Image

Njia bora na sahihi inayomjengea mtoto misingi bora ya maisha yake ya baadae.

Katika #Malezi ya mtoto ni muhimu kujua njia bora na sahihi inayomjengea mtoto misingi bora ya maisha yake ya baadae. Kwa mujibu wa tafiti mbalimbali juu ya malezi ya watoto, kuna aina kuu nne za malezi.
1. Malezi ya kimabavu: Wazazi katika aina hii ya malezi huamini watoto lazima wafuate sheria na maelekezo yote wanayopewa bila kupuuza wala kukaidi.
 
2. Malezi ya mamlaka (demokrasia): Kama ilivyo kwa wazazi wenye malezi ya kimabavu, wazazi wenye malezi ya mamlaka huweka sheria na miongozo, lakini hutoa nafasi kwa watoto wao kujieleza na kuelezea mitazamo yao.
 
3. Malezi huru: Wazazi wenye malezi huru ni wavumilivu, na hawawafuatilii watoto wao sana. Huingilia na kuonekana pale tu panapojitokeza tatizo kubwa dhidi ya watoto wao.
 
4. Malezi huria: Wazazi wenye malezi huria, kimsingi hutarajia watoto wajilee wao wenyewe. Wazazi hawatumii nguvu nyingi kutafta mahitaji ya watoto wao. Wakati mwingine wazazi hawa, hawafahamu juu ya maendeleo ya watoto wao.
Aina zote za Malezi zinaathiri tofauti tabia ya mtoto. Tafiti zinaonyesha kuwa Malezi ya mamlaka (demokrasia) yana manufaa kwa watoto zaidi ya aina nyingine.
 
Je, ni aina ipi kati ya hizi umekua ukitumia kukuongoza katika safari yako ya Malezi?
 
Kama una swali lolote kuhusu malezi ya mtoto usisite kupiga namba 116, Huduma ya Simu kwa Mtoto inayopatikana kupitia mitandao yote Tanzania bila malipo.
 
Source: Sema Tanzania
Imesomwa mara 781
Nasra Sozi

Anwani ya barua pepe hii inalindwa kutokana na spambots. JavaScript lazima iwe itawezeshwa kwa kuweza kuona.