Ni muhimu kwa mzazi/ mlezi kufahamu aina ya chakula kimfaacho mtoto wake hususani yule aliye katika umri wa miezi tisa na nusu mpaka miaka sita. Aina hizi za vyakula na jinsi ya uandaaji wake hutofautiana sana na zile anazokula mtoto mkubwa au mtu mzima. Leo, mtaalamu wetu wa mapishi, Chef Issa anatuletelea ratiba ya chakula cha mtoto wa umri huo.

