Tatizo la kunyonyoka nywele hujulikana kitaalamu kama alopecia (tamka ‘’ alopesia’’). Hali hii ya kunyonyoka nywele husabababishwa na mfumo wa kinga ya mwili kushambulia mwili wa mtu husika (autoimmune disorder).
Kwenye alopecia, mfumo wa kinga ya mwili hushambulia mizizi ya nywele (hair follicles) na hivyo kusababisha kunyonyoka kwa nywele.
Wingi wa kunyonyoka nywele hutofautiana kati ya mtu mmoja na mwingine.Kwa baadhi ya watu, nywele hunyonyoka sehemu ndogo na kusababisha mabaka mabaka madogo ambayo mwanzoni sio rahisi mtu kugundua.Baadae mabaka haya huungana na kuwa sehemu moja kubwa iliyonyonyoka nywele na hatimaye mtu anaweza kugundua.
Kwa wengine, nywele hunyonyoka kwa wingi sana. Baadhi ya wagonjwa wameota nywele baada ya awali kunyonyoka na kisha nywele hizo hunyonyoka tena. Mara chache hutokea kwa mgonjwa alienyonyoka nywele kuota tena nywele hizo kwa maisha yake yote.
Alopecia haina uhusiano wa umri wala jinsia ya mtu.Kwa hiyo, mtu yoyote anaweza kupata hali hii.
Kwa kawaida, meno ya mtoto ya utotoni (meno ya awali) huanza kutoka kuanzia miaka 6. Kwa baadhi ya watoto, huweza kuchelewa kuanza kutoka meno ya utotoni hadi wanapoanza mwaka wA 7.
Meno ya kwanza yanayoanza kutoka ni yale mawili ya chini ya kati (lower central incisors) na hufuatiwa na yale ya juu ya kati (upper central incisors) (. Baada ya hapo, hufuatiwa na meno ya kutafunia ya kwanza na ya pili.
Kwa kawaida, meno ya ya awali hukaa bila kutoka mpaka pale meno ya kudumu yanapotaka kuanza kuchomoza, hivyo hulisukuma jino la utoto na kusababisha kutoka. Endapo mtoto atatoka meno mapema au jino litatoka kwa sababu ya ajali au kuoza, basi jino la kudumu litaziba pengo hilo baada ya muda kufika. Hii inaweza kusababisha meno kutokuwa na mpangilio mzuri kwakuwa wakati linachomoza kulikuwa na meno mengine ya utotoni, hivyo unashauri kuwasiliana na daktari wa kinywa na meno kwa ushauri zaidi.
Pale mtoto anapoanza kutoka meno, tafadhali zingatia kanuni bora za Afya ya kinywa na meno kama ;
- Kuhakikisha anasubua meno angalau mara mbili kwa siku. Mkazanie kwa sababu umakini unahitajika.
- Msaidie mtoto kusugua meno kila siku
- Hakikisha anakula chakula bora na kupunguza matumizi ya vyakula vitamu
- Weka miadi na daktari wa kinywa nameno
Kwa mazingatio haya, utaweza kuhakikisha afya bora ya kinywa na meno ya mtoto wako. Pia, unaweza kusoma makala zaidi juu ya Afya ya kinywa na meno wakati wa makuzi ya mtoto
Afya bora ya kinywa na meno kwa mtoto ni muhimu sana na ina uhususiano wa moja kwa moja na afya yake kwa ujumla. Humuepusha mtoto kupata maumivu, uwezekano wa uambukizo, kumfanya aweze kutafuna vizuri ili kupata virutubisho muhimu kwa ajili ya kujenga kinga dhidi ya magonjwa, na kusaidia ukuaji. Afya nzuri ya kinywa na meno pia itamfanya mtoto aweze kuhudhuria masomo ipasavyo na hivyo kupata matokeo mazuri.
Umuhimu wa meno ya utoto
Wazazi /walezi wengi hujiuliza kwanini wahangaike kutunza meno ya utoto ambayo yanatarajiwa kung’oka na kuota ya ukubwa. Meno ya utoto ni muhimu kutokana na sababu zifuatazo:
Humsadia mtoto kutafuna na hivyo kumwezesha kupata virutubisho muhimu
Hutunza nafasi kwa ajili ya meno ya ukubwa
Hali ya afya ya meno ya utoto huathiri hali ya afya ya meno ya ukubwani
Husadia uumbaji wa maneno (kuongea)
Kama mzazi / mlezi unatakiwa kuwa mstari wa mbele kutunza meno ya mtoto wako kwani, watoto hupenda kujifunza kutokana na mfano wa wazazi.
Zifuatazo ni dondoo muhimu kwa wazazi/walezi kwa ajili ya kutunza afya bora ya mtoto:
Umri wa kuzaliwa mpaka miezi 6
- Mnyonyeshe mtoto maziwa ya mama pekee hadi umri wa miezi sita.
- Maziwa ya mama ni muhimu sana kwa ukuaji na kinga dhidi ya magonjwa.
Umri wa miezi 7 hadi miezi 18
- Usimlaze mtoto akiwa na chuchu ya maziwa au chuchu ya mama mdomoni ili kuzuia ugonjwa wa kuoza kwa meno (rampant caries)
- Mpatie mtoto maji badala ya juisi akiwa na kiu.
- Iwapo utampa mtoto juisi ya boksi unashauriwa kuongeza kiwango cha maji sawa na kile cha juisi ili kupunguza kiasi cha sukari kilichomo ndani ya juisi.
- Ukitengeneza juisi nyumbani kwa ajili ya mtoto, jiepushe kuiongezea sukari.
- Jino la kwanza litakapoota, anza kusafisha kinywa cha mtoto kutumia kitambaa laini kilicholoweshwa kwenye maji safi au mswaki laini bila dawa.
- Panga miadi ya kwanza ya kumwona daktari wa meno (first appointment) wakati mwanao hana maumivu au shida yoyote ili kujenga mahusiano mazuri kati ya mtoto na daktari
Umri wa miezi 18 hadi miaka 6
- Dhibiti ulaji wa vyakula vyenye sukari na zingatia ulaji wa vyakula vinavyojenga afya ya mtoto kama matunda, mboga mboga, karanga, maziwa na samaki.
- Safisha meno ya mtoto kutumia maji safi na mswaki laini na dawa ya meno (zingatia kiwango cha dawa: kiasi cha mbegu ya kunde) asubuhi na jioni kila siku.
- Mtoto asukutue mdomoni ili kupunguza kiwango cha dawa itakayobaki.
- Chunguza mara kwa mara meno ya mtoto ili kugundua dalili za mwanzo za ugonjwa wa kuoza kwa meno (rangi kuwa nyeupe au kahawia zaidi katika eneo husika baada ya kukausha) na pia matatizo mengine kama uvimbe, vijipu au kutoka damu kwenye fizi.
- Mpeleke mtoto kwa daktari wa meno angalau mara moja kwa mwaka na mara unapogundua tatizo lolote kinywani mwake.
Umri wa miaka 6 hadi 12
- Msimamie mtoto kusafisha kinywa na meno mara mbili kwa siku.
- Mtoto ateme dawa itakayobaki ila asisukutue na maji baada ya kupiga mswaki.
- Mjengee mtoto tabia ya kusukutua na maji kila baada ya kula vyakula vyenye sukari kama keki, chokoleti au juisi.
- Chunguza mara kwa mara meno ya mtoto ili kugundua dalili za mwanzo za ugonjwa wa kuoza kwa meno na matatizo mengine kinywani.
- Mpeleke mtoto kwa daktari wa meno angalau mara moja kwa mwaka na mara unapogundua tatizo lolote kinywani mwake.
Umri wa miaka 12 na zaidi
- Mtoto anaweza kuanza kusafisha kinywa na meno bila ya usimamizi.
- Dhibiti ulaji wa vyakula vyenye sukari na zingatia ulaji wa vyakula vinavyojenga afya ya mtoto kama matunda, mboga mboga, karanga, maziwa na samaki.
- Mpeleke mtoto kwa daktari wa meno angalau mara moja kwa mwaka na mara unapogundua tatizo lolote kinywani mwake.
CREDIT: Muhimbili University of Health and Allied Sciences (MUHAS)
Assalamu’alaikum Warahmutullahi Wabarakatuh. Natumai mu wazima wa afya na mnaendelea vyema na majukumu ya kila siku.
Waumini wa dini ya Kiislam duniani kote wameingia katika mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani. Hivyo,katika muendelezo wa makala zinazohusu kisukari, tunaoenda tujikumbushe au tujifunze mambo machache ya kufanya kabla, wakati na baada ya kipindi takatifu cha mfungo wa Ramadhani.
Tukiwa tuna amini kuwa watu wengi wanaoishi na tatizo la Kisukari hasa aina ya pili ya kisukari wanatamani sana kufunga Ramadhani katika kutimiza moja ya nguzo za imani ya dini ya Kiislam, na kwa imani Funga ni dawa kiroho na kimwili pia.
Jambo la kwanza kwa mtu mwenye kisukari ni kujiweka tayari kwa funga miezi mitatu au minne kabla, kuitayarisha akili na nafsi,hii itakusaidia kuwa mwangalifu sana katika ulaji wako na mfumo mzima wa ulaji.
Kufanya kipimo cha hba1c ni muhimu kwa sababu inaonesha kiwango cha sukari miezi mitatu na hii inakufanya ujue kama utaweza kufunga ramadhan bila kuwa tatizo lolote au hutaweza kufunga. Kupima sukari kabla na baada ya kula kabla ya mfungo wa ramadhani pia ni muhimu,kabla ya kula ni lazima sukari iwe chini ya sita(6) na masaa mawili baada ya kula iwe chini ya nane (8) na kama majibu yatakuwa hivyo kila mara hii itakuonesha kuwa unaweza kufunga bila tatizo.
Jambo la pili ni kuhakikisha unapata ushauri kutoka kwaa daktari wako wa kisukari, Shauriana naye, usiamue kufunga Ramadhani bila ya kushauriana na daktari wako, hii ni muhimu kwa sababu anaweza kukupa ushauri kulingana na kiwango chako cha sukari kwa miezi mitatu nyuma.(hba1c) na kipimo cha sukari cha kila siku unachopima kabla na masaa mawili baada ya kula.
Wakati wa mfungo ni lazima mtu mwenye kisukari atambue kuwa anaweza kufunga baada ya ushauri na ruhusa dakitari wake,na endapo akifunga, ni lazima pia awe anapima kiwango cha sukar kabla ya kuanza ,mfungo,kwa mfano, kabla ya kula daku ni lazima apima,hii itamsaidia kujua kama ataweza kufunga kwa siku hiyo ama Lah, kama akipima na kiwango cha sukari kikiwa sita (6) au saba(7) anaweza kufunga lakini indapo akipima akikuta kwango cha sukar iki chini ya sita (6), labda ni tano(5) au nne (4) hatoweza kufunga kwa sababu moja ya kisababisho cha sukari kushuka ni kukaa bila kula kwa muda mrefu.
Kutokupata choo au kuhisi kwenda kujisaidia haja kubwa na kutofanikiwa kutoa choo au mtu kupata choo chini ya mara tatu kwa wiki hujulikana kitaalamu kama constipation.Mtu mwenye tatizo hili la kufunga choo hupata choo kigumu,kikavu na chenye kupita kwa taabu kwenye njia ya haja kubwa.
Tafiti nyingi zinaonyesha kwamba angalau kila mtu katika maisha yake huwa anapata tatizo hili la kufunga choo. Kufunga choo ni tatizo ambalo watu wengi bado huhisi ni jambo la aibu sana hata kulizungumzia na hubaki na tatizo kwa muda mrefu mpaka pale wanapopata madhara ya kiafya ndio hutafuta msaada wa kitabibu.
Dalili zifuatazo zinaweza kutumika kuelezea tatizo la choo kufunga;
- Kupata choo kigumu na kinachoambatana na maumivu makali wakati wa kwenda haja kubwa
- Kutokupata choo kwa muda mrefu (infrequent bowel movements)
- Mtu kuhisi kama hajamaliza haja kubwa licha ya kupata choo
Tafiti nyingi zilizowahi kufayika zinaonyesha kwamba takribani asilimia 16 (16%) ya watu wazima hupata tatizo hili la kufunga choo,waathirika wengi wakiwa ni watu wenye umri kati ya 60-110 (asilimia 35%).
Kwa nini wazee hupata tatizo hili la kufunga choo?
Sababu zifuatazo huchangia wazee kutokupata choo au kufunga choo;
- Hali ya uzee husababisha mmeng’enyo wa chakula kufanyika taratibu (slow metabolism)
- Ukosefu wa lishe bora
- Kutokunywa maji ya kutosha
- Kutofanya mazoezi
- Magonjwa ya uzee kama pelvic floor prolapse na utumiaji wa dawa aina ya antacids na dawa za kupunguza maumivu
- Pia uzee husababisha meno kung’oka hivyo wazee huchagua vyakula laini na vyenye ufumwele (fiber) kidogo
Wanawake wajawazito ni miongoni mwa watu wanaopata tatizo hili la kufunga choo mara kwa mara.
Visababishi vya choo kufunga (constipation) ni kama ifuatavyo;
- Kutokula mlo wenye ufumwele (fiber) wa kutosha
- Kutokunywa maji ya kutosha
- Kutumia sana dawa za kulainisha choo
- Kutokufanya mazoezi au
- kuishi maisha ya unyongovu (stressful life)
- Madawa kama aspirin (NSAID), morphine, dawa za presha(thiazides, verapamil, furosemide), dawa za sonono (antidpressants), madawa ya saratani n.k
- Magonjwa ya mfumo wa mmengenyo wa chakula au vichocheo vya mwili (hormonal disorders) kama hypothyroidism
- Ujauzito- Mama mjamzito yupo kwenye hatari zaidi ya kupata choo kigumu au constipation hasa katika miezi ya mwisho ya ujauzaito wake kwa sababu ya kuongezeka kwa vichocheo mwili aina ya sex hormones, kupungua kwa mmeng’enyo kwenye tumbo na kuchelewa kwa tumbo kupitisha chakula (delayed interstinal emptying)
- Magonjwa ya tumbo kama colorectal dysfunction, diverticulitis, irritable bowel syndrome, saratani za matumbo hasa utumbo mkubwa
- Chronic Idiopathic constipation- Sababu zisizojulikana
Kama ambavyo tumejifunza sababu na makundi wa watu ambao wapo kwenye hatari zaidi. Tatizo hili linaweza kumpata mtu yoyote wa rika lolote hata watoto wachanga. Hivyo fuatilia makala zetu zijazo ili kujua uchunguzi,matibabu na jinsi ya kuepukana na tatizo hili la kufunga choo.Kama tayari una tatizo hili tafadhali fika kituo cha afya kilichokaribu nawe kwa ajili ya uchunguzi, matibabu na ushauri wa kitaalamu.
Watoto wanapozaliwa, tayari wanakuwa na meno ambayo yamefunikiwa kwa fizi. Meno huanza kutoka kwa mara ya kwanza mtoto akiwa na umri wa miezi sita ( 6) japo umri huu unaweza tofautiana kutoka kwa mtoto mmoja hadi mwingine.
Meno mawili ya kwanza yanayoonekana mara nyingi ni yale ya kinywa cha chini katikati yakifuatiwa na ya kinywa cha juu katikati. Watoto wengi hufikisha meno yote 20 ya kwanza wakiwa na umri wa miaka 3.
Baadhi ya watoto hawaoti meno kama watoto wengine, yao huchelewa au kutokuota kabisa. Hii husababishwa na vitu mbalimbali. Kama mtoto wako hajaota jino hata moja hadi umri wa miezi 18 basi ni muhimu umpeleke hospitali aonane na daktari wa kinywa na meno kwa ajili ya uchunguzi zaidi.
Sababu za meno kuchelewa kuota
Zipo sababu nyingi za meno kuchelewa kuota. Wakati mwingine tatizo la meno kuchelewa kuota huwa ni tatizo la kwenye familia hivyo linaweza kurithishwa kwa vizazi vinavyokuja. Mzazi pia ujiulize kama meno yako yalichelewa kuota, kama ni ndio basi tambua kwamba hata ya mwanao yataota tu japo kwa kuchelewa.
Sababu zinazochangia meno kuchelewa kuota kwa mtoto ni kama zifuatazo;
- Utapia mlo na upungufu wa madini na vitamini mwilini- Watoto wenye utapia mlo meno huchelewa kuota kwa sababu ya kukosa virutubisho muhimu vya ukuaji wa meno. Aidha madini ya calcium na vitamini D ni muhimu sana katika ukuaji wa meno. Hivyo mtoto akipungukiwa na virutubisho hivi meno huchelewa kuota.
- Ugonjwa wa jeni unaofahamika kama Down Syndrome- Huu ni miongoni mwa mgonjwa wa kuzaliwa nayo (congenital).Ugonjwa huu unatokana na hitilafu kwenye kinasaba cha 21 (chromosome 21). Ugonjwa huu huambatana na tatizo la meno kuchelewa kuota.
- Magojwa ya yatokanayo na hitalifu kwenye chromosomes (chromosome anomalies)
- Mtoto kuzaliwa njiti-Kuzaliwa njiti au na kuzaliwa na uzito mdogo kupita kawaida (chini ya 1.5kg) kunahusishwa na kuchelewa kuota kwa meno kwa mtoto. Watoto hawa wanaweza kuwa na matatizo ya meno yenyewe.
- Magonjwa kama Amelogenesis na Regional Odontodysplasia
Amelogenesis ni ugonjwa wa kuzaliwa nao (congenital disease) ambapo mtoto anazaliwa na hitilafu kwenye kwenye protini zinazotengeneza enameli (nyeupe ngumu ya jino) hii hupelekea kuwa na enameli isiyo ya kawaida na meno yanakuwa ya njano. Hii huambatana na meno kuchelewa kuota.
Regional odondodysplasia ni hitilafu katika ukuaji inayohusisha mesodermal na ectoderm (hizi ndizo zinazotengeneza jino la ndani na nje) za meno. Ugonjwa huu huwa unaathiri sehemu moja tu ya kinywa (localized). Huu sio ugonjwa wa kurithi.
Kwanini uwe na wasiwasi kuhusu meno ya mtoto yanapochelewa kuota?
Watoto ambao hawajaota meno hadi umri wa miezi 18 wapelekwe kumuona daktari wa meno. Watoto wengi huwa na meno manne wakifikia umri wa miezi 12 na huwa na yote 20 wakiwa na miezi 27.
Kama meno ya mtoto wako hayajaota kwa wakati inaweza kuwa ni ishara ya ugonjwa au upungufu wa madini au vitamini fulani mwilini.
Je, meno kuchelewa kutoa ni dalili mbaya?
Meno kuchelewa kuota sio jambo kubwa sana ila linaweza kuongeza uwezekano wa mtoto kupata matatizo ya meno ukubwani. Tafiti nyingi zinaonyesha kuwa watoto waliopata tatizo la meno kuchelewa kuota wana nafasi kubwa ya kuhitaji matibabu ya meno wakiwa na umri wa miaka 30.
Meno kuota kwa wakati kwa mtoto humsaidia kutafuna vizuri na husaidia meno ya pili kujipanga vizuri kwenye kinywa.
Meno yakichelewa kuota husababisha mtoto kukosa au kupata virutubisho vichache maana atakuwa hawezi kutafuna vizuri hivyo kupata shida ya kumeng’enya chakula.
Jinsi ya kutunza meno mapya ya mtoto wako
- Epuka vyakula na vinywaji vyenye sukari
- Safisha fizi kwa kutumia kutambaa kisafi mara mbili kwa siku
- Epuka kumlaza mtoto na chupa ya maziwa kitandani
- Kumbuka kuswaki na kusafisha meno yaliyoota
Utaanza kutumia dawa ya meno pindi mtoto akifikisha miaka 2.
Naweza Kunywa Pombe kama nina Ugonjwa wa kisukari?
Wagonjwa wengi wa kisukari wameniuliza kuhusu swali hili.Aghalabu, hata wengine ambao wanasoma makala hii pia watakuwa na shauku ya kutaka kujua kama kweli wanaweza kunywa pombe ilihali wanaugua ugonjwa wa kisukari bila kupata madhara yoyote ya afya.Swali hili ni la msingi sana hasa unapokuwa kwenye matibabu ya ugonjwa wa kisukari.
Ugonjwa wa kisukari ni moja kati ya magonjwa mengi yasiyoambukiza (non-communicable diseases) ambayo yanongezeka kwa kasi na kusababisha vifo na ulemavu.
Taarifa ya International Diabetes Federation imesema watu millioni 463 duniani wanaishi na kisukari na millioni 19 ya hao wapo bara la Afrika pekee.
Shirika hili katika taarifa yake ya mwaka 2020 limesema kwamba uwezekano wa kupata ugonjwa wa kisukari nchini Tanzania ni kwa asilimia 3.7 huku idadi ya wagonjwa wa kisukari watu wazima imefika takribani watu 997,400.
Unywaji wa pombe uliopitiliza kwa watu wenye kisukari husababisha madhara makubwa ikiwemo kuongeza hatari ya kupata shinikizo la damu, magonjwa ya moyo,macho na kuharibika kwa mishipa ya fahamu.
Aidha Pombe au vileo vingi vina idadi kubwa ya wanga na sukari hivyo husababisha kupanda kwa haraka kwa sukari kwenye damu. Pia vina kalori nyingi hii upelekea kuwepo hatari ya kuongezeka uzito uliopitiliza ambapo hupunguza unyeti (sensitivity) na utolewaji wa kichocheo aina ya insulin mwishowe husababisha ugumu wa kudhibiti sukari yako mwilini.
Sasa je naweza kunywa pombe kama ni ugonjwa wa kisukari?
jibu ni NDIO japo inabidi ujenge tabia ya kuwa na tahadhari pindi unapokunywa pombe.
Utatumia pombe pale tu ambapo sukari yako imedhibitiwa vizuri na kwa hali yoyote epuka unywaji pombe kupitiliza.
Najua kuna swali unaliwaza kuwa nisinywe kupitiliza unaamanisha nini?
Hili ni swali zuri na la msingi.Kulingana na shirika la ugonjwa wa kisukari la marekani (American Dabetes Association), imetoa vipimo vifuatavyo vya unywaji wa pombe kwa watu wenye kisukari.
Mwanamke mwenye kisukari asinywe zaidi ya chupa moja ya bia sawa na 350mls, au 147 mls za wine na 44 mls za pombe kali kwa siku.
Kwa mwanamume, asinywe zaidi ya bia mbili sawa na 700mls, au 294 mls za wine au 88 mls za pombe kali.
USHAURI
Kabla ya kunywa pombe hebu jiulize masawali yafuatayo;
Je sukari yangu imedhibitiwa?
Je daktari wangu anakubali nitumie pombe au kilevi cha aina yoyote ile?
Je najua jinsi pombe inaweza kuniathiri mimi pamoja na sukari yangu?
Kama majibu yako yote ni ndio basi waweza kunywa pombe. Ila kumbuka pombe pia husababisha sukari kushuka. Ni vizuri kufahamu kiwango cha sukari yako mwilini kabla, wakati na baada ya kunywa pombe angalau kwa kipindi cha masaa 12.
Usikose kutembelea TanZMED kwa makala zaidi za afya kwa lugha ya kiswahili.
U-hali gani msomaji wetu wa makala zetu za kisukari, karibuni tena katika makala nyingine ya kisukari, leo tunaangalia kwa ufupi tu siku na mwezi ya kisukari duniani, na pia tutadadavua kwanini kuna mwezi wa kisukari na malengo yake hasa ni nini na pia kwa kuwa sio wote wananojua kuhusu mwezi wa kisukari, karibuni.
Kila mwaka ifikapo mwezi wa November ni siku ya kisukari duniani, mwezi huu wote umetengwa kuwa ni mwezi maalum kwa kueleza elimu na uelewa juu ya tatizo hili ya kisukari, pia kuboresha matibabu ya maradhi yanayotokana na kisukari, maadhimisho wake ni tarehe kumi na nne (14) ya mwezi November.
Kwanini iwe mwezi wa November, tarehe kumi na nne(14)? Inawezekana unajiuliza hili swali kila mara na kila ifikapo mwezi November, shirika ya afya duniani na shirikisho ya kimataifa la kisukari yalikutana na kukubalia kutenga tarehe kumi na nne (14) November kuwa ni mwezi wa kisukari duniani kwa sababu ni mwezi ambayo ndugu Frederick Banting ambaye ni mgunduzi wa kichocheo kiitwacho INSULIN ambacho hutumika kama dawa kwa wengi aina ya kwanza ya kisukari alizaliwa. Katika kumuenzi mgunduzi huyu mashirika haya mawili wakaona ni busara kutenga mwezi huu na tarehe hii kuwa ni siku ya kisukari duniani kote.
Ni moja kati ya magonjwa sugu yahusuyo mfumo wa kinga ya mwili kushambulia mwili wako na huwa na mtindo wa kuwa na kipindi cha kupata nafuu na kuwa kama umepona na kipindi cha kushambulia na kuwa hoi.
Huathiri zaidi wanawake, hadi asilimia 90 ya wagonjwa huwa wanawake. Na mara nyingi huanza kwenye umri wa uwezo wa ubebaji mimba.
Vipele ambavyo hutokea kipindi cha jua huathiri Ngozi (picha kwa hisani ya Dr. Erik Stratman, Marshfield Clinic)
Dalili
Ugonjwa huu huathiri karibu kila kiungo kwenye mwili
Dalili 3 kubwa ambazo hutokea ni:
- Homa
- Maumivu ya viungo
- Vipele
Picha inaonyesha vipele usoni hasa kwenye mashavu na pua kitalaamu Butterfly rash (Picha Kwa hisani ya affordablehealthinsurance.org)
Dalili nyingine ni:
- Uchovu
- Kupungua uzito
- Figo kushindwa kufanya kazi vizuri
- Dege dege
- Maji kujaa kwenye mapafu, shinikizo la mapafu
- Maumivu ya tumbo, kichefu chefu
- Upungu wa damu, upungufu wa chembe chembe sahani
Vipimo:
Vipimo vya uhakika kuthibitisha ugonjwa huu ni;
- Kipimo cha vinasaba kitaalamu double strand DNA antibodies na
- Kingine kitaalamu Antinuclear antibody (ANA)
Vipimo vingine ni:
- CBC- kujua wingi wa damu, na chembe chembe sahani
- Kipimo cha damu kujua uwezo wa figo kufanya kazi (RFT)
- Kipimo cha damu cha kujua uwezo wa ini kufanya kazi (LFT)
Matibabu:
Ugonjwa huu hauna tiba ziaidi ni kutibu dalili na kupunguza makali yake
Moja kati ya dawa ambazo hutumika ni:
- Dawa za malaria - ambazo husaidia kupunguza makali yak inga kuushambulia mwili bila kuishusha kinga ya mwili. Dawa hizi pia huzuia na kutibu vipele ambavyo husababishwa na ugonjwa huu. Mfano wa dawa hizi ni: Hydroxychloroquine sulfate (Plaquenil)
- Dawa za maumivu- ambazo husaidia kupunguza homa, maumivu ya kichwa na maumivu ya viungo. Mfano wa dawa hizi ni: Ibuprofen (advil, motrin)
- Dawa za kupunguza kinga ya mwili- dawa hizi hupunguza kinga ya mwili hivyo kupunguza makali ya kushambulia mwili hivyo kupunguza makali ya ugonjwa, mfano wa dawa hizi ni: cyclophosphamide na methotrexate
- Na kutibu kila dalili zitakazo jitokeza ipasavyo
Moja ya matatizo yanayoathiri sana jamii kubwa ya watanzania hususani watoto ni ugonjwa wa sickle cell. Ugonjwa huu wa kinasaba huathiri hemoglobin, sehemu iliyo muhimu sana katika muundo na ufanisi wa chembe nyekundu za damu.
Kazi kuu ya hemoglobin katika chembe nyekundu za damu ni kubeba, kusafirisha na kusambaza wa hewa ya oksijeni katika mwilini.
Watu wenye ugonjwa huu, hupata mabadiliko ya vinasaba ambayo hutokea katika nafasi ya sita ya mnyororo wa beta globin (beta chain) katika hemoglobin ambapo kiasili cha valine ambacho ni mojawapo ya tindikali muhimu za amino (amino acid) huchukua nafasi ya kiasili cha glutamate na hivyo kubadili kabisa umbo la chembechembe nyekundu za damu na kuzifanya zishindwe kufanya kazi zake vile inavyopaswa.
Kuna aina mbali mbali za sickle cell, nazo ni HbSS, HbAS, HbSC, HbSD na HbSO. HbSS huwaathiri watu wengi zaidi wakati wenye HbAS huitwa carriers au sickle cell traits kwa vile ndiyo wanaobeba tatizo hili la kijenetekia na kueneza kwa wengine ingawa wao mara nyingi kama siyo zote hawaoneshi dalili zozote za ugonjwa huu.
Dalili za ugonjwa wa sickle cell ni zipi?
Dalili za ugonjwa wa sickle cell hutegemea sana na kiwango cha uathirikaji wa chembe nyekundu za damu.
Kiujumla dalili zinaweza kuwa ni zile zinazohusiana na upungufu wa chembe nyekundu za damu mwilini yaani anemia, unaotokana na kuharibika kwa chembe hizo. Hizi ni pamoja na
- Kushindwa kupumua vizuri
- Kizunguzungu
- Maumivu ya kichwa
- Ubaridi katika viganja na miguuni
- Unjano katika macho na ngozi au jaundice
- Weupe katika viganja, na eneo la macho liitwalo conjuctiva, ulimi na midomo
- Maumivu ya tumbo
- Homa
- Maumivu ya viungo (joint pains)
- Maumivu ya kifua
- Damu katika mkojo (hematuria)