Tendo la ndoa husaidia kupunguza ama kutoa msongo wa mawazo, na kama tunavyojua kuwa msongo wa mawazo huchangia kupandisha sukari kwa mtu mwenye Kisukari na pia hutoa au hupunguza hatari ya kupata shinikizo la damu,kasi ya mapigo ya moyo wakati wa tendo la inaweza kupunguza hatari ya kupata shinikizo la dawa na kupanda kwa sukari,wataalamu wanasema sio tu kwa mtu mwenye tatizo la kisukari ila hii ni kwa kila mtu,kufanya tendo la ndoa.
Majibu ya tafiti iliyofanya na chuo kikuu cha Yale huku nchini Marekani, ulionesha kuwa watu wenye tatizo la Kisukari hupata shida kupata usingizi,uchovu wa akili, na pia husahau mara kwa mara, Tendo la ndoa hasa kwa wenye Kisukari linasaidia kumpatia mtu amani, utulivu wa mwili na akili na pia huboresha afya ya akili.
Kwa kumalizia basi, kwa yeyote kwenye tatizo ya Sukari, asiogope kufanya tendo la ndoa kwa kuhofia labda unaweza kupata tatizo, kama nilivyosema mwanzoni kuwa tendo la ndoa hupunguza presha kwenye damu, husaidia kuchoma mafua au kuyeyusha mafuta mwilini,husaidia kuboresha afya ya mwili na akili, huondoa msongo wa mawazo na uchovu,huongeza furaha katika maisha na vyote hivyo zinasaidia kudhibiti kiwango cha sukari.