Image

Jinsi ya kupunguza maumivu wakati wa hedhi

Zipo njia nyingi ya kutibia maumivu ya hedhi.

Mojawapo ni kuweka chupa au mfuko wenye maji ya moto kwenye sehemu ya chini ya tumbo (isiwe moto mkali wa kuunguza ngozi).


Dawa za kutuliza maumivu kama ibuprofen, mefenamic acid, naproxen.


Matumizi ya vidonge vya uzazi wa mpango pia husaidia kupunguza maumivu ya hedhi. Kama ilivyo kwa dawa nyingine, ni muhimu kupata ushauri wa kitaalam kabla ya kuanza kutumia dawa hizi. 

Iwapo njia hizi hazifanikiwi kutuliza maumivu ya hedhi, vipimo zaidi vinahitajika ili kugundua chanzo cha maumivu hayo.

Miongoni mwa vipimo vinavyohitajika ni vipimo vya magonjwa ya infection ya njia ya uzazi pamoja na upasuaji ili kuona uwepo wa endometriosis na kuiondoa (picha zinaonyesha jinsi upasuaji huo unavyofanyika kwa matundu madogo na kamera bila kafungua tumbo).

Iwapo maumivu ni makali sana na hayatibiki kwa dawa, mgonjwa asiyekuwa na mpango wa kupata mtoto hushauriwa kuondoa kifuko cha uzazi.

Imesomwa mara 5737 Imehaririwa Jumatano, 13 Machi 2019 16:07
Dr Khamis

Dr. Khamis H.Bakari (MD PhD) ni daktari bingwa,mhadhiri katika chuo cha afya cha Chuo  Kikuu cha Dodoma,mtaalamu wa Tiba na Uchunguzi kwa kutumia mionzi ya nyuklia (Nuclear medicine).

Anwani ya barua pepe hii inalindwa kutokana na spambots. JavaScript lazima iwe itawezeshwa kwa kuweza kuona.