Image
×

Onyo

JUser: :_load: Haiwezi kupakia mtumiaji aliye na kitambulisho: 797

Ni ugonjwa unaoshambulia ini na husababishwa na virusi au bacteria wa aina za A, B, C, D

Na vile vile huweza kusababishwa na :

  • Fangasi
  • Unywaji wa pombe (alcoholic hepatitis)
  • Dawa
  • Magonjwa yanayosababishwa na kinga ya mwili kuushambulia mwili (autoimmune)
  • Magonjwa ya kimetaboliki

Magonjwa yanayosababiswa na virusi au bacteria husambazwa kutokana na aina zake:

Homa ya Ini isababishwao na aina A (Hepatitis A), E

  • Kwa kula kinyesi kilichochanganyika na aina hii ya vimelea kwenye Maji, chakula

Homa ya Ini isababishwao na aina B (hepatitis B), C, D, G

  • Mchanganyiko wa damu ambao hutokana na:
    • Ngono zembe
    • Kutumia Sindano zilikwishatumika wakati wa matumizi ya madawa ya kulevya
    • Wakati wa kuwekewa damu
    • Kwenye kusafisha figo kwa wenye shida za figo

Mwaka 2013 virusi vya homa ya ini vilishika nafasi ya saba kwenye sababu ya vifo duniani,  mara nyingi homa ya Ini husababishwa na virusi zaidi ya hizo sababu nyingine.

Na homa ya ini imeganwanyika kama ifuatavyo

  • Ya hapo kwa papo kitaalamu acute hepatitis
  • Sugu kitaalamu chronic hepatitis

Dalili za Homa ya Ini

Kwa wagonjwa wengine wanaweza kukaa bila dalili mpaka madhara ya ugonjwa huu yanapoathiri ini.

Dalili ambazo hutokea ni:

  • Kichefuchefu
  • Kutapika
  • Ladha kubadilika mdomoni
  • Kupoteza hamu ya kula
  • Uchovu
  • Kuwashwa
  • Kukojoa mkojo mweusi
  • Maumivu ya tumbo upande wa juu wa kulia
  • Manjano kuonekana kwenye viganja vya mkono na machoni
  • Maumivu ya misuli na viungo
  • Homa

Madhara ambayo yanaweza kutokea baada ya kuugua homa ya Ini

  • Ini kuoza (hepatic necrosis)
  • Ini kukakamaa na kuota vinundunundu (cirrhosis)
  • Ini kushindwa kufanya kazi (hepatic failure)
  • Saratani ya Ini (hepatocellular carcinoma)

Vipimo

  1. Maabara
  • Kipimo cha damu kujua aina ya homa ya ini
  • Kipimo cha kuangalia ufanyaji kazi wa ini, kupitia kuangalia vimenge’nyo vya kwenye ini
  1. Picha
  • Kipimo cha kuangalia ini kitaalamu ultrasound

Tiba

Ni vyema kwenda hospitali na kufanyiwa uchunguzi kusudi upewe dawa na matibabu muhimu.

Baadhi ya wagonjwa huweza kunufaika na matibabu ya dawa, na madhumuni ya dawa ni kuzuia kuendelea kuathirika kwa ini

Dawa ambazo mgonjwa hupewa kitaalamu ni: ( interferons [IFNs], antivirals, and corticosteroids)

Lamivudine na Adenofir zimeonyesha matokeo ya kuaminika kwenye matibabu ya homa ya ini aina B.

 

 

Imesomwa mara 11313 Imehaririwa Jumatatu, 11 Juni 2018 13:23
Dr.Mayala

Dr.Henry A Mayala ni daktari bingwa Wa Tiba ya moyo katika taasisi ya Jakaya Kikwete Cardiac Institute (JKCI), ambaye kwasasa anasomea shahada ya uzamivu (PhD) ya Tiba ya Moyo katika Chuo Kikuu cha Tongji  nchini China.

Anwani ya barua pepe hii inalindwa kutokana na spambots. JavaScript lazima iwe itawezeshwa kwa kuweza kuona.