Image

Raia mmoja nchini Italia mwenye umri wa miaka 71 alipata mishtuko ya mioyo yake yote miwili na kupoteza fahamu kwa sekunde kadhaa lakini hatimaye aliweza kuokolewa maisha yake. Mtu huyo alikimbizwa katika hospitali ya Verona nchini Italia baada ya kupata maumivu ya kifua na mapigo ya mioyo yake kuwa si ya kawaida.

Taarifa kutoka jarida la American Emergency Medical Journal inaeleza kuwa mtu huyo aliwahi kufanyiwa upasuaji wa moyo na kupandikizwa moyo mwingine miaka kadhaa iliyopita katika upasuaji unaojulikana kama double heart transplant (heterotopic heart transplantation).

Hii ni aina ya upasuaji ambapo moyo hupandikizwa na kufanya kazi sambamba na moyo wa awali (wa mgonjwa mwenyewe) ambao huwa umeadhirika kutokana na maradhi. Chemba za damu za kwenye mioyo hiyo huunganishwa ili moyo uliopandikizwa uweze kusaidia moyo wa mgonjwa.

Ripoti zinasema kuwa moyo mmoja ulianza kuwa na nguvu zaidi kuliko mwingine na hivyo kusababisha mapigo yake kutofautiana na mwingine. Madaktari walijaribu kurekebisha mapigo ya mioyo hiyo ili yaendane sawa kwa kutumia dawa lakini mioyo hiyo iliacha kupiga kabisa na mtu huyo kuacha kupumua.

Hata hivyo, waliweza kumrejesha katika hali ya kupumua kwa kutumia kifaa maalum cha Defibrillator kabla ya kumfanyia upasuaji na kubadilisha kifaa kinachosaidia kuweka sawa mapigo ya moyo kinachojulikana kama pacemaker.

 

Kuharibika kwa chujio ama Glomerulonephritis ni aina ya ugonjwa wa figo unaoathiri sehemu maalum ya figo (chujio) inayohusika na uchujaji wa maji pamoja na uchafu kutoka katika damu. Sehemu hii huitwa glomelurus au chujio kama tutakavyokuwa tukitumia katika mada hii.
Visababishi
Mara nyingi chanzo halisi cha kuharibika kwa chujio za figo (glomerulonephritis) huwa hakijulikani. Hata hivyo wakati mwingine uharibifu huu unaweza kusababishwa na kushambuliwa na mfumo wa kinga ya mwili. Uharibifu katika chujio husababisha damu pamoja na protini kuingia katika mkojo.
Tatizo hili hukua kwa haraka na figo linaweza kupoteza uwezo wake wa kuchuja maji na uchafu kwa kasi ndani ya muda mfupi wa kati wiki chache mpaka miezi kadhaa. Aina hii ya kuharibika kwa chujio za figo kwa haraka hujulikana kitalaamu kama rapidly progressive glomerulonephritis.
Ukubwa wa tatizo na vihatarishi vyake
Takribani robo ya watu wanaopatwa na tatizo sugu la glomerulonephritis huwa hawana historia ya kuwa na ugonjwa wowote wa  figo hapo kabla.
Kuna mambo kadhaa yanayoweza kumfanya mtu awe katika hatari ya kupata glomerulonephritis. Mambo hayo ni pamoja na:
•Matatizo katika mfumo wake wa damu au lymph
•Kuwahi kutumia vimiminika vilivyotengenezwa kwa kemikali za hydrocarbon
•Wenye historia ya saratani
•Maambukizi ya bacteria aina ya streptococcus, virusi, majipu au maambukizi katika moyo 
Mambo mengine yanayoweza kuongeza hatari ya kupatwa na glomerulonephritis ni pamoja na:
•Magonjwa ya mishipa ya damu kama vile vasculitis au polyarteritis
•Matumizi yaliyopitiliza ya dawa za kutuliza maumivu za jamii ya Non steroidal anti-inflammatory drugs kama vile aspirin
•Magonjwa ya mfumo wa kinga ya mwili kama vile Anti-glomerular basement membrane antibody disease na IgA nephropathy
•Makovu katika chujio (Focal segmental glomerulosclerosis) au hali ya chujio kuwa na kuta nene kuliko kawaida (Membranoproliferative GN)
•Magonjwa yanayoathiri viungo mbalimbali vya mwili kama vile Henoch-Schonlein purpura, Goodpasture’s syndrome au Lupus nephritis 
•Ugonjwa wa kimetaboliki wa Amyloidosis
Dalili
Dalili kuu za glomerulonephritis ni kuwa na damu katika mkojo (hali inayoufanya mkojo kuwa na rangi kama nyeusi, kutu au samawati; mkojo kuwa kama wenye povu jingi (kwa sababu ya kuwa na protini nyingi kuliko kawaida) na kuvimba uso, macho, miguu au tumbo (hali inayojulikana kama edema)
Dalili nyingine ni pamoja na 
•Maumivu ya tumbo 
•Kutapika damu 
•Kuharisha au kupata choo kikubwa chenye kuchanganyika na damu 
•Kukohoa pamoja na kupumua kwa shida
•Kukojoa kupita kiasi 
•Homa
•Maumivu ya misuli na viungo, uchovu, maumivu ya mwili mzima pamoja na kukosa hamu ya kula 
•Kutokwa na damu puani
Baada ya muda, figo hushindwa kufanya kazi na mgonjwa huanza kuwa na dalili za mtu mwenye ugonjwa sugu wa figo.
Uchunguzi na vipimo
Kwa kawaida tatizo la uharibifu wa chujio za figo hutokea tatratibu sana hali inayoweza kufanya ugunduzi wake kuchelewa pia. Wengi wa wagonjwa wenye tatizo hili hugunduliwa pale wanapokwenda hospitali kwa ajili ya uchunguzi wa matatizo mengine. Mara nyingi hali hii hujifhihirisha kwa kuwepo na hitilafu katika kipimo cha urinalysis.  
Mambo makuu matatu yanaweza kuonesha kuwepo kwa uharibifu katika chujio za figo. Mambo hayo ni upungufu wa damu (anemia), shinikizo la damu kuwa juu na ishara za kupungua kwa utendaji kazi wa figo.
Vipimo vinavyoweza kufanywa hujumuisha vipimo vya mkojo, damu pamoja na picha kama vile Ultrasound, CT au SPECT/CT.
Vipimo vya mkojo kama vile urinalysis husaidia kuonesha:
•Utendaji kazi wa figo yaani Creatinine clearance pamoja na Urine creatinine
•Uchunguzi wa mkojo kwa kutumia hadubini
•Kiasi cha protini katika mkojo 
•Kiasi cha tindikali ya urea katika mkojo 
•Chembe nyekundu za damu (RBC) katika mkojo 
Specific gravity ya mkojo na kiasi cha chumvi kwenye mkojo (yaani urine osmolality)
Vipimo vingine ni pamoja na CT scan, ultrasound ya figo, X-ray ya kifua au Intravenous pyelogram (IVP)
Vipimo vya damu husaidia kuonesha:
•Kiasi cha protini ya albumin katika damu
•Utendaji kazi figo kuchunguza kiasi cha BUN na creatinine katika damu
•Viasili vinavyohusika katika mfumo wa kinga ya mwili kama vile Anti-glomerular basement membrane antibody, Anti-neutrophil cytoplasmic antibodies (ANCAs), Anti-nuclear antibodies au Complement levels.
Ili kuthibitisha uwepo wa tatizo hili na aina yake, kipimo cha biopsy (renal biopsy) hutumika. 
Matibabu
Matibabu ya glomerulonephritis hutegemea sana na kisababishi cha tatizo hili, aina yake pamoja na ukubwa wa tatizo lenyewe yaani wingi wa dalili pamoja na uzito wake. Dalili ya muhimu sana kuithibiti ni ongezeko la shinikizo la damu ingawa kwa kawaida huwa ni ngumu sana kuthibiti shinikizo la damu kuwa katika kiwango cha kawaida.
Mgonjwa anashauriwa pia kupunguza kiasi cha chumvi katika chakula chake na pia kiasi cha protein na maji anayokunywa ili kusaidia utendaji kazi wa figo. 
Dawa zinazoweza kutumika kwa mgonjwa mwenye tatizo hili ni pamoja na:
•Zile za kushusha na kuthibiti shinikizo la damu hususani za jamii ya Angiotensin-converting enzyme (ACE) inhibitors kama vile captopril, Lisinopril au Enalapril; na zile za jamii ya Angiotensin receptor blockers kama vile losartan, Valsartan na Irbesartan.
•Zile za jamii ya Corticosteroids kwa ajili ya kupunguza na kuondoa mcharuko mwili
•Zile za kupunguza nguvu ya mfumo wa kinga ya mwili
Iwapo dawa za kupunguza nguvu ya kinga ya mwili zimeshindwa kufanya kazi na kuna uthibitisho kuwa glomerulonephritis imesababishwa na mashambulizi ya seli za kinga ya mwili katika figo, mgonjwa anaweza kufanyiwa tiba inayoitwa plasmapheresis. Katika tiba hii, sehemu ya damu yenye seli za kinga ya mwili zijulikanazo kama antibodies huondolewa kwa kubadilishwa na maji maji (plasma) yasiyo na antibodies zozote zile. Kuondoa antibodies husaidia kupunguza mcharuko mwili na uharibifu zaidi katika chujio za figo.
Iwapo figo zitashindwa kufanya kazi kabisa, mgonjwa anaweza kuhitaji kufanyiwa dialysis au kupandikizwa figo mpya.
Matarajio
Kuharibika kwa chujio za figo kunaweza kuwa ni tatizo la muda na lenye kurekebishika au linaweza kudorora na kuwa la kudumu. Kudorora kwa chujio za figo kunaweza kusababisha kupungua kwa utendaji kazi wa figo au ugonjwa sugu wa figo kushindwa kufanya kazi (chronic renal failure), au kufa kabisa kwa figo zote ( end-stage renal disease). 
Madhara
Pamoja na kusababisha shinikizo la damu kuwa juu, uharibifu katika chujio za figo unaweza pia kusababisha mlinganyo usio sawa wa madini katika damu (electrolytes imbalance) kama vile ongezeko la madini ya potassium (hyperkalemia); maambukizi yanayojirudia katika njia ya mkojo, uwezekano wa kupata maambukizi ya mwili, mrundikano wa maji mwilini hali inayoweza kusababisha moyo kushindwa kufanya kazi (congestive heart failure) au maji kujaa katika mapafu (pulmonary edema); au ugonjwa wa figo ujulikanao kama Nephrotic syndrome (utaelezwa katika makal zijazo). 
Kinga
Inawezekana kuzuia uharibifu wa chujio za figo kwa baadhi ya watu ingawa, kwa ujumla ni ngumu kufanya hivyo. Baadhi ya mambo ya kufanya ili kuepuka kupatwa na tatizo hili ni pamoja na kuepuka matumizi ya vimiminika vyenye kemikali za hydrocarbons, matumizi ya madini ya zebaki pamoja na matumizi ya muda mrefu ya dawa za jamii ya nonsteroidal anti-inflammatory drugs (NSAIDs) kama vile Aspirin.

Huu ni ugonjwa unaoathiri zaidi ndege wa jamii mbalimbali. Hata hivyo virusi wanaosababisha ugonjwa huu, wana uwezo wa kujibadilisha umbo na tabia zake (mutation) na kisha kumuathiri mwanadamu. Mabadiliko haya ya kimaumbile na kitabia husababisha kutokea kwa milipuko (epidemic) ya mafua ya ndege sehemu mbalimbali duniani hali ambayo isipothibitiwa inaweza kusambaa na kuathiri sehemu kubwa ya dunia kwa wakati mmoja (pandemic).

Visababishi vya mafua ya ndege

Mafua ya ndege husababishwa na jamii ya virus wajulikanao kama Avian Influenza virus. Virusi vya kwanza kabisa kumuathiri binadamu na kumsababishia mafua ya ndege vilihusishwa na kuku na viligunduliwa mwaka 1997 huko nchini Hong Kong na kupewa jina la avian influenza A (H5N1). Huu ulikuwa ni mlipuko wa kwanza wa ugonjwa huu kuwahi kuripotiwa. Kuna matukio machache sana ya maambukizi kutoka kwa binadamu kwenda binadamu yaliyowahi kuripotiwa mpaka sasa.

Influenza virus ni nini?

Kuna aina kuu tatu za virusi wa influenza, A, B na C. Mafua ya ndege husababishwa na jamii ya influenza A ambao wana uwezo wa kuingia na kuishi katika seli za ndege. Umbo la kinasaba la virusi hawa wa influenza A limeundwa na kamba nane za protein aina ya RNA.

Aidha virus wa Influenza wanaweza pia kuainishwa kulingana na aina ya protein inayounda maumbo yao. Protini hizo zipo katika aina mbili nazo ni hemagglutinin (H) pamoja na neuraminidase (N). Protini hizi zina kazi mbalimbali katika umbo la virusi. Kadhalika protini hizi nao pia zimeganyika katika aina mbali, ambapo virusi hatari wa mafua ya ndege wanaundwa na aina ya 5 ya protin ya hemagglutinin na aina ya 1 ya protini ya neuraminidase na hivyo ndiyo maana hujulikana kama H5N1 influenza A virus.

Hii ni aina ya saratani inayokumba tezi ya thyroid. Ikumbukwe kuwa tezi ya thyroid ipo sehemu ya mbele ya shingo ya mwanadamu ikiwa na sehemu mbili (lobes) moja kila upande wa shingo.

Visababishi na ukubwa tatizo

Saratani ya thyroid huwapata watu wa umri mbalimbali, kuanzia watoto mpaka watu wazima. Watu waliowahi kupigwa mionzi sehemu ya mbele ya shingo wapo katika hatari kubwa ya kupata aina hii ya saratani. Kadhalika watu wazima ambao waliwahi kupigwa mionzi kipindi cha utotoni nao pia wana hatari kubwa zaidi ya kupata saratani ya thyroid hata kama hawakuwahi kupata tatizo hilo wakati wanakua.

Tiba ya mionzi maeneo ya shingoni ilikuwa ikitumika sana zamani kwenye miaka ya 50 mpaka 60 kwa ajili ya matibabu ya uvimbe wa tezi ya thymus, mafindofindo (tonsils), au baadhi ya magonjwa ya ngozi. Hata hivyo ni nadra sana kwa tiba hii kutumika katika zama hizi.

Vihatarishi vingine vya saratani ya tezi ya thyroid ni pamoja na kuwepo kwa historia ya tatizo hili miongoni mwa wanafamilia na kuwa na goita iliyodumu muda mrefu bila kutibiwa.

Aina za saratani ya tezi ya thyroid

Kulingana na aina ya seli zinazounda tezi ya thyroid zinazoshambuliwa, saratani ya thyroid inaweza kugawanywa katika aina zifuatazo

Gauti (Gout) ni aina ya ugonjwa unaoathiri viungo vya mwili unaosababishwa na kuwepo kwa kiasi kikubwa kuliko kawaida cha tindikali ya Urea (uric acid) katika damu.

Ongezeko la uric acid husababisha madhara katika jointi (joint) (joint ni sehemu ya mwili inapokutana/ inapoungana mifupa miwili). Gauti inaweza kutokea ghafla (acute gout) au ikawa sugu (chronic gout). Gauti inayotokea ghafla huwa na maumivu makali na mara nyingi huathiri jointi moja tu wakati gauti sugu inaweza kuathiri jointi zaidi ya moja na huambatana na hali ya kujirudia ya maumivu na uvimbe kwenye jointi.

Visababishi

Gauti husababishwa na kuwepo kwa kiwango kikubwa kuliko kawaida cha uric acid katika damu. Hali hutokea iwapo mwili  wa mgonjwa unatengeneza uric acid nyingi kuliko kawaida au unashindwa kutoa uric acid mwilini kama inavyotakiwa.

Ongezeko hili husababisha mrundikano wa uric acid katika maji maji yanayozunguka jointi yanayoitwa synovial fluid na hatimaye kutengeneza vijiwe vidogo vidogo vya tindikali ya urea yaani uric acid crystals ambavyo husababisha jointi kuvimba na hatimaye kuathirika.

Vihatarishi (risk factors)

Ingawa chanzo hakieleweki vema, ugonjwa wa gauti hutokea kuwapata baadhi ya watu walio katika familia moja. Wanaume huathiriwa zaidi kuliko wanawake ingawa wanawake waliokoma kupata hedhi huathiriwa zaidi kuliko wale wanaoendelea kupata hedhi.

Aidha unywaji pombe unachangia kwa kiasi kikubwa kuwepo kwa ugonjwa huu pamoja na matumizi ya baadhi ya madawa kama vile dawa za kutoa maji mwilini ambazo kwa ujumla husababisha ongezeko la kiwango cha uric acid katika damu.

Vihatarishi vingine vya gauti ni pamoja na kuwa na ugonjwa wa kisukari, magonjwa ya figo, unene uliopitiliza, ugonjwa wa sickle cell anemia au aina nyingine za upungufu wa damu, pamoja na saratani ya damu (leukemia).

Hali kadhalika, gauti inaweza kusababishwa na matumizi ya dawa ambazo utendaji wake kazi huingiliana na utoaji wa uric acid mwilini.

Dalili

  • Dalili za gauti kwa kawaida uhusisha jointi moja au joint chache. Jointi zinazoathiriwa zaidi ni pamoja na kidole kikubwa ha mguuni, magoti, au kiwiko cha mguu.
  • Wagonjwa huwa na maumivu yanayoanza kwa ghafla hususani nyakati za usiku. Mara nyingi mgonjwa hudai anasikia maumivu makali kama kitu kinachokata, kupwita au mifupa inayosagana.
  • Jointi hubadilika na kuwa na joto, kuvimba na kuwa na nyekundu (hujionesha zaidi kwa watu wenye ngozi nyeupe). Kwa kawaida mgonjwa hulalamika maumivu makali ikiwa ataguswa kwenye jointi yenye matatizo.
  • Shambulio linaweza kudumu kwa siku kadhaa kabla mgonjwa hajapata nafuu, lakini pia laweza kujirudia mara kwa mara.
  • Pia mgonjwa anaweza kujihisi homa.

Baadhi ya wagonjwa hupata gauti sugu ambayo huwaletea madhara sugu katika jointi (chronic arthritis) hali ambayo husababisha mgonjwa kujihisi maumivu na muda mwingi kushindwa vizuri kutumia jointi zake. Wagonjwa wenye gauti kwa muda mrefu huwa pia na vinundu chini ya ngozi inayozunguka jointi zilizoathirika. Vinundu hivi kwa kitaalamu huitwa trophy na ni ishara ya muhimu kwa madaktari.

Vipimo

Vipimo vya gauti hujumuisha

  • Kiwango cha uric acid katika damu. Hata hivyo, si kila aliye na kiwango kikubwa cha uric acid katika damu huwa na gauti.
  • Kiwango cha uric acid katika mkojo
  • Uchunguzi wa maji maji yanayozunguka jointi (synovial fluid) kuchunguza vijiwe katika jointi
  • X ray ya jointi iliyoathirika
  • Uchunguzi wa utando unaozunguka jointi (synovial biopsy)

Matibabu

Matibabu ya gauti hujumuisha matumizi ya dawa, lishe pamoja na mabadiliko katika mfumowa maisha wa mgonjwa.
Dawa hutumika mara tu mgonjwa anapopata shambulio la ghafla. Dawa hizo ni pamoja na

  • Dawa za kutuliza maumivu kama vile codeine, paracetamol
  • Dawa za kutuliza mcharuko mwili (nonsteroidal anti-inflammatory drugs (NSAIDs) kama vile ibuprofen (brufen), indomethacin (indocid), diclofenac n.k. Pia ni muhimu mgonjwa kumfahamisha daktari wake iwapo ana matatizo yasiyoendana na matumizi ya dawa hizi kama vile vidonda  vya tumbo au mzio.

Dawa hizo husaidia kupunguza maumivu, uvimbe, na mcharuko mwili (inflammation). Baadhi ya madaktari huchoma sindano dawa ya corticosteroids kwenye jointi iliyoathirika kwa ajili ya kupunguza maumivu na uvimbe. Kwa kawaida maumivu huondoka saa 12 baada ya kuanza matibabu, na mgonjwa hupata nafuu kamili baada ya saa angalau 48.

Ili kupunguza kiwango cha uric acid katika damu, mgonjwa hupewa dawa za allopurinol au probenecid kila siku. Wagonjwa wanaotumia dawa hizi ni wale ambao hupata mashambulizi ya mara kwa mara ndani ya mwaka au wale ambao hupata mashambulia makali, wagonjwa waliopata madhara mkubwa kwenye jointi, wagonjwa walio na vinundu (trophy) au wagonjwa wenye vijiwe vya uric katika figo.

Lishe na mabadiliko katika mfumo wa maisha husaidia pia kuthibiti na kumuepusha mgonjwa na mashambulizi ya mara kwa mara ya gauti. Njia hizi ni pamoja na:

  • Kuacha kunywa pombe
  • Kupunguza ulaji wa vyakula vyenye viasili vya purine (aina ya protini) kama vile nyama ya mbuzi, samaki jamii ya sardines na herring, nyama ya maini au figo, mkate mtamu, maharage yaliyokaushwa, njegere, baadhi ya aina za uyoga, spinachi, n.k.
  • Thibiti pia ulaji wa nyama kwa kila mlo unaokula
  • Jiepushe na matumizi ya vyakula vya mafuta kama vile ice creams, mayonise au vyakula vya kuokwa
  • Kula kiasi kikubwa cha wanga
  • Iwapo utaamua kupunguza uzito, hakikisha unapunguza kidogo kidogo kwa sababu upunguzaji wa kasi unaweza kusababisha vijiwe vya uric kujitengeneza katika figo

Matarajio

Wagonjwa wanaofuata masharti na ushauri wa daktari huweza kuishi maisha ya kawaida. Hata hivyo, ni vema kufahamu kuwa mara nyingi gauti ya ghafla hatimaye huwa gauti sugu.

Madhara ya gauti

  • Gauti inaweza kusababisha matatizo sugu kwenye jointi (chronic gouty arthritis)
  • Vijiwe katika figo
  • Mrundikano wa uric acid unaoweza kusababisha ugonjwa sugu wa figo

Kinga

Kwa kawaida gauti haizuiliki, hata hivyo mgonjwa anashauriwa sana kujiepusha na vitu vinavyoweza kuchochea shambulizi na dalili za ugonjwa huu (rejea lishe na mabadiliko katika mfumo wa maisha hapo juu).

Leukemia ni saratani inayoshambulia tishu za mwili zinazohusika na utengenezaji wa damu zikiwemo supu ya mifupa (bone marrow) na mfumo wa lymph (lyphatic system). Kwa maneno rahisi, leukemia humaanisha saratani ya damu. Kuna aina mbalimbali za leukemia, nyingine zikiathiri watoto na nyingine zikiathiri zaidi watu wazima.

Kwa kawaida leukemia huanzia kwenye chembe nyeupe za damu yaani white blood cells, ambapo mwili huzalisha kiwango kikubwa cha seli zenye maumbo mabaya ambazo hazina uwezo wa kufanya kazi zake sawasawa. Kazi ya chembe nyeupe za damu ni kulinda mwili dhidi ya vimelea waletao maradhi mbalimbali.

Leukemia husababishwa na nini?

Kama zilizo kwa aina nyingi za saratani, mpaka sasa chanzo halisi cha leukemia hakijulikani. Hata hivyo, wanasayansi wanadai kuwa leukemia hutokea kutokana na mkusanyiko wa vyanzo mbalimbali vikiwemo vinavyohusu sababu za kinasaba (genetic factors) na kimazingira.

Kwa ujumla, leukemia hutokea pindi chembe nyeupe za damu zinapobadilika muundo wake wa kinasaba yaani viasili vyake vya DNA, ambavyo kwa kawaida hubeba maelekezo yanayoifanya seli yeyote ya kiumbe hai iweze kuishi, kutenda kazi zake, kujizaa na hata kufa, vinapobadilika maumbile na muundo wake kutokana na sababu mbalimbali. Kitendo cha kubadilika kwa maumbile na muundo wa DNA hujulikana kama mutation. Ndiyo kusema basi, seli yeyote iliyopatwa na tatizo hili huwa na tabia ya kukua kwa haraka na kujizaa (kujigawa) kwa kasi zaidi kuliko kawaida, na pindi inapofikia muda wake wa kufa seli hiyo hugoma kufa badala yake huendelea kujizaa zaidi hatimaye kusambaa kwa wingi katika mfumo mzima wa damu, hali inayosababisha saratani ya damu.

Je, kuna vihatarishi vya leukemia?

Malaria is known to be the largest single  component of the burden of diseases in Tanzania for both morbidity and mortality especially for under fives and pregnant women. In Dodoma region, the prevalence of malaria among underfives is 12.5% while, in Bahi District Council, about 60,000 people of all ages suffer from malaria every year.

Malaria diagnosis is first suspected on defined features and then confirmed by laboratory tests mainly through microscope; however in the year 2010, the cheapest and easiest laboratory test was introduced in Bahi District Council namely Malaria Rapid Diagnostic Test (m-RDTs).

Malaria Rapid Diagnostic Test (m-RDT) is a test that assists in the diagnosis of malaria by providing evidence of presence of malaria parasites in the human blood within a very short period of time and it’s considered to be user friendly as it doesn’t need one to have advanced lab training.

The prevalence of malaria in our district council was reported to be higher prior to introduction of m-RDTs, and malaria was always ranked number one in the district’s top ten diseases. However, after the introduction of  m-RDTs in the year 2010 there has been changes on the trend of the top ten diseases as the number of malaria cases is  currently on the decline compared to the same period of time before the use  this rapid test. The aim of this study was to determine the success obtained after introduction of m-RDT as a tool for diagnosis of malaria in Bahi District Council.

The study design was descriptive comparative study, in which District Health Information System data base gathered from Health facility reports were used. The information obtained was organized and computerized in a soft ware. Analyses were based on descriptive and comparisons between two periods of January – June 2011 and the same time period of the year 2010. All tests were done using relevant statistical tests.

The findings reported a high number of malaria cases between January and June 2010 when both microscope and clinical diagnosis for malaria were still used in the diagnosis of malaria, compared to the same six months-period of January to June, 2011 when we started using malaria rapid diagnostic tests (m-RDTs) as an adjuvant doagnostic modality for malaria. In overall malaria case diagnosis was reduced by 65% for under fives, 58% for above five years and 63% for patients of all ages. This difference was found to be statistically significant. In the year 2010 malaria was leading among the district’s top ten diseases reporting 39,295 cases followed by Acute Respiratory Tract Infection (ARI) which had 17,126 cases. On the contrary, until June 2011, ARI was reportedly leading with 21,244 cases followed by malaria with 17,126 cases.

Microscope remains the gold standard for malaria diagnosis, however due to reasons such as lack of skilled laboratory personnel and unavailability of microscopes and reagents, the best diagnostic modality at the moment would be malaria rapid diagnostic tests which can help in the over- and/or mis-diagnosis of malaria and patients’ mismanagement who actually have other diseases than malaria.

From our findings we recommend that, it is time now we review our malaria treatment guidelines including its testing algorithms  in order to improve the quality of health care delivery through proper management of malaria cases by use of m-RDT especially for the developing countries.

The author declares no conflicts of interest.


The author is Public Health Specialist, and a District Medical Officer (DMO) for Bahi District Council in Dodoma, Tanzania.


 

Photo Credit: NMCP

Ugonjwa sugu wa figo hutokea pale figo zinazopoteza uwezo wa kutenda kazi unaotokea taratibu na kudumu baada ya kitambo fulani. Hali hii hutokea taratibu, na huchukua muda wa takribani miezi kadhaa hata miaka. Ugonjwa sugu wa figo umegawanywa katika hatua kuu tano, kulingana na ukubwa wa tatizo.

Figo linapopoteza uwezo wake wa kutenda kazi, kusanyiko na limbikizo la maji, uchafu na sumu hutokea mwilini mwa mgonjwa. Aidha kushindwa kufanya kazi kwa figo husababisha pia kutokea kwa maradhi mengine kama vile upungufu wa damu mwilini (anemia), shinikizo la damu (hypertension), ongezeko la tindikali kwenye damu (acidosis), ongezeko la lehemu na mafuta kwenye damu, na magonjwa ya mifupa.

Hatua ya tano ya ugonjwa sugu wa figo hujulikana pia kama kushindwa kufanya kazi sugu kwa figo (chronic kidney disease au end-stage-renal disease).

Tofauti ya Ugonjwa sugu wa figo na kushindwa kufanya kazi kwa figo kwa ghafla (AKI) ni kwamba AKI hutokea ghafla, huchukua muda mfupi kati ya siku hadi wiki kadhaa kuwa tatizo kubwa zaidi. Tofauti nyingine ni kuwa AKI hutokana na tatizo linaloathiri figo moja kwa moja, mishipa yake ya damu au mtiririko wa mkojo unaotoka kwenye figo. Aidha ARF mara nyingi huweza kurekebishwa na mgonjwa akapona kabisa, ingawa kwa baadhi ya wagonjwa sehemu fulani ya figo inaweza isipate nafuu na ikaendelea kudorora kiutendaji kazi.

Hatua za Ugonjwa Sugu wa Figo

Hatua hizi zimegawanywa kulingana na kiwango cha GFR kilichofikiwa na figo husika. GFR kwa kirefu Glomerular Filtration Rate ni kiwango kinachoonesha uwezo wa utendaji kazi wa figo. GFR hupima uwezo wa glomeruli (chujio) la figo katika kuchuja uchafu, maji pamoja na sumu nyingine kwa kila dakika moja kwa mtu mwenye wastani wa urefu wa mita za mraba 1.73. Kadiri jinsi GFR inavyopungua, ndivyo inavyoashiria ukubwa wa tatizo katika figo.

Katika muendelezo wa magonjwa ya moyo ya kuzaliwa nayo, leo nitagusia kuhusu Tundu katika kuta za juu za moyo (atrial walls) au kwa kitaalamu Atrial septal defect (ASD).

Wakati kijusi (fetus) kinapo endelea kukua, kuta kati ya atria mbili za moyo nayo hukua (kitaalamu interatrial septum) ili kutenganisha chemba ya kulia na kushoto. Lakini katika kipindi hiki huwa kuna tundu kati ya kuta hizi kitaalamu huitwa foramen ovale.

Tundu hili ni la kawaida kwa kipindi hiki cha kijusi, tundu hili husababisha damu yenye oksijeni  kutoka kwenye kondo la mama (placenta) kutokwenda kwenye mapafu amabayo hayaja komaa na kuelekea sehemu nyingine za mwili hasa kichwani. Kipande cha tishu kinachoitwa kitaalamu septum primum hufanya kazi kama valvu katika tundu hili. Mara tu mtoto anapozaliwa, shinikizo katika mishipa ya damu ya mapafu (pulmonary circulatory system) hushuka na kusababisha tundu hili (foramen ovale) kufunga kabisa.

Tundu hili huwa halifungi kabisa kwenye karibu asilimia ishirini na tano ya watu wazima, hivyo pindi shinikizo likiongezeka katika mishipa ya damu ya mapafu (hali inayoweza kutokea kwa sababu ya kuwepo kwa shinikizo la damu kwenye mapafu (pulmonary hypertension) kutokana na sababu mbalimbali, au kuwa na matatizo ya kikohozi cha muda mrefu), husababisha tundu la foramen ovale kutofunga na kubaki wazi. Hali hii kitaalamu huitwa patent foramen ovale (PFO).

Aina za tundu katika kuta za juu za moyo

Mpaka sasa, zipo aina kuu sita za tundu katika kuta za juu za moyo, ambazo ni

Utangulizi

Ugonjwa wa Alzheimer's ni miongoni mwa magonjwa ya ubongo yanayoathiri zaidi wazee au watu wa umri wa makamo. Ugonjwa huu ambao huanza polepole na kuchukua muda mrefu kujitokeza kwa kawaida hauoneshi dalili ya kupata nafuu mara unapoanza.

Ugonjwa wa Alzheimers’s ni miongoni mwa makundi ya magonjwa ya akili yanaitwa kitaalamu kama dementia na ambao huathiri zaidi watu wenye miaka 65 au zaidi.

Ugonjwa wa Alzheimer’s unasababishwa na nini?

Mpaka leo hii, chanzo halisi cha ugonjwa wa Alzheimer’s bado hakijajulikana. Hata hivyo, kuna nadharia kadhaa zilizoibuliwa na wanasayansi kuhusiana na baadhi ya visababishi vya ugonjwa huu. Nadharia inayoonekana kukubalika mpaka sasa ni ile ya uhusiano wa kuwepo kwa jamii ya protein inayoitwa amyloid na ugonjwa huu.

Wanasayansi wameonesha kuwa mabadiliko katika vinasaba vinavyodhibiti uzalishwaji wa protini hii ya amyloid ndiyo chanzo kikuu cha ugonjwa huu. Aidha ushahidi uliooneshwa na watafiti hao unasema kuwa mabadiliko haya ya vinasaba yamethibika kwa takribani zaidi ya nusu ya wagonjwa wote waliogunduliwa kuwa na ugonjwa huu.

Katika wagonjwa wote hawa waliofanyiwa utafiti imeonekana kwamba mabadiliko hayo ya vinasaba yamesababisha uzalishwaji uliopitiliza katika ubongo wa aina fulani ya vipande vya protini ijulikanayo kitaalamu kama ABeta (Aβ). Wataalamu wengi wanaamini kuwa, kukosekana kwa udhibiti wa uzalishaji wa aina hii ya protini kunakosababisha protini hii kuwa nyingi mno kwenye ubongo kuliko inavyoweza kuharibiwa ndiko kunakosababisha ugonjwa huu.

Ukurasa 10 ya 12