Kifafa ni milipuko na mivurugano ya mfumo wa umeme wa kwenye ubongo kunakoweza kupelekea kupoteza fahamu kwa dakika kadhaa pamoja, kujikolea ama hata kutokwa na haja kubwa. Ugonjwa huu unaweza kufafanishwa na volcano za milima zinavyotokea. Baadhi ya vifafa huambatana na mabadiliko ya kitabia (psychosis).
Kitabibu, kuna aina mbili za Kifafa, aina ya kwanza kinaweza kutokea sehemu moja ya ubongo (focal) ama ubongo mzima (generalized).
UKWELI KUHUSU KIFAFA
- Hakiambukizi
- Hakitokani na laana
VIHATARISHI VYAKE
- Homa kali kwa watoto wadogo
- Mtu anayetoka kwenye familia yenye maradhi ya kifafa
- Ajali za ubongo
- Saratani za ubongo
DALILI ZAKE
Hutegemea sehemu gani ya ubongo ilipoanzia ila mara nyingi ni
- Kukazia macho sehemu moja ama kuyapepesa haraka haraka kabla halijatokea
- Kupumbazwa
- Kutoka mate mdomoni na Kujing’ata ulimi
- Kukakamaa mikono na/au miguu
- Kupoteza fahamu na kisha kufuatiwa na Kujikolea na/au kujinyea
- Kwa wale ambao hawajapoteza fahamu, kupoteza baadhi ya hisia za ladha, harufu na sauti.
MAKOSA WAKATI WA KUMHUDUMIA MGONJWA WA KIFAFA
- Kumfunga Kamba
- Kumpa kitu mdomoni
MATIBABU YAKE
Kumuacha mgonjwa wa kifafa kwa dakika chache mpaka pale litakaposimama lenyewe kama uko mbali na hospitali na kama haliachi basi kumkimbiza haraka hospitali kwa matibabu zaidi.
Madaktari na wauguzi watamuanzishia dawa za kuchoma za kusimamisha degedege kisha kukushauri kuhusu kupima vipimo vya damu na EEG.
Baada ya kudhibiti hali ya dharura, ni vizuri ndugu wa karibu kufahamisha kuhusu kuzifahamu dalili za mgonjwa wao na jinsi ya kuishi nae ili kumuepusha na madhara Zaidi.