Image

Mtoto ale chakula muda gani?

Chai ya asubuhi

Saa 12:00 mpaka 2:00 kutegemeana na ni muda gani mtoto anakwenda shule. Jambo la muhimu ni kuwa, mzazi/mlezi ahakikishe mtoto anakula asubuhi ili asiende shle akiwa na njaa, ikibidi mzazi/mlezi amfungie mtoto chakula abebe.

Chakula cha mchana

Muda wa kati ya saa 5:30 mpaka saa 7:00 mchana.

Chakula cha jioni

Saa 10:00

Chakula cha usiku

Saa 1:00 usiku

Jinsi ya kuandaa chakula cha siku ya Jumatatu

Asubuhi

Kifungua kinywa (Breakfast)

Mlo 1: Chapati Maji Na Juisi Ya Chungwa

Mahitaji: 250 gram Unga wa ngano, 1 yai, 100 gram maziwa ya maji, 20 gram mafuta ya mahindi, 10 gram baking powder

Jinsi ya kuandaa chapati maji

Changanya vitu vyote katika bakuli kisha piga na mchapo mpaka upate mchanganyiko safi na laini kabisa. Iwapo mchanganyiko bado mzito ongeza maji kiasi.

Jinsi ya kuandaa juisi ya chungwa: Menya chungwa safi kabisa ili kuondoa uchungu wa gesi iliyopo katika maganda. Kisha tumia chombo maalumu cha kukamulia juice, kamua kisha hifadhi katika friji bila kuweka sukari ili ikae kwa muda bila kuharibika. Kumbuka pia kuweka sukari wakati wa kunywa.

Mlo 2: Uji wa Ulezi na Mtindi

Mahitaji: 200 gram unga wa ulezi, 100 gram maziwa ya maji, 350 gram maji, 100 gram mtindi usio na ladha ya matunda

Jinsi ya kuandaa uji wa ulzei na mtindi: Changanya unga wa ulezi na maziwa katika bakuli kisha chukua sufuria weka maji kiasi cha gram 350. Chemsha maji yakishachemka weka mchanganyiko wa maziwa na unga wa ulezi koroga mpaka uchemke na kuchanganyika safi kabisa ili uji wako usishike chini na kuungua. Acha uchemke vizuri kisha onja ukipata ladha ya kuiva kwa nafaka utakua tayari.

Toa jikoni weka katika bakuli litakalotumiwa na mtoto kisha changanya mtindi usio na ladha ya matunda pamoja na sukari tayari kwa mtoto kunywa.

Mchana

Chakula cha mchana

Mlo: Glass ya maziwa na mkate wa nyama za kusindika

Jinsi ya kuandaa: Mpatie mtoto 200 gram za maziwa sawa na glasi moja ya uvuguvugu au ya baridi lakini kumbuka yawe yamechemshwa vizuri na yakapoa kwa ajili ya usalama.

Kisha chukua vipande viwili vya mkate paka siagi au mayonaisi. Kisha chukua beef salami na beef backon weka kati kati pamoja na slice ya nyanya na tango mbichi mpatie mtoto ale.

Jioni

Chakula cha jioni

Mlo: Sahani ya mchanganyiko wa mboga mbichi

Jinsi ya kuandaa: Chukua caroti, tango, pilipili hoho nyekundu na ya kijani zote mbichi na zuchini ichemshe kidogo kisha weka mtindi wenye ladha ya matunda kwa ajili ya kulia hizo mboga.

Huu ndio muonekano wa sahani ya mchanganyiko wa mboga kama mtoto ni mdogo sana zisage kwenye mashine ya kusagia nyama kisha utapata mchanganyiko laini mpatie mtoto asiyeweza kutafuna hizo mboga mbichi.

Usiku

Chakula cha usiku

Mlo 1: Supu ya uyoga

Mahitaji: 300gram Uyoga fresh au wa kopo, 50 gram kitunguu maji, 10 gram kitunguu swaumu, 10 gram tangawizi, 50 gram leeks, 100 gram viazi mbatata, 100 gram maziwa fresh, 50 gram mafuta ya kupikia, 300 gram maji

Jinsi ya kuandaa supu ya uyoga: Kaanga katika mafuta ya kupikia vitunguu maji na vitunguu swaumu pamoja na tangawizi. Kisha weka viazi mbatata, leeks na uyoga kaanga tena kiasi kisha weka maziwa na maji acha ichemke mpaka viazi viive kisha toa na saga kwenye blenda. Rudisha jikoni kama itakuwa nzito sana ongeza maziwa au maji kiasi. Usisahau kuweka chumvi kulingana na ladha.

Mlo 2: Kuku maziwa, muhogo na njegere

Mahitaji: 200 gram nyama ya kuku isiyo na mifupa, 100 gram njegere, 200 gram maziwa, 150 mihogo iliyochemshwa kwanza, 300 gram maji

Kulia ni machine ya kusagia nyama utakayoitumia kwa ajili ya kusagia vyakula mbali mbali.

Jinsi ya kuandaa kuku maziwa, muhogo na njegere: Chemsha vyote kwa pamoja kuku na njegere mbichi pamoja na muhogo uliokwisha chemshwa kwanza mpaka ikaribie kukauka mchuzi  kisha toa jikoni. Chuja kisha weka mchuzi pembeni.

Chukua mchanganyiko wa njegere, kuku na muhogo. Tumia machine ya kusagia nyama weka huo mchanganyiko kisha saga upate rojo zito kisha rudisha katika sufuri, changanya na ule mchuzi uliochuja ongeza chumvi kulingana na ladha mpe mtoto ale chakula kikiwa cha moto.

Kama huna mashine ya kusagia nyama tumia mwiko kuponda itakua safi kabisa kisha unachanganya na ule mchuzi uliochuja.

Kwa mtoto mkubwa usisage. Baada ya kuchemsha ikaiva ongeza chumvi kisha mpakulie ale chakula cha moto atafurahia sana mchanganyiko wa ladha ya chakula hiki.

Orodha kwa ajili ya manunuzi siku ya Jumatatu

Uyoga wa kopo au fresh, mihogo mibichi, pili pili hoho, tangawizi, unga wa ngano, mayai, maziwa, sukari, chumvi, njegere, nyama ya kuku, tango, zucchini, mtindi usio na ladha ya matunda, mtindi wa ladha ya matunda, baking powder, viazi mbatata, mafuta ya mahindi na leeks.

Vitu hivi vyote sio vingi na unaweza kuvitumia siku inayofuata maana menu yetu ina uwiano safi kabisa. Vitu vingi vinatumika karibu kila siku na manunuzi yake sio ghali kabisa. Mpe mwanao raha kwa kula chakula safi na salama.

Kwa maelezo zaidi, tembelea blog ya www.activechef.blogspot.com ambapo Chef Issa anachambua na kuelezea namna ya kuandaa mapishi mbali mbali kwa ufundi na ubora wa hali ya juu. Kwa mawasiliano, unaweza kumuandikia kupitia email yake ya issakesu@gmail.com

Tafsiri za maneno “rampant caries” ni nyingi katika fani ya meno lakini la msingi ni kuoza kwa meno kunako enea kwa kasi na kuharibu vichwa (crowns) vya meno mengi au yote yaliyoota. Hii ni hali mbaya ya kuoza kwa meno ambayo hushambulia zaidi meno ya utotoni (milk teeth or primary dentition), japo wakati mwingine hata ukubwani.

Ugonjwa huu unajidhihirisha kwa kuanza na kuongezeka kwa kasi na kwa namna unavyo yashambulia meno na vyanzo vyake. Meno hushambuliwa kwa mpigo hasa kuanzia meno ya juu mbele, ingawa meno ya chini mbele ni mara chache kushambuliwa kwa vile yanakingwa na visababisha vya kuoza na ulimi.

Ugonjwa huu hushambulia hata maeneo ya meno ambayo kwa hali ya kawaida si rahisi kuoza, kama sehemu ya kukatia kwa meno ya mbele (incisal edges) na sehemu ya mbele kati na nyuma kati (facial and lingual surfaces).

Nini husababisha meno kuoza kwa kasi utotoni?

Kwa nini watoto wachanga wanalia? 

Ni kawaida kwa watoto kulia. Hata watoto wanaozaliwa na afya njema kabisa wanaweza kulia kwa jumla ya wastani wa kati ya saa moja mpaka matatu kwa siku. Kwa vile watoto hawawezi kujifanyia chochote wao wenyewe zaidi ya kutegemea wazazi, walezi ama watu wengine wanaowazunguka katika kuwapatia chakula, joto, na faraja, kilio ni njia ya mtoto ya kuwasilisha moja ya mahitaji hayo. 

Kama mzazi mpya, wakati mwingine inakuwa vigumu kutambua mtoto wako anahitaji nini anapolia. Mzazi anaweza kuwa na maswali kadhaa kichwani mwake, je, mtoto ana njaa, anasikia baridi, ana kiu, anaumwa ama amechoka? Katika siku za mwanzo, hali ya namna hii inawawia vigumu wazazi wengi, wasijue nini la kufanya. Hata hivyo, kwa kadiri siku zinavyopita mzazi mpya ataweza kutambua kuwa kilio cha mtoto wake kinamaanisha anahitaji nini kutokana na mfumo wake wa kulia. 

Kadiri watoto wanavyokua npyo ambavyo hujifunza hatua mbalimbali za kuwasiliana na wazazi ama walezi wao. Wanakuwa na namna nzuri ya kuwasiliana kwa mfano kwa macho, na kutoa sauti, na hata kutabasamu ambavyo vyote kwa pamoja hupunguza haja ya kulia.

 

Sababu zinazofanya watoto kulia 

Tuangalie sababu kadhaa zinazosababisha mtoto kulia na nini anachotakiwa mzazi ama mlezi kufanya pindi mtoto anapolia. 

1. Hitaji la chakula 

Njaa ni mmoja ya sababu kubwa inayowafanya watoto wengi kulia. Uwezekano wa mtoto kulia unaendana sana na umri wa mtoto. Kadiri jinsi mtoto alivyo mdogo zaidi npyo uwezekano wa kulia sana pindi anapohisi njaa unavyokuwa mkubwa, isipokuwa katika siku mbili za mwanzo baada ya kuzaliwa ambapo watoto hula kwa kiasi kidogo sana. Kwa kawaida katika siku mbili za mwanzo tangu mtoto kuzaliwa, maziwa ya kujilimbikizia mapema sana yaani ‘colostrum’ huwa ni kidogo sana kwa mama walio wengi na huanza kuongezeka kuanzia siku ya tatu baada ya kujifungua.

Pia tumbo la mtoto katika kipindi hiki huwa bado dogo sana na hivyo uwezo wake wa kuhifadhi maziwa anayonyonya huwa bado mdogo hali ambayo humfanya mtoto kujisikia njaa. Hivyo kama mtoto wako analia, uwezekano mkubwa ni kuwa ana njaa na hivyo mzazi unashauriwa kumnyonyesha. Inawezekana mtoto asiache kulia mara moja, lakini mama unashauriwa kuendelea kumnyonyesha taratibu na mtoto anaweza kuacha kulia kwa kadiri anavyoburudika na chakula na kuanza kushiba. Iwapo mama unadhani mtoto wako ameshiba lakini bado anaendelea kulia, inawezekana kuna sababu nyingine zaidi. 

Utangulizi

Miongoni mwa dharura zinazoweza kuwatokea baadhi ya wajawazito, ambayo husababisha mama kupoteza damu nyingi, kufa kwa mtoto na hata mama mwenyewe ni Placenta abruptio. Neno Placenta abruptio humaanisha hali ya kujitenga kwa kondo la nyuma (placenta) kutoka sehemu ilipojishikilia kwenye ukuta wa tumbo la uzazi (uterus) kabla hata ya mtoto kuzaliwa. Kondo la nyuma au placenta ni kiungo kinachofanya kazi ya kumlisha mtoto akiwa tumboni kwa mama yake. Katika hali ya kawaida, kondo la nyuma hujitenga na ukuta wa mfuko wa uzazi mara baada ya mtoto kuzaliwa.

Hali hii husababishwa na nini?

Tatizo la kukosa hedhi ni jambo ambalo linawakumba wanawake wengi waliovunja ungo.Aidha suala hili limekuwa likiwaletea usumbufu mwingi wa kisaikolojia wanawake wengi waliowahi kukumbana nalo.
Tatizo la kukosa hedhi au amenorrhea linaweza kutokea awali kabisa (primary) au baadaye kabisa maishani (secondary).

Primary amenorrhea

Hiii hali ya kukosa hedhi inayoweza kumtokea msichana aliye katika umri wa kuvunja ungo na ambayo huweza kuendana na hali ya kukosa mabadiliko ya kubalehe kama vile kuota matiti au nywele za kinena, au msichana anaweza kuwa na mabadiliko ya kubalehe lakini asipate hedhi.

Secondary amenorrhea

Hii hali ya kukosa hedhi inayomtokea mwanamke ambaye si mjamzito, hanyonyeshi, na ambaye hajavuka umri wa kukosa hedhi (menopause) na wala hatumii njia za uzazi wa mpango kama vile sindano au vidonge, na ambaye hapo awali alikuwa akipata hedhi kama kawaida lakini akasimama kwa miezi mitatu au zaidi.

Mwanamke hupataje hedhi?

Ili mwanamke aweze kuwa na mzunguko ulio sahihi wa hedhi, ni lazima matezi yake ya hypothalamus na pituitary pamoja na kiwanda cha kutengeneza mayai ya kike (ovaries) na mji wa mimba (uterus) vifanye kazi zake sawasawa.

Hypothalamus huchochea tezi la pituitary kuzalisha hormone chochezi ya follicle au follicle-stimulating hormone (FSH) pamoja na homoni ya luteinizing (LH). Hizi FSH na LH kwa pamoja huchochea ovaries kuzalisha homoni za estrogen pamoja na progesterone. Kazi za estrogen na progesterone ni kusababisha mabadiliko katika ukuta wa uterus yaani endometrium ikiwepo kupata hedhi. Ili damu ya hedhi iweze kutoka nje, njia ya uzazi ya mwanamke haina budi kuwa huru yaani isiyo na matatizo yeyote yale.

Homa ya mapafu ni aina ya maambukizi yanayoathiri mapafu. Ni ugonjwa ambao unaua watoto wengi hasa katika nchi zinazoendelea duniani. Inakadiriwa kwamba watoto karibu milioni 1.6 walio chini ya miaka 5 wanakufa kila mwaka kutokana na ugonjwa huu. Kutokana na vifo vingi vinavyotokana na homa ya mapafu tarehe 12 ya mwezi wa Novemba kila mwaka imefanywa kuwa siku rasmi ya homa ya mapafu duniani, ambapo nembo ya siku hiyo ni nguo za rangi ya bluu.

Muundo wa Mapafu

Mapafu yanajumuisha mirija mikubwa ya hewa (bronchi) ambayo hugawanyika kufanya mirija midogo zaidi ya hewa (bronchioles), ambayo nayo hutengeneza vifuko vidogo vidogo ya hewa (alveoli). Vifuko hivi vidogo vya hewa (alveoli) vina mishipa ya kupitisha damu (capillaries) ambayo husaidia kuchuja na kusafirisha hewa safi ya oksijeni tunayovuta kuingia kwenye damu na hewa chafu ya ukaa (kaboni dioksidi) kuondolewa kwenye damu na kuingizwa kwenye mapafu tayari kwa kutolewa nje ya mwili.

Kwa kawaida vifuko hivi vidogo hujaa hewa muda wote tayari kwa kusafirishwa. Inapotokea mtu akapata homa ya mapafu, vifuko hivi hujaa maji au usaha hivyo kuathiri upitishaji wa hewa safi kwenye damu na kusababisha tatizo la kupumua.

Homa ya mapafu husababishwa na nini?

Kuna aina kadhaa ya vimelea ambao vinaweza kusababisha maambukizi ya mapafu. Vimelea hivi hujumuisha bakteria, virusi, parasite na fangasi.

Vimelea hawa hushambulia mwili wa binadamu kulingana na umri na kinga ya mwili. Kwa mfano, bakteria wanaosababisha homa ya mapafu kwa watoto wachanga ni tofauti na wale wanaosababisha ugonjwa huo kwa watoto wakubwa.

Makala hii ni muendelezo wa makala ya kwanza kuhusu Sababu na Dalili za Kuharibika kwa Mimba, katika sehemu ya kwanza ya Sababu na dalili za Kuharibika kwa Mimba - Sehemu ya Kwanza tuliangalia maana ya kuharibika kwa mimba na baadhi ya visababishi vyake sehemu ya kwanza. Katika makala hii tutaangalia kuharibika kwa mimba miezi mitatu ya mwisho ya kipindi cha ujauzito (Third trimester miscarriage).

Kuharibika kwa mimba kwa kipindi hiki sio sana kama kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo.

Visababishi vya kuharibika kwa mimba ni;

  • Kukaa vibaya kwa kitovu cha mtoto au hata kuwepo kwa fundo (knot) kwenye kitovu cha mtoto
  • Kulegea na kulainika kwa shingo ya kizazi (Cervical Incompetence)
  • Matatizo ya viashiria vya asili ambavyo havikugundulika hapo awali (Chromosomal defects)
  • Bawasiri (Hemorrhages)
  • Kukosekana kwa uwiano wa vichocheo mwilini (hormonal imbalance)
  • Utapia mlo
  • Vipimo vya vina saba kama Amniocentesis or Chorionic Villus Sampling (CVS) ambavyo hufanyika wiki ya 16 ya ujauzito
  • Maambukizi kama ugonjwa wa mafua, surua na ugonjwa wa mishipa ya fahamu au neva
  • Uvimbe katika mfuko wa uzazi (fibroids)
  • Mimba kupitiliza umri wake zaidi ya wiki 41 za ujauzito (post maturity )
  • Matatizo ya maumbile ya mfuko wa uzazi (Uterine structural abnormalities/defects)
  • Matumizi ya madawa ya kulevya kama cocaine
  • Uvutaji sigara na unywaji pombe
  • Matatizo ya kondo la nyuma la uzazi -Abruptio placenta au Placenta Previa

Abruptio Placenta ni kuachia kwa kondo hili kutoka kwenye ukuta wa mfuko wa uzazi. Ikumbukwe ya kwamba kondo hili ndilo linalohusika kumpa mtoto chakula pamoja na hewa ya oksijeni wakati wa ujauzito.

Chanzo cha tatizo hili hakijulikani isipokuwa kinahusishwa na ugonjwa wa kisukari, presha (140/90mmHg au zaidi), uvutaji sigara, matumizi ya madawa ya kulevya kama cocaine, kuwepo kwa historia ya kupata tatizo hili hapo awali,maumivu kwa mama mjamzito kutokana na kupigwa, kuzaa watoto wengi haya yote huchangia uwezekano wa kupata tatizo hili.

Viashiria vyake ni pamoja na kutokwa damu kwenye tupu ya mwanamke na maumivu makali sana ya tumbo.

Baadhi ya vichagizi (risk factors) vya kuharibika kwa mimba kipindi hiki ni;

  • Kubeba mimba yenye watoto wengi (Multiple pregnancy)
  • Kushika mimba tena ndani ya muda mfupi baada ya kujifungua hapo awali
  • Hypothyroidism-Ugonjwa wa tezi koo
  • Kutopata choo (Constipation)
  • Kuharisha
  • Polycystic ovary syndrome 

Viashiria vya kuharibika kwa mimba kipindi hiki ni kama ifuatavyo;

  • Kutokwa damu sana kupitia tupu ya mwanamke (Heavy vaginal bleeding)
  • Kuona matone ya damu kutokwa na matone ya rangi kutoka kwenye tupu ya mwanamke
  • Maumivu makali na kuhisi maumivu yanavuta sehemu za tumbo (cramps)
  • Maumivu ya kiunoni
  • Kichefuchefu, kutapika na kuharisha
  • Maumivu kwenye bega
  • Kubana na kuvimbiwa tumbo

Sio siri duniani kuna baadhi ya nchi ambazo zimeruhusu mama mjamzito kufanya uamuzi wa kutoa mimba (abortion) bila kuwepo kwa sababu zozote za msingi za kitabibu. Baadhi ya nchi hizo ni Marekani, Canada, Visiwa vya Guyana, Bahrain (isizidi umri wa mimba wa wiki 12),Uturuki, China, Singapore, Ubelgiji, Uswisi, Uholanzi nk. Kwa bara la Afrika ni nchi mbili tu ambazo zimeruhusu mama mjamzito kufanya uamuzi huu ambazo ni Afrika Kusini na Tunisia. Katika nchi hizi mbili za kiafrika, mama mjamzito ataruhusiwa kutoa mimba (abortion) iwapo mimba itakuwa na umri wa chini ya wiki 12 za umri wa mimba.

Suala la utoaji mimba bado haliruhusiwi katika mataifa mengi duniani isipokuwa tu pale panapokuwa na sababu za msingi za kitabibu ambazo zinaruhusu mimba hiyo iharibiwe/itolewe (abortion) pasipo mhusika/mama mjamzito kukumbana na mkono mkali wa sheria. Jamhuri ya muungano wa Tanzania ikiwa ni moja za nchi hizo ambazo haziruhusu mama mjamzito kutoa mimba ila pale tu kuna  sababu za msingi za kitabibu zinazoruhusu mama mjamzito kufanya hivyo.

Kuharibu/kutoa mimba kutokana na sababu za kitabibu ambazo kama mama ataendelea kubeba  ujauzito huo  hadi kipindi cha kujifungua  basi atahatarisha maisha yake mwenyewe au maisha ya kiumbe alichobeba ndio hujulikana kitaalamu kama induced abortion.

Leo tutaangalia sababu zinazompa mama haki ya kutoa mimba bila kukumbana na mkono wa sheria.Sababu hizi zimegawanyika katika makundi mawili

  • Sababu kwa upande wa mama
  • Sababu kwa upande wa mtoto

Kwa upande wa mama sababu  hizi  ni kama zifuatazo

  • Magonjwa ya moyo kama ugonjwa wa presha, ugonjwa wa presha wa mishipa ya palmonari (Pulmonary hypertension), kuwepo kwa historia ya mama kupata ugonjwa wa moyo unaosababishwa na ujauzito (Pregancy induced cardiomyopathy) na Eisenmenger's syndrome.
  • Magonjwa ya jenetikali/asili kama marfan syndrome
  • Ugonjwa wa mfumo wa damu kama Thrombotic thrombocytopenic purpura
  • Magonjwa ya mfumo wa fahamu (Neurological disease)-Kutotibiwa kwa ugonjwa wa mfumo wa damu wa ubongo (Untreated cerebrovascular malformations) kama aneurysm au arteriovenous malformation
  • Ugonjwa wa figo-Kupungua kwa uwezo wa figo kufanya kazi mwanzoni kabisa mwa kipindi cha ujauzito
  • Saratani-Saratani ya shingo ya kizazi (Cervical cancer) au saratani yoyote ile ambapo tiba ya mama inahusu kutumia dawa za saratani (chemotherapy) au kupewa tiba ya mionzi ya saratani (radiotherapy)
  • Magonjwa ya mfumo wa umengenyaji chakula (Metabolic disease)-Proliferative diabetic retinopathy

Kichwa maji au hydrocephalus (kwa lugha ya  kitaalamu) ni mkusanyiko usio wa kawaida wa maji yanayojulikana kitaalamu kama (cerebral spinal fluid) kwenye ventrikali (ventricles) au nafasi zilizo wazi (cavities) kwenye ubongo. Tafiti zinaonyesha kuenea (prevalence) kwa kichwa maji  duniani ni; kwa kila watu 100,000 basi watu 85 wana tatizo la kichwa maji na hii inatofautiana kulingana na umri.

 kwa watoto;kati ya watoto 100,000 watoto 88 wana tatizo kichwa maji.

Hali hii huweza kusababisha kuongezeka kwa shinikizo katika fuvu (increased intracranial pressure).  Hydrocephalus limetokana na lugha ya kigiriki ambalo humaanisha: Hudro - Maji , na Kephalos - Kichwa

Kwa kawaida kwa kila mtu huwa na maji yanayoitwa kitaalamu cerebral spinal fluid kifupi CSF ambayo huzunguka ndani ya ventrikali za ubongo, nje na ndani ya ubongo na kuelekea kwenye uti wa mgongo (spinal cord) ambapo hufyonzwa na kurudi kwenye damu. Kichwa maji husababishwa na uzuiwaji wa mzunguko wa CSF, au kufyonzwa kwake au uzalishwaji wa CSF kwa wingi kupita kiasi kama kwenye papilloma of choroid plexus. Ikumbukwe ya kwamba kichwa maji huweza hata kusababisha kifo.

Kuna aina mbili za kichwa maji ambazo ni

Communicating hydrocephalus (Non obstructive hydrocephalus)

Aina hii husababishwa na kutokufyonzwa kwa maji ya CSF ingawa hakuna uzuiwaji wake wa mzunguko baina ya ventrikali na nafasi iliyopo kwenye ubongo inayojulikana kama Subarachnoid space. Hii inaweza kuleta madhara kama uvujaji wa damu baina ya ventrikali au kwenye Subarachnoid space, ugonjwa wa uti wa mgongo (meningitis) nk. Aina hii ya kichwa maji nayo imegawanyika katika sehemu mbili, ambazo ni

  • Normal Pressure Hydrocephalus (NPH) – Katika aina hii ventrikali za kwenye ubongo zimeongezeka ukubwa na kuongeza pressure ya CSF.
  • Hydrocephalus ex vacuo – Katika aina hii, pia kuna kuongezeka ukubwa kwa vetrikali za ubongo na subarachnoid space kutokana na kusinyaa kwa ubongo ambapo kunaweza kusababishwa na ugonjwa wa dementia, baada ya kupata ajali ya kichwa au matatizo ya akili kama Schizophrenia.

Non communicating hydrocephalus (Obstructive hydrocephalus)

Aina hii husababishwa na uzuiwaji wa mzunguko wa CSF kwenda kwenye Subarachnoid space kutokana na uvimbe wa kwenye ventrikali.
Kwa hiyo mtu anaweza kuwa na kichwa maji kutokana na kuzaliwa nacho (congenital) au akakipata baadae maishani (acquired) baada ya kupata maradhi kwenye mfumo wa neva mwilini (CNS infections), ugonjwa wa uti wa mgongo (meningitis), uvimbe kwenye ubongo, ajali ya kichwa, kuvuja damu kwenye ventrikali nk. Kichwa maji anachopata mtu baadae maishani huwa kinaambatana na maumivu makali sana.

Kipindi cha kunyonyesha ni kipindi kigumu sana kwa mama kwani huambatana na uchovu mwingi unaotokana na kuongezeka kwa majukumu ya kumhudumia mtoto mchanga ambayo huchangia kwa mama kutokuwa katika hali nzuri ya kufikiria kufanya tendo la ndoa

Baada ya kujifungua, wanawake wengi hawaoni tendo la ndoa kama ni muhimu sana kwao hata kufikia hatua ya  kutojali hisia za wenza wao. Mwanamke anapojifungua huwa na kidonda, mchubuko na hata kuchoka  kwenye sehemu za tupu  yake kama atakuwa amejifungua kwa njia ya kawaida.

Kwa aliyejufungua kwa njia ya upasuaji, mama huyu huwa na kidonda kinachotokana na upasuaji kwenye tumbo lake na kwenye mfuko wa kizazi.

Je ni muda gani sahihi kwa mama aliyejifungua kuanza tena kujamiana?

Kitaalamu mama aliyejifungua hushauriwa  kusubiri mpaka wiki sita (baada ya kuanza kliniki- postnatal clinic) ndio aweze tena kufanya tendo la ndoa.

Kuzaa huathiri vipi tendo la ndoa?

Kipindi cha kupona baada ya kujifungua hutegemea na njia ya kujifungua aliyotumia mama.

Kwa wale ambao wakati wa kujifungua waliongezewa njia kwa ajili ya kurahisisha kupita kwa mtoto (Episiotomy) au walichanika (Tear) na kushonwa, nyuzi hupotea baada ya siku 10 mwilini na wiki mbili za ziada mpaka michibuko na kidonda/vidonda kupona kabisa. Mama huyu anashauriwa  kufanya staili (wakati wa kujamiana) ambazo zitapunguza kuegemewa kwa sehemu ya mshono. Staili ambazo mama hulazimika kunyanyua miguu au kukunja miguu mpaka kwenye kitovu chake ni bora akaziepuka. Anatakiwa kuwa muangalifu sana wakati wa kujamiana pamoja na kufanya tendo la ndoa kwa taratibu (slow and gentle).

Kwa mama aliyejifungua kwa njia ya kawaida (Spontaneous Vaginal Delivery, SVD) pasipo kuongezewa njia au kuchanika, kupona kwake ni haraka na anaweza kuanza tena kufanya tendo la ndoa mara tu damu inayotoka (Lochia) kuacha, mara nyingi  damu hii kutoka huacha kabisa ndani ya wiki nne hadi wiki sita.

Mama aliyejifungua kwa njia ya upasuaji (Caesarean section) huwa na wasiwasi , hofu kutokana na kidonda cha upasuaji, hivyo ni vyema kwa mama huyu kusubiri mpaka nyuzi kutoka  kabla ya kufanya tendo la ndoa na pia azingatie kufanya kwa utaratibu (gentle).Staili zitakazoongeza kugandamizwa kwa eneo la mshono ni bora akaziepuka.

Je, kunyonyesha huathiri tendo la ndoa?

Baada ya mama kujifungua, kunakuwepo na mabadiliko ya viwango vya vichocheo  mwilini mwake ambavyo ni;

  • Kupungua kwa kiwango cha Oestrogen-Kupungua kwa homoni hii husababisha;
  1. Mama kupata kinga dhidi ya kushika tena ujauzito ndani ya muda mfupi kwa kumzuia kuingia katika hatua ya ovulation.
  2. Ukavu kwenye tupu ya mwanamke (Dryness of vagina) kwa baadhi ya wanawake
  • Kupungua kwa hamu ya tendo la ndoa na hata kukosa msisimko kwenye kisime (Low clitoris sensation).
  • Kupungua kwa kiwango cha kichocheo aina ya testerone pia husababisha kupungua kwa hamu ya tendo la ndoa.
  • Kuongezeka kwa kiwango cha homoni aina ya Prolactin (ambacho pia hupatikana kwenye maziwa ya mama) husababisha mama kujihisi hali ya kuridhika kimapenzi.

Zifuatazo ni sababu za mama kupoteza hamu ya tendo la ndoa baada ya kujifungua:

  • Uchovu—Kutokana na kuongezea kwa majukumu ya kumlea na kumhudumia mtoto
  • Mabadiliko ya muonekano wa mwili-Kina mama wengi baada ya kujifungua hupoteza hali ya kujiamini kutokana na mabadiliko ya mwili kama kuongezeka uzito, matiti kuwa makubwa na hata kubadilika muonekano wa matiti yao, kubadilika shepu nk. Na hivyo kuchangia kupoteza hamu ya tendo la ndoa
  • Wasiwasi au hofu kuwa tendo la ndoa linaweza kuleta maumivu baada ya kujifungua
  • Kuogopa kushika ujauzito tena mara tu baada ya kujifungua
  • Ukavu kwenye tupu ya mwanamke kutokana na kupungua kwa homoni aina ya oestrogen (hutokea kwa baadhi ya wanawake)
  • Hali ya kuridhika kimapenzi kutokana na homoni ya Prolactin
  • Kupungua kwa kichocheoa aina ya Testerone

Mambo ya kuzingatia  Kwa mama aliyejifungua kabla ya kufanya tendo la ndoa tena

  • Mama anahitaji kuzungumza na baba mtoto na kumueleza ukweli kuhusu hisia zake juu ya tendo la ndoa
  • Baba anashauriwa kuwa mvumilivu kama mama bado anapata maumivu wakati wa kufanya tendo la ndoa kwani hali hii ni ya muda tu
  • Kumsaidia na kumpa ushirikiano mama katika kulea na kumtunza mtoto ili apate muda wa kupumzika na hivyo kuongeza utayari wa mama katika kufanya tendo la ndoa
  • Kumpenda, kumjali na kumjengea mama uwezo wa kujiamini kutokana na mabadiliko ya mwili wake yaliyotokana na ujauzito (kuongezeka uzito, kubadilika muonekano  wa matiti, shepu nk)
  • Mama anashauriwa  kuweka mazingira mazuri ya kukutana  kimwili na baba mtoto kwani hata yeye bado anamuhitaji katika kipindi hiki.
  • Kuchagua muda mzuri usiokuwa na usumbufu wowote ule kutoka kwa mtoto (muda mzuri ni baada ya kumnyonyesha mtoto)
  • Mama anatakiwa kujikagua na kujichunguza kwenye tupu yake taratibu kwa kutumia vidole vyake ili aweze kufahamu kama anaweza kupata maumivu wakati wa kujamiana

Kama unaendelea kupata maumivu, au uke kuwa mkavu sana ni vyema kumuona daktari kwa ajili ya ushauri na matibabu.

Kipindi hiki cha wiki sita ni muhimu sana kwa mama kuwa karibu sana mwenza wake na kumpa ushirikiano mpaka wote watakapo kuwa tayari kwa tendo la ndoa.

Ni vyema kutumia njia za uzazi wa mpango hata kama unanyonyesha  kwani unaweza kushika mimba usiyoitarajia, mimba hizi nyingi  zimepatikana katika kipindi hiki.

Kama bado mnaona hampo tayari kwa tendo la ndoa, ni vyema kuendeleza mapenzi mubashara  kama kupigana busu, kutomasana, kukumbatiana,  kupapasana sehemu tofauti za mwili ili hisia za tendo la ndoa zirudi kama hapo awali.

Usikose makala ijayo ya faida za kunyonyesha mtoto katika tovuti yako unayoipenda ya afya ya TanzMED.

Endapo una swali linalohusiana na makala hii, usisite kuuliza kwenye jukwaa la maswali hapa

Ukurasa 4 ya 5