Image

Ute wa ukeni ni majimaji yanayotengenezwa na tezi ndogo ndani ya uke na shingo ya kizazi. Majimaji haya huvuja kutoka ukeni kila siku ili kuondoa seli za zamani na uchafu ukeni, kudumisha uke na njia ya uzazi kuwa safi na yenye afya. Ute huu hutofautiana kulingana na rangi, uzito, harufu na hata mtindo wake wa utokaji. Ute huu pia unaweza kuwa na msaada kukuwezesha kujua ishara nyingi ikiwemo siku za uchavushwaji, uwepo wa magonjwa na mengineyo, hivyo katika makala hii itaangalizia aina za ute, ishara gani zinamaanisha kwako kama mwanamke na ni vitu gani vya msingi kuzingatia au ni lini utahitaji msaada wa kitabibu. 

Madoa kwenye nguo za ndani?

Kutokwa na ute sehemu za haja ndogo ni jambo la kawaida kabisa kwa wanawake waliopevuka. Ute huu wakati ukiwa unatoka, huwa na rangi nyeupe au mara nyingine usio na rangi kabisa. Lakini, baada ya kukauka mara nyingi huacha madoa (alama)kwenye nguo ya ndani, kama ukiwa umevaa nguo nyeupe utaweza kuona kiurahisi zaidi. Madoa hayo ni kitu cha kawaida kabida kisichohitaji kuwa na hofu ikiwa:

  • haina harufu yoyote
  • Hauambatani na kuwashwa au uke kuwaka moto

Ikiwa ute unaotoka una harufu mbaya au unahisi kuwashwa au uke kuwaka moto, au una wasiwasi yoyote kuhusu utokaje wake, basi ni muda muafaka kuwasiliana na daktarin wa magonjwa ya wanawake aliye karibu nawe. Pia unaweza kuwashiliana na Daktari wa TanzMED kwa njia ya mitandao.

Muundo wa ute

Kwa maumbile ya mwanamke aliyepevuka, Ute ni majimaji ya kawaida kama vile mate.Lakini kabla hatujaendelea inabidi tujue, kwanini mwili wa mwanamke hutengeneza huu ute? Ute huu ni sehemu ya kawaida katika kulinda na kuhifadhi viungo vya uzazi vya mwanamke.Utando wa ute wa uke na tezi kwenye shingo ya kizazi hutoa majimaji ili kudumisha afya ya viungo vya uzazi. 

 Kwa kawaida, ute huu huundwa na vitu vifuatavyo, Ute wa njugumono (Mucus secretions) unatengenezwa na tezi za shingo ya kizazi na tezi za Bartholin, Maji maji yanayopita kupitia ukuta wa mishipa (vessel walls) yanayosambaza damu kwenye viungo vya uzazi, Ute unaotengenezwa na tezi za mafuta na tezi za jasho katika sehemu ya nje ya uke, Seluli zilizokufa kutoka kwenye epiteliamu ya uke na shingo ya kizazi, Makoloni makubwa ya bakteria, ikiwa ni pamoja na wale wa manufaa ambao huzuia maambukizi kuzaliana na kudumisha kiwango cha pH cha uke kuwa cha asidi.  

Aina za ute

Baada ya kuangalia msingi wa ute na muundo wake, sasa tuangalie aina za ute na maana zake. Ikimbukwe kuwa, kiwango na na aina ya ute unaotoka hutofautiana kati ya mtu mmoja na mwingine. Pia,rangi, muundo, na wingi pia unaweza kubadilika kutoka siku hadi siku, kulingana na hatua ya mzunguko wa hedhi ya mtu: 

Siku 1-5: Mwanzoni mwa mzunguko, mara nyingi huwa na ute mwekundu au wa damu wakati mwili unaandaa utando wa damu kwenye mji wa kizazi (uterine lining).

Siku 6-14: Baada ya kipindi cha hedhi, mtu anaweza kugundua ukeni kuna utokaji wa ute kidogo kuliko kawaida. Kadiri yai linavyoanza kuendelea na kukomaa, ute wa shingo ya kizazi utakuwa wa rangi ya mawingu na mweupe . Unaweza kuonekana kuwa wa kunata.

Siku 14-25: Siku chache kabla ya uchavushwaji, ute utakuwa mwepesi na wenye kunata, kama sehemu nyeupe ya yai nyakati hizi kuambatana na ongezeko la hamu ya kufanya tendo la ndoa. Baada ya uchavushaji, ute utarejea kuwa wa rangi ya mawingu au  mweupe ,

Siku 25-28: Ute wa shingo ya kizazi utapungua na mtu atauona kidogo kabla ya kuanza kwa kipindi cha hedhi kingine.

 

Nyekundu

Hii mara nyingi huwa ni nyekundu iliyopooza au ile inayokaribia rangu ya kutu. Nyekundu mara nyingi ni husababishwa na damu inayotoka wakati wa hedhi. Kwa kawaida, wanawake hupata hadi kila baada ya siku 28, lakini ni jambo la kawaida kupata hedhi kati ya siku 21 hadi 35. Na wengi hukaa kwenye hedhi kwa muda wa siku 3 hadi 5. Endapo utaona damu katika kipindi siyo cha kawaida, basi unashauriwa kuwasiliana na daktari ingawa ni kitendo cha kawaida kwa wanawake wengi kutokwa na damu katikati ya kipindi cha hedhi (intermenstrual bleeding), kuna baadhi ya muda, inaweza kuwa ni ishara ya tatizo la kiafya. 

Kwa mtu yoyote aliyefikia ukomo (monopause) na hajawahi kupata hedhi kwa kipindi cha mwaka mmoja au zaidi, halafu ikatokea akaona ute wa rangi nyekundu / damu ya hedhi, anashauriwa kuonana na daktari haraka kwani inaweza kuwa ni ishara ya ugonjwa wa saratani ya utando wa kizazi (endometrial cancer) 

 

Nyeupe

Ute huu huwa na rangi inayoanzia nyeupe, inaenza maziwa hadi njano. kama hauna dalili nyingine yoyote, basi ute mweupe ni inshara ya ute wa kawaida kama kilainishi shemu ya uzazi. Hata hivyo, ikiwa utoaji wa nyeupe una muundo kama wa jibini , maziwa au unakuja na harufu kali, inaweza kuashiria maambukizi hivyo unatakiwa anapaswa kumwona daktari. 

Ute mweupe, mzito, wenye harufu kali mara nyingi unaashiria maambukizo ya fangasi (yeast infection), ambayo pia inaweza kusababisha kuwashwa au kuchomachoma.

 

Njano-Kijani

Ikiwa ute una rangi ya njano iliyofifia sana, inaweza isiwe ni ishara ya tatizo.  Hii inawezekana zaidi, haswa ikiwa rangi hiyo inahusiana na mabadiliko katika lishe au virutubisho vya chakula. 

Ikiwa ute una rangi ya njano iliyokoza, au njano-kijani au kijani, inaashiria kuna maambukizi ya bakteria au magonjwa ya zinaa (STI). Tafadhali muone daktari mara moja ikiwa utoaji wa ukeni ni mzito au umegandaganda, au una harufu mbaya. 

 

Pink:

Ute unaweza kuwa pinki iliyopooza au ile iliykoza,. Mara nyingi hii huwa imechanganyika na damu kidogo. Utoaji wa ute wenye rangi ya pinki mara nyingi hutokea kidogo kabla ya kipindi cha hedhi. Lakini, pia inaweza pia kuwa ni kiashiria cha awali cha uwepo wa ujauzito.

Baadhi ya watu wanaweza kutoa damu kidogo baada ya uchavushaji, ambayo pia inaweza kusababisha ute kuwa wa rangi ya pinki. Utoaji wa pinki unaweza kutokea baada ya kufanya tendo la ndoa ikiwa tendo lenyewe limeleta nyufa ndogo au vijijeraha katika uke au shingo ya kizazi.

Hauna Rangi

Ute wa kawaida huwa hauna rangi au mweupeoaji wa kawaida wa ukeni kwa kawaida ni wazi au mweupe. Unaweza kuwa na unyevu au muundo wa utakasa wa yai.

Kijivu

Utoaji wa ute wa rangi ya kijivu sio dalili nzuri kiafya na inaweza kuwa dalili ya maambukizo ya bakteria wanaoitwa bacterial vaginosis (BV).

Kawaida, maambukizi ya bakteria wa BV huambatana na dalili nyingine, ikiwa ni pamoja na: 

  • Kuwashwa
  • Kuhisi kuchomwachomwa
  • Harufu kali
  • Kuvimba karibu na vulva au sehemu ya nje ya uke 

Mtu yeyote mwenye ute wa kijivu anapaswa kumwona daktari mara moja. Baada ya kuthibitisha ugonjwa huo, kwa kawaida daktari humpa mgonjwa dawa za kuua bakteria (antibiotiki) kwa ajili ya matibabu ya BV. Epuka kutumia madawa ya antibiotiki bila kuandikiwa na daktari kwani kila dawa hutumia kulingana na ukubwa wa tatizo, aina ya ugonjwa na sababu nyingine zaidi za kitabibu ambazo huamuliwa na daktari baada ya kuona hali halisi ya ugonjwa na mgonjwa.

Mwanamke anaweza kuona ute msafi, unaoteleza sana siku chache kabla ya cuhavushaji (ovulation), wakati wa kujamiiana, na wakati wa ujauzito. 

Je ni kwa kiwango gani huwa ni kawaida?

Kwa mwanamke mwenye Afya njema, kwa kawaida hutoa wastani kati ya mililita 1 hadi 4 ya ute kila ndani ya masaa 24. Hata hivyo, kiasi hicho kinaweza kutofautiana kutoka kwa mtu hadi mtu, kwa hvyo ikiwa utapata zaidi ya hapo inawezekana kabisa ni kawaida. 

Pia, ni muhimu kukumbuka kwamba utoaji wa ute huongezeka sana wakati wa uchavushaji (kuwa na ute mwingi), ujauzito, na unapotumia vidonge vya uzazi wa mpango. 

Ute wakati wa kujamiiana

Lengo kuu la ute kwenye sehemu za siri za mwanamke ni kufanya kuwe na unyevunyevu. Lakini ute huu wa kawaida hata pale unapokuwa umetoka katika kiwango chake cha juu kabisa (sanasana wakati wa uchavushaji), bado hauna uwezo wa kufanya sehemu za siri kuwa zimeloa vya kutosha kwa ajili ya kitendo cha kujamiiana. Hivyo kunahitajika ute mwingine wa ziada kuhakikisha kunakuwa na mtelezo wa kutosha. 

Wakati wa tendo la ndoa, sehemu kubwa ya kiungo cha uzazi cha mwanamke kinakuwa kimepata damu ya kutosha hivyo hufanya vijimishipa vya shemu hii kutanuka kitendo kinachosababisha majimaji kupita kwa urahisi. Tezi za Bartholin zinazopatikana kwenye mashavu ya uke (ulvar vestibule) pia tezi za Skene zinazopatikana kwenye mrija wa mkojo (urethra) zote zinatumika kutengeneza ute ute. 

Uteute huu husaidia kuongeza mtelezo wakati wa tendo la kujamiiana na kupunguza michubuko na msuguano wakati wa tendo.Kiwango halisi cha ute ute huu hutegemeana na mtu, umri, kiwango cha homoni and tarehe za hedhi. 

Wakati gani nimuone daktarin? 

Unatakiwa kuwahi kumuona daktari ikiwa utahisi ute una harufu au muonekano ambao sio wa kawaida.Pia anapaswa kutafuta huduma ya matibabu ikiwa unapata dalili kama vile: 

  • Kuwashwa
  • Maumivu au kujisikia vibaya
  • Ute unaofanana na jibini cha krimu
  • Kutokwa damu kati ya hedhi au baada ya ukomo wa hedhi
  • Kutoka damu mara kwa mara baada ya tendo la ndoa
  • Ute wa rangi ya kijivu, kijani, au manjano
  • Harufu kali ukeni
  • Maumivi makali wakati wa kukojoa

Daktari atafanya uchunguzi wa viungo vya uzazi vya mwanamke (pelvic exam). Wanaweza pia kuhitaji kuchukua sampuli ya ukeni kwa ajili ya uchunguzi wa kimaabara.  

Maswali ya Mara Kwa Mara: (FAQ)

 

Je, ni kawaida kwa wasichana wadogo kutokwa na ute?

Ndiyo, wasichana wa kila umri wanaweza kutokwa na ute, kawaida kwa kiasi kidogo hadi wanapokaribia kuingia kwenye umri wa kupevuka (Kuvunja ungo). Pia, huwa unatofautiana katika kiasi na rangi (kutoka hamna rangi hadi manjano au nyeupe). Hakuna haja ya wasiwasi isipokuwa ikiwa haueleweki, una rangi nyingine, au harufu isiyo ya kawaida.

 Nawezaje kuzuia ute?

Utoaji wa ute ni jambo la kawaida na muhimu kwa afya ya uzazi wa kike. Hakikisha hamna harufu, au rangi zisizo za kawaida, pia ukiwa hauwashwi hauoni au kuchomwachomwa, hakuna haja ya kuchukua hatua yoyote. 

Je, utokaji wa ute ni dalili ya ujauzito?

Ikiwa utokaji wa ute umeongezeka kwa kiasi na ni mwepesi, wa maziwa, na una harufu nyepesi, inaweza kuwa dalili ya ujauzito wa awali. Hii inaitwa leukorrhea na inaweza kujitokeza mapema kama wiki moja hadi mbili baada ya kushika ujauzito. Wakati wa ujauzito, utoaji wa ute utabadilika kulingana na muundo, kujirudia (frequency), na kiasi. 

Umri gani Wasichana wanaanza kutokwa na ute?

Kwa kawaida wasichana huanza kupevuka kuanzia miaka 8 hadi 13. Lakini, baadhi ya vijana huanza kuonyesha dalili za ujana nje ya muda huo. Kwa ujumla, hedhi huanza takriban mwaka mmoja baada ya kuvunja ungo, ambayo mara nyingi hutokea akiwa bado mdogo sana. 

Ni rangi gani ya ute inayohusiana na fibroids?

Fibroid ya kizazi (pia inaitwa leiomyoma, fibromyoma, au myoma) kwa kawaida ni ukuaji usio wa kansa ndani ya kizazi. Ute unaohusiana na fibroids unaweza kuwa kuanzia usio na rangi hadi mweupe au rangi ya damu hadi kijivu au kahawia. Kutokwa na damu nje ya kipindi cha hedhi ni jambo la kawaida kwa watu wenye fibroids. 

Nini husababisha utokaji wa ute mwingi?

Utoaji wa ute zaidi ya kiwango cha kawaida inaweza kuwa ishara ya: 

  • uchavushaji
  • Athari ya mzio
  • Msongo wa mawazo
  • Homoni kutokuwa kwa uwiano
  • Matumizi ya antibiotics
  • Matumizi ya dawa za kuzuia mimba 

Je, ute mweupe ni ishara ya hedhi?

Ndiyo, ute mzito, mweupe, wa maziwa ni ishara ya kawaida ya kukaribia kipindi cha hedhi kinakaribia. Hiyo ni matokeo ya viwango vya juu vya progesterone, homoni inayosimamia ujauzito na mzunguko wa hedhi. Aina hii ya utokaji wa ute inaaminika kuwa ni ya kawaida ikiwa haiendani na harufu mbaya. Kwa kulinganisha, wakati viwango vya estrogeni vinaongezeka, ute huwa huwa hauna rangi na unavutika.

Je unafahamu inakadiriwa kuwa, mwanamke hupata hedhi wastani wa mara 400 katika maisha yake? Pia, neno linalotumika sana kuwakilisha hedhi ni "period", neno hili lilianza kutumika kwa mara ya kwanza kwenye miaka ya 1822 likimaanisha tukio linalotokea ndani ya muda fulani au linalojirudia baada ya muda fulani. Leo hii tuangalie mambo mengine 5 muhimu kuyajua kuhusiana na hedhi.

1. Kwa wastani, mwanamke huanza kupata hedhi yake ya kwanza kabisa akiwa na umri wa miaka 12.

2. Mzunguko wa siku za hedhi huwa kati ya siku 21 hadi 35. Ingawa wengi huwa na mzunguko wa siku 28, lakini kuzidi wiki moja au kuwahi kwa wiki moja ni kitu cha kawaida.

3. Mwanamke huzaliwa na mayai milioni 1 hadi 2. Mayai haya, mengi hufa jinsi mwanamke anavyoendelea kuishi na ni mayai 400 tu ndiyo hukadiriwa kufika hatua ya ukomavu tayari kwa uchavushwaji.

4. Msichana anaweza kupata ujauzito kabla ya kuanza hedhi yake ya kwanza. Hii ni kwa sababu, yai huanza kukomaa kabla ya kuona hedhi yake ya kwanza, hivyo kama atashiriki tendo bila kinga, kuna uwezekano wa kupata ujauzito.

5. Wanawake wengi hufikia ukomo wa kupoata hedhi (menopause) wakiwa na umri wa miaka 48 hadi 55.

Utafiti uliofanyika nchini Uingereza kwa kuhusisha wanawake 46,000 umesema ya kwamba matumizi ya dawa za uzazi wa mpango hupunguza hatari ya kupata saratani ya mayai ya mwanamke (ovarian cancer), saratani ya mfuko wa kizazi (uterine cancer) na ya utumbo mpana wa chakula (bowel cancer).Watafiti hao wamesema kinga anayopata mwanamke dhidi ya saratani hizi kutokana na matumizi ya dawa hizi za uzazi wa mpango ni ya muda mrefu mpaka miaka 35 baada ya mwanamke huyo kuacha kutumia dawa hizi za uzazi wa mpango.

Katika utafiti huu, wanawake wa Uingereza walitumia dawa hizi za uzazi wa mpango kwa wastani wa miaka mitatu na nusu wakati wakiwa na umri kati ya miaka 20 mpaka miaka 30.Kinga dhidi ya saratani kwa wanawake hawa waliotumia dawa hizi za uzazi wa mpango kipindi cha ujana wao ilionekana kuwepo mpaka walipotimiza miaka 50, 60 na 70, umri ambao wanawake wanakuwa kwenye hatari kubwa ya kupata saratani.

Watafiti hawa kutoka chuo kikuu cha Aberdeen nchini Uingereza,waliendelea kusema ya kwamba  wanawake waliotumia dawa za uzazi wa mpango walikuwa na hatari pungufu ya  theluthi moja kupata saratani ya mayai ya mwanamke au saratani ya ukuta wa mfuko wa kizazi cha mwanamke (endometrial cancer).Pia wanawake hawa waligundulika kuwa na hatari pungufu ya moja ya tano kupata saratani  zozote zile ikilinganishwa na wanawake ambao hawakutumia dawa hizi za uzazi wa mpango.

Karibia wanawake milioni 3.5 nchini Uingereza hutumia njia hii ya uzazi wa mpango kama njia rahisi kwao. Utafiti huu uliochapishwa katika jarida la American Journal of Obstetrics and Gynaecology utabadilisha mtazamo wa watu kuhusu athari na faida za dawa hizi za uzazi wa mpango.

Mara nyingi wanawake wameambiwa ya kwamba dawa za uzazi wa mpango zinawaweka kwenye hatari ya kupata saratani ya matiti au ya shingo ya kizazi  (cervical cancer) lakini utafiti huu umeonyesha hatari hii huondoka kabisa ndani ya miaka mitano baada ya mwanamke kuacha kutumia dawa hizi za uzazi wa mpango.Wakati mwanamke anapotimiza umri wa kukoma kupata hedhi, kipindi ambacho kwa kawaida huongeza hatari ya kupata saratani za aina tofauti tofauti, lakini kwa wale ambao walitumia dawa za uzazi wa mpango hapo awali hawako kwenye hatari yoyote ile ya ziada ya kupata saratani, walisema watafiti hao kutoka nchini Uingereza.

Fibroids ni moja ya matatizo yanayowasumbua wanawake wengi , kwa lugha ya kawaida, Fibroids maana yake ni uvimbe wa msuli wa kifuko cha uzazi. Uvimbe huu unaweza kuwa na ukubwa tofauti kuanzia kama punje ya harage mpaka ukubwa wa nazi. Wakati mwingine unaweza kudhani ni ujauzito!

Sio kila mwenye fibroids anakuwa na matatizo kiafya. Zinaweza kuwepo miaka mingi bila matatizo yoyote. Hata hivyo inashauriwa kila mwenye fibroids awe anapimwa na daktari angalau mara moja kwa mwaka ili kuona jinsi zinavyoendelea na kuhakikisha kuwa hazikui kwa kasi au kuhatarisha kuwa kansa.

Kwa wale zinaowaletea matatizo, fibroids husababisha kutokwa na damu nyingi za hedhi, maumivu ya tumbo, mimba kuharibika zikiwa changa, kuzaa watoto njiti na fibroid kukandamiza viungo vingine kama kibofu cha mkojo na kusababisha kukojoa mara kwa mara au matatizo ya haja kubwa.

Njia ya kugundua uwepo wa fibroid ni kupimwa na daktari na kufanyiwa ultrasound.

Matibabu yake yapo ya aina kuu tatu:

1. Kunywa dawa. Hata hivyo dawa zilizopo sasa hazina matokeo mazuri kuondoa fibroids ila husaidia kupunguza ukuaji wake.

2. Kuiondoa fibroid kwa operation. Ziko aina nyingi za operation kupitia kwenye tumbo au kupitia ndani ya kifuko cha uzazi. Aina ya operation hutegemea mahali ilipo fibroid.

3. Kuondoa kifuko cha uzazi. Njia hii huwafaa wale ambao hawana mpango wa kupata mtoto.

Kuna nadharia mbalimbali juu ya vitu vinavyosababisha fibroids lakini hakuna kitu kilichothibitika moja kwa moja kuwa chanzo cha fibroids. Kwa wale wenye uzito mkubwa inashauriwa kupunguza mwili kunaweza kupunguza uwezekano wa kupata fibroids.


Zipo tafiti zinazoonyesha kuwa matumizi ya vidonge vya uzazi wa mpango vinapunguza uwezekano wa kupata fibroids.

Kunyonyesha kuna faida nyingi sana kwa mtoto mchanga pia na kwa mama. Na mara nyingi hili huwa ni umamuzi wa mtu binafsi ila ushauri wa msisitizo unatolewa na chama cha madaktari wa watoto na chama cha madaktari wa magonjwa ya wakina mama vyote vya marekani.

Faida kwa Mtoto

  • Virutubisho vilivyomo kwenye maziwa ya mama ni muhimu kwa mtoto mchanga , maana maziwa ya mama huwa uwiano mzuri wa vitamin, protini, na mafuta mazuri na kumuwezesha mtoto kukuwa vizuri
  • Vilevile maziwa ya mama huwa na virutubisho vyenye uwezo wa kumkinga mtoto kupata magonjwa kitaalamu antibodies, ambavyo humkinga mtoto mchanga dhidi ya vimelea (bakteria na virusi)
  • Maziwa ya mama hupunguza uwezekano wa mtoto mchanga kupata pumu au aleji
  • Na vilevile watoto wakinyonyeshwa kwa miezi sita mfululizo bila kuchanganyiwa na vyakula vingine hupunguza hatari ya kupata maambukizi ya masikio, mfumo wa hewa na magonjwa ya kuharisha
  • Kuna tafiti ambazo zinaonyesha maziwa ya mama yanaongeza upeo wa kufikiri wa mtoto atakapo kua

Maambukizi katika mfumo wa uzazi wa mwanamke kwa kitaalamu Pelvic Inflamatory Diseases au kwa kifupi PID, ni moja ya matatizo ambayo huwaathiri sana wanawake. Kwa kawaida maambukizi haya huusisha shingo ya uzazi (cervix) hali ambayo hujulikana kama cervicitis, nyama ya mfuko wa uzazi (endometrium) ambayo kitaalamu huitwa endometritis, na mirija ya uzazi (fallopian tubes) hali ijulikanayo kitabibu kama salpingitis.

 PID husababishwa na nini? 

Pamoja na aina kadhaa za vimelea kuhusishwa na PID, vimelea vya jamii ya Neisseria Gonorrhoeae pamoja na Chlamydia trachomatis ndivyo vinavyoongoza kwa umaarufu zaidi katika kusababisha PID kwa akina mama.

Je mwanamke huambukizwaje PID?

Kuna njia kadhaa ambazo mwanamke anaweza kuambukizwa PID. Njia hizo ni pamoja na

  • Kufanya ngono isiyo salama
  • Maambukizi ya njia ya uzazi hasa kipindi mara baada ya kujifungua (au postpartum period)
  • Maambukizi ya njia ya uzazi mara baada ya kutoa mimba kwa njia zisizo salama (post abortion) au mara baada ya mimba kutoka (miscarriage)
  • Kutumia vipandikizi vya ndani ya mfuko wa uzazi (IUCD) kama njia mojawapo ya uzazi wa mpango, na
  • Kuambukizwa kupitia damu iliyo na vimelea vya PID.

Dalili za PID ni zipi?

Zipo dalili kadhaa za ugonjwa huu wa PID. Miongoni mwa dalili hizi ni

Tunaendelea na mfululizo wa makala juu ya hali za dharura kipindi cha ujauzito. Leo tunazungumzia placenta previa. 

Placenta previa ni miongoni mwa hali za hatari na dharura inayowapata baadhi ya mama wajawazito ambapo kondo la nyuma hujipachika katika sehemu ya chini ya mfuko wa uzazi, kukua na kisha kufunika sehemu ndogo au kubwa ya njia ya uzazi inayoelekea kwenye shingo ya uzazi na hivyo kuzuia kabisa uwezekano wa mtoto kuzaliwa kwa njia ya kawaida.

Chanzo chake ni nini?

Wakati wa ujauzito, kondo huongezeka ukubwa na kutanuka kadiri jinsi mfuko wa uzazi unavyotanuka na kukua. Kipindi cha awali cha ujazito, ni jambo la kawaida kwa kondo kuwa maeneo ya chini ya mfuko wa uzazi (low-lying palcenta). Lakini, kadiri mimba inavyokua ndivyo mfuko wa uzazi unavyopaswa pia kulivuta kondo kutoka sehemu za chini na kulipandisha sehemu za juu za kuta zake. Mpaka ifikapo theluthi ya tatu ya ujauzito, kondo linapaswa kuwa karibu kabisa na juu ya mfuko wa uzazi ili kufanya njia ya uzazi kuwa wazi kwa ajili ya kurahisisha utokaji wa mtoto.

Masundosundo au vigwaru au Genital warts ni vinyama laini vidogo vinavyoota kwenye ngozi au utando laini unaozunguka maeneo ya siri. Vinaweza kutokea kwenye uume, uke, mrija wa mkojo [urethra], vulva, shingo ya kizazi [cervix], au maeneo ya kuzunguka njia ya haja kubwa au ndani yake.

Huu ni ugonjwa unaoenezwa kwa njia ya kujamiiana [sexually transmitted infection (STI)].

Visababishi

Ugonjwa wa masundosundo husababishwa na jamii ya virusi wanaoitwa Human papilloma virus (HPV). Kuna zaidi ya aina 70 tofauti za virusi wa HPV ingawa si wote wanaosababisha masundosundo kwenye maeneo ya siri [genital warts]. Baadhi ya aina nyingine za HPV husababisha masundosundo kwenye ngozi inayozunguka sehemu nyngine za mwili kama vile kwenye mikono au miguu. 

Tafiti kadhaa zimeonesha kuwa baadhi ya aina za virusi wa HPV pia husababisha saratani ya shingo ya kizazi [carcinoma of the cervix] kwa wanawake au saratani ya njia ya haja kubwa [anal cancer] kwa jinsia zote mbili. Aina hii ya virusi hujulikana pia kama high-risk HPV.

Pamoja na kwamba ugonjwa wa masundosundo kwenye maeneo ya siri umejitokeza kwa kasi kubwa hasa baada ya kuwepo kwa janga la UKIMWI, watu wengi waliopatwa na ugonjwa huu huwa hawaoneshi dalili zozote zile. Kwa mfano, kwa wanawake, virusi wa HPV wana uwezo wa kusambaa mpaka maeneo ya ndani kabisa ya kuta za uke au shingo ya kizazi [cervix] bila kuonekana wala kuhisiwa kwa urahisi. 

Kama tulivyotangulia kueleza hapo awali, maambukizi ya HPV husambaa kutoka kwa mtu mmoja mpaka mwingine kwa njia ya kujamiiana kunakohusisha njia ya haja kubwa, uke au ngono ya mdomoni. Mara baada ya kuambukizwa, huweza kuchukua mpaka muda wa wiki sita hadi miezi 6 kwa masundosundo kuwa dhahiri, ingawa baadhi ya wagonjwa wanaweza kukaa hata miaka kadhaa bila kuwa na dalili yeyote ile. Aidha imeonekana pia kuwa si kila mtu anayejamiina na aliye na maambukizi ya HPV au mwenye masundosundo anaweza naye kupata ugonjwa huu. 

Siku hizi, kumekuwa na taarifa nyingi juu ya masuala ya uzazi. Taarifa hizi hutokana na imani tofauti zilizopo kwenye jamii. Na, nyingi ya imani hizi hazina uhakika wa kitaalamu. Moja ya imani ni kutokukojoa kwa mwanamke baada ya tendo la ndoa ili kuzuia mbegu za kiume kutoka.

Kukojoa baada ya kufanya tendo la ndoa ni njia mojawapo inayotumiwa na wengi kusaidia kupunguza uwezekano wa kupata maambukizi ya njia ya mkojo (UTI).  Na inashauriwa sana kukojoa punde baada ya tendo la ndoa ili kujikinga na uwezekano wa kuambukizwa ugonjwa wa UTI kama anavyoelezea Dr. Leah Millheiser . Hivyo, kama na wewe ni mmoja wapo, basi unaweza kuendelea. Kukojoa baada ya tendo la ndoa hakuwezi kupunguza uwezekano wako wa kupata ujauzito.

Wakati wa tendo la ndoa, kuna mbegu kati ya milioni 20 hadi 400 hutotelwa na mwanamume kwenye manii (semen) kwa pamoja , na inakadiriwa kuwa mpaka 65% ya mbegu hufanikiwa kutoka kwenye bao na kuingia kwenye mlango wa uke ikisaidiwa na majimaji ya ukeni yanayotoka wakati wa tendo la ndoa (vaginal discharge) au kwa kitaalamu cervical mucus.

Asilimia kubwa ya mbegu hizi hupenya kwenye lango la uzazi wa mwanamke na kuacha sehemu kubwa ya manii ikiwa na maji maji mengine ambayo yana kiasi kidogo sana cha mbegu za kiume /shahawa (kumbuka manii za mwanamume zinajumuisha vitu vingi vingine zaidi ya shahawa  kama protini , ute wa kusaidia shahawa kuelea au kwa kitaalamu  Seminal fluid nk). Kwenye kila manii (bao) moja la mwanamume (manii yote unayoiona), inakadiriwa  kuwa ni 1% tuu ndiyo shahawa / mbegu za mwanamume, hivyo unapoona kama manii zinamwagika, sehemu kubwa siyo mbegu bali ni majimaji mengine yanayotumika kwenye kuhifadhi mbegu za mwanamume.

Kumbuka: Shahawa(sperms) ni sehemu ya manii (semen ) inayotoka wakati mwanamume akifika kilele. Shahawa huelea kwa kutumia kimiminika kiitwacho Seminal fluid  inayopatikana kwenye manii, Hivyo, siyo maji yote ya kwenye manii ni shahawa.

Kimsingi, mpaka muda anaenda kukojoa, mbegu huwa zimeshafika kwenye lango la uzazi, (cervix) hivyo kiasi kidogo sana cha mbegu zilizoshindwa kutoka kwenye manii ndiyo huendelea kubaki kwenye majimaji ambayo yatatoka dakika au masaa kadhaa baada ya tendo la ndoa.

Kati ya mambo ambayo watu wengi hawatilii maanani sana ni unywaji wa pombe wakati wa ujauzito. Nimekuwa nikiwaona akina mama wajawazito wengi wakinywa pombe kwenye sehemu za starehe na sherehe mbalimbali. Hata hivyo si nia ya makala hii kuwazuia kunywa pombe bali kuwapa elimu sahihi juu ya unywaji wa pombe wakati wa ujauzito.

Ukurasa 1 ya 3