Uzoefu wa mawasiliano wanaopata watoto ni muhimu sana katika kuwajengea watoto uwezo wa kuwasiliana na watu wengine nje ya familia kwa kwa njia bora zaidi.
Matokeo yetu yameonyesha ya kwamba, chakula cha pamoja cha familia sio tu kinajenga mazingira mazuri nyumbani bali pia ni nafasi nzuri kwa wazazi kuendelea kuwafunza na kuwaendeleza watoto kama watu muhimu kwenye jamii,’’ aliendelea kusema Professor Linda Pagani
Professor Pagani alishirikiana na mwanafunzi wa shahada ya uzamivu (PhD student) Marie-Josee Harbec, katika kuwafanyia uchunguzi watoto waliozaliwa katika Jimbo la Quebec kati ya mwaka 1997 na 1998.
Watoto waliohusika kwenye tafiti hii,walianza kufuatiliwa tokea wakiwa na umri wa miezi mitano mpaka walipotimiza umri wa miaka 10.
Walipofikisha umri wa miaka sita,wazazi wao walianza kutoa taarifa kama walikuwa wakijumuika pamoja na watoto wao wakati wa kula chakula au la.Na pia walipotimiza umri wa miaka 10, wazazi,walimu na watoto wenyewe walitoa maelezo kuhusiana na ukuaji wao,tabia zao za maingiliano na watu wengine na afya zao kiakili na kimwili.
‘’Tuliamua kuangalia faida za muda mrefu za kula chakula kwa pamoja kama familia kwa watoto na kulinganisha na watoto walio na umri sawa na watoto hawa lakini ambao wazazi,ndugu na walezi hawajumuiki nao wakati wa kula chakula,’’ aliendelea kusema Professor Linda Pagani.
Uwepo wa mjumuiko wa pamoja wakati wa kula chakula kwa watoto wenye umri wa miaka sita husababisha watoto hao kuwa na afya njema kiakili na kimwili wanapotimiza umri wa miaka 10.
‘’Kwa sababu tulikuwa na taarifa nyingi za watoto kabla ya kutimiza umri wa miaka sita,zikiwemo taarifa za kiwango chao cha hasira, uwezo wao kiakili,kiwango cha elimu ya wazazi wao, kujumuika na mwingiliano wa familia, ilikuwa rahisi kwetu kuchanganua taarifa zetu na hivyo kupata matokeo mazuri ya tafiti yetu’’ alisema Dr. Harbec
Ushauri kutoka TanzMED
Ni vizuri kwa familia kuzingatia matokeo ya tafiti hii hasa kupenda kujumuika pamoja wakati wa kula chakula ili kuwasaidia watoto katika kujijengea uwezo wa kuwasiliana, kujiamini na kupata malezi mema.