Image

Utangulizi

Kibofu cha mkojo kinapatkana sehemu ya chini ya maeneo ya tumbo na ni kiungo ambacho kina uwazi/tundu ndani yake na kazi yake kubwa ni kukusanya na kuhifadhi mkojo unaotolewa na figo kabla ya kuutoa nje ya mwili wa binadamu. Kibofu cha mkojo kina kuta (layers) aina tatu za tishu ambazo ni;

1.Mucosa layer – Kuta ya ndani kabisa ambayo ndio inayokutana na mkojo wa binadamu. Kuta hii nayo inakuta nyingi sana za seli au chembechembe zinazojulikana kama transitional epithelium cells ambazo pia hupatikana kwenye sehemu ya mirija inayojulikana kama ureters, urethra na kwenye figo. Seli hizi zinazuia uvujaji wa mkojo kwenda kwenye sehemu nyengine ya mwili.

Ureter huingiza mkojo kutoka kwenye figo na urethra hutoa mkojo kutoka kwenye kibofu cha mkojo wakati wa kukojoa.

2.Lamina propia – Kuta ya katikati nyembamba sana kati ya kuta  hizi tatu na  ambayo mishipa ya damu na neva inapatikana hapa na ni muhimu sana  wakati wa kupanga makundi ya saratani ya kibofu cha mkojo wakati wa tiba.

3.Muscularis layer -  Kuta ya nje ambayo ndani yake kuna destrusor muscle na ndio kuta nene kati ya hizi tatu. Kazi yake kubwa ni kupumzisha kibofu cha mkojo ili mkojo uingie ndani na ukishajaa basi hukaza kibofu (contracts) na kufanya mkojo kutoka nje.

Nje ya hizi kuta tatu, kibofu cha mkojo kimezungukwa na  mafuta ambayo hukinga kibofu kutokana na mtikisiko wowote na kukitenganisha na viungo vengine. Kuna saratani aina tatu kutokana na kuta hizi tatu nilizotaja hapo juu za kibofu cha mkojo

Saratani ni aina ya ugonjwa unaosababisha ukuaji wa seli za mwili kubadilika na kukua bila mpangilio maalum.

Saratani ya matiti hutokea kwenye titi ambalo kwa kawaida lina sehemu ya kutengeneza maziwa ijulikanayo kama lobules na aina fulani ya mishipa inayounganisha hizi lobules na chuchu za titi. Sehemu kubwa iliyobakia ya matiti inajumuisha mafuta na tishu ambazo kitaalamu tunazoita connective and lymphatic tissue. Saratani ya matiti inayotokea kwenye lobules huitwa lobular carcinoma na ile inayotokea kwenye ducts huitwa ductal carcinoma.

Baadhi ya saratani ya matiti zinaongeza ukubwa kutokana na kuwa na vishikizi aina ya receptors zinazojulikana kama estrogen receptors kwenye seli zao ambazo husababisha ukuaji wa saratani ya matiti.

Kuna wanawake wengine wana viashiria vya asili vinajulikana kama HER2 positive breast cancer ambacho husaidia seli kuongezeka, kugawanyika na kujirekebisha pale zinapoharibika. Kiashiria hiki kinaaminika ndicho kinachosababisha wanawake hawa kuwa na saratani ya matiti yenye madhara zaidi na kuwa na uwezekano mkubwa wa kujirudia kwa saratani baada ya tiba tofauti na wale ambao hawana kiashiria hiki cha HRE2.

Vihatarishi vya Saratani

Kuna mambo kadhaa ambayo yameonekana kuwa na uhusiano, ama wa moja kwa moja au kwa kupitia vitu vingine, wa kusababisha saratani ya matiti, au kumfanya mtu au kundi la watu kuwa katika hatari ya kupata ugonjwa huu kuliko wengine. Mambo hayo ni pamoja na

Utangulizi

Saratani ya shingo ya kizazi ni saratani inayoongoza kwa kusababisha vifo vya wanawake wengi duniani. Inakadiriwa kuwa asilimia 85 ya vifo hivi hutokea katika nchi zinazoendelea. Kwa Tanzania, wastani wa wanawake 6,241 huugua saratani hii kila mwaka, ambapo 4,355 kati yao hufa, hii ni kwa mujibu wa ripoti ya shirika la afya duniani (W.H.O) ya mwaka 2010

Saratani ya shingo ya kizazi ndio saratani ya kwanza kwa wanawake nchini Tanzania, na Saratani namba moja kwa wanawake walio kati ya umri wa miaka 15 hadi 44. Tanzania ina wanawake milioni 10.97 walio na umri wa miaka 15 na kuendelea, ambao wako kwenye hatari kubwa ya kupata saratani hii. Kwa afrika mashariki, asilimia 33.6 ya wanawake wote, wanasadikiwa kuwa na virusi aina ya human papilloma virus ambavyo ndio visababishi vya ugonjwa huu.

Je nini kinasababisha saratani ya shingo ya kizazi?

Maambukizi ya human papilloma virus ndio yanayosababisha saratani ya shingo ya kizazi. Kuna zaidi ya aina 150 ya virusi hivi vya human papilloma virus, ambapo aina tatu (yaani ainaya 26,53,66) ndio venye hatari sana ya kusababisha ugonjwa huu, aina ya 16 na 18 ndivyo vinavyojulikana kusababisha zaidi ya asilimia 70 ya ugonjwa wa saratani ya shingo ya kizazi. Virusi hivi huambukizwa kwa njia ya kujamiana au kugusana kwa ngozi ya mtu mmoja na mwengine, na huambukiza wanaume na wanawake.

Vihatarishi vya saratani ya shingo ya kizazi

  • Kuanza kufanya ngono mapema – Wanawake wanaoanza kujamiana wakiwa na umri wa miaka 16 wako kwenye hatari baadae kupata saratani ya shingo ya kizazi.
  • Kuwa na wapenzi wengi – Mwanamke mwenye wapenzi wengi au mwenye mwanamume mwenye wapenzi wengi yupo kwenye hatari ya kupata ugonjwa huu. Utumiaji wa kondomu hupunguza hatari ya kupata saratani hii, lakini ikumbukwe ya kwamba kondomu sio kinga ya ugonjwa huu.
  • Maambukizi ya human papilloma virus
  • Uvutaji sigara – Kemikali zilizopo kwenye sigara huchanganyikana na seli au chembechembe za shingo ya kizazi hivyo kuleta mabadiliko katika shingo ya kizazi hatimaye kusababisha saratani.
  • Utumiaji wa vidonge vya kupanga uzazi kwa muda mrefu hasa wale wanaotumia kwa zaidi ya miaka mitano (miaka 5)
  • Ugonjwa wa genital warts ( dalili ni matezi na muda mwingine vidonda katika sehemu ya siri ya mwanamke). Hii husababishwa na virusi vya human papilloma virus.
  • Lishe duni au utapia mlo

Utangulizi

Saratani ya koo ni miongoni mwa magonjwa ya kutisha. Ingawa baadhi ya wagonjwa wa saratani ya koo wanaweza kutibiwa na kupona kabisa, kuna mjadala miongoni mwa matabibu juu ya tiba sahihi ya ugonjwa huu. Bila kujali ni aina gani inayotumika, karibu aina zote za tiba za saratani hii huwa na madhara kwa mgonjwa na wakati mwingine kusababisha kifo badala ya kuponya.

Muundo wa Koo

Ili tuweze kujadili vizuri ugonjwa huu, ni vema kwanza tuangalie muundo wa koo. Koo ni sehemu mojawapo ya mfumo wa chakula likiwa na urefu wa takribani sentimita 25 kuanzia mdomoni mpaka kwenye mfuko wa tumbo yaani stomach.

Ukuta wa koo unajengwa na tando (layers). Tando hizi zimetengenezwa kwa aina tofauti ya chembe hai au seli ambazo kila moja ina kazi zake maalum. Sehemu ya ndani kabisa ya ukuta wa koo huitwa mucosa ambayo hufanya kazi ya kulowanisha chakula ili kiweze kupita vizuri kuelekea kwenye mfuko wa chakula.

Chini ya utando huu, kuna utando mwingine unaoitwa submucosa ambao umejaa tezi zenye kuzalisha ute unaoitwa mucus ulio na kazi ya kulainisha koo na kulifanya liwe na hali ya umajimaji muda wote. Utando wa tatu unajulikana kama muscle layer. Utando huu umejaa misuli inayosaidia koo kusukuma chakula kuelekea tumboni. Utando wa juu kabisa unaolizunguka koo huitwa outer layer ambao una kazi ya kulinda koo kwa ujumla.

Hii ni aina ya saratani inayokumba tezi ya thyroid. Ikumbukwe kuwa tezi ya thyroid ipo sehemu ya mbele ya shingo ya mwanadamu ikiwa na sehemu mbili (lobes) moja kila upande wa shingo.

Visababishi na ukubwa tatizo

Saratani ya thyroid huwapata watu wa umri mbalimbali, kuanzia watoto mpaka watu wazima. Watu waliowahi kupigwa mionzi sehemu ya mbele ya shingo wapo katika hatari kubwa ya kupata aina hii ya saratani. Kadhalika watu wazima ambao waliwahi kupigwa mionzi kipindi cha utotoni nao pia wana hatari kubwa zaidi ya kupata saratani ya thyroid hata kama hawakuwahi kupata tatizo hilo wakati wanakua.

Tiba ya mionzi maeneo ya shingoni ilikuwa ikitumika sana zamani kwenye miaka ya 50 mpaka 60 kwa ajili ya matibabu ya uvimbe wa tezi ya thymus, mafindofindo (tonsils), au baadhi ya magonjwa ya ngozi. Hata hivyo ni nadra sana kwa tiba hii kutumika katika zama hizi.

Vihatarishi vingine vya saratani ya tezi ya thyroid ni pamoja na kuwepo kwa historia ya tatizo hili miongoni mwa wanafamilia na kuwa na goita iliyodumu muda mrefu bila kutibiwa.

Aina za saratani ya tezi ya thyroid

Kulingana na aina ya seli zinazounda tezi ya thyroid zinazoshambuliwa, saratani ya thyroid inaweza kugawanywa katika aina zifuatazo

Leukemia ni saratani inayoshambulia tishu za mwili zinazohusika na utengenezaji wa damu zikiwemo supu ya mifupa (bone marrow) na mfumo wa lymph (lyphatic system). Kwa maneno rahisi, leukemia humaanisha saratani ya damu. Kuna aina mbalimbali za leukemia, nyingine zikiathiri watoto na nyingine zikiathiri zaidi watu wazima.

Kwa kawaida leukemia huanzia kwenye chembe nyeupe za damu yaani white blood cells, ambapo mwili huzalisha kiwango kikubwa cha seli zenye maumbo mabaya ambazo hazina uwezo wa kufanya kazi zake sawasawa. Kazi ya chembe nyeupe za damu ni kulinda mwili dhidi ya vimelea waletao maradhi mbalimbali.

Leukemia husababishwa na nini?

Kama zilizo kwa aina nyingi za saratani, mpaka sasa chanzo halisi cha leukemia hakijulikani. Hata hivyo, wanasayansi wanadai kuwa leukemia hutokea kutokana na mkusanyiko wa vyanzo mbalimbali vikiwemo vinavyohusu sababu za kinasaba (genetic factors) na kimazingira.

Kwa ujumla, leukemia hutokea pindi chembe nyeupe za damu zinapobadilika muundo wake wa kinasaba yaani viasili vyake vya DNA, ambavyo kwa kawaida hubeba maelekezo yanayoifanya seli yeyote ya kiumbe hai iweze kuishi, kutenda kazi zake, kujizaa na hata kufa, vinapobadilika maumbile na muundo wake kutokana na sababu mbalimbali. Kitendo cha kubadilika kwa maumbile na muundo wa DNA hujulikana kama mutation. Ndiyo kusema basi, seli yeyote iliyopatwa na tatizo hili huwa na tabia ya kukua kwa haraka na kujizaa (kujigawa) kwa kasi zaidi kuliko kawaida, na pindi inapofikia muda wake wa kufa seli hiyo hugoma kufa badala yake huendelea kujizaa zaidi hatimaye kusambaa kwa wingi katika mfumo mzima wa damu, hali inayosababisha saratani ya damu.

Je, kuna vihatarishi vya leukemia?

Ultrasound ni chombo ambacho kimekuwa kikitumiwa na madaktari wengi sehemu mbalimbali duniani kwa ajili ya kuchunguza matatizo mbali mbali yaliyo ndani ya mwili wa mgonjwa.

Mojawapo ya matumizi maarufu ya chombo hiki kwa wanawake ni utambuzi wa jinsi mtoto alivyokaa tumboni mwa mama mjamzito,kuchunguza umbo la mfuko wa uzazi, matatizo katika mfumo wa uzazi na pia kuangalia iwapo kiumbe kilichopo ndani ya tumbo la mama mjamzito ni hai ama la.

Hivi karibuni huko nchini Uingereza, madaktari wamebuni kipimo cha Ultrasound kinachoweza kugundua kansa ya mfuko wa kizazi mapema kabla ya hata dalili hazijaanza kujitokeza kwa mgonjwa. Kipimo hicho kina uwezo wa kugundua kansa ya mfuko wa uzazi kwa mwanamke ikiwa katika hatua za awali kabisa kabla hata ya dalili zake kuanza kujitokeza rasmi.

Watafiti hao wamesema kwamba hii ni hatua kubwa katika kukabiliana na Ugonjwa wa kansa ya mfuko wa kizazi kwa kina mama katika nchi zinazoendelea, na wanatarajia kwamba chombo hiki kinaweza kuanza kutumika muda si mrefu hasa katika nchi zinazoendelea.

Watafiti hao wamedai kuwa ni matarajio yao kuwa chombo hiki kitakapoanza kutumika, kitakuwa ni miongoni mwa vipimo vya lazima kabisa ambavyo mgonjwa anatakiwa kufanyiwa (Routine) wakati wa kuwafanyia kina mama uchunguzi wa afya zao.

Kuna wastani wa wagonjwa wapya 60,000 wa kansa ya mfuko wa kizazi kila mwaka wengi wao wakiwa kwenye umri wa miaka 60. Aidha kwenye nchi zilizoendelea, ugonjwa huu husababisha wastani wa vifo 1,700 kila mwaka. Tangu mwaka 1970, idadi ya wagonjwa wa kansa ya mfuko wa kizazi imeongezeka kwa asilimia 50, huku wataalamu wa afya wakisema imetokana na wanawake wengi kupenda kuzaa watoto kidogo  pamoja na kuongezeka uzito (Obesity).

Watafiti hao kutoka chuo Kikuu cha London, nchini Uingereza wamesema kipimo hicho cha ultrasound (Ultrasound specialist test) kina uwezo wa kupima unene wa mfuko wa uzazi hivyo kutoa picha zinazowezesha kugundulika kwa kansa mapema.

Katika utafiti wao, kati ya wanawake 96 waliopimwa kwa kutumia chombo hicho, asilimia 80 waligundulika kuwa na kansa ya mfuko wa uzazi kwa usahihi kabisa hata kabla hawajaanza kuonesha dalili kama za kutoka damu kwa wingi kwenye sehemu zao za siri.

Watafiti hao bado wanaendelea kuwapima kina mama zaidi ili kujua uhakika wa kipimo chao katika kugundua kansa katika hatua za awali. Kwa kawaida iwapo kansa itagundulika mapema, mgonjwa ana nafasi kubwa ya kuishi iwapo atapata tiba mapema kabla hata kansa haijasambaa au kuenea mwilini.

Kansa ya mfuko wa kizazi huwapata kina mama ambao wameshafikia ukomo wa kupata hedhi kila mwezi na ambao wana umri kati ya miaka  60 hadi 69. Aidha wanawake wanakuwa katika hatari kubwa zaidi iwapo kiwango cha homoni aina ya oestrogen kitakuwa juu kuliko kawaida.

Kwa kawaida homoni hii ya oestrogen huwa katika kiwango cha chini sana wakati wa ujauzito, na wanawake wenye watoto wachache huwa na kiwango kikubwa cha homoni hii hivyo kuwa kwenye hatari ya kupata kansa hii ya mfuko wa uzazi.

Wanawake wanene (Obese) nao wapo kwenye hatari ya kupata aina hii ya kansa kwa vile wengi wao huwa na kiwango cha juu sana cha homoni hii ya oestrogen kwa vile mafuta yaliyolundikana mwilini hubadilisha homoni za aina nyingine kuwa oestrogen.

Ian Jacobs, mtafiti mkuu katika utafiti huo uliochapishwa katika jarida maarufu la afya la The Lancet amesema, “Miaka kadhaa ijayo, wanawake wanene, waliozaa mara chache, na wenye matatizo ya ugonjwa wa shinikizo la damu wanastahili kufanyiwa uchunguzi wa mifuko yao ya uzazi mapema kwa kutumia kipimo hicho ili kutambua kama wana kansa hii ya mfuko wa kizazi au la”.

Mkurugenzi wa kitengo cha utafiti wa kansa nchini Uingereza, ambao ndio waliofadhili utafiti huo, Bi. Kate Law, amesema matokeo ya utafiti huo yameonesha kuwa kipimo cha Ultrasound kinaweza kutumika na madaktari katika kuwawezesha kugundua aina ya kansa hiyo mapema.

Aina mbili ya chembe chembe za asilia za mwanadamu (genes) zinazohusishwa na kansa hii zimegundulika, ambazo pia huongeza hatari ya ugonjwa mwingine wa mfuko wa uzazi unaoitwa  Endometriosis kwa asilimia 20.

Ugunduzi huo ni hatua muhimu katika utengenezaji wa dawa ya kutibu kiini cha kansa hiyo na pia unafungua njia katika kubuni vipimo vya damu vya kugundua kansa hii kwa haraka. Chembe chembe hizo za asili (genes) zinahusika katika utengenezaji wa ukuta wa mfuko wa uzazi pamoja na kutengeza homoni za  aina nyingi, watafiti hao wamesema.

Ugonjwa huu wa Endometriosis ambao husababisha matatizo ya uzazi, hutokea baada ya ukuta wa mfuko wa uzazi kuanza kuota katika sehemu nyingine za mwili wa mwanadamu.

Inatarajiwa kwamba pindi utafiti huu utakapokamilika, kipimo hiki kitaanza kutumika muda si mrefu katika nchi nyingi duniani ili kuokoa vifo vya kina mama wengi duniani.

Ini ni kiungo muhimu sana katika mwili wa binadamu. Ndicho kiungo kikubwa kilichopo ndani ya mwili. Ugonjwa wa cirrhosis ni ugonjwa wa 12 duniani kati ya magonjwa yanayosababisha vifo vitokanavyo na  maradhi. Cirrhosis husababishwa na unywaji pombe kupindukia, ugonjwa wa hepatitis B, C, na ugonjwa wa fatty liver disease. Kwa wagonjwa wengine chanzo halisi cha ugonjwa huu hakijulikani. Kabla ya kuangalia ugonjwa wa cirhosis  (tamka sirosis kwa kiswahili), kwanza tuangalie kazi ya ini kwenye mwili wa binadamu.

Ini linahusika na

  • Kushughulikia chakula kilichosagwa kutoka kwenye utumbo mdogo (small intestine)
  • Hulinda mwili dhidhi ya magonjwa
  • Kutengeneza  nyongo (bile)
  • Hudhibiti kiwango cha mafuta, sukari na chembechembe zijulikanazo kama amino acids kwenye damu
  • Huhifadhi vitamini, madini ya chuma na kemikali nyengine muhimu
  • Huvunjavunja chakula na kutengeneza energy inayohitajika mwilini
  • Ini hutengeneza chembechembe zinazozuia damu kuganda mwilini kama fibrinogen, prothrombin, factor V, VII, IX, X  na X, protini C na S, antithrombin na nk.
  • Huharibu sumu na madawa ambayo yameingia mwilini.
  • Hutengeneza homoni aina ya angiotensinogen  ambayo inahusika kupandisha presha ya damu mwilini wakati inapokutana na enzyme ya renin, enzyme hii ya renin hutolewa na figo wakati figo inapohisi presha imeshuka mwilini.
  • Husafisha damu kutokana na chembechembe  mbaya na bakteria.
  • Hutengeneza enzyme na protini ambazo zinahitajika mwilini kwenye shughuli nyingi na hata kurekebisha tishu zilizoharibika.

Ugonjwa wa cirrhosis ni nini?

Cirrhosis ni matokeo ya ugonjwa sugu wa ini ambao  hubadilisha tishu za kawaida za ini kwa njia ya fibrosis, scar tishu, matezi (regenerative nodules),  kuziba damu kuingia kwenye ini  na hivyo kufanya ini kushindwa  kufanya kazi yake vizuri.

Visababishi vya ugonjwa huu

Cirhosis husababishwa na mjumuiko wa magonjwa mengi ambayo ni

Ugonjwa wa ini unaosababishwa na unywaji wa pombe kupindukia kwa muda mrefu ( alcoholic liver disease) . Inakadiriwa asilimia 10 – 20 ya wanywaji pombe kupindukia kwa miaka 10 au zaidi  ndio wanaopata ugonjwa huu. Yule anayekunywa pombe kwa muda mrefu huwa na asilimia kubwa ya kupata ugonjwa huu kutokana na kiwango cha pombe kuongezeka au kuwa kingi kwenye mwili wake. Pombe huharibu ini na kusababisha lishindwe kufanya kazi yake dhidhi ya mafuta, protini, na wanga (carbohydrates).

Ugonjwa huu wa ini unaotokana na unywaji pombe kwa muda mrefu (alcoholic liver disease) hauathiri wanywaji pombe wote na si lazima uwe mnywaji pombe ili upate ugonjwa huu.

Wanywaji pombe kupindukia pia wanaweza kupata tatizo la utapia mlo (malnutrition) kutokana na pombe kukosa virutubisho muhimu vinavyohitajika  mwilini, kupungua kwa hamu ya kula, na kupungua kwa ufyonzwaji wa virutubisho  vya chakula  kwenye utumbo. Utapia mlo pia husababisha ugonjwa wa ini.

Unywaji wa pombe kupindukia huweza kusababisha ugonjwa aina ya alcoholic hepatitis ambao huambatana na homa, manjano kwenye mboni au ndani ya macho na kwenye ngozi, kuongeza ukubwa wa ini (hepatomegaly) na kudhoofika  kwa mgonjwa (anorexia). Alcoholic hepatitis ni hatari sana kwani unaweza kusababisha kifo.

Non alcoholic steatohepatitis (NASH)  ama Non alcoholic liver cirrhosis   – Mafuta hujikusanya kwa wingi kwenye ini na kusababisha huharibifu wa tishu za ini (scar tishu). Ugonjwa huu unahusishwa na kisukari, unene uliopitiliza, utapia mlo wa protini (protein malnutrition), baadhi ya magonjwa ya moyo na baadhi ya madawa aina ya corticosteroids. Mgonjwa hapa hana historia ya unywaji pombe.

Ugonjwa aina ya hepatitis B, C, na D, ambayo husababishwa na virusi vya hepatitis. Hepatitis B ndio chanzo kikuu cha ugonjwa wa cirhosis kati ya hepatitis zote duniani. Hepatitis C ndio sababu kuu ya wagonjwa wengi kuhitaji ini la kupandikizwa (liver transplant) duniani.

  • Autoimmune hepatitis – Husababishwa na mfumo wa kinga mwilini ambao huathiri ini na kuharibu chembechembe au seli za ini na hivyo kusababisha ugonjwa wa cirrhosis.
  • Magonjwa ya kurithi kama cystic fibrosis, wilson’s  disease, galactosemia, alpha 1 antitrypsin deficiency, hemochromatosis na glycogen storage disease. Watu wenye tatizo la ukosaji wa alpha  - 1  -antitrypsin  ambayo inakuwa kwenye mapafu ya binadamu na husaidia kukinga tishu zisiharibiwe na enzyme za seli za uhabirifu hasa nuetrophil elastase, wanaweza kupata mjumuiko wa magonjwa yanayoathiri mfumo wa upumuaji  (COPD)  kama watakuwa na historia ya uvutaji sigara.
  • Cardiac  cirrhosis  - Hutokana na ugonjwa sugu wa moyo unaoathiri  sehemu ya kulia ya moyo na hivyo kuufanya moyo kushindwa kufanya kazi yake vizuri na hatimaye kulileletea madhara ini. Husababishwa na tatizo kwenye kizibo cha moyo (valve problem), kuathiriwa kwa moyo na maradhi ya bakteria au virusi, uvutaji sigara na nk.
  • Madawa na sumu  zinazoharibu na kudhuru ini
  • Ugonjwa wa kichocho (schistosomiasis)
  • Magonjwa yanayojulikana kama  primary biliary cirrhosis na primary  sclerosing  cholangitis

Dalili na viashiria vya ugonjwa wa cirrhosis

Wagonjwa wengi wa cirrhosis hawaonyeshi dalili zozote kwenye hatua za awali za ugonjwa huu. Dalili zinatokana na

  • Kushindwa kufanya kazi kwa ini kadri ugonjwa unavyoongezeka
  • Kuharibika kwa umbile na ukubwa wa ini kutokana na kitu tunachoita kitaalamu kama scarring

Dalili za cirrhosis ni

  • Uchovu
  • Ulegevu
  • Kichefuchefu
  • Kupungua hamu ya kula hatimaye kupungua uzito
  • Kupungua hamu ya kufanya mapenzi

Hata hivyo, dalili na viashiria vingi vinaweza visitokee hadi mtu atakapopata madhara ya cirrhosis. Dalili na viashiria hivyo ambavyo hutokea baada ya madhara kutokea ni kama zifuatavyo;

  • Kuwa rangi ya manjano kwenye macho na ngozi kutokana na ukusanywaji  wa bilirubin kwa wingi kwenye viungo hivi.
  • Kutapika
  • Homa
  • Kuharisha
  • Maumivu ya tumbo kutokana kuongezeka ukubwa wa ini au kutokana na vijiwe kwenye gall bladder (gallstones)
  • Kuwashwa mwili  kutokana na bile salts iliyopo kwenye ngozi
  • Tumbo kuwa kubwa au kuvimbiwa kutokana na maji kujikusanya sehemu ya tumbo (ascites)
  • Kuongezeka uzito kwa sababu ya ukusanywaji wa maji mwilini
  • Kutoka damu kwenye fizi au pua, husababishwa na kutokuwepo na chembechembe zinazozuia damu kuganda
  • Kuvimba kwa miguu
  • Kupumua kwa shida
  • Kupungua nyama mwilini (Loss of muscle mass)
  • Kwa wanawake, kuwa na hedhi isiyokuwa ya kawaida kutokana kupungua kwa utolewaji wa homoni zinazosaidia wakati wa hedhi.
  • Damu kwenye matapishi au haja kubwa kutokana kuharibika mfumo wa kuzuia damu kuganda.
  • Spider angiomata – Kutokea kwa mabaka yanayofanana na utandu wa buibui ambao katikati yake kuna rangi nyekundu. Hii inatokana na mishipa ya damu inayoonekana kwa sababu ya kuongezeka  kiwango cha estradiol.
  • Kuongezeka mikunjo ya kwenye viganja vya mikono (palmar erythema) husababishwa na kupungua kwa homoni za mapenzi (sex hormone)
  • Kuongezeka kwa matiti kwa wanaume (gynecomastia) kutokana na kuzidi kwa kiwango cha homoni aina ya estradiol mwilini, hutokea kwa asilimia 66 ya wagonjwa wa cirrhosis.
  • Kupungua kwa korodani  kwa sababu ya kushindwa kufanya kazi vizuri kwa hypothalamus na pitituary gland. Hii husababisha uume kushindwa kusimama (kusimika),  kushindwa kutia mimba mwanamke (infertility), na kupungua hamu ya kufanya mapenzi.
  • Mabadiliko ya kucha – Kucha zinaweza kuwa na mistari (Muehrcke’s lines), au kuwa za rangi nyeupe pembezoni mwake na rangi nyekundu kwa mbele (terry’s nails) au kujikunja kwa kucha pembeni (finger clubbing).
  • Bandama kuongezeka ukubwa (splenomegaly)
  • Kuongezeka unene  na kufupika kwa ngozi ya viganja vya mikono na hivyo kusababisha vidole na viganja kuwa kwenye umbile la kujikunja (dupuytren’s contracture)
  • Ini linaweza kuongezeka ukubwa, kupungua au kuwa la kawaida.
  • Kuonekana kwa mishipa ya damu sehemu ya tumbo (caput medusa)
  • Mgonjwa kuwa na harufu kali kama ya maiti kwenye pumzi kutokana na kuongezeka kwa dimethyl sulfide
  • Cruveilhier   Bumgarten murmur – Sauti fulani ambayo daktari anaweza kuisikia  wakati akimpima mgonjwa kutumia stethoscope  maeneo ya tumboni.
  • Mapigo ya moyo kwenda haraka mtu anapojaribu kusimama
  • Kusikia kiu sana
  • Mdomo kuwa mkavu au kukauka mate
  • Asterixis
Caput medusa kama inavyoonekana

Vipimo vya uchunguzi

  • Vipimo vya damu (Complete blood count) – Upungufu wa damu (anaemia),  kupungua kwa chembechembe bapa  za damu au platelets (thrombocytopenia), kupungua chembechembe nyeupe za damu (leukopenia) na chembechembe aina ya neutrophils (neutropenia) na kupungua kwa madini aina ya sodium.
  • Kipimo cha ufanyaji kazi wa  ini (Liver function test) – Kupungua kwa albumin, kuongezeka kwa aminotraferases AST na ALT (AST > ALT), alkaline phosphatase, bilirubin, gamma glutamyl transferase. Kuongezeka kwa protini aina ya globulin.
  • Kipimo cha kuangalia chembechembe za kuzuia damu kuganda (coagulation test)
  • Liver biopsy
  • Vipimo vya damu kuangalia kiwango cha immunoglobulins (IgG, IgM, na IgA), Alpha 1 antitrypsin, ferritin na  transferrin saturation, copper na ceruloplasmin.
  • Serology for hepatitis virus, autoantibodies
  • Kipimo cha wingi wa mafuta aina ya cholestrol na sukari                                                                            
  • Vipimo vya mionzi
  • Kipimo cha ultrasound – Inaweza kugundua saratani ya ini, portal hypertension nk.
  • CT scan ya tumbo ili kutofautisha na magonjwa mengine kama saratani aina mbalimbali, magonjwa ya kongosho (pancrease), ini, figo nk.
  • Liver/bileduct MRI
  • Gastroscopy – Kipimo cha kuangalia mpira wa kupitishia chakula kwenda kwenye tumbo, tumbo na sehemu ya duedonum ili kuhakikisha kama kuna oesophagus varices na kuzitibu ikiwezekana.

Tiba ya ugonjwa wa cirrhosis inahusisha

  • Kuacha kunywa pombe kabisa kwa kupata ushauri nasaha pamoja na mgonjwa kuhudhuria programu za kusaidia kuacha kunywa pombe (rehabilitation center). Kama ugonjwa wa cirrhosis  bado haujatokea, mgonjwa akiacha pombe ini linaweza kupona.
  • Kutibu tatizo la utapia mlo kwa kutumia vitamini na folic acid.
  • Kutibu  chanzo cha ugonjwa wa  cirrhosis
  • Kuzuia uhabirifu zaidi wa ini kwa kuzuia utumiaji wa dawa aina ya paracetamol pamoja na pombe.
  • Chanjo dhidhi ya hepatitis B na C
  • Mgonjwa kupewa dawa za kuongeza damu na kama upungufu wa damu mwilini ni mkubwa basi atahitaji kupewa damu
  • Kuzuia madhara ya cirrhosis kwa
  • Kuzuia utumiaji wa chumvi kwenye chakula
  • Kupunguza vyakula venye protini nyingi
  • Kutumia dawa za antibiotics ambazo daktari atakushauri
  • Kutumia dawa aina ya lactulose ili kupunguza madhara ya heptic encephalopathy kwa kupunguza kiwango cha ammonia mwilini na pia husaidia mgonjwa kupata choo laini.

Madhara ya cirrhosis ni yapi?

Madhara ya cirrhosis ni kama yafuatayo

  • Saratani ya ini ambayo husababisha vifo vingi sana
  • Kuvimba kwa tumbo kwa sababu ya kujaa maji
  • Kuwashwa mwili mzima
  • Kuwa wa manjano kwenye macho na ngozi
  • Kudhurika rahisi na madawa
  • Kutoka damu kwenye fizi, puani na nk.
  • Kuongezeka kwa mifupa ya kwenye mikono na miguu na hivyo kusababisha maumivu makali sana, kukakamaa na kuvimba miguu.
  • Esophageal varices
  • Portal hypertension
  • Hepatic encephalopathy – Hali ya kuchanganyikiwa, kupungua kwa umakini, kusahau haraka, kuwa na hasira, kupungua uwezo wa kujiamulia, mgonjwa kutojali muonekano wake,  kubadilika badilika hisia, kuona watu au vitu ambavyo haviko (hallucination), matatizo ya kulala, hii inatokana na kuongezeka kwa ammonia ndani ya damu ambayo hupelekwa kwenye ubongo.

Madhara ya cirrhosis yakishindwa kudhibitiwa au kama ini litashindwa kufanya kazi kabisa, basi mgonjwa atahitaji kupandikizwa ini jingine.