Image

Upungufu wa akili ni tatizo ambalo kwa ujumla hutokea kabla ya mtu kuwa mkubwa (adulthood) na huambatana na dalili za kupunguwa uwezo wa akili ya utambuzi na kutafakari (cognitive functions) pamoja na kushindwa kukua kwa tabia za kuendana na mazingira yanayomzunguka mtu (adaptive behavior). Pia kitaalamu, upungufu wa akili hujulikana kama mtu yoyote mwenye IQ (Intelligence Quotient) chini ya 70.

Upungufu wa akili ni hali ya kuwa na mapungufu katika ukuaji (development deficit) yanayoanza utotoni ambayo husababisha kupungua uwezo wa kusoma (intellect), kutafakari, utambuzi na kutoweza kuendana na majukumu ya kila siku ya maisha.

Ukubwa wa Tatizo (Epidemiology)

Upungufu wa akili ni tatizo kubwa sana duniani.Huathiri asilimia 1-2 ya watu wote duniani.Huonekana sana kwa wanaume kuliko wanawake (inakisiwa huonekana mara mbili zaidi kwa wanaume kuliko wanawake). Upungufu wa akili wa kati (mild mental retardation) huonekana sana kwa watu wa kipato cha chini lakini upungufu wa akili wa kiwango cha juu hutokea uwiano sawa katika jamii ya matabaka yote na huonekana sana katika umri kati ya miaka 10 hadi 14.

Upungufu wa akili sio ugonjwa (axis II disorder in DSM-IV) kutokana na dalili na viashiria vyake bali ni tatizo la mfumo wa utambuzi wa watu wenye kuhitaji huduma za kijamii na elimu maalum ili kuweza kumudu majukumu yao ya kila siku. Mara nyingi upungufu wa akili hutokea kabla ya mtu kufikisha umri wa miaka 18.

Tungependa kwa yoyote mwenye takwimu kutoka afrika mashariki za tatizo hili la upungufu wa akili kutoka katika hospitali za magonjwa ya akili za Butabika National Referral and Teaching Mental Hospital (Kampala, Uganda), Port Reitz District Hospital (Mombasa, Kenya), Mathare Mental Hospital (Nairobi, Kenya), Lutindi Mental Hospital (Tanga, Tanzania) na Mirembe Psychiatric Referral Hospital (Dodoma, Tanzania).

Tabia za Kuendana na Mazingira (Adaptive behavior) ni nini?

Tatizo la kiakili la kujihisi mnene na kupoteza hamu ya kula au Anorexia nervosa ni tatizo linawaathiri watu wengi na kuwafanya kupoteza uzito zaidi ya ule unaokubalika kulingana na umri na urefu wa muhusika.

Watu wenye tatizo hili wana hali ya kuwa na hofu isiyo kifani ya kuongezeka uzito hata kama, kiukweli, wana uzito mdogo (wamekonda) kuliko kawaida. Wanaweza kujinyima au kupunguza kula makusudi (dieting), kufanya mazoezi ya kupunguza uzito kuliko kawaida au hata kufanya njia nyingine zozote ilimradi wapungue uzito.

Chanzo na vihatarishi vya tatizo hili

Chanzo halisi cha tatizo hili bado hakifahamiki rasmi. Hata hivyo, mambo kadhaa yanahusishwa na kutokea kwake. Mambo hayo yanajumuisha sababu za kinasaba (genetic factors) na vichocheo mwili (hormones). Aidha masuala ya kijamii yenye kuchochea wana jamii kama vile baadhi ya wasichana kupenda maumbo madogo (vimodo) nayo pia yanahusishwa.

Kipindi cha nyuma, masuala kama matatizo katika familia yalikuwa yakihusishwa na uwepo wa tatizo hili pamoja na matatizo mengine yanahusiana na ulaji wa muhusika ingawa kwa sasa uhusiano wake unaonekana kuwa si wa nguvu sana.

Vihatarishi vya anorexia nervosa vinajumuisha

 Upungufu wa akili ni tatizo ambalo kwa ujumla hutokea kabla ya mtu kuwa mkubwa (adulthood) na huambatana na dalili za kupunguwa uwezo wa akili ya  utambuzi na kutafakari  (cognitive functions) pamoja na kushindwa kukua kwa tabia za kuendana na mazingira yanayomzunguka mtu (adaptive behavior). Pia kitaalamu, upungufu wa akili hujulikana kama mtu yoyote mwenye IQ (Intelligence Quotient) chini ya 70.
Upungufu wa akili ni hali ya kuwa na mapungufu katika ukuaji (development deficit) yanayoanza utotoni ambayo husababisha kupungua uwezo wa kusoma (intellect), kutafakari, utambuzi na kutoweza kuendana na majukumu ya kila siku ya maisha.
 
Ukubwa wa Tatizo (Epidemiology)

Upungufu wa akili ni tatizo kubwa sana duniani.Huathiri asilimia 1-2 ya watu wote duniani.Huonekana sana kwa wanaume kuliko wanawake (inakisiwa huonekana mara mbili zaidi kwa wanaume kuliko wanawake). Upungufu wa akili wa kati (mild mental retardation) huonekana sana kwa watu wa kipato cha chini lakini upungufu wa akili wa kiwango cha juu hutokea uwiano sawa katika jamii ya matabaka yote na huonekana sana katika umri kati ya miaka 10 hadi 14.
Upungufu wa akili sio ugonjwa (axis II disorder in DSM-IV)  kutokana na dalili na viashiria vyake bali ni tatizo la mfumo wa utambuzi wa watu wenye kuhitaji huduma za kijamii na elimu maalum ili kuweza kumudu majukumu yao ya kila siku. Mara nyingi upungufu wa akili hutokea kabla ya mtu kufikisha umri wa miaka 18. Tungependa kwa yoyote mwenye takwimu kutoka afrika mashariki za tatizo hili la upungufu wa akili kutoka katika hospitali za magonjwa ya akili za Butabika National Referral and Teaching  Mental Hospital (Kampala, Uganda), Port Reitz District Hospital (Mombasa, Kenya), Mathare  Mental Hospital (Nairobi, Kenya), Lutindi Mental Hospital (Tanga, Tanzania) na Mirembe Psychiatric Referral Hospital (Dodoma, Tanzania).
 
Tabia za Kuendana na Mazingira (Adaptive behavior) ni Nini? 

Tabia za kuendana na mazingira ni jinsi mtu anavyoweza kumudu matakwa ya kujihudumia mwenyewe kila siku pasi na kumtegemea mtu yoyote kutokana na umri wake, tabaka lake, utamaduni pamoja na jamii inayomzunguka  kutokana  na vipengele viwili kati ya hivi vifuatavyo;

  • Mawasiliano (Kuweza kuwasiliana na watu)
  • Kuweza kujihudumia  katika shughuli zinazohitaji kutumia akili (functional academic skills)
  • Kuweza kuishi mazingira ya nyumbani na kazini
  • Kuwa na uwezo wa kuchanganyikana na jamii katika masuala ya afya na usalama wake
  • Kuweza kutumia huduma za jamii ambazo zitamfanya kuishi maisha ya furaha 


Ni vizuri kutambua ya kwamba tabia hizi hutegemea sana elimu, uhamasishaji, tabia za mtu binafsi, kupewa fursa za kijamii na za kiufundi (vocational skills), matatizo ya akili na magonjwa mbalimbali ya akili.
Intelligence kitaalamu ni uwezo wa ubongo katika kufikiri, kutatua matatizo, kuchagua au kuwa na busara (reason), na kuelimika.
 
IQ= Mental age (Umri wa akili)                                             ×  100

Chronological age (Umri wa kawaida wa binadamu)
 
Makundi ya Upungufu wa Akili                                                            Kundi Kipimo cha IQ

Upungufu wa akili uliopitiliza kabisa (Profound Mental Retardation)         Chini ya 20

Upungufu wa akili mkubwa (Severe Mental Retardation)                          20-34

Upungufu wa akili wa kati (Moderate Mental Retardation)                        35-49

Upungufu wa akili  (Mild Mental Retardation)                                            50-69

Upungufu wa akili wa kawaida (Borderline Intellectual  Functioning)         70-84
 
Mtu aliye kwenye kundi la upungufu wa akili (Mild Mental Retardation) anaweza kuelimika, na Yule aliye na upungufu wa akili wa kati, mtu huyu anaweza kufunzwa kazi za kumuwezesha kumudu maisha yake ya kila siku. Wale walio na upungufu wa akili mkubwa (Severe MR) na kundi la waliopitiliza (Profound MR) hawawezi kufunzwa chochote na kufundishika.
Kwa hiyo mtoto aliye na umri sawa wa akili na umri sawa wa kibinadamu atakuwa na kipimo cha akili 100 (yaani IQ=100). Kwa wale watoto wenye vipaji maalum, kipimo cha akili yao huwa zaidi ya 100 (IQ>100), na kwa wale wenye akili ya kawaida kipimo cha akili huwa chini ya 100 lakini hakishuki chini ya 85.
 
Upungufu wa Akili wa Kawaida (Borderline Mental Retardation)

Huwa na akili yakipimo cha IQ= 70-85%. Wanauelewa mdogo shuleni (Slow learners) lakini wanaishi maisha ya kawaida yaani bila kupata taabu yoyote katika maisha yao ya kila siku na wanaweza kuajiriwa.
 
Upungufu wa akili (Mild Mental Retardation)

Huwa na akili ya kipimo cha IQ=50-70. Asilimia kubwa ya watu wenye upungufu wa akili huwa kwenye kundi hili (asilimia 85-95). Wanatambulika kama wanaoweza kuelimika. Wanaweza kujifunza kusoma, kuandika, na kufanya hesabu rahisi rahisi (simple arithmetic calculations). Hawa wanahitaji shule maalum ili waje kuweza kumudu majukumu yao ya maisha ya kila siku baada ya muda mrefu.Wanakuwa na upungufu mdogo katika uwezo wao wa kuhisi na utambuzi wa vitu (minimal sensorimotor deficits) na ni vigumu kutambua kwamba wanaupungufu wa akili mpaka baadae maishani. Katika ujana wao wanaweza kupata elimu hadi darasa la sita.Ukubwani, hupata uwezo wa kujihudumia wenyewe katika mahitaji yao ya kila siku lakini wanahitaji uangalizi, ushauri, kupewa mwongozo katika majukumu yao ya kifamilia na hasa wanapopata msongo wa mawazo au wakati wamepata matatizo ya kiuchumi.
 
Upungufu wa Akili wa Kati (Moderate Mental Retardation)

Huwa na akili yakipimo cha IQ=35-50. Asilimia 10 tu ya watu wote wenye upungufu wa akili ndio huwa kwenye kundi hili.Wanatambulika kama wasioweza kufundishika (untrainable) ingawa wengi wao wanaweza kuelimika. Utotoni mwao wanakuwa na mawasiliano mabaya ya kijamii, lakini wanaweza kujifunza kuzungumza, kutambua majina yao na baadhi ya maneno rahisi ambapo kutokana na haya ambayo nimeelezea hapo juu, kwa sasa wanatambulika kama kundi linaloweza kufundishika.Kawaida, huacha shule baada ya kufika darasa la pili (Standard 2). Wanaweza kufundishika katika kazi ambazo hazihitaji kutumia akili ama kazi za mikono.Msongo wa mawazo huathiri mafunzo yao hivyo ni muhimu kuboresha  mazingira yao na kuwahudumia vizuri ili wasipate msongo wa mawazo. 


Mara nyingi, uwezo wao wa kuelewa watu wanapozungumza ni mzuri kuliko uwezo wao wa kuzungumza na hii huwafanya kupata msongo wa mawazo. Uzungumzaji wao ni wa kawaida na hueleweka vizuri na wale wanaoishi nao au wale wanaofahamiana nao vizuri. Vitendo kama uvaaji nguo, kula, na kujiweka msafi, huchukua muda mrefu kwao kujifunza. Wanahitaji msaada katika matumizi ya hela na hata kuvuka barabara.
 
Upungufu wa Akili Mkubwa (Severe Mental Retardation)

Huwa na akili ya kipimo cha IQ=20-35 na huonekana kwa watu wenye upungufu wa akili kwa asilimia 5 tu. Hutambulika mapema kwa kutokuwa na uwezo wa kutambua vitu mbalimbali (Poor motor development). Watu hawa hawana uwezo wa kuzungumza na kuwasiliana au hupata uwezo huo baadae maishani. Huitaji shule maalum pamoja na wataalamu wa tiba ya sauti ili waweze kujifunza kuzungumza.Chini ya uangalizi, huweza kujifunza shughuli ndogondogo.
 
Upungufu wa Akili Uliopitiliza (Profound Mental Retardation)

Huwa na akili ya kipimo cha chini ya 20 yaani IQ<20. Asilimia 1-2 ya watu wenye upungufu wa akili ndio walio kwenye kundi hili. Mara nyingi wanakuwa na ugonjwa au matatizo ya sehemu ya mishipa ya fahamu ambayo husababisha upungufu wa akili.Dalili za kuwa na uwezo finyu wa kutambua na kuhisi mambo mbalimbali, kushindwa kuelimika, kujihudumia, kufanya kazi, kujitunza huonekana mapema sana. Huitaji msaada wa kijamii pamoja na kuhudumiwa katika maisha yao ya kila siku.
 
Aina za Upungufu wa Akili

Kuna aina mbili za upungufu wa akili ambazo ni;
1.Syndromic  mental retardation – Hii ni upungufu wa akili (intellectual deficits)  unaoambatana na magonjwa mbalimbali  pamoja na  viashiria  na dalili za kitabia (behavioral signs).
2.Non syndromic mental retardation – Upungufu huu wa akili hausiani na magonjwa au ugonjwa wowote.
 
Pathofiziologia (Pathophysiology)

Upungufu wa akili ni mjumuiko wa matatizo katika mfumo wa fahamu (CNS functions) ambapo sehemu inayojulikana kama cortical structures (ambayo huusisha pamoja na sehemu zingine kama hippocampus na medial temporal cortex) ndio huathirika. Watu wengi wenye upungufu wa akili hawaonyeshi kuathirika katika mfumo wao wa fahamu. Ni aslimia 10-15 ya watu wote wenye upungufu wa akili ambao ndio wanaonyesha kuathirika katika mfumo wao wa fahamu.
Matatizo katika mfumo wa fahamu ambayo huonekana sana ni kichwa maji (hydrocephalus), neural tube defects, microcephaly na (disorders of migration- the lissencephalis na muunganiko wa mwatuko wa ubongo {agenesis of corpus carlosum} ambayo huonekana mara chache).


Watu wengi wenye upungufu wa akili aina ya mild mental retardation na wenye matatizo mengine ya ufahamu (other learning disorders), huwa hawana matatizo katika mfumo wao wa fahamu, madhara katika neva na dysmorphisms lakini wanauwezekano mkubwa wa kutoka katika familia zenye hali duni ya kiuchumi, familia yenye kipimo cha akili ndogo (low IQ), na elimu duni.
 
Nini husababisha upungufu wa akili?

Zipo sababu nyingi ambazo husababisha upungufu wa akili ambazo ni kama ifuatavyo;

  • Matatizo ya kurithi (genetic factors)
  • Antenatal factors
  • Postnatal factors
  • Matatizo ya kijamii na kitamaduni (socio-cultural factors)

Magonjwa ya akili (psychiatry disorders)
 
Thuluthi moja (1/3) ya watu wenye upungufu wa akili chanzo hasa hakijulikani.
 
Matatizo ya viashiria vya urithi (genetic factors)

  • Chromosal abnormalities kama down syndrome, fragile X syndrome (mgonjwa anakuwa na kichwa kikubwa, masikio makubwa kama ya popo, uso mrefu, korodani kubwa kupitiliza na nyayo zinakuwa bapa {flat feet},huwa na matatizo ya lugha na sauti, hii husababishwa na matatizo katika ncha ya mkono mrefu wa chromosome)
  • Metabolic disorders kama phenylketonuria, homocystinuri, galactosemia nk.
  • Magonjwa kwenye ubongo (Gross disease of the brain) kama cerebral dysgenesis, tuberose sclerosis, neurofibrosis nk.

Madhara ya kwenye ubongo (brain malformations) kama  nueral tube defects, kichwa maji na microcephalus
 
Antenatal factors

  • Matatizo ambayo hutokea wakati mtoto bado hajazaliwa (yaani yanayompata mtoto wakati bado yupo tumboni mwa mama yake). Haya yanaweza kuwa;
  • Magonjwa kama ugonjwa wa kaswende (syphilis), TORCH
  • Sumu (intoxications) kama madini ya risasi (lead), madawa ya kulevya, unywaji pombe wakati wa ujauzito nk.
  • Physical damage – Tiba ya mionzi au vipimo vya mionzi, injury, ukosefu wa hewa ya oksijeni kwa mtoto (hypoxia).
  • Matatizo ya kondo la uzazi (Placental dysfunctions) – Toxaemia, ukosefu wa virutubisho sahihi katika ukuaji wa kondo (Nutritional growth retardation).
  • Matatizo katika mfumo wa vichocheo mwilini (Endocrine disorders) – Hypothyroidism (ugonjwa wa tezi la koo), ugonjwa wa kisukari kwa mama mjazito, hypoparathyroidism.

 
Perinatal factors

  • Matatizo yanayotokea wakati mtoto anazaliwa (wakati wa kujifungua kwa mama mjazito)
  • Ukosefu wa hewa ya oksijeni (Birth asphyxia), cerebral palsy nk
  • Madhara ya mtoto kuzaliwa njiti (complications of prematurity) kama uvujaji damu ndani ya ubongo (intraventricular haemorrhage).
  • Hypoxic Ischemic encephalopathy
     


Post-natal factors

  • Matatizo yanayotokea baada ya mtoto kuzaliwa
  • Injury – Head injury (kuumia kichwa)
  • Sumu (Intoxication) kutokana na madini ya risasi, mercury nk.

Magonjwa kama ugonjwa wa uti wa mgongo (meningitis), encephalitis (maambukizi kwenye ubongo)
 
Socio-cultural factors (Matatizo ya kijamii na kitamaduni)

Kutokuwa na uwezo wa kujumuika na jamii huchochewa na ukosefu wa elimu, kiwango duni cha uhamasishaji, tabia ya mtu, ucheshi wa mtu,utapia mlo, mimba za utotoni (kwani huleta umaskini, utapia mlo, afya duni, kuathirika kwa mama na hivyo kumuathiri mtoto), vocational opportunities pamoja na magonjwa ya akili na magonjwa mbalimbali.

Kukosekana kwa vichocheo hivyo au kuwepo kwa magonjwa ya akili na baadhi ya magonjwa mbalimbali huweza kusababisha upungufu wa akili. Ikumbukwe ya kwamba akili ya mtoto huwa inakuwa kwa hiyo ni muhimu apewe fursa ya kuweza kukuza akili yake.
 
Magonjwa ya akili (Psychiatric disorders)

  • Pervasive developmental disorders (Autistic spectrum disorders). 

 

Image Source: https://newrepublic.com

Katika sehemu ya kwanza ya makala ya upungufu wa akili tuliona makundi ya upungufu wa akili, ukubwa wa tatizo hili, visababishi na pathofiziolojia yake.
 
Sehemu hii ya pili tutaangalia dalili, vipimo vya uchunguzi, tiba yake pamoja na jinsi ya kujikinga na tatizo hili la upungufu wa akili.

Dalili na Viashiria vya Upungufu wa Akili

  • Kuchelewa katika ukuaji wa uwezo wa kuongea/kuzungumza
  • Upungufu wa kumbukumbu (deficits in memory skills)
  • Matatizo katika kufahamu mambo ya kijamii
  • Upungufu wa uwezo wa kutatua matatizo
  • Kuchelewa kukua kwa tabia za vitendo vya kujihudumia mwenyewe (kama kufunga vifungo vya shati nk)
  • Kuendelea kuwa na akili za kitoto
  • Kupungua uwezo wa kusoma

Utangulizi

Mada hii ina lengo la kuzungumzia tatizo la kuwa na hofu au wasiwasi uliopita kiasi au kwa kitaalamu Generalized anxiety disorder (GAD). Kwa ajili ya kutofautisha kati ya hofu iliyopitiliza na hofu ya kawaida ambayo yaweza kumkumba mwanadamu yeyote, wakati fulani fulani mwandishi atatumia maneno anxiety au GAD katika kuwasilisha ujumbe wake.

Hofu iliyopitiliza au au anxiety au GAD huambatana na hali ya kuwa na wasiwasi kupita kiasi juu ya maisha ya kila siku pamoja na matukio yake bila hata muhusika kuwa na sababu maalum ya kuwa na hofu hiyo. Kwa maneno mengine ni kuwa, watu wenye anxiety hujihisi hofu kubwa bila ya kuwa na sababu yeyote ya msingi ya kuwafanya wawe hivyo. Mara nyingi watu wenye tatizo hili huwa na tabia ya kuhisi kwamba janga kubwa litawatokea karibuni au maafa yatamkumba katika maisha yake na daima hawaachi kuwa na hofu isiyo na sababu juu ya familia zao, pesa, afya, ajira, masomo au hata biashara zao.

Maisha yao ya kila siku huwa na mchanganyiko wa hofu, wasiwasi na huzuni, kiasi kwamba hatimaye hofu hutawala mawazo  ya muhusika kiasi cha kuingilia utendaji wake wa kila siku ikiwemo kazi, masomo, shughuli zake za kijamii, na hata mahusiano na mwenza wake wa ndoa.

Dalili za hofu iliyopitiliza (anxiety) ni nini?

Utangulizi

Ugonjwa wa Alzheimer's ni miongoni mwa magonjwa ya ubongo yanayoathiri zaidi wazee au watu wa umri wa makamo. Ugonjwa huu ambao huanza polepole na kuchukua muda mrefu kujitokeza kwa kawaida hauoneshi dalili ya kupata nafuu mara unapoanza.

Ugonjwa wa Alzheimers’s ni miongoni mwa makundi ya magonjwa ya akili yanaitwa kitaalamu kama dementia na ambao huathiri zaidi watu wenye miaka 65 au zaidi.

Ugonjwa wa Alzheimer’s unasababishwa na nini?

Mpaka leo hii, chanzo halisi cha ugonjwa wa Alzheimer’s bado hakijajulikana. Hata hivyo, kuna nadharia kadhaa zilizoibuliwa na wanasayansi kuhusiana na baadhi ya visababishi vya ugonjwa huu. Nadharia inayoonekana kukubalika mpaka sasa ni ile ya uhusiano wa kuwepo kwa jamii ya protein inayoitwa amyloid na ugonjwa huu.

Wanasayansi wameonesha kuwa mabadiliko katika vinasaba vinavyodhibiti uzalishwaji wa protini hii ya amyloid ndiyo chanzo kikuu cha ugonjwa huu. Aidha ushahidi uliooneshwa na watafiti hao unasema kuwa mabadiliko haya ya vinasaba yamethibika kwa takribani zaidi ya nusu ya wagonjwa wote waliogunduliwa kuwa na ugonjwa huu.

Katika wagonjwa wote hawa waliofanyiwa utafiti imeonekana kwamba mabadiliko hayo ya vinasaba yamesababisha uzalishwaji uliopitiliza katika ubongo wa aina fulani ya vipande vya protini ijulikanayo kitaalamu kama ABeta (Aβ). Wataalamu wengi wanaamini kuwa, kukosekana kwa udhibiti wa uzalishaji wa aina hii ya protini kunakosababisha protini hii kuwa nyingi mno kwenye ubongo kuliko inavyoweza kuharibiwa ndiko kunakosababisha ugonjwa huu.

Introduction

Bahi district is one amongst six districts that make up Dodoma region. It extends between latitude 4o and 8o South and between longitude35o and 37o East. The district has an area of 5948 square km, and borders Kondoa district to the north, Manyoni to the west, Dodoma municipal to the south west and Chamwino district to the East. The district is divided into 4 divisions of Chipanga, Bahi, Mundemu and Mwitikila. The four divisions have a total of 21 wards, 56 villages and 1559 hamlets. The 2002 national census projected a population density of about 238,951 (District Council profile, 2010).

Health care facilities

Bahi district council has no district hospital, however, it has a total number of 35 health care facilities. Among these heath care facilities, six are health centers and 29 are dispensaries. There are 27 health care providers who have been trained to manage mental illnesses.

Background on Mental Health

The WHO defines health as a state of complete physical, psychological and social well being, and not just the absence of disease or infirmity.