Saratani ya ubongo ni uvimbe uliotokana na mkusanyiko wa chembebehai za ubongo zilizotengenezwa kwa wingi bila mpangilio kutokana na kubadilika kwa DNA. Ikiwa chembehai hizo ni za kawaida basi uvimbe hujulikana kama BENIGN, na kinyume chake ni CANCER.
Saratani za ubongo ziko kwenye makundi makuu mawili; yaani PRIMARY ambayo imeanzia kwenye ubongo wenyewe au SECONDARY (METASTASIS) endapo imetokea sehemu nyingine ya mwili mbali na ubongo.
Ukweli kuhusu saratani za ubongo
- Kuna aina 120 au Zaidi za saratani ya ubongo.
- Dalili na madhara yake hutegemeana na aina, ukubwa na mahali ilipo kwenye ubongo.
Vihatarishi vyake
- Umri na jinsia ya kike.
- Baadhi ya mionzi au mionzi tiba.
- Baadhi ya magonjwa ya kinasaba kama vile Neurofibromatosis.
- Saratani za sehemu nyingine za mwili kama vile tezi la thyroid, mapafu, titi na ini.
Dalili zake
- Maumivu ya kichwa
- Kupungua nuru ya macho au upofu.
- Kupungua usikivu na kupepesuka.
- Kupoteza kumbukumbu na haiba.
- Kupooza mkono au mguu vya upande mmoja.
- Kupata degedege ama kupoteza fahamu.
- Kushindwa kumeza chakula.
Matibabu Yake
- Kufanyiwa vipimo vya damu, CT scan ama MRI ya ubongo.
- Kufanyiwa upasuaji na kupewa dawa