Image

Tatizo la madawa ya kulevya limetokea kuwa janga kubwa duniani kote, watu wengi wameathirika na janga hili. jinsia zote wanaume, wanawake, na vilevile rika zote vijana na wazee pia.

Hapa tutaongelea aina mbili za madawa ya kulevya yaani Cocaine na Heroin.

Cocaine

Hutokana na majani ya mmea uitwao kitaalamu Erythroxylum coca bush.

Aina hii ya dawa ya kulevya hutolewa kwa mifumo ifuatayo

  • Unga ambapo mitaani hujulikana kama ‘coke’ na hutumika kwa kuvutwa puani kama unga, au kuyeyushwa na maji na kuchomwa kwenye mshipa wa damu.
  • Crack ambapo mitaani hujulikana kwa jina hilohilo crack au rock, na hutengenezwa kwa kuchanganywa na kemikali. Na hutumika kwa kuvutwa kama sigara.

Cocaine pindi inapoingia kwenye damu huenda kwenye ubongo na kuzuia ufyonzwaji wa vihisishi vifuatavyo: dopamine, norepinephrine na serotonin, kutoka kwenye ubongo. Hivyo ubakia kwenye ubongo. Na vihisishi hivi husababisha ile hali ya furaha, mchangamfu na kujisikia mwenye nguvu kitaalamu euphoria. Na huweza kuwa kwenye hali hii kwa nusu saa tu.
Mara tu baada kutumia dawa hii dalili zifuatazo hutokea

  • Mishipa ya damu husinyaa (constricted blood vessels)
  • Joto la mwili huongezeka
  • Mapigo ya moyo huongezeka
  • Shinikizo la damu
  • Dilated pupils

Matumizi ya muda mrefu ya dawa hii ya kulevya huleta madhara yafuatayo, Pamoja na kwenda kwenye ubongo husambaa sehemu nyingine za mwili na mzunguko wa damu

  • Moyo - Kwenye moyo huweza kuleta Shambulizi la moyo (heart attack) na vilevile mapigo ya moyo yasiyo na mpangilio (Arrhythmia) hivyo unaweza kufa ghafla tu.
  • Ubongo - Mishipa ya damu kwenye ubongo inaweza kusinyaa na kupelekea kupata Kiharusi, hata kwa kijana. Vilevile unaweza kupata ugonjwa wa akili (substance abuse pyschosis).
  • Mapafu na mfumo wa hewa - Uvutaji kupitia pua huweza kupelekea tatizo sugu la kutokwa damu puani kila wakati na mafua yasiyo pona, kupoteza mfumo wa harufu, na ikivutwa kama sigara kuharibu mapafu moja kwa moja.
  • Mfumo wa chakula - Cocaine husababisha kusinyaa kwa mishipa ya damu kwenye tumbo na utumbo hivyo kusababisha vidonda na kuweza kuharibu kabisa mfumo huu kwa utumbo kuoza.
  • Mafigo - kutokana na shinikizo la damu mafigo yanaweza kushindwa kufanya kazi vizuri, vilevile cocaine inaweza kuleta madahara moja kwa moja kwenye mafigo kitaalamu Rhabdomyolysis.
  • Ngono - ingawa cocaine huweza kutumika kama njia ya kuongeza hamu ya ngono huweza kusababisha kushindwa kumaliza kile ulichokianza. Matumizi sugu ya dawa hii ya kulevya huleta madhara kwa jinsia zote yani kwa wanaume na wanawake.
  • Na vilevile huweza kufanya kuwa tegemezi wa dawa hii.
  • Kwa wanaotumia sindano na kushea wanaweza kupata maambukizi ya virusi ya hepatitis na vya ukimwi.

Nini hutokea baada ya matumizi ya muda mrefu ya kokeni?

Baada ya kutumia cocaine kwa muda mrefu punde unapoacha tu kutumia dalili zifuatazo hutokea;

  • Unyogovu
  • Uchovu
  • Kushindwa kuzingatia na kutokuwa makini
  • Kukosa uwezo wa kuwa na furaha au kusikia raha
  • Kuongezeka kwa tama zaidi ya kutumia cocaine
  • Kujisikia kuumwa, maumivu, baridi na kutetemeka.

Ikitokea mtu akitumia zaidi ya kiwango kinachotakiwa kwa muda mfupi yaani overdose, kifo cha ghafla huweza kutokea kutokana na madhara yafuatayo;

  • Moyo kushindwa kufanya kazi
  • Kiharusi
  • Degedege mara kwa mara
  • Mfumo wa hewa kushindwa kufanya kazi

Heroin

Hujulikana vilevile kama diamorphine, hutokana na mmea huitwao kitaalamu opium poppy. Heroin kwa mfumo wa Morphine hutumiwa hospitalini kama dawa ya maumivu makali ya ghafla (acute pain) kwenye maumivu makali ya kifua wakati wa shambulizi la moyo, na kwa maumivu ya mtu aliyepata ajali, vilevile baada ya upasuaji, na maumivu sugu kwenye kansa. Hivyo hutolewa kwa kuangalifu mkubwa.

Aina hii ya dawa ya kulevya huweza kutumika kwa kuvuta kwa pua, kuvuta kama sigara na kwa kuchoma kwenye mshipa. Siku hizi watu hutumia njia ya haja kubwa na kwenye uke, ambapo kuta hufyonza heroin na kuanza kufanya kazi ndani ya sekunde arobaini.

Heroin mara tu baada ya kuingia kwenye damu kuenda kwenye mfumo wa neva na kukandamiza ufanyaji kazi wake, ndio huweza kutumika kupunguza maumivu.

Dalili za mtu aliyetumia heroin

Dalili ambazo hutokea mara tu anapotumia Heroin:

  • Kujisikia mwenye furaha na raha
  • Kupishana Kusikia hali usingizi na tahadhari
  • Midomo kuwa mikavu
  • Misuli kuishiwa nguvu
  • Kuhema polepole
  • Warm skin flushing
  • Mikono na miguu kuwa mizito
  • kope za macho kulegea

Nini madhara ya matumizi ya muda mrefu ya heroin?

Madhara ya matumizi ya muda mrefu wa dawa hii ya kulevya hutokana zaidi na matumizi ya sindano na vifaa vingine visivyo salama

  • Maambukizi kwenye kuta na milango ya moyo
  • Maambukizi ya ini na virusi (kama hepatitis C na HIV),
  • Maambukizi ya figo
  • Maambukizi ya mfumo wa hewa
  • Maambukizi ya ngozi na majipu

Dalili ambazo hutokea mara tu unapoacha kutumia heroin

  • Kutotulia
  • Maumivu ya misuli na mifupa
  • Kutapika
  • Dalili hizi hufikia kilele ndani ya masaa 48 hadi 72 na hufika kikomo baada ya wiki.
Kitunguu swaumu ni jamii ya vitunguu ambayo kwa kitaalamu huitwa Allium sativum. Jamii hii ilianza kutumika katika mabara mbalimbali duniani hususani Asia, Afrika na Ulaya takribani miaka 6000 iliyopita. Matumizi makuu nyakati hizo yakiwa viungo katika mboga na tiba.
 
Kitunguu swaumu kimetajwa kwenye vitabu mbalimbali vya dini vikielezea faida zake katika kutibu maradhi mbalimbali yasababishwayo na bakteria, matatizo katika mapafu, matatizo katika mfumo wa umen'genyaji chakula, na matatizo ya kuishiwa nguvu.
 
Historia inaonesha kuwa, vitunguu swaumu vilianza kutumika China mwaka 510 K.K na pia vilitumiwa na wanajeshi wa Ugiriki na Roma. Aidha wasafiri wa vyombo vya baharini na vijijini pamoja na wakulima barani Afrika walivitumia sana.
 
Mwaka 1858, mtafiti na mwanasayansi wa nyakati hizo, Louis Pasteur aligundua uwezo wa kitunguu swaumu katika kuua vimelea mbalimbali vinavyosababisha magonjwa, na hivyo vikaanza kutumika kama dawa ya kusafishia vidonda na kuzuia kidonda ndugu hasa zama za vita ya kwanza na pili ya dunia. Isitoshe, mpaka sasa zipo dawa kadhaa zilizotengenewa kwa kutumia jamii hii ya vitunguu swaumu ikiwemo dawa ya kusafisha mdomo (mouth wash) ingawa watumaiji wake wengi huilalamikia dawa hiyo kwa sababu ya harufu mbaya ya dawa hiyo inayowasababishia kunuka kwa mdomo.

Faida za vitunguu swaumu

Katika tafiti mbalimbali vitunguu swaumu vimeonekana kuwa na uwezo wa kutibu maambukizi ya bakteria, fangasi na virusi vya aina mbalimbali. Aidha husaidia kuzuia magonjwa ya moyo ikiwemo kuondoa lijamu katika mishipa ya damu na hivyo kusaidia katika kurekebisha shinikizo la damu. Faida nyingine za vitunguu swaumu ni pamoja na

Wiki chache zilizopita tuliandika makala kuhusu madai kuwa mafuta ya nazi yana uwezo wa kutibu ugonjwa wa kusahau unaowapata wazee maarufu kama Alzheimer’s disease. Katika makala hiyo iliyonukuliwa kutoka tovuti ya www.wavuti.com, mwandishi Dada Subi alijaribu kutoa rai kwa wataalamu wetu wa afya kufanya tafiti ili kuthibitisha madai ya uwezo huo wa mafuta ya nazi ili kusaidia kutatua tatizo hili ambalo limewakumba wazee wengi.

Katika kuzungumzia rai ya Dada Subi, msomaji wetu mmoja alituandikia maoni akitaka kufahamu hasa uhusiano kati ya mafuta ya nazi na uwezo wake katika kutibu ugonjwa huu. Ifuatayo ni makala inayojaribu kuzungumzia uhusiano kati ya mafuta ya nazi na jinsi inavyodaiwa kuwa na uwezo wa kutibu ugonjwa wa kusahau wa Alzheimers.........

Kumekuwepo taarifa kuhusu uwezo wa mafuta ya nazi kutibu ugonjwa wa kusahau unaowakumba wazee uitwao Alzheimer’s disease wakati huo huo ikiripotiwa kuwa baadhi ya dawa zilizokuwa zikitumika kutibu ugonjwa huo hapo awali zinaonesha kushindwa kufanya kazi inavyopaswa. Hivi karibuni, makampuni makubwa ya madawa duniani ya Pfizer yalikiri kuwa dawa mpya aina ya dimebon ilionesha kushindwa kutibu ugonjwa huo na huku ikifanya hali za wagonjwa kuzorota zaidi.

Wakati taarifa za kushindwa kwa dawa hizo zikizidi kutolewa, madaktari na watafiti wameendelea kutafuta mbinu nyingine za kukabiliana na ugonjwa huu. Mojawapo ikiwa ni matumizi ya mafuta nazi.