Image
×

Onyo

JUser: :_load: Haiwezi kupakia mtumiaji aliye na kitambulisho: 797

Tafiti iliyofanywa na Chama cha Kisukari Tanzania mwaka 1999, ilionesha kuwa maradhi yasiyo ya kuambukiza (maradhi ya moyo,figo,saratani, kisukari na mengineyo yasiyo ya kuambukiza) huchangia karibu asilimia 60 ya vifo vyote duniani na asilimia 43 ya ukubwa wa tatizo la maradhi hayo kote duniani.Maradhi haya yasiyo ya kuambukiza yanaongezeka na kukua kwa kasi hasa katika nchi zinazoendelea ikiwepo Tanzania. Tanzania inakisiwa kuwa ifikapo mwaka 2020 maradhi haya yatasababisha asilimia 73 ya vifo vyote duniani na ukubwa wa tatizo litaongezeka mpaka asilimia 60. (Tanzania Diabetes Association. 2013)

Kwa aina ya kwanza ya kisukari,ambayo hii huwapata watoto kwenye umri wa mwaka 1-25 inazidi kuongezeka katika nchi nyingi duniani,baadhi ya tafiti zilizowahi kufanywa zinaonesha katika watoto 79,000 ambayo wapo chini ya umri wa miaka 15 wapo katika hatari ya kupata tatizo la aina ya kwanza ya kisukari duniani kote,aina hii ya kwanza sio kama aina ya pili,aina ya ya kwanza,hasababishwi na mfumo wa maisha, au uzito uliopitiliza, na pia aina ya kwanza haiwezi kuzuilika tofauti na aina ya pili ya kisukari.inakadiriwa kuwa takriban 497,000 ya watoto wanaishi na aina ya kwanza ya kisukari duniani kote na pia nusu ya idadi hiyo ya watoto wanaishi katika mazingira magumu hasa kimatibabu na dawa.(International Diabetes Federation, IDF Diabetes Atlas.2014)

Watu takriban milioni 371 wamepata  kisukari kote duniani,ikiwa asilimia 80 ya idadi hiyo wanaishi katika nchi zenye uchumu wa kati na nchi masikini.katika tanzania, inasemekana kuwa katika watu 9 kwa kila watu 100 ya watanzania wenye umri wa miaka 25 na kuendelea wana tatizo la kisukari na pia katika idadi hiyo ya watu 9 ni wawili tu wanajijua kuwa wana tatizo la kisukari.(Tanzania Diabetes Association. 2013)

Namba, idadi na takwimu zinaonesha dhahiri shahiri ni kiasi gani kisukari ni tatizo kubwa endapo tu kama jamii haitapewa elimu ya kutosha kuhusu tatizo hili, jamii pia ni lazima ijue kwa upana na undani zaidi kuhusu chanzo,dalili na jinsi ya kuepuka na kuishi na kisukari.tatizo hili la kisukari mara nyingi napenda kusema sio ugonjwa ila inakuwa ni ugonjwa endapo tu mtu hatakuwa makini katika kudhibiti kiwango cha sukari.

 

 Shinikizo la damu ni moja ya tatizo linaloathiri watu wengi duniani.

Nini maana ya shinikizo la damu?

Ni msukumo wa damu ulioko juu kuliko inavyotakiwa kwa muda mrefu. Msukumo wa damu huitajika mwilini ili kusambaza chakula,oksijeni na kutoa uchafu.

Uanishaji wa shinikizo la damu

Uanishaji

Systolic BP

Diastolic BP

Kawaida (normal)

<120

<80

Prehypertension

120-139

80-89

Kali (mild hypertension)

140-159

90-99

Kali kiasi (moderate hypertension)

160-179

100-109

Kali sana (severe Hypertension)

≥180

≥110

Shinikizo la damu hupimwa kutumia kifaa kinachoitwa Sphygmomanometer

Shinikizo la damu husababishwa na nini?

Aina ya kwanza

Asilimia 90-95 sababu huwa hazijulikani na kitaalamu huitwa primary or essential hypertension. Ingawa vitu vifuatavyo vimehusishwa kupelekea kupata aina hii ya shinikizo la damu. Navyo ni:

  • Uvutaji sigara
  • Unene (visceral obesity)
  • Unywaji wa pombe
  • Upungufu wa madini ya potassium
  • Upungufu wa vitamin D
  • Kurithi
  • Umri mkubwa
  • Chumvi na madini ya sodium kwa ujumla
  • Ongezeko la kemikali kwenye figo (renin)
  • Kushindwa kufanyakazi kwa kichocheo kiitwacho insulin

Aina ya Pili

Asilimia 5 huwa na sababu dhahiri zinazopelekea kupata aina hii ya shinikizo la damu na huitwa kitaalamu secondary hypertension. Na sababu hizi ni:

  • Hali ya kukosa hewa usingizini (sleep Apnea)
  • Kasoro ya kuzaliwa nayo katika mshipa mkubwa wa damu (Coarctation of Aorta)
  • Saratani za figo (wilm’s tumor, renal cell carcinoma)
  • Saratani ya tezi iliyo juu ya figo (pheochromocytoma)
  • Ujauzito – wapo wakina mama wajawazito ambao hupata shinikizo la damu na huwa hatarini kupata kifafa cha mimba (eclampsia)
  • Magonjwa ya figo (renal artery stenosis, glomerulonephritis)

Dalili

Mara nyingi huwa hamna dalili zozote, na kama zikiwepo mgonjwa huwa na dalili zifuatazo

  • Uchovu
  • Maumivu ya kichwa
  • Kuhisi mapigo ya moyo kwenda haraka
  • Kichefuchefu
  • Kutapika
  • Damu kutoka puani
  • Kutoweza kuona vizuri (blurred vision)
  • Kusikia kelele masikioni
  • Na mara chache kuchanganyikiwa

Vipimo na uchunguzi

Huitaji kupima angalau mara tatu angalu wiki moja tofauti ilikuweza kusema mgonjwa ana shinikizo la damu kwa kutumia kifaa kinachoitwa kitaalamu Sphygmomanometer. Vipimo vingine ni:

  • Damu kuchunguza wingi wa lijamu mwilini (cholesterol), na pia vitu kama (BUN, na electrolytes)
  • Kipimo cha mkojo (Urinalysis)
  • Electrocardiogram (ECG)
  • Echocardiography
  • Ultrasound ya mafigo

Matibabu

Lengo ni kuzuia madhara ambayo yanaweza kuletwa na shinikizo la damu. Dawa zifuatazo hutumika kutibu shinikizo la damu: dawa jamii ya Alpha blockers, dawa jamii ya Angiotensin converting enzyme inhibitor (ACEI), dawa jamii ya Angiotensin receptor blocker (ARB), dawa jamii ya Beta blocker, dawa jamii ya Calcium channel blocker, dawa jamii ya Diuretics, dawa jamii ya Renin inhibitors na dawa jamii ya Vasodilators.

Madhara yanayoweza kuletwa na shinikizo la damu

  • Kiharusi
  • Moyo kushindwa kufanya kazi ( congestive heart failure)
  • Madhara katika mshipa mkubwa wa damu ambapo ukuta wa ndani huchanika na damu hukusanyika katika ukuta wa mshipa huo(aortic dissection)
  • Magonjwa ya mishipa ya damu
  • Kushindwa kuona
  • Athari katika ubongo

Jinsi ya kuzuia shinikizo la damu

Chakula cha afya kisicho na mafuta mengi na chenye madini ya potassium kitaalamu kinaitwa DASH diet (dietary approaches to stop hypertension)

  • Mazoezi mara kwa mara- angalau nusu saa kwa siku
  • Kwa wavutaji sigara kuacha kuvuta sigara
  • Punguza au kama unaweza acha unywaji wa pombe ( kwa wanaume angalau bia 2 kwa siku na wanawake bia 1)
  • Punguza utumiaji wa chumvi hasa ya kuongeza mezani (usitumie zaidi ya gramu 1.5)
  • Punguza msongo mawazo
  • Hakikisha unakuwa kwenye uzito wa afya, kama uko kwenye uzito wa hatari fanya mpango wa kupunguza uzito.
  • Matumizi ya mafuta ya samaki husaidia kupunguza shinikizo la damu, kwa wenye shinikizo la damu.

Tatizo la kiakili la kujihisi mnene na kupoteza hamu ya kula au Anorexia nervosa ni tatizo linawaathiri watu wengi na kuwafanya kupoteza uzito zaidi ya ule unaokubalika kulingana na umri na urefu wa muhusika.

Watu wenye tatizo hili wana hali ya kuwa na hofu isiyo kifani ya kuongezeka uzito hata kama, kiukweli, wana uzito mdogo (wamekonda) kuliko kawaida. Wanaweza kujinyima au kupunguza kula makusudi (dieting), kufanya mazoezi ya kupunguza uzito kuliko kawaida au hata kufanya njia nyingine zozote ilimradi wapungue uzito.

Chanzo na vihatarishi vya tatizo hili

Chanzo halisi cha tatizo hili bado hakifahamiki rasmi. Hata hivyo, mambo kadhaa yanahusishwa na kutokea kwake. Mambo hayo yanajumuisha sababu za kinasaba (genetic factors) na vichocheo mwili (hormones). Aidha masuala ya kijamii yenye kuchochea wana jamii kama vile baadhi ya wasichana kupenda maumbo madogo (vimodo) nayo pia yanahusishwa.

Kipindi cha nyuma, masuala kama matatizo katika familia yalikuwa yakihusishwa na uwepo wa tatizo hili pamoja na matatizo mengine yanahusiana na ulaji wa muhusika ingawa kwa sasa uhusiano wake unaonekana kuwa si wa nguvu sana.

Vihatarishi vya anorexia nervosa vinajumuisha

Wiki iliyopita niliongelea kulika kwa meno kama hali inayotokea wakati sehemu ngumu ya nje ya meno huondoka na kusababisha sehemu ya ndani kuwa wazi.

Nilitaja kuwa ziko aina mbali mbali za kulika kwa meno kulingana na nini kinasababisha tatizo. Aidha kinga au tiba hutegemea nini kinasababisha tatizo hilo. Nikaongelea kwa undani kulika kwa meno kunakosababishwa na meno kusagana yaani attrition.

Leo nitaongelea aina nyingine ya kulika kwa meno

Kuyeyuka kwa meno (tooth erosion)

Huku ni kulika kwa meno kunakosababishwa na kemikali hasa tindikali. Tindikali inayoyeyusha meno haya yaweza kutoka nje au ndani ya mwili wenyewe.

Kuyeyuka kwa meno kunakosababishwa na tindikali toka nje ya mwili: Baadhi ya vyakula na vinywaji tunavyokula na kunywa vina kiwango kikubwa cha tindikali (acid), hivyo vyakula na vinywaji hivyo vikikaa kinywani kwa muda huweza kusababisha meno kuyeyuka.

Ugonjwa wa pumu ni ugonjwa ambao huathiri sehemu ya kupitisha hewa kwenda kwenye mapafu ya binadamu zinazojulikana kitaalamu kama bronchioles.

Mtu mwenye pumu huwa na mcharuko mwili sugu (chronic Inflammation) kwenye mirija yake ya kupitishia hewa (bronchioles tubes) hali ambayo husababisha kuvimba kwa kuta za mirija hii, kujaa kwa ute mzito (mucus) na kupungua kwa njia ya kupitishia hewa, hali ambayo humfanya muathirika kushindwa kuvuta na kutoa hewa nje na hivyo kupumua kwa shida sana. Hali hii inaweza kudumu kwa muda mfupi au mrefu kiasi cha kuhitaji tiba ili kumuwezesha mgonjwa kupata nafuu.

Kutokana na  kuwepo kwa msuguano na uzuiaji wa kupitisha hewa wakati wa kupumua  nje, pumu hujulikana pia kama obstructive lung disease . Mtu aliye na pumu, huwa nayo kipindi chote cha maisha yake.  

Makundi ya Pumu

Pumu inaweza kugawanywa katika makundi mawili;

  • Pumu ya ghafla (Acute asthma):  Wagonjwa wanaopatwa na kundi hili la pumu huwa na hali ya kawaida  katika njia zao za hewa isiyobadilika kati ya shambulizi moja na jingine.
  • Pumu sugu (Chronic Asthma): Kundi hili la pumu huwa na tabia ya kuwa na njia nyembamba za kupitisha hewa  na kadiri jinsi mgonjwa anavyoendelea kupata matukio zaidi ya pumu, njia za hewa huzidi kuwa nyembamba zaidi.

Aina za ugonjwa wa pumu

Bila kujalisha mgonjwa anaingia katika kundi gani, ugonjwa wa pumu unaweza kugawanywa katika aina kuu nne, ambazo ni

1.Pumu inayobadilika (brittle asthma): Kulingana na tabia ya kujirudia rudia kwa matukio ta ugonjwa huu na madhara yake kwa mgonjwa, aina hii ya pumu inaweza kugawanywa zaidi katika aina nyingine mbili, ambazo ni

  • Aina ya kwanza ya pumu inayobadilika (type 1 brittle asthma) ni pumu yenye tabia ya kuwa na matukio na mashambulizi ya kubadilika kila mara japokuwa mgonjwa anaweza kuwa anapata matibabu kadhaa.
  • Aina ya pili ya pumu inayobadilika (type 2 brittle asthma)  ni pumu ambayo mgonjwa anatokea kupata shambulizi la ghafla (asthmatic attack) wakati hapo awali ugonjwa wake uliweza kuthibitiwa kwa matibabu.

 

Maana ya Kiharusi

Kiharusi ni hali inayotokea pale mishipa inayosambaza damu kwenye ubongo inapopatwa na misukosuko kiasi cha kushindwa kupeleka damu kwenye ubongo na hivyo kuathiri ufanyaji kazi wa ubongo kwa zaidi ya masaa 24.

Kulingana na shirika la afya duniani kiharusi ni nakisi katika neva ambayo hutokana na tatizo katika mishipa ya damu ya ubongo na ambalo huendelea zaidi ya masaa 24 au kukoma ndani ya masaa 24. Muda wa masaa 24 umechukuliwa ili kutofautisha kiharusi na kiharusi cha kukosa oksijeni katika ubongo (ischemia) ambacho hutokea na kudumu kwa muda mfupi yaani (transient ischemic attack).

Kwa kawaida dalili za TIA hupotea na mtu kurudia hali yake ya kawaida ndani ya masaa 24.

Aina za kiharusi

Kiharusi kimegawanyika katika aina kuu mbili kulingana na jinsi kinavyotokea (visababishi vyake). Aina hizo ni

Kiharusi cha kukosa hewa kwenye Ubongo (Ischemic stroke)

Aina hii ya kiharusi hutokea iwapo usambazaji wa damu katika sehemu ya  ubongo hupungua na kupelekea tishu za ubongo za eneo liliathirika kushindwa kufanya kazi zake vizuri.

Aina hii ya kiharusi husababishwa na nini?

  • Damu iliyoganda kuziba mishipa midogo ndani ya ubongo (cerebral thrombosis) au
  • Kipande cha damu kumeguka na kwenda kuziba mshipa wa damu kwenye ubongo(cerebral embolism)
  • Kupungua kwa usambazaji wa damu kwa ujumla kwa mfano shock.
  • Vena thrombosis

Kiharusi cha kuvuja damu ndani ya Ubongo (Haemorrhagic Stroke)

Aina hii ya kiharusi hutokea pale ambapo mishipa midogo ya damu ndani ya ubongo hupasuka na kusababisha kusambaa kwa damu ubongoni (cerebral hemorrhage). Mara nyingi aina hii ya kiharusi hutanguliwa na dalili za kichwa kuuma, au kuwepo kwa historia ya ajali ya kichwa.

Visababishi vya Kiharusi (kwa ujumla)

  • Wakati fulani, mishipa ya damu huzungukwa na aina fulani za mafuta yasiyofaa mwili, hali inayoitwa kitaalamu kama atherosclerotic plaque. Hali hii husababisha kuganda kwa damu katika mishipa (thrombosis) hiyo. Kuganda huku kwa damu kunaweza kutokea kwenye mishipa mikubwa au midogo inayopeleka damu kwenye ubongo. Baadhi ya mishipa mikubwa ya damu inayoweza kuathirika na tatizo hili ni pamoja na arteri za common carotid na interior carotid arteries, na arteri za vertebral. Nyingine ni mishipa midogo inayounda eneo linaloitwa circle of willis lililo katika ubongo.
  • Kuganda kwa chembe nyekundu za damu za mgojwa wa sickle cell kunaweza pia kusababisha kuziba mishipa ya damu hivyo kusababisha Kiharusi.
  • Kuganda kwa damu (embolus) kwenye mishipa ya damu ya sehemu nyingine za mwili au (hewa, mafuta, kusanyiko la vijimelea kama bakteria waletao ugonjwa wa endocarditis) huweza kusababisha kuziba kwa mishipa inayosambaza damu kwenye ubongo na hivyo kusababisha kiharusi.
  • Upungufu wa usafirishaji damu mwilini (systemic hypoperfusion) - Wakati fulani moyo hushindwa kusukuma damu vizuri kwenda sehemu mbalimbali za mwili ikiwemo ubongo kutokana na kufa kwa sehemu za nyama ya moyo kwa kukosa damu ya kutosha (Ischaemic Heart Diseases) au kutokana na kujaa kwa maji kwenye gamba lake la nje (pericardial effusion) au kupungua kwa damu mwilini, kunakoweza kusababishwa na mambo kadhaa. Hali hii husababisha sehemu kubwa ya mwili ikiwemo ubongo kukosa oksijeni ya kutosha na kusababisha kuathiriwa kwa sehemu ya ubongo.
  • Shinikizo la damu la muda mrefu lisilothibitiwa linaweza kusababisha kupasuka kwa mishipa midogo inayosambaza damu kwenye ubongo na hivyo damu kujaa kwenye ubongo (Intracerebral hemorrhage).

Dalili za kiharusi

Dalili za kiharusi hutegemea na eneo la ubongo liliathiriwa.

  • Iwapo sehemu ya ubongo mkubwa ( Cerebellum) itaadhirika, mgonjwa atakuwa na dalili kama kushindwa kutembea vizuri, hivyo kuathiri mwendo wake, kujihisi kizunguzungu na pia kutapika.
  • Iwapo sehemu ya ubongo wa kati (cerebral cortex) itakuwa imeathirika, mgonjwa atakuwa na dalili za kushindwa kuongea,kushindwa kuelewa lugha inayozungumzwa, kushindwa kuona vizuri, kuwa na ukosefu wa kumbukumbu, kuwa na mvurugiko wa mpangilio wakw wa kufikiri, kuchanganyikiwa, na kubadilika kwa mwendo wa harakati za hiari.
  • Iwapo mgonjwa ataadhirika sehemu ya ubongo kwenye shingo kuelekea kwenye uti wa mgongo (brain stem), mgonjwa anaweza kuwa na dalili za kuhisi mabadiliko ya harufu, ladha, kusikia na kuona; kulegea kwa misuli ya macho (ptosis); kupungua kwa ufahamu na kulegea kwa misuli ya uso; Ulegevu wa Ulimi (kushindwa kutoa nje au kusogeza upande upande); kupungua uwezo wa kumeza; ulegevu wa misuli ya shingo na kushindwa kugeuza shingo upande mmoja; kushindwa kusimama sawasawa na kuona vitu kwa hali ya utofauti; mabadiliko ya upumuaji na kiwango cha moyo kudunda.
  • Iwapo sehemu mojawapo ya mfumo mkuu wa neva (central nervous system) imeathirika, mgonjwa atakuwa na dalili za kupoteza ufahamu kwa upande mmoja wa mwili na kulegea kwa misuli ya uso, kuhisi ganzi mwilini, na kupungua kwa ufahamu wa hisia na hisia mtetemo.

Aidha bila kujalisha eneo lililoathiriwa, mgonjwa pia anaweza kuwa na dalili za kupoteza fahamu, maumivu makali ya kichwa na kutapika. Dalili hizi za kuumwa kichwa na kutapika kwa kawaida hutokea kwa mgonjwa mwenye kiharusi cha kuvuja damu (hemorrhagic stroke) ambacho husababisha ongezeko la shinikizo na mgandamizo wa ubongo ndani ya fuvu kutokana na kuvuja kwa damu.

Vipimo

  • Mionzi                                                           
  • CT-scan
  • MRI
  • PET
  • SPECT

Vipimo vingine ni

  • ECG, ECHOCARDIOGRAM huwezesha kutambua hitilafu katika mapigo ya moyo (arrhythmia) na kama kuna damu iliyoganda kwenye moyo ambayo inaweza kufika kwenye ubongo
  • Holter monitor husaidia kutambua hitilafu katika mapigo ya moyo (arrhythmia) zinazotokea kwa vipindi
  • Angiogram huwezesha kugundua matatizo kwenye mishipa ya damu, na ni mishipa ipi ya damu iliyoziba.
  • Vipimo vya damu huwezesha kutambua uwepo wa lijamu mwilini (hypercholesterolemia) na mabadiliko mengine katika damu

Vihatarishi vya kiharusi

Vitu vinavyoweza kumuweka mtu katika hatari ya kupata kiharusi ni pamoja na

  • Shinikizo la damu lisilothibitiwa
  • Kisukari
  • Uvutaji sigara
  • Unywaji pombe kupita kiasi
  • Kutofanya mazoezi kabisa
  • Fetma (obesity)
  • Kuwa na cholesterol nyingi kwenye damu
  • Atrial fibrillation

Matibabu

Matibabu ya kiharusi hutegemea pia aina na visababishi vyake .

Matibabu ya kiharusi kinachotokana na ubongo kukosa hewa (Ischemic stroke)

Mgonjwa hutibiwa kwa kutumia dawa za kuyeyusha damu iliyoganda (thrombolytics) au kwa kuondoa damu iliyoganda kwa njia mbalimbali (thrombectomy). Dawa nyingine kama vile junior Aspirin na Clopidogrel hutolewa kwa ajili ya kuzuia chembe sahani kukusanyika na kuganda.

Matibabu ya kiharusi kinachotokana na damu kuvujia kwenye ubongo (Hemorrhagic stroke)

Aina hii ya kiharusi huitaji tathmini ya upasuaji wa neva ili kuchunguza na kutibu sababu ya damu kuvuja. Angalizo: ni hatari kumpa mgonjwa wa aina hii ya kiharusi dawa za kuyeyusha damu iliyoganda au za kuzuia kuganda maana uhatarisha maisha ya mgonjwa badal ya kumsaidia. Kwahiyo ni vizuri kwa wataalamu kufanya ufanya uchunguzi wa kutosha ili kuwa na uhakika na tatizo.

Huduma na Matunzo kwa mgonjwa wa Kiharusi

Mojawapo ya mambo muhimu ya kufanya kwa mgonjwa aliyepata kiharusi ni kumuongoza na kumuelimisha ili arudishe ujuzi wake wa maisha ya kila siku. Hapa uhitaji ushirikiano wa wauguzi, wataalamu wa viungo, wataalamu wa ushauri wa kazi na daktari. Kuna umuhimu pia wa kuwaelimisha ndugu kuhusu hali ya mgonjwa ili waweze kumsaidia katika matunzo yake nyumbani na kwenye jamii inayomzunguka.

Matarajio (prognosis)

Asilimia 75 ya wagonjwa wa kiharusi wanaonusurika kifo huwa walemavu na kusababisha kuathirika kwa ufanyaji kazi wao na kuajiriwa. Ulemavu unaweza kuwa wa kimwili au kiakili au vyote kwa pamoja.

Ulemavu wa kimwili ni pamoja na

  • Ulegevu wa misuli
  • Kujihisi ganzi sehemu mbalimbali za mwili hususani zilizoathirika
  • Kujikojolea
  • Kutoona vizuri
  • Kushindwa kuendelea na shughuli za kila siku
  • Vichomi
  • Vidonda shinikizo
  • Kukosa hamu ya chakula.

Ulemavu wa akili hujumuisha vitu kama

  • Mgonjwa kuwa na wasiwasi
  • Hofu ya mashambulizi, na
  • Unyongovu.

Jinsi ya kuzuia kiharusi

  • Zuia au tibu shinikizo la damu
  • Dhibiti kisukari
  • Fanya mazoezi
  • Acha kuvuta sigara
  • Punguza uzito
  • Acha kunywa pombe kupita kiasi
  • Tumia Junior Aspirin
  • Kula chakula kisichokuwa na mafuta mengi na kisicho na chumvi nyingi.
  • Tumia dawa za kupunguza mafuta mwilini (statins)kwa mfano Simvastatin

Kulika kwa meno ni hali ambapo sehemu ngumu ya nje ya meno huondoka na kusababisha sehemu ya ndani kuwa wazi. Tatizo hili huanza kwa kuondoka sehemu ngumu ya nje (enamel) na kuiweka wazi sehemu ya kati ambayo ni ngumu pia (dentine). Tatizo likiendelea bila matibabu hufanya kiini cha jino, sehemu ambayo kuna mishipa ya damu, mishipa ya fahamu na chembe chembe mbali, kuwa wazi (dental pulp exposure).

Dalili hutegemea na kiwango cha ulikaji wa jino. Ikiwa ni sehemu ya nje kabisa imetoka, dalili huweza kuwa msisimko (sensitivity) wakati wa kunywa vinywaji vya baridi, vya sukari na hata meno yakipulizwa na upepo. Kama kiini cha jino kitakuwa wazi basi maumivu huanza na yanaweza kuwa makali kabisa.

Matibabu hutegemea kiwango cha uharibifu. Kama uharibifu ni kidogo, utumiaji wa dawa za meno zenye madini zaidi hasa ya fluoride unaweza kuondoa dalili. Wakati mwingine kutumia dawa za kupaka kitaalam, kuziba na kuvalisha kofia ngumu (crown) meno husika na mwisho ni kufanya matibabu ya mzizi wa jino (root canal treatment) au kung’oa jino kama kiini cha jino kimebaki wazi.

Ziko aina mbali mbali za kulika kwa meno kutokana na nini kinasababisha tatizo, na kinga au tiba hutegemea nini kisababishi.

Kusagika kwa meno (attrition)

Huku ni kulika kwa meno kwenye sehemu ambapo meno ya juu na chini hukutana (occlusal surfaces). Katika hali ya kawaida meno hulika sehemu hizi kutokana na kadri yanavyoendelea kutumika kusaga vyakula. Hali hii huendelea polepole kadri mtu anavyoendelea kuishi (umri), kitaalamu inajulikana kama physiological attrition.

Ni tatizo ambalo huathiri wote wanaume na wanawake, vilevile watu wa rika yote kwa ujumla. Tatizo hili husababishwa na mpasuko au mchaniko katika eneo la mwisho la mfereji wa haja kubwa.

Nini husababisha mwatuko wa mfereji wa haja kubwa?

Aina yoyote ya ajali katika mfereji wa haja kubwa husababisha mwatuko kama ifuatavyo:

  • Kupata choo kingi na kigumu kwa muda mrefu
  • Tatizo sugu la kuharisha
  • Kuvimba kwa eneo la mfereji wa haja kubwa (inflammation)

Sababu nyinginezo ni kama zifuatazo

  • Ngono ya njia ya haja kubwa
  • Kansa
  • Virusi vya ukimwi
  • Kaswende
  • Kifua kikuu

Watu gani wanaweza kupata tatizo hili?

  • Watoto chini ya mwaka mmoja (infants)
  • Umri mkubwa- kwasababu kuna upungufu wa ugavi wa damu katika mfereji wa njia ya haja kubwa
  • Kupata choo kigumu kwa muda
  • Wanawake wakati wa kujifungua
  • Crohn’s disease

Dalili

  • Maumivu mara baada ya haja kubwa
  • Damu kwenye kinyesi na huonekana kwenye karatasi ya chooni (toilet paper)
  • Maumivu huweza kuwa makali mpaka kumfanya mtu ajizuie kwenda msalani
  • Kuwashwa

Vipimo na uchunguzi

  • Sigmoidocopy
  • Colonoscopy

Matibabu

Huweza kutibiwa kwa dawa katika hatua za awali

  • Dawa za kulainisha choo
  • Sitz bath
  • Cream za kupaka (Anusol, zinc oxide)
  • Nitroglycerin
  • Botox
  • Calcium channel blockers (nifedipine and diltiazem)

Kama tatizo hili limekuwa sugu na halitibiki kwa tiba nyingine, basi Upasuaji ndio huwa tiba mwafaka

  • Partial lateral internal sphicterotomy
  • Anal dilation

Jinsi ya kuzuia mwatuko wa mfereji wa haja kubwa

  • Vyakula vya kulainisha choo - matunda na mbogamboga
  • Kunywa maji mara kwa mara
  • Na fanya mazoezi

Mzio au aleji (allergy) ni matokeo ya mpambano uliopitiliza kati ya kinga ya mwili na kitu chochote (ambacho kwa ujumla huwa hakina madhara kwa mwili) inapotokea kimeingia ndani ya mwili au kimegusa sehemu fulani ya mwili.

Aleji husababishwa na nini?

Kuwa na mzio ni jambo la kawaida. Haishangazi basi kuona kuna baadhi ya watu wanakuwa na mafua karibu kila siku au wengine wanashindwa kuvaa baadhi ya vitu kama saa au cheni za dhahabu kwa vile tu huvimba mwili au kuwashwa pindi wanapofanya hivyo.

Kwa kawaida kinga ya mwili huulinda mwili dhidi ya vitu mbalimbali hatari kwa afya kama vile vimelea vya bakteria na virusi, lakini wakati mwingine inaweza kupambana pia na vitu ambavyo havina madhara yeyote kwa mwili (ambavyo huitwa allergens). Watu wenye aleji/mzio huwa na hisia zisizo za kawaida za mwili dhidi ya baadhi ya vitu.

Mwili unapokumbana na vitu vinavyosababishia aleji (yaani allergens), mfumo wa kinga ya mwili huzalisha kemikali mbalimbali ikiwemo histamine ambayo hupambana na allergens hizo. Mpambano huu ndo husababisha mtu kuwa na dalili za aleji/mzio.

Matatizo ya kinasaba pamoja na hali tofauti tofauti za kimazingira zote zinahusika sana katika kusababisha mtu kuwa na mzio. Baadhi ya vitu vinavyosababisha mzio (allergens) ni pamoja na vumbi vumbi, baadhi ya dawa, baadhi ya vyakula, kung'atwa na wadudu kama vile nyuki, aina fulani ya uyoga, vumbi vumbi la maua (pollens) n.k.Wapo baadhi ya watu ambao hukumbana na mzio pindi wanapokuwa katika mazingira ya joto au baridi wakati wengine hupatwa na mzio pindi wanapopigwa na jua kali. Wakati mwingine, hata msuguano kidogo tu wa ngozi unaweza kuwasababishia baadhi ya watu dalili fulani fulani za mzio.

Kama nina aleji mtoto wangu pia anaweza kupata aleji hiyo hiyo?

Kwa kawaida, mzio wa aina fulani huwa haurithishwi miongoni mwa wanafamilia. Kwa mfano kama mzazi ana aleji na baridi si lazima watoto wake pia wawe na aleji hiyo hiyo ya baridi ingawa wanaweza kuwa na aina nyingine ya aleji. Uwezekano wa mtoto kupata aleji huongezeka zaidi iwapo wazazi wote wawili wana aleji na vitu fulani fulani na huwa mkubwa zaidi iwapo mama ndiye mwenye aleji.

Bado tupo katika mwendelezo wa Makala yetu kuhusu kisukari na jinsi ya kuishi na kisukari. Katika makala ya kwanza katika mfululizo huu wa makala za kisukari, Ishi kwa kujiamini, kisukari sio mwisho wa Maishatulianza kwa kuangazia jinsi ya kuishi na kisukari, pia mambo makuu manne ya kuzingatia kwa wagonjwa wenye kisukari.

Baada ya kupata ufahamu juu ya umuhimu wa kujiamini kwa mtu anayeishi na kisukari,katika makala ya Jinsi ya kula kwa watu wenye Kisukari, tuliangazia  suala la jinsi ya kula, maana hapo ndipo tatizo lilipo, watu wengi wenye tatizo la kisukari hawafahamu ni aina gani ya vyakula wanapaswa kula na wengine wanaingia kwenye gharama kubwa kununua vyakula tofauti wakiamini kuwa ni maalum kwa wenye kisukari.

Leo tunaangalia suala zima la udhibiti wa kisukari kwa mtu mwenye kisukari. Lazima ufahamu kuwa wewe mwenye kisukari ni Tabibu wa kwanza wa tatizo lako. Kuna matatibu wengi sana mitaani na wote wana utaalamu tofauti,pia kuna taarifa nyingi mitaani na  kwenye mtandao ila ni jukumu lako wewe kujua ni taarifa gani sahihi na inayokufaa.

Unaweza kuambiwa kula aina hii ya chakula, usile aina ile ya chakula,acha kabisa kula aina hii ya chakula,kula sana aina ile ya chakula, mara kula sana aina hii ya matunda,usile aina ile ya matunda. Kwa mfano, wengi wanaambiwa wale ndizi changa kwa wingi,labda na ugali wa uwele,dona au ulezi kwa wingi. Sasa mathalani, umeenda sehemu ambapo hakuna ndizi changa,hakuna dona,ulezi au uwele, unataka kusema hautakula chakula? Utashinda na njaa? La Hasha, utakula tu, mwenye kisukari anakula  aina zote za chakula, iwe wali,ndizi za kupika,pilau,biryani,viazi vya aina yote, maboga,sembe,dona n.k, cha msingi ni kujua ni jinsi gani au kwa utaratibu gani unaweza kula vyakula hivyo.

Tusipikiwe au tusitengewe chakula tofauti na cha familia, hapana, tunakosea sana, chakula cha familia  ndio na wewe  mwenye ugonjwa wa kisukari unaweza kula chakula hicho hicho, hakuna chakula maalum cha mtu mwenye kisukari,isipokuwa tu wewe mwenyewe ni lazima ufahamu ni jinsi gani unatakiwa ule au ni kwa utaratibu gani unatakiwa ule, ndio maana ninasema wewe mwenye kisukari ndiyo tabibu wa kwanza wa kisukari.mimi nitakushauri,mpishi atapika tu na chakula kitawekwa mizani, ila wewe ndiyo utajua jinsi ya kula.Wewe ni Tabibu wa kwanza wa kisukari chako.

Ukurasa 3 ya 12