawake. Uvutaji sigara hupunguza vichocheo aina ya testerone kwa wanaume, na kitendo cha kuwa na kiwango kidogo cha homoni hii husababisha wavutaji sigara wengi kupata tatizo la kupungukiwa uwezo wa kujamiana. Kadhalika uvutaji sigara hupunguza mzunguko wa damu unaopita kwenye uume hivyo kumfanya muhusika kushindwa kusimika au jongoo kushindwa kupanda mtungi (vascular impotence) na hatimaye kukosa uwezo wa kujamiana. Kwa wanaume, uvutaji sigara hupunguza kiwango na uzito wa shahawa (concentration of spermatozoa in semen) kwa takribani asilimia 22-57, wakati uwezo wa mbegu za kiume kuogelea kufikia mirija ya uzazi ya mwanamke nao pia hupungua kwa asilimia 20 ikilinganishwa na wasiovuta. Aidha tafiti kadhaa zimethibitisha uvutaji sigara unaweza kusababisha kuzalishwa kwa mbegu za kiume zisizo na maumbile ya kawaida hivyo kuongeza uwezekano wa kuharibika kwa mimba itakayotungwa (spontaneous abortion) au kuzaliwa kwa mtoto mwenye hitilafu za kimaumbile (birth defects). Pia uvutaji sigara uharibu mirija ya seminiferous tubules (sehemu ambapo mbegu za kiume hutengenezwa) iliyopo kwenye korodani na hivyo hupunguza wingi na uzito wa mbegu hizo. Mambo haya huweza kumfanya mwanaume ajihisi aibu kufanya mapenzi na mwenza wake hali ambayo ikiendelea kwa muda mrefu huwa sugu na kusabsbisha kukosa hamu ya kujamiana moja kwa moja.

Sababu nyingine ni pamoja na umri kuwa mkubwa. Wanaume wenye umri wa kuanzia miaka 40 huwa na ongezeko kubwa la kiwango cha homoni ya prolactin ambayo husababisha kuongezeka kwa kichocheo kingine cha dihydro-testerone inayosababisha kuvimba kwa tezi dume hatimaye kupunguza uwezo wa kusimika kwa mwanaume, na mwishowe kukosa au kupungua hamu ya kujamiana.

Na mwisho ni tabia ya kuendesha baiskeli kwa muda mrefu (kwa kipindi kimoja) ambayo hugandamiza neva na mishipa ya damu inayopeleka damu kwenye uume na kusababisha mtu kupungukiwa na uwezo wa kusimamisha kwa muda na hatimaye kupungukiwa hamu ya kujamiana.

Si mara chache tumewahi kushuhudia au kusikia mtu au kundi la watu likiugua ghafla baada ya kula chakula katika mkusanyiko au sherehe. Bila shaka nawe ni mmojawapo wa waliowahi kukumbwa na hali hii.

Aidha tumewahi pia kusikia au kushuhudia hata baadhi ya watu wakiamini kulishwa sumu baada ya kula chakula katika shughuli au sherehe fulani. Hali hii imewahi kuzusha tafrani na sintofahamu miongoni mwa wanajamii kwa vile si wengi wanaofahamu hasa chanzo cha hali hiyo.

Lakini usumu au maambukizi katika chakula (food poisoning) ni nini hasa?

Food poisoning ni hali ya kuchafuka kwa chakula kunakotokana na uwepo wa vimelea mbalimbali kama vile bacteria, virusi, au parasites au sumu zao ndani yake. Hali hii hutokea wakati unapokula chakula au kunywa vinywaji/maji yaliyochanganyika na vimelea hawa hususani vya bacteria wa jamii ya Staphylococcus au Escherichia coli (E. coli).

Ieleweke kuwa food poisoning haimaanishi sumu inayowekwa na mtu/watu kwenye chakula bali hutokana na vijidudu vya magonjwa mbalimbali kama vile bacteria.

Vihatarishi vyake

Kwa kawaida food poisoning hutokea zaidi baada ya kula vyakula vilivyoandaliwa kwenye mikusanyiko kama vile cafeteria za shule au kazini, kwenye misiba, matanga, hitma, maulid, ngoma, harusi, mahoteli, na mikusanyiko mingine yeyote ambayo inahusisha ulaji wa chakula cha pamoja; ambapo mtu mmoja au kundi la watu hupatwa na usumu huo na kuwa wagonjwa.

Ripoti ya utafiti iliyochapishwa katika jarida la Health Physiology na kuchapwa katika wavuti ya WebMD inadai kuwa watu wazima wenye tabia ya kufanya mazoezi ya kuendesha baiskeli au kujinyosha viungo vyao huongeza uwezo wa kukumbuka zaidi kuliko wale wasiofanya kabisa.

 

Utafiti huo unadai kuwa pamoja na kwamba kimuundo ubongo haufanani na misuli lakini kadri mtu anavyozeeka kuingia utu uzima, ufanyaji mazoezi husaidia kuimarisha uwezo wake wa kukumbuka na hata kufikiria mambo mapya.

Jambo la kutia moyo ni kuwa huna haja ya kufanya mazoezi mazito kwa vile mazoezi mepesi tu kama ya kunyoosha nyoosha viungo yanatosha kuleta kabisa matokeo ya kuridhisha.

Uchunguzi huo ambao ulihusisha watu wazima waume kwa wake waliokuwa wakiendesha baiskeli au mazoezi ya kunyoosha viungo kwa muda wa saa mbili kwa wiki kwa muda wa miezi sita ulionesha kuwepo kwa maendeleo makubwa katika uwezo wao wa kukumbuka mambo na hata kufikiria mambo mapya.

Mmoja wa watafiti hao Kirsten Hotting kutoka chuo kikuu cha Hamburg, Ujerumani anasema kuwa mtu anayefanya mazoezi ya aina mbalimbali kwa pamoja ana uwezekano wa kupata matokeo mazuri zaidi.

Ripoti hii inaweza kutafsiriwa kama changamoto kwa watu walio katika nafasi mbalimbali za kutoa maamuzi kiuongozi kuwa tabia ya ufanyaji mazoezi inaweza kuimarisha sana uwezo wao wa kukumbuka mambo na kufikiria mambo mapya, na hivyo kuzidi kuongeza tija katika utendaji wao wa kila siku. Aidha hii ni changamoto hata kwa watu wengine kuanzisha utaratibu wa kujifanyia mazoezi mepesi kwa ajili ya kuimarisha afya ya akili na mwili kwa ujumla.

Ripoti ya utafiti huu inapatikana katika Jarida la Health Psychology

Mwanamke mmoja mwenye umri wa miaka 47 kutoka jimbo la Michigan nchini Marekani amepata ugonjwa adimu sana(rare disease) wa mifupa baada ya kunywa chai iliyotengenezwa kwa aina mia moja ya majani ya chai kwa wingi (lita 3 kwa siku) kwa miaka 17 mfululizo, watafiti kutoka Marekani wamesema.

Mwanamke huyo alikwenda hospitali kuonana na Daktari baada ya kuwa na maumivu makali kwenye kiuno,mikono,miguu na kiuno kwa miaka mitano.

Baada ya kufanyiwa kipimo cha X-ray iligundulika mama huyo ana ugonjwa huo adimu ambao huonyesha dalili za kuongezeka kwa uzito wa mifupa ya uti wa mgongo(dense spinal vertebrae) pamoja na kushikana(calcifications of ligaments) kwa viunganishi vya mifupa ya kwenye mikono’’ alisema mmoja wa watafiti Dr. Sudhaker D. Rao, Daktari bingwa wa magonjwa vichocheo vya mwili na virutubisho vya mifupa na vya mwili (Endocrinologist and bone and mineral metabolism physician) katika hospitali ya Henry Ford Hospital,Marekani.

Dr. Rao alihisi mama huyo ana ugonjwa wa mifupa unaojulikana kama skeletal fluorosis unaosababishwa kwa kutumia kwa wingi madini aina ya fluoride (Fluoride hupatikana kwenye maji au chai)

Kiwango cha madini ya fluoride katika damu ya mama huyo kilikuwa juu mara nne zaidi ya kiwango kinachohitajika kwenye mwili wa mwanadamu.

Ugonjwa wa skeletal fluorosis huonekana sana kwenye maeneo ambayo kiasili yana madini ya fluoride kwa wingi kama baadhi ya maeneo nchini India na China (katika nchi nyingi kiwango kidogo cha fluoride huweka kwenye maji, dawa za meno kama kinga dhidhi ya ugonjwa wa meno unaojulikana kama cavities)

‘’Mgonjwa alipewa rufaa ya kuja kuniona kwa sababu madaktari walie muona mwanzo walidhani ana saratani ya mifupa, lakini baada ya mimi kuona X-ray za mgonjwa,mara moja nilitambua kuwa ni ugonjwa wa skeletal fluorosis kutokana na kuwahi kuona wagonjwa wa aina hiyo nilipokuwa kwetu nchini India’’alisema Dr. Rao

For quality health care delivery, continuous supportive supervision is needed in order to be able to fill gaps that are experienced by health care providers at the lower health care level who for some reasons can not deliver what is expected from the community. Supervision is an excellent opportunity to provide follow-up training, improve performance, and solve other systemic problems that contribute to poor health care delivery.

Following a number of challenges experienced during ordinary supportive supervision, in the year 2010, Bahi District Council introduced cascade supervision to its health care facilities. The cascade supervision is all about empowering staffs at the health centers to be able to conduct supportive supervision to the dispensaries’ staffs who in then provide supervision to the communities within their catchment areas.

Prior to the introduction of cascade supervision, we conducted training to the people dealing with this system including all in-charges of health care facilities and health officers. The district was then divided into four zones (so called the cascade zones) and 31 nodes (so called cascades nodes).

In each cascade zones there was one health center while each node has one dispensary. Within its zone, each health center supervises an average of seven dispensaries and each dispensary, on the other hand, supervises communities within its catchment area. Upon implementation of cascade supervision we have been able to cut down costs by 25% which, would have otherwise, come from ordinary supportive supervision.

Bahi District Council with an area of 5948 sq km has a total of 35 health care facilities (4 health centers and 31 dispensaries). Nevertheless, process for construction of the district hospital is underway. Through the experience of Bahi District Council, cascade supportive supervision remains to be an option for effective delivery of quality health care for resource limited settings like Bahi District Council which has very diverse geography with some areas being difficult to reach especially during rainy seasons.

Bahi District Council represents many districts in Tanzania which experience difficulties in conducting cost effective supervision. Therefore cascade supervision proves to be a alternative choice for improving health care delivery in resource limited settings.

As we believe this is the high time, we urge other stakeholders in the health sector in other districts, to implement this strategy in order to improve the quality of health care delivery in their districts and in the whole country.

The Author is also the District Medical Officer of Bahi District, Dodoma, Tanzania

  

 Nikiwa kama mjukuu kipenzi wa bibi yangu, huwa napenda sana kutumia muda wangu wa mapumziko kujadiliana naye mambo mbalimbali yanayohusu jamii, iwe yaliyokuwa yanatokea hapo awali au yanayoendelea kutokea. Ilikuwa ni siku ya jumapili baada ya kutoka kwenye mihangaiko, niliingia ndani na kumuita bibi kwa jina lake la utani ‘Nyaksi’ ili twende nje tukapunge upepo na mazungumzo ya hapa na pale.

Nikipata Ushauri wa Afya toka kwa Dk Mayala

   Kama ilivyo ada yangu, huwa napenda sana kutafiti mambo mbalimbali, nikamuuliza bibi, eti bibi nimewahi kusikia kuwa wakati wa enzi zenu mlikuwa hamruhusiwi kula mayai wakati wa ujauzito kwa kuwa mtoto atazaliwa bila nywele? Bibi Nyaksi huku akitabasamu akanigeukia na kusema, "umeshaanza, kwanza usikumbushe enzi zile bado nipo mbichi" akimaanisha wakati yupo msichana. Wote tukatabasamu kwa pamoja. Nyaksi akaendelea kusema sio mayai tu, bali vyakula vyote nyenye virutubisho kwa wingi ambavyo ninyi vijana wa leo mnaviita ‘purotini’, akiitamka protini kwa lafudhi ya kizee. Nyaksi alisema tulizuiliwa kula vyakula hivyo kwa mlengo wa mwiko, akaendela kusema, unajua Babu (jina langu alilopenda sana kuniita Nyaksi) wazee walitumia mwiko ili kututisha lakini ukweli ni kuwa wakati ule hakukuwa na tekenolojia (akimaanisha teknolojia) hivyo kama utakula vyakula vyenye virutubisho sana vitamfanya mtoto awe mkubwa, na hivyo kama utashindwa kujifungua kwa njia ya kawaida basi hakutakuwa na njia nyingine ya kukusaidia. Nyaksi akaendelea ninyi vijana wa siku hizi mna raha, hospitali nyingi, madaktari wengi huku mna njia nyingi mbadala ikiwemo ya upasuaji na nyinginezo. 

   Nilimuacha Bibi Nyaksi amalizie maneno yake, halafu nikamuuliza, kama sisi tuna teknolojia na njia nyingi za kisasa, sasa inakuwaje urefu wa maisha wa vizazi vyetu unazidi kupungua kadri teknolojia inavyozidi kukua? Nyaksi alicheka sana, huku akipigapiga makofi ili kuvuta hisia alisema " hakuna kizuri kisicho na kasoro". Baada ya hapo tukaacha kuongelea masuala ya afya na kuketi chini ili kupunga upepo uliokuwa ukivuma kwa kasi kutokea Kinyanyiko. 

   Kipindi chote naburudika na upepo uliokuwa unavuma ukitokea kwenye mabonde ya Kinyanyiko nilikuwa natafakari mambo mengi kuhusu maneno ya Nyaksi. Misemo yake ilikuwa inazungukazunguka kichwani kwangu , huku maneno "Hakuna kizuri kisicho na kasoro " na " ninyi mnaishi kwenye ulimwengu wenye tekinolojia" vikijitokeza mara kwa mara. Lakini je, hizi teknolojia zinatunufaisha vipi? Zipi faida na hasara zake? Hivyo nikawa nachorachora chini nikiainisha viambatanishi vyote vya hii tunayoiita teknolojia, nikarudi haraka nyumbani na kuchukua iPad yangu kuanza kuandika makala hii ambapo tutaiangalia teknolojia kwa mapana na jinsi gani teknolojia inavyoweza kuongeza ufanisi katika medani ya afya.