Image

Madhara ya Ugonjwa wa Kaswende katika Mfumo wa Mishipa ya Fahamu (Neurosyphilis)

 

Madhara ya ugonjwa wa kaswende katika mfumo wa mishipa ya  fahamu hutokea  miaka 10-20 baada ya mtu kuugua ugonjwa wa kaswende na ambaye hakupata tiba yoyote hapo awali. Madhara haya huonekana kwenye uti wa mgongo na kwenye ubongo.
Kuna aina nne ya neurosyphilis kama ifuatavyo:
1.Asymptomatic – Katika aina hii mgonjwa anakuwa hana dalili zozote. Aina hii ndio huonekana sana kwa wagonjwa ambao hawakupata tiba hapo awali.
2.General paresis
3.Meningovascular
4.Tabes dorsalis
General paresis hutokana na kuathirika kwa ubongo na hivyo kuleta upungufu katika ufanyaji kazi wa ubongo (impairement of mental function). Aina hii pia huweza kutokea kwa wagonjwa wa kisonono (gonorrhoea).
 
Dalili za general paresis
•Kupungua uwezo wa kuzungumza (aphasia)
•Kupungua uwezo wa kufanya maamuzi (impaired judgement)
•Kutokuwa na uwezo wa kuhesabu kitu chochote
•Kupungua kuhamasishika (impaired motivation)
•Kutokuwa na kumbukumbu ya vitu vilivyopita muda mrefu (loss of long term memory)
•Kutokuwa na kumbukumbu ya vitu vilivyopita karibuni/muda mfupi (loss of short term memory or recent events)
•Degedege
•Kushindwa kutembea au kutumia miguu, mikono na viungo vyengine vya mwili
•Personality changes  kama 
a.Delusions, kuona au kusikia vitu ambavyo visivyokuwepo (hallucinations)
b. Kukasirika kwa haraka (irritability)
c.Inappropiate moods
d.Low mood
 
Viashiria vya general paresis
•Mboni za jicho kuwa katika umbile ambalo si la kawaida
•Mboni kushindwa kupepesuka  (changes in pupil response)
•Loss of sense of vibration or position
•Kushindwa kusimama wakati mtu amefunga macho (romberg test)
•Kushindwa kutembea vizuri
•Viungo vya mwili kuwa dhoofu
•Matatizo ya kusahau
 
Vipimo vya uchunguzi
•FTA- ABS – Kipimo cha damu kinachofanya kuangalia antibodies za bakteria aina ya Treponema Pallidum  wanaosababisha kaswende
•RPR  (Rapid Plasma Reagin) – Kipimo hiki pia huangalia antibodies za Treponema Pallidum katika damu ya  wagonjwa wa kaswende
•VDRL (Veneral Disease Research Laboratory)- Kipimo cha kuangalia antibodies za  Treponema Pallidum, kipimo hiki kimeshahabiana sana na kipimo cha RPR.
•Lumbar Puncture – Kipimo cha kuchukua maji ya uti wa mgongo ili kuangalia kiwango cha sukari katika maji hayo, presha yake, protini, chembechembe nyekundu na nyeupe za damu, rangi yake, madini ya chloride. Kipimo hiki ni muhimu sana kwani husaidia kutambua kama kuna magonjwa mengine kama ugonjwa wa uti wa mgongo, multiple sclerosis, hypoglycemia, kiharusi, saratani, jipu nk.
•Cranial CT na MRI – CT Scan ya kichwa pamoja na kipimo cha MRI ili kuangalia kama kuna magonjwa mengine mbali na kaswende na kuangalia sehemu ipi ya ubongo iliyoathirika.
•Nerve conduction test – Kipimo cha neva za mwilini
•Vipimo vya macho
 
Dalili za meningovascular ni;
•Mboni kuwa ndogo
•Kupooza kutokana na kuathirika kwa neva mbalimbali
•Kuharibika mishipa ya damu mwilini
•Kupooza upande mmoja wa mwili
•Matatizo ya kumeza chakula – Kumeza chakula kwa shida
•Degedege
•Kupooza neva ya jicho (optic neuropathy)
•Chorioretinitis
•Kiziwi
•Vertigo nk.
 
Vipimo vya uchunguzi vya meningovascular
A.Vipimo vya hepatitis
B.ELISA for HIV – Kipimo cha ugonjwa wa ukimwi
C.PCR (Polymerase Chain Reaction) – Kipimo cha kuangalia vina saba vya bakteria mbalimbali kama Chlamydia trachomatis, Trichomonas vaginalis nk.
D.Urinalysis (urine test) – Vipimo vya mkojo
Tabes Dorsalis husababisha kudhoofika kwa viungo vya mwili kutokana na kuathirika kwa uti wa mgongo pamoja na mishipa ya fahamu. Hali hii ni hatari sana kwani ina kawaida ya kuwa endelevu na huweza kusababisha kifo kwa mgonjwa.
 
Dalili za Tabes Dorsalis
•Kutembea kwa shida
•Mgonjwa kutembea huku ametanua miguu sana (wide based gait)
•Kudhoofika viungo vya mwili
•Loss of coordination
•Abnormal sensation (lightening pains)
•Loss of reflexes
 
Vipimo vya uchunguzi vya Tabes Dorsalis
•CBC (Complete Blood Count) – Kipimo cha wingi wa damu, kuangalia aina za chembechembe za damu nk.
•Urinalysis – Kipimo cha mkojo
•Lumbar Puncture for CSF – Kipimo cha kuangalia maji ya uti wa mgongo kama nilivyoeleza hapo juu.
•CT Scan – Kipimo cha CT Scan ya kichwa, uti wa mgongo, moyo, mishipa ya damu.
•MRI ya kichwa
•VDRL, RPR, FTS-ABS, MHA-TP – Vipimo vya kuangalia antibodies za bakteria aina ya Treponema Pallidum kama nilivyowahi kueleza.
 
Tiba ya Neurosyphilis
Tiba ya aina zote za neurosyphilis huusisha kwanza kutibu ugonjwa wa kaswende kwa kutumia dawa za antibiotics aina ya penicillin G au doxycyline kwa wale wanaopata madhara ya penicillin. Hata hivyo kwa wale wenye matatizo na penicillin ni bora kumueleza Daktari mapema ili achukue hatua zinazostahili.
Kwa wale wagonjwa wasioweza kula, kuvaa nguo, wale waliopooza viungo, wasioweza kuzungumza, watahitaji tiba mbalimbali kama rehabilitation therapy, physical therapy, occupation therapy, speech therapy nk.
Dawa za maumivu na  degedege zinaweza kutumika kwa wale wenye kupata maumivu na degedege. Kwa wale viziwi, watahitaji vifaa maalum vya kuwasaidia kusikia (hearing aids) baada ya kuonana na Daktari wa masikio, pua na koo.
Imesomwa mara 506
Dr Khamis

Dr. Khamis H.Bakari (MD PhD) ni daktari bingwa,mhadhiri katika chuo cha afya cha Chuo  Kikuu cha Dodoma,mtaalamu wa Tiba na Uchunguzi kwa kutumia mionzi ya nyuklia (Nuclear medicine).

Anwani ya barua pepe hii inalindwa kutokana na spambots. JavaScript lazima iwe itawezeshwa kwa kuweza kuona.